Tibaijuka achia madaraka umetuibia vya kutosha

Father of All

JF-Expert Member
Feb 26, 2012
6,376
6,726
Waliosikia hotuba mbovu ya prof Anna Tibaijuka kwanza wameshangaa mantiki ya uprofesa wake ukiachia mbali kuonyesha ujinga wa ajabu.

Alidai hana hatia wakati alipokea fedha chafu na ya wizi. Pia alisema fedha ni kwa ajili ya maendeleo.

Maendeleo gani kwa fedha ya wizi na kwa ajili ya nani. Aliogeza kuwa hajiuzulu kana kwamba uwaziri ni kazi yake binafsi.

Aliwahi kusema eti James Rugemalayer ni kaka yake. Mbona kwenye mgao hatuoni ndugu wengine?

Huyu mama asimlaumu mtu bali upofu na uroho wake. Anaposema kuwa taarifa za kukatiwa kitu ni uvumi anadharau Bunge na Kamati yake iliomkuta na hatia.

Namshauri akitoe asitujazie mbu. Ameishakatiwa chake basi aishie na kwenda kuajiriwa na Rugemalayer kama alivyofanya Patrick Rutabanzibwa aliyesifika kuwa mzalendo wakati ni fisi kwenye ngozi ya kondoo.

Unafiki mtupu kusema eti Tibaijuka haoni kosa wala hana hatia wakati ameneemeka na fedha ya wizi tena wa kuibia watu maskini wa taifa ombaomba linaloongozwa na majambazi wezi na mafisadi.

Nenda Tibaijuka nenda wala usigeuke nyuma. Nenda mwanakwenda tu umeishatuibia. Nenda hatukutaki tena fisadi mkubwa.
 
Kuanzia jana huyu mama nimemdharau kwenye mambo ya uongozi, anazidi kutidhihirishia kwamba kuna shida katika hawa wasomi wetu wa kiwango cha u-prof na Dr.
 
Amekuibia nini wewe mtu mwenyewe hata baiskeli ya miti huna toa uongo wako hapa
 
mtanivumilia wahusika.
kuanzia leo nawaweka wahaya kwenye number 2 ya wezi wakuu wa nchi hii. na nafasi ya tatu inashikiliwa na wakurya. mwizi number moja anajulikana. wakipata madaraka ya umma wanafikiria kuiba tu. nothing else. they are good in nothing.
lengo wajirekebishe.
kuanzia leo popote ninapowaona najua nimekutana ni mwizi.
 
Amekuibia nini wewe mtu mwenyewe hata baiskeli ya miti huna toa uongo wako hapa

Yeye ni Waziri ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi, halafu anapokea fedha toka kwa mfanyabiashara kwa ajili ya shule yake. Je ikitokea mfanyabiashara huyu akatumia hela yake kumkandamiza mwananchi wa chini kwa kunyang'anya eneo lake, Je unategemea huyu Waziri atatoa maamuzi ya haki kati ya Mfanyabiashara aliyemfadhili na mwananchi wa kawaida? Lazima ukubali tu kitendo cha Waziri kuchukua hela kwa mfanyabiashara si kizuri na enzi za mwalimu huyu mama hata ubalozi wa nyumba kumi asingepewa.
 
Tibaijuka alipaswa kunyang'anywa uprofesa wake mara moja! Jana ameeleza utumbo ambao hauelezeki kamwe!
 
Tibaijuka ni mchapa kazi sana na ni muadilifu

Kweli ni mchapakazi lakini sio muadilifu. Anaweza asitoe haki ikitokea kuna mgogoro wa ardhi kati ya Rugemalira na mwananchi wa kawaida. Ni kama kazibwa mdomo na Rugemalira. Hawa wafanyabiashara huwa na malengo yao ambayo wakati mwingine yanaumiza watu wa chini.
 
Huyu mama Tibaijuka alikuwa Habitat ofisi za Nairobi,hata huko alikuwa na kashfa ya ufisadi.
 
Mama Tibaijuka naomba ufafanuzi ni kwanini fedha hizi ziingizwe kwenye A/c yako na si kwenye a/c ya shule? Mzee Ruga anajuwa kuwa pesa ilipelekwa kwenye a/c ya shule au ni a/c yako? Naomba mama kwa kulinda hadhi yako kimataifa achia ngazi. li sababu unazozisema leo kajitetee mahakamani.
 
mtanivumilia wahusika.
kuanzia leo nawaweka wahaya kwenye number 2 ya wezi wakuu wa nchi hii. na nafasi ya tatu inashikiliwa na wakurya. mwizi number moja anajulikana. wakipata madaraka ya umma wanafikiria kuiba tu. nothing else. they are good in nothing.
lengo wajirekebishe.
kuanzia leo popote ninapowaona najua nimekutana ni mwizi.

Nitamshangaa atakayekushangaa
Maana wewe ni Abunuas
 
Amekuibia nini wewe mtu mwenyewe hata baiskeli ya miti huna toa uongo wako hapa

Kwani hujui kuwa hata hicho kikopo ulichonacho wewe chanzo chake ni kodi ya masikini asiye hata na nyumba! Mfike mahali mchague maneno. Ndio maana mama yenu amejikuta katumbukia na namna ya kutoka hana. Na kama nyie ndio washauri wake amekwisha. Hutumii hata logic kum-crash nwenzio.
 
Hujui usemayo kihiyo wewe. Yaani hayo mabilioni huoni kuwa ni ya watanzania nami ni mmojawapo. Ungejua utajiri wangu usingesema uliyosema fisadi mwenye akili chafu wewe.
 
Back
Top Bottom