Thierry Henry astaafu soka rasmi

mwekundu

JF-Expert Member
Joined
Mar 4, 2013
Posts
22,477
Reaction score
21,025

Thierry Henry

Mshambuliaji wa zamani wa Klabu ya Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa Thierry Daniel Henry ametangaza kustaafu kucheza soka rasmi.

Nyota huyu alietwaa kombe la dunia mwaka 1998 akiwa na timu ya Ufaransa alijiondoa kwenye klabu yake New York Red Bulls mapema mwezi huu na kukawa na tetesi atachagua kujiunga na klabu nyingine kubwa barani ulaya.

" Napaswa kuwashukuru mashabiki wote, nawashukuru wachezaji wenzangu na watu binafsi wanaohusika na AS Monaco, Juventus, Arsenal FC, FC Barcelona,na New York Red Bulls na pia Timu ya taifa ya Ufaransa waliufanya wakati wangu wa mchezo kuwa Maalumu".
Henry alianza kuwika katika soka la kimataifa akianzia klabu ya Monaco kisha akaelekea Juventus ,kabla ya kutua Arsenal alikocheza kwa mafanikio makubwa.

Chanzo:BBC
 
safi sana chogo nilikupenda ulikuwa na nidhamu ya hali ya juu hongeraaaa
 
[h=1]Henry retires and joins Sky[/h]Thierry Henry has announced his retirement from football and will join Sky Sports as a football expert and ambassador from the start of 2015.
 

Thank you King Thiery Henry "titi"; you entertained us with your awesome soccer skills; you will forever stand tall; you are among the best soccer 'magicians the world has ever seen; Best wishes "Titi" in your next undertaking and happy holidays
 
Sometimes later we need you at the Emirates as a super coach ..welcome back home son!
 
Sometimes later we need you at the Emirates as a super coach ..welcome back home son!

Hawa wachezaji wa zamani wanaendaga kuharibu kurudi kwenye timu zao kama makocha wanapokuwa pundits. Huwa hawachelewi kuwakosoa makocha wao. Ukiwa pundit lazima useme ukweli, Henri sidhani kama kuna siku atamkosoa Wenger, hapo ndo eidha ataharibu SkySports au ataharibu Arsenal. Nampenda Garry Neville, yuko neutral, hamna mahaba!
 
Henry ndio mchezaji bora wa muda wote hutaki unaacha
 
T14!
Kuna mechi ya Arsenal T14 alifunga akiwa amelipa kisogo goli la wapinzani..... kuna lile goli alilowafunga R. Madrid ya Beckham ..... afu kuna lile goli Liver na Arsenal, Gerrard anatoa boko kwa back passs ..... afu kuna yale magoli aliyowashughulikia Inter, pale San SIRO ktk UEFA, daaaaah..., huyu mtu huyu, alikuwa bora ktk zama zake! Sasa ukitaka kujua namna nilivocheza soka enzi zangu, T. Henry ndio copy yangu!
 
Shadow nitakuja kuazima hii albaum ya T14
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…