TLS, MAT, Media na possibly Bunge...Magufuli sasa unapoteza pambano mzee!

Ki Mun

JF-Expert Member
Oct 6, 2014
3,442
4,388
Ewe Mkuu uliyetukuka na unayejiamini mno...amini usiamini you are proving to us kwamba unapoteza pambano mzee, nakuona unapaisha tu mipira juu ya lango la timu pinzani kama si tu umebaki umepaki bus golini mwako!

Umesema wewe unajiamini lakini nashangaa kwanini huthubutu kutembea bila walinzi,

Unasema unajiamini lakini nashangaa kwanini unaogopa mikutano ya vyama vya siasa na bunge huru,

Sasaa...nakuona umeamua makusudi kugombana na vyombo vya habari, TLS walishakupiga na MAT wanakugomea fikra zako...kuna uwezekano mkubwa bunge la bajeti pia litakuhenyesha kuanzia mwezi ujao...sasa Mkuu huoni kama umetokezea Buguruni wakati ulikuwa ukielekea Mwenge?

Simama, Tafakari, Chukua hatua mzee japo nimekusikia anyway ukitutangazia mbele ya Rais wa Benki ya Dunia kwamba wewe hushauriwi!
 
Back
Top Bottom