The Septemba 11

The Septemba 11

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,018
Reaction score
20,489
Yote haya yalikuwa yamefanywa wakati wa kipindi cha Cliton, “kitu gani

kinakusumbua sana siku hizi? Boren alimwuliza Tenet asubuhi hiyo. “Bin laden,”

Tenet alijibu akimanisha kiongozi wa ugaidi Osama Bin laden raia wa Saudi

Arabian aliyekuwa akiishi ukimbizini Afghanistan ambaye alikuwa ameanzisha

mtandao wa Al Qaeda dunia nzima neno ambalo kwa kiarabu linamaanisha “

Kituo kikuu”.

“Oh, Tenet!” Boren alisema kwa muda wa miaka miwili iliyopita alikuwa

akisikiliza wasiwasi wa rafiki yake kuhusiana na Bin laden,je, mtu mmoja

binafsi angewezaje bila ya kutumia utajiri wa serikali ya kigeni akawa tishio

kubwa kama hili? aliuliza, “huwezi kufahamu uwezo na kiwango cha yale

wanayoyapanga”, Tenet alisema.

Boren alikuwa na wasiwasi kwamba rafiki yake alikuwa ameamua kuwa na chuki

za ajabu dhidi ya Bin laden. Karibu miaka miwili hapo nyuma muda mfupi tu

kabla ya sherehe za kutimia kwa mwaka 2000 Tenet alikuwa amechukua hatua

ambayo haikuwa ya kawaida kwa kumwonya binafsi Boren asisafiri au kutokea

kwenye matukio makubwa ya wazi katika mkesha wa mwaka mpya kwa sababu

alitegemea kungekuwa na mashambulizi makubwa.

Na siku za karibuni zaidi, Tenet alikuwa na wasi wasi kwamba kungekuwa na

mashambulizi wakati wa sherehe za tarehe 4 Julai 2001. japokuwa hakuyafichua

hayo kwa Boren, kulikuwa na matukio 34 ya habari zilizonaswa miongoni mwa

washirika wa Bin laden zikielezea matamshi kama vile “siku ya kiama ni kesho”

au “ “tukio la ajabu ni kesho”

Kulikuwepo na unaswaji mkubwa wa habari kama hizi katika mitandao ya

ujasusi na ripoti nyingi zilisema kulikuwa na shambulio kubwa dhidi ya balozi za

marekani au dhidi ya makundi ya watalii wa marekani nchi za nje, lakini habari

za kijasusi hazikuweza kufahamu ni lini wapi na kwa njia gani. Hapakutokea

chochote, lakini Tenet alisema kwamba suala hilo lilikuwa linamfanya akose usingizi.

Ghafla mara walinzi wa Tenet walikuja mbio kuelekea mezani alikokuwa.Uh-oh,

Boren aliguna moyoni “Bwana Mkurugenzi”, mmoja wao alisema “kuna tatizo

kubwa”. “Ni nini”” Tenet aliuliza akionyesha kwamba kwake ilikuwa ni vyema

kumpa mtu uhuru wa kuzungumza bila woga . “mnara wa kituo cha Biashara

umeshambuliwa.” Mmoja wao alimpa Tenet simu ya mkono na akapiga simu

makao makuu.

“Kumbe wameigongesha ndege kwenye jengo lenyewe?” Tenet aliuliza akiwa

haamini. Aliamuru watu wake muhimu kukutana katika chumba cha mkutano

kwenye makao makuu ya CIA, Akaagiza kuwa angekuwa amefika huko katika

kipindi cha dakika 15 hadi 20. “Yote haya siku zote yamekuwa ni Bin Laden,”

Tenet alimwambia Boren. “Lazima niondoke” pia alifahamu kwamba uwezekano

halisi ni kwamba CIA na shirika la upelelezi la Marekani (FBI) havikufanya yote

yanayotakiwa ili kuzuia shambulio hilo la kigaidi.”

24


“Nashangaa,” Tenet alisema, “iwapo hii inahusiana na jamaa huyu ambaye

anachukua mafunzo ya kurusha ndege.” Alikuwa akizungumza kuhusu Zacarias

Moussaoui raia wa Ufaransa mwenye asili ya Morocco ambaye FBI ilikuwa

imemtia kizuizini huko Minnesota mwezi uliopita baada yakuonyesha tabia za

ajabu wakati akiwa katika shule ya mafunzo ya kurusha ndege.

Tukio hilo la Moussaoui likiwa bado liko katika mawazo yake. Mnamo Agosti, FBI

ilikuwa imeomba CIA na wakala wa Usalama wa Taifa kufuatia simu zote

ambazo Moussaoui alikuwa amezipata nchi za nje. Mtu huyo alikuwa tayari faili

lake limetuna makaratasi ya unene wa inchi tano katika ofisi hiyo ya ujasusi

wakati Tenet anaingia katika gari lake kwenda kwenye makao makuu ya CIA

ambayo yana eneo la hekta 258 huko Langley Virginia, juhudi zake za kupigana

dhidi ya ugaidi wa siku za nyuma zilikuwa zikipishana kichwani mwake.

CIA ilikuwa inamwinda Bin laden kwa zaidi ya miaka mitano na juhudi hizo

zikazidi baada ya ulipuaji mabomu wa mwaka 1998 wa balozi wa Marekani

nchini Kenya na Tanzania ambao ulisimamiwa na Bin laden na kuacha watu

zaidi ya 200 wakiwa wamekufa. Wakati huo, Rais Clinton alielekeza jeshi la

Marekani kufyatua makombora 66 katika kambi za magaidi ambako Bin laden

anasadikiwa kuwa alikuawa akifanya mkutano muhimu . Lakini ni wazi alikuwa

ameondoka masaa machache kabla ya makombora hayo kufika sehemu hiyo.

Mwaka 1999, CIA ilianzisha harakati za siri za kutoa mafunzo kwa makomandoo 60

kutoka katika shirika la ujasusi la Pakistan ili kuingia Afghanistan kumteka Bin

laden. Lakini harakati hizo zilikwama kutokana na mapinduzi ya kijeshi

yaliyotokea nchini Pakistan. Njia nyingi zaidi na za hatari zilikuwa zimepangwa

katika mfululizo wa mikutano na maofisa wa ngazi za juu wa usalama wa taifa

katika utawala wa Clinton.

Moja ya chaguo ambalo lilikuwa limefikiriwa lilikuwa ni shambulio la usiku

kutoka kwenye helikopta dhidi ya Bin laden kwa kutumia kikosi kidogo maalum

cha Marekani chenye watu wapatao 40, shambulio hilo lingehitaji ndege

kupatiwa mafuta zikiwa angani kwani helkopta hizo zingelazimika kusafiri kiasi

cha maili 900.

Lakini mpango huo ulivurugika kutokanaka na oparesheni “Desert One” ya

mwaka 1980 ambayo Rais Carter aliamuru ifanywe ili kuwaokoa mateka wa

Marekani waliokuwa wanashikiliwa nchini Iraq ambapo ndege kadhaa zilianguka

jangwani na kuangushwa, kama helikopta mbili aina ya “Black hawk” nchini

Somalia mwaka 1993 na kusababisha vifo vya Wamarekani 18.

Jeshi lilisema kwamba shambulio dhidi ya Bin Laden lingeweza kushindwa na

kusababisha hasara kubwa kwa askari wa Marekani, Habari za kijasusi pia

zilionyesha kwamba Bin Laden alikuwa akifuatana na familia yake, na Clinton

alikuwa anapinga oparesheni yoyote ambayo ingeweza kuua wanawake na

watoto.

25


Kikosi maalum cha Marekani na askari wa jeshi la maji wenye uwezo wa

kurusha makombora aina ya ‘cruise’ waliwekwa katika tahadhari lakini walihitaji

masaa sita hadi kumi kuweza kupata tahadhari ya mahali alipokuwa Bin Laden.

Moja ya siri zenye kulindwa zaidi katika CIA ilikuwa ni ile ya mawakala 30 wa

kijasusi wa Afghanistan waliokuwa wakiendesha shughuli zao chini ya maneno

ya siri GE/SENIORS, ambao walikuwa wamepewa fedha kwaajili ya kufuata

nyendo za Bin laden nchini Afghanistan. Katika miaka mitatu iliyopita kundi

hilo ambalo lililipwa dola 10,000 kila mwezi liliweza kusafiri pamoja au

kugawanyika katika vikundi vidogo vya watu watano. CIA kila siku ilikuwa na

vyombo salama vya mawasiliano “the Seniors” kama walivyokuwa wakiitwa, na

walikuwa wamenunuliwa magari na pikipiki lakini kuzifuatia nyendo za Bin laden

likawa jambo gumu zaidi kwani aliweza kusafiri bila mpangilio na kila mara

akiondoka nyakati za usiku au kuwalamba chenga za visigino akipita milimani.

Kitu cha ajabu ni kwamba seniors hao waliweza kujua wakati wote mahali

alipokuwa lakini kamwe hawakuweza kutoa habari thabiti za vitendo yaani

kusema kithibiti kwamba angeendelea kukaa mahali hapo kwa muda unaotakiwa

ili kuweza kulenga makombora ya ‘cruise’ mahali hapo. Na CIA ilishindwa kupata

mtu wa kuaminika ili kufanya ujasusi miongomi mwa watu wa Bin laden ambaye

angeweza kuwadokeza kuhusu mipango yake.

Kulikuwa na watu katika utawala wa Clintoni na vyombo vya usalama wa taifa

walikuwa hawana imani na seniors kwa vile kuna wakati kulikuwa na habari za

kupingana kuhusiana na mahali alipokuwa Bin laden. Na nchini Afghanistan watu

hususani wenye kuleta habari za kijasusi walikuwa wananunuliwa na kutoa

habari kwa watu wengine .Hadi sasa, si Clinton au Bush waliokuwa wametoa

madaraka kwa CIA kutuma seniors au mawakala wengine wenye kulipwa

kwenda kumuua Bin laden. Amri ya kirais kupiga marufuku mauaji ambayo

ilisainiwa kwanza na Rais Gerald Ford , ilikuwa na nguvu ya kisheria.

Katika kipindi kimoja kiongozi wa Seniors wa Afghanistan alikuwa amekutana

mara kadhaa na mkuu wa kituo cha CIA kutoka Islamabad, Pakistan, ambaye

alikuwa anawapa maelekezo na kuwalipa. Kiongozi huyo wa seniors alidai

kwamba walikuwa wameurushia risasi msafara wa Bin laden katika matukio

mawili katika kujihami, jambo ambalo lilikuwa linaruhusiwa lakini alitaka

kuufuatilia msafara huo kwa njia nyingine akiwa anapendekeza kuvamia kwa

kushitukiza ambapo kitu chochote kilicho karibu kitapigwa risasi, kuua kila mtu

na kisha kukimbia.Mkuu wa kituo cha CIA alisema, Hapana hamuwezi kufanya

hivyo jambo hilo litavunja sheria za Marekani.

Kwa kutilia maanani fedha iliyokuwepo, vitengo mbali mbali vya siri na

mazingira yaliyokuwepo, Tenet aliona kwamba CIA ilikuwa imefanya kila kitu

kilichotakiwa kufahamika. Lakini kamwe hakuomba kubadilishwa kwa sheria

alikuwa hajamwambia Clinton kuwepo kwa mfumo wa kijasusi ambao

ungewaruhusu Seniors kumvamia kwa kumshambulia Bin laden.

Mwanasheria kwenye Wizara ya sheria Ikulu aliamini wangekataa na kusema

kwamba hali hiyo ingekuwa imevunja sheria ya kupiga marufuku mauaji ya

26


watu. Tenet aliona amefungamanishwa na msimamo wa Clinton na washauri wake.

Kila kitu kimefungiwa “sheria ya kufa”, alikuwa akisema lakini na yeye pia

alikuwa amechangia katika hali hiyo katika kipindi chake cha miaka mitano na

nusu akiwa kama mkuu wa habari za Ujasusi wa Clinton na Naibu wa idara hiyo.

Sheria ilikuwa inasema kwamba CIA ingeweza kumkamata Bin laden na kumfikisha

katika vyombo vya sheria. Operesheni kubwa ya kufanya kazi hiyo iliwekwa katika

ratiba za njama siri za idara hiyo. Tenet alikuwa ana amini kwamba Bin laden

asingekubali kuchukuliwa akiwa hai, hivyo operesheni kama hii, iwapo

ingefanikiwa, ingepelekea katika mauti yake.

Lakini wataalam wote wa CIA katika kurugenzi ya Uendeshaji walifikiri

isingefanya kazi na kwamba ingesababisha watu wengi kuuawa na si lazima

awemo Bin laden.

Na Tenet alikubali Mpango huo kamwe haukuendelea zaidi ya hapo.

Pendekezo la Saudi Arabia kwamba CIA iweke silaha maalum katika mizigo ya

mama wa Bin laden ambaye alikuwa anasafiri kutoka Saudi Arabia kwenda

kumwona mwanaye nchini Afghanistan, pia lilikataliwa kwa vile lingekuwa la

hatari na kwamba lisingefanikiwa.

27


CRAIG KELLY AMPA UJUMBE POWELL.

Huko mjini Lima, Peru, asubuhi hiyo, waziri wa mambo ya Nje Colin L. Powell

alikuwa ndiyo kwanza ameanza kupata kifungua kinywa na rais mpya Alejandro

Toledo. Powell alikuwa anahudhuria mkutano wa nchi za umoja wa Nchi za

Amerika. .Alikuwa na mategemeo ya mawasiliano mema na mawaziri wa nchi za

nje au viongozi 34 wa nchi 35 za eneo hilo.Cuba ilikuwa haikukaribishwa,

Toledo alikuwa anasisitiza kuhusu mgao wa soko wa nguo kutoka Marekani .

Alitaka kuondolewa kwa kodi katika pamba ya hadhi ya juu ambayo alidai

isingeweza kushindanishwa na pamba ya hadhi ya chini iliyokuwa inazalishwa

katika mataifa ya kusini ya Marekani ambayo ilikuwa inataka pawepo mgao huo

katika soko.

Ghafla mlango ukafunguliwa na Craig Kelly, msaidizi mtendaji wa Powell,

aliingia haraka akiwa na ujumbe uliokuwa umeandikwa katika kipande cha

karatasi kilichokuwa kimechanwa kutoka katika kitabu cha kumbukumbu .Ndege

mbili zimejibamiza katika kituo cha Biashara cha kimataifa .

Ndege mbili, si tukio la ajali, Powell alitambua .ujumbe wa pili ulisema kwamba

ndege hizo zilikuwa ni za injini ya “jet” .Powell akafikiri, nilazima niende nyumbani.

Hata kama kimetokea nini, hali ilikuwa ni mbaya mno kwake kuendelea kukaa katika

mkutano wa mawaziri wa mamboya nje mjini Peru. “Hebu tayarisha ndege,

alimwambia Kelly, Nenda kawaambie tunasubiri”.

Ingechukua kiasi cha saa moja kuitayarisha ndege, hivyo Powell aliueleza mkutano

huo. Mawaziri wengine walitoa hotuba za kumpa pole.Powell alizungumza kwa

ufupi, akiwashukuru wajumbe wa mkutano huo kwa pole zao na kuahidi kwamba

Marekani inachukua hatua mara moja “Mkasa mkubwa sana umeikumba nchi

yangu,” alisema “Lakini….lazima mfahamu kwamba Amerika itapambana na

wakosaji watafikishwa mbele ya haki. Mfahamu kwamba pamoja na siku hii kuwa

mbaya kwetu, nilazima tutashinda kwani sisi ni taifa lenye nguvu na linalo jiamini

duniani’ Wajumbe wengine walisimama nakupiga makofi.

Mara tu baada ya ndege kuondoka Powell alifahamu kwamba asingezungumza na

mtu yeyote kwavile vyombo vyake vya mawasiliano vilikuwa vimeunganishwa na

mfumo wa mawasiliano nchini Marekani ambao ulikuwa umejaa habari mbalimbali

za ma wasiliano. Bila yasimu au barua pepe, alikuwa ni sawa na mtu ambaye hakuwa

na nchi. Baada ya dakika kadhaa alikwenda mbele ya ndege kupiga mawasiliano ya

radio. Hiyo ilimaanisha mawasiliano hayo hayakuwa na usalama. Alimpata Richard

L Armitage, naibu waziri wa mambo ya nje na rafiki yake mkubwa, walizungumza

mara kadha, lakini mazungumzo ya maana hayakuwezekana.

Armitage ambaye alihitimu chuo cha jeshi la maji mwaka 1967 alikuwa

ametumikia jeshi mara nne nchini Vietnam na baadaye akawa Naibu waziri wa

ulinzi katika utawala wa Reagan. Alikuwa ni mtu mwenye kupenda kusema

ukweli mwenye tambo kubwa na kifua kipana ambaye hakupenda kuzungumzia

diplomasia yenye kujificha.

28


Hata kabla hawajawa wakuu wa wizara ya mambo ya nje Powell na Armitage

walikuwa wakizungumza mara kadhaa kila siku. “Mtu huyu ninamwamini kuhusu

uhai wangu, watoto wangu, hadhi yangu, kila kitu ambacho ninacho,” alikuwa

akisema Powell kuhusiana na Armitage. Katika mambo yote ambayo Powell

alikuwa anayachukia, ni kushindwa kuchukua hatua yoyote wakati wa tatizo

ndilo jambo lililokuwa linashika nafasi ya kwanza.

Jambo kuu katika upangaji wa sera za usalama wa taifa, na timu ya Ikulu au ya

usalama wa taifa ingetaka kuweka msimamo gani katika upangaji wa sera

kulikuwa kuna utaratibu wa kipekee katika nyakati za matukio makubwa. Hali ya

migogoro ndiyo ilitoa fursa ya kuwepo hatari kubwa zaidi na fursa kubwa zaidi

za utendaji wa kazi. Ni mmarekani wa kwanza mweusi kuweka historia ya

kuhudumu katika ngazi za juu za utawala wa Marekani

Akiwa na umri wa miaka 64 katika kipindi cha mgogoro Powell alikuwa tayari

amekaa katika viti vitatu vya chumba cha dharura vya Ikulu ambavyo ni

mshauri wa kitaifa kwa Rais Regan kwa muda wa mwaka mmoja, kisha akawa

mwenyekiti wa Muungano wa Wanadhimu kwa Rais Bush wa kwanza wakati wa

vita vya Ghuba, na wakati mgogoro alikuwa ni Waziri wa mambo ya nje kwa rais

George W. Bush.

Ripoti nyingine ilifuata ikisema kwamba makao makuu ya jeshi yalikuwa

yameshambuliwa, na kulikuwa na ripoti na uvumi usioaminika kwamba kulikuwa

na ndege nyingine zikiruka kila mahali. Powell alianza kuandika notisi kwa ajili

ya matumizi yake, aliandika hivi, “Watu wangu watakuwa na majukumu gani”?

Je, ulimwengu na Marekani zitajibu vipi tukio hili? Je, hali itakuwa vipi kwa Umoja

wa Mataifa? Je, Umoja wa kujihami wa NATO? Je, nitaanzaje kuwaita watu mbali

mbali wakusanyike? Masaa saba kutowasiliana na mtu yeyote yalionekana kama

miaka isiyohesabika kwa mtu huyo ambaye angekuwa mkuu wa majeshi.

Mnamo 1995, miaka miwili Powell akiwa amestaafu kutoka jeshini, alikuwa

amefikiria kugombea urais. Aliandika kitabu cha simulizi ya maisha yake

kiitwacho My America Journey (Safari yangu ya Amerika) ambacho kilishika

nafasi ya kwanza kitaifa katika idara ya mauzo. Alikuwa amejichimbia katika

siasa za Marekani akiwa katika kiwango cha makadirio ya juu kiumaarufu

ambacho uteuzi wa chama cha Repblican ulikuwa ni wa kutaka aseme tu, na urais

alikuwa karibu sana kuufikia.

Armitage alikuwa amekipinga kitu hicho kwa nguvu “hapana haja. “Achana nacho”

alimshauri rafiki yake huyo, “sidhani kama uko tayari kwa kitu kama hicho”.

Shughuli ya kuendesha kampeni ni jambo ambalo Powell alikuwa halipendi,

“inajumuisha kila kitu kibaya unachoweza kukifikiria.” Powell alikuwa anapenda

mipango iliyotayarishwa vyema utaratibu mwema wenye kuweza kutabirika, na

kiwango cha uhakika jambo ambalo halikuwa ni sehemu ya siasa za haraka haraka

za Marekani.

29


Ilikuwa inafahamika wazi kwamba mkewe, Alma, alikuwa hapendi jaribio hilo

kugombea nafasi hizo. Kilichokuwa siri ni kwamba Alma alikuwa amemwambia

wazi kwamba iwapo angegombea urais angemwacha. “Ukigombea tu naondoka”,

alisema. Alma alikuwa anaogopa kwamba (mumewe) angeshambuliwa au

kupingwa risasi. Mumewe kugombea urais, “akishinda” na yeye kuwa mke wa rais

ni mambo ambayo mwanamke huyo alikuwa hayataki maishani mwake .

“Itabidi uyafanye mambo hayo peke yako,” alisema.

Baada ya Bush kushinda uteuzi wa kugombea urais wa chama cha Repblican

mwaka 2000, Powell alisaini makubaliano ya kutoa msaada, lakini Karl Rove

aligundua kwamba kampeni hiyo ilikuwa ifanye juu chini kumwezesha aonekane

katika tukio lolote sambamba na Bush. Karibu wafuasi wote muhimu wa

Repblican walikubaliana kwamba chaguo la kugombea urais siyo Powell. Watu

wake walitaka kufahamu ni nani mwingine ambaye angekuwepo kwenye tukio

muhimu la chama hicho, kitu gani kingesemwa, nani wangehudhuria, na lengo la

kisiasa lilikuwa nini. Yote haya yalikuwa yamepangwa kuelekeza mgawanyiko

dhidi ya Powell na si Bush.

Isitoshe ni nyenzo za kumweka Bush katika siasa za mlengo wa kati na baadaye

akawa ndiye chaguo kuu la kuwa waziri wa mambo ya nje iwapo Bush

angechaguliwa kuwa rais. Katika sura ya nchi zaidi kulikuwa na hisia kubwa kuwa

walifahamu kuwa walikuwa wanachagua timu si Bush na makamu mgombea

mwenza wake, Waziri wa ulinzi wa zamani Dick Cheney, pia Powell. Wakati

mahakama kuu ilipomtangaza Bush kuwa mshindi kwa kura 537 katika

mkanganyiko wa uchaguzi huko Florida washauri wa Powell walikuwa na imani

kwamba bosi wao alikuwa amesaidia kwa kiwango kikubwa sana katika ushindi

huo.

Katika miezi yake ya kwanza akiwa waziri wa mambo ya nje Powell alikuwa

hajaliziba pengo la uhusiano wake na Bush ambalo halikuwafanya wawe karibu

zaidi kama alivyokuwa na uhusiano wa karibu na watu wengine. Kulikuwa na

pengo kati ya watu hao wenye kuunganishwa na maelewano ya kirafiki. Bush na

Powell walikuwa wanataniana wakiwa na watu wengine lakini walifanya hivyo

mara chache sana wakiwa wawili. Rove alihisi kwamba Powell alikuwa anajidukiza

mno kisiasa na kuendesha shughuli zake nje ya cheo chake. “Lazima ufahamu siku

zote kwamba vyote hivi ni siasa na mimi ndiye nitaushinda mchezo huu wa

kisiasa,” Rove alimwambia kwa faragha Powell.

Kila mara Powell alipokuwa katika mandhari ya mbele kuhusiana na suala fulani

na kuonekana kuwa ndiyo sura ya utawala,shughuli za kisiasa na mawasiliano

huko Ikulu zilihakikisha zina mweka pembeni mwa mandhari na mwanga wa

kisiasa. Rove na Karen P. Hughes mkurugenzi wa muda mrefu wa mawasiliano

wa Bush ambaye wakati huo alikuwa ni mshauri Ikulu waliamua nani miongoni

mwa viongozi angetokea katika kipindi cha mazungumzo cha jumapili kipindi

maarufu cha televisheni kuhusu habari za jioni na asubuhi. Iwapo Ikulu

isingetoa taarifa kupendekeza kwamba akubali mwaliko wa kutokea kwenye

kipindi hicho Powell alikuwa anafahamu utaratibu mzima. Aliwaambia

watayarishaji wa kipindi hicho.

30


Mnamo Aprili 2001 wakati ndege moja ya ujasusi wa kijeshi ya Marekani aina ya

EP-3E ilipokingamwa na ndege za kivita katika pwani ya China, ikalazimishwa

na serikali ya China kutua na kukamatwa mateka wote 24 waliokuwa katika

ndege hiyo. Ikulu ilikuwa imedhamiria kuona kwamba Bush hajihusishi na suala

hilo ili rais huyo asionekane kuwa mzungumzaji katika mgogoro huo. Ilikuwa ni

kama vile hapakuwepo na mgogoro wa mateka, hii ilikuwa ni kwa kutia maanani

jinsi mgogoro wa mateka huko Iran ulivyomdhoofisha Rais Carter na jinsi

mgogoro wa mateka huko Lebanon ulivyokuja kumwathiri Rais Reagan katikati

ya miaka ya 1980.

Suala hilo lilipelekwa kwa Powell ambaye alifanikisha kuachiliwa kwa mateka hao

baada ya siku 11. Ulikuwa ni ushindi mkubwa lakini hata hivyo, Ikulu haikutaka

atokee kwenye televisheni kupata sifa alizostahili. Powell na Armitage walikuwa

wanataniana na kusema kwamba Powell alikuwa amewekwa katika kisanduku

cha barafu au kwenye friji ambapo alikuwa anatumiwa tu wakati akitakiwa.

Muda mfupi kabla ya mashambulizi ya September 11, jarida la times lilikuwa

limeandika habari moja kuu kuhusiana na Powell ikiwa na kichwa cha habari

“Umekwenda wapi Colin Powell”? Habari hiyo ilisema kwamba alikuwa

akiacha nyoyo zikiwa kwenye kina kirefu kuhusiana na sera mbali mbali na

kuonekana kuwa amemezwa na watu wenye msimamo mkali katika utawala

uliokuwa madarakani. Habari hiyo ilitoa changamoto kubwa kwa Ikulu ambako

maofisa kadhaa walikuwa wamewashikilia waandishi kuthibitisha kwamba

Powell alikuwa akifanya kazi kama kawaida wakati mwingine akiwa amekata

tama. Mara nyingi akifanya kazi kwa upweke akiwa amejikita pembeni na utawala

huo mpya.

Rove akiwa miongoni mwa maofisa hao alikuwa akisema chini chini kwamba

alikuwa anahisi Powell alikuwa ameteleza sehemu fulani na kwamba ilikuwa si

kawaida kumwona akiwa katika hali isiyoonyesha furaha akiwa na Rais.

31


TUNAINGIA VITANI.

Powell na watu wengine miongoni mwa washiriki wake walikuwa wametumia

masaa mengi na waandishi wa jarida la Times wakijaribu bila mafanikio

kuwajulisha kwamba habari waliyoandika haikuwa ya kweli. Lakini Powell na

Armitage walifahamu nguvu iliyokuwepo Washington ambako kuibuka na

kuanguka kwa umaafuru wa mtu ni jambo jepesi.

Tatizo lilikuwa kwamba msimamo huo wa habari hiyo ungeonekana kuwa

ndiyo ukweli hata kama haikuwa hivyo. Tatizo kubwa zaidi lilikuwa kwamba

habari hiyo kwa sehemu fulani ilikuwa ni kweli. Powell alikuwa haanzishi sera

mpya ya nchi za nje alikuwa akipangiwa majukumu ya kufanya na alikuwa

akikabili migogoro midogo mmoja bada ya mwingine. Lakini kama alivyowahi

kusema mara moja katika faragha, “ili kuweza kuendelea bila matatizo katika

ngazi za juu lazima uwe mjanja katika mchezo wako.”

Alipokuwa mwenyekiti wa jopo la Wakuu katika jeshi aliwahi kuandika baadhi

ya misemo aliyokuwa anaipenda zaidi na kuipenyeza chini ya kioo kilichokuwa

juu ya deski lake katika makao makuu ya Wizara ya Ulinzi. Moja ya misemo hiyo

ilikuwa “kamwe usiwaruhusu wakwambie kwamba unatapa tapa”.

Rais Bush alikuwa akiwahutubia wanafunzi katika shule ya Emma E. Booker

Elementary School huko Sarasota Florida wakati Rove alipomjulisha kwamba

ndege moja ilikuwa imeubamiza Mnara wa Kaskazini wa kituo cha biashara cha

kimataifa mwanzoni ilionekana kuwa tukio hilo lilikuwa ajali au labda kosa la

rubani ambaye huenda alikuwa na mshitulo wa moyo, Bush alifikiri.

Alikuwa amekaa kwenye stulu darasani akiwa amevaa suti yenye rangi nyeusi

shati la bluu na tai nyekundu, Ubao mdogo wa ukutani uliokuwa nyuma yake

ulikuwa na maandishi yasemayo “ Kusoma kunaifanya nchi istawi”.!

Andrew H. Card Jr mnadhimu wa Bush na msaidizi wa zamani wa Reagan na Bush

mkubwa aliingia na kumnong’oneza rais huyo moja kwa moja sikioni mwake

“ndege ya pili imeubamiza mnara wa pili, Marekani inashambuliwa”.

Picha ya hali iliyotokea wakati huo imebakia katika historia, mikono ya rais

huyo ilikuwa imekunjwa juu ya miguu yake wakati anageuka kusikiliza maneno

ya Card. Uso wake ukawa na sura tulivu kwa mbali japokuwa kulikuwa na

mshitukopamoja na kuchanganyikiwa.Bush anakumbuka vizuri kabisa

alivyokuwa, ‘nafikiri watu hawa wametangaza vita dhidi yetu, na nimeamua wakati

huu kwamba tunaingia vitani.” Alisema Bush.

Bush aliamua kwamba alihitaji kuwaeleza wananchi wake mambo kadhaa. Saa 3.30

asubuhi alitokea mbele ya kamera za televisheni katika kituo cha habari cha shule

hiyo ya Booker ili kutoa taarifa yenyewe. “kwa nini niliyarudia maneno hayo hayo

labda huo ulikuwa ni mwangwi wa matukio ya nyuma” rais huyu alisema

baadaye. “Sifahamu ni kwa nini nitakueleza ukweli kwamba hatukukaa kuyapanga

maneno haya. Nilisimama na kujikuta nikiyasema. “Mlichokiona ndiyo hasa mimi

mwenyewe nimeonyesha hulka yangu.”

32


Msururu wa magari ya rais huyo kwa kasi ulielekea kiwanja cha ndege cha

kimataifa cha Sarasota Bradenton. Alichepuka haraka akipanda ngazi na kuingia

katika chumba cha ofisi yake ya faragha ya ndege yake ya serikali ya Air Force

One. “hakikisheni mke wangu na mabinti zangu wanalindwa” hiyo ndiyo ilikuwa

amri yake ya kwanza kwa maofisa wa vyombo vya upelelezi. “Bwana Rais

alisema mmoja wa maofisahaokwa unyonge, “tunatakaukae haraka

iwezekanavyo.”Bush alikaa kitini na kujifunga mikanda na ndege ikaanza

kuondoka taratibu na muda si mrefu ikapaa angani kwa kasi.

Mke wa Rais huyo Laura Bush akiwa amevaa suti nyekundu na mikufu miwili ya

mapambo ya lulu shingoni mwake alikuwa katika chumba cha Caucus katika

jengo la Ofisi ya Seneti la Russe mjini Washingtoni akiwa tayari kutoa hoja

kuhusu watoto kuanza elimu mapema mbele ya kamati ya Seneta Robert M.

Kennedy mara wakapata habari kuhusu ajali hiyo na bibi Bush, Seneta Kennedy

na watu wengine wakaondoka kupitia mlango wa pembeni. Baada ya maelekezo

ya tukio hilo Bibi Bush alifanya juu chini kujituliza. Uso wake ulipauka mara

moja machozi yakimlenga na midomo yake ikitetemeka kwa woga.

Kisha makao makuu ya jeshi la Marekani yakashambuliwa, na wapelelezi na polisi

wa kamzingira. Walimweleza nia ya kumpeleka katika eneo lenye usalama. Kundi

hilo mara moja likaondoka haraka.

Saa 3.50 Bibi Bush alikuwa akisubiri watu wa kumsindikiza katika msongamano

wa magari kutoka jengo la bunge la Seneti (Capito), ilichukua dadika 45

kumfikisha kwenye makao makuu yake na alipelekwa katika chumba cha

Mikutano cha Wood. Saa 4.51 ndipo vyombo vya usalama vilipoamua Kend

kumficha katika Ofisi ya New Havana mtu mmoja aliyejuliakana kwa jina la

Turquoise ambalo lilikuwa jina la siri la Barbar Bush Bint wa rais huyo

aliyekuwa na umri wa miaka 19 akisoma huko . Twinkle jina jingine la siri la

binti mwingine pacha wa Rais Bush. Akiwa anasoma Chuo kikuu cha Texas huko

Austtin alipelekwa kufichwa katika Hotel ya Driskill dakika sita baadaye.

Ilikuwa saa 3.39 asubuhi ambapo ndege ya America Air lines Safari namba 77

aina ya Boeing 757 ilipobamizwa katika jengo la makao makuu ya jeshi la

Marekani. Dakika tano baadaye aliweza kuwasiliana kwa simu na makamu wake

wa rais Dick Cheney ambaye alikuwa amekimbizwa kutoka katika ofisi yake ya

upande wa magharibi na maofisa wa usalama na kupelekwa katika kituo cha

shughuli za Dharura cha Rais (Presidential Operations Center - POC) ambacho

ni handaki maalum la dharura lililo chini ya viwanja vya Ikulu.

33
 
Mkuu hebu tudokeze hivi una mawasiliano na Ben saanane?
 
LAZIMA TUWAOKOE WATU WETU,

“Uko sahihi kabisa” Tenet hatimaye alimwambia Black nafikiri sheria zote

zimebadilika asubuhi hii. Maelfu ya watu walikuwa tayari wamekufa katika jiji la

New York na makao maku ya jeshi (Pentagon). Black aliona kulikuwa kuna

badiliko muhimu. Watu, akiwemo mkurugenzi wake, walikuwa wakipata wimbi

la busara mbele ya macho yake katika muda mfupi sana wakijitoa katika kanuni

za urasimu na kukubali matukio yaliyokuwa yamejaa hatari, hata kifo. Black

hakushangaa sana na shambulio hilo lakini alishituliwa na kiwango cha mauaji

hayo.

Katika nafasi yake ya miaka mitatu akiwa mkuu wa idara ya kupiga vita ugaidi

alikuwa amefikia imani kwamba iwapo mkuu wa CTC hakuwa mwenye msimamo

mkali zaidi ya wakuu wake bali kazi hiyo ilikuwa haimfai. Alikuwa ameendesha

harakati dhidi ya Al Qaeda alipokuwa mkuu wa kituo mjini Khartoum Sudan,

alikuwa na lengo la shambulio la kushitukiza na jaribio la kumuua la mwaka

1994.Alikuwa amepanga mipango kadhaa ya siri na ya nguvu na ya mauaji ili

kumpata Bin Laden, lakini ilikuwa imekataliwa. Alifikiri na kuona kwamba

kutokana na mazingira, hali hiyo ilikuwa ni lazima iwe hivyo. Hivi sasa yote hayo

yaliku wa yamebadilika. Tenet alitoa amri ya watu wote kuondoka katika jengo

hilo,isipokuwa wale tu waliokuwa katika idara ya GRC.

Kwenye saa 3.50 asubuhi, Tenet alikuwa katika ofisi yake iliyokuwa katika

ghorofa ya saba. ndege mbili za abiria tayari zilikuwa zimebamizwa kwenye

minara yote miwili ya jengo la kituo cha Biashara cha kimataifa (World Trade

Center) na ya tatu ikabamizwa kwenye makao makuu ya jeshi la Marekani

(Pentagon) ndege ya nne iliyokuwa imetekwa ilikuwa katika anga la jimbo la

Pennsylvania ikiwa moja kwa moja inaelekea eneo la Washington.

Ripoti mbali mbali zilikuwa zimeenea katika mizunguko ya kijasusi kwamba

malengo ya siku za baadaye yalikuwa ni pamoja na Ikuli, Bunge, Wizara ya

mambo ya nje, Makao makuu ya CIA, eneo linaloonekana vyema na kufahamika

karibu na mto Potomac lilikuwa moja wapo ya malengo dhahiri. Wachunguzi

walifahamu kwamba Ramzi Yousef gaidi wa kundi la Al Qaeda aliyeendesha

shambulio la kwanza kwenye kituo hicho mwaka 1993 alikuwa na mipango ya

kurusha ndege iliyokuwa imejaa mabomu na kuibamiza kwenye majengo ya CIA.

“Ni lazima tuwaokoe watu wetu”, Tenet aliwaambia viongozi wake wa ngazi za juu.

“Ni lazima tuwahamishe watu.” Alitaka kila mtu aondoke sehemu hiyo hata mamia

ya wafanyakazi kutoka katika kituo cha kupiga vita Ugaidi (CTC) kilichokuwa

katika sehemu ya chini ya jengo hilo ambako hapakuwa na madirisha.

Cofer Black, mkuu wa CTC, aliiona amri yake hiyo kuwa haikuwa na msingi, na

alifanya hivyo akikaribia kutingisha kichwa chake. Akiwa na umri wa miaka 52,

Black alikuwa mkongwe wa kuendesha shughuli za siri na mmoja wa wafanyakazi

hodari wa shirika hilo, Alikuwa amesaidia katika kukamatwa kwa gaidi wa

kimataifa (Carlos) the Jackal ambaye labda alikuwa ndiye gaidi mwenye sifa mbaya

zaidi duniani kabla ya Bin laden.

34


Black alikuwa na nywele ambazo zilikuwa zinazidi kupungua na alikuwa akivaa

mawani makubwa alikuwa anafanana sana na Karl Rove, mpangamikakati mkuu

wa kisiasa wa Rais Bush. Alikuwa ni mtu mashuhuri sana wakati shirika hilo

lilipokuwa na watu wenye mvuto na wale wa ajabu. Wakati karibu kila mmoja

katika CIA alimwita Black kwa jina lake hilo la kwanza, Black alikuwa na

nidhamu ya kizamani ya shuleni, ambapo alikuwa anapenda kuita “Bw.

Mkurugenzi” au “Bwana”

“Bwana,”Black alisema itabidi CTC tuwaache katika mpango huo kwa vile

tunataka watu wetu wafanye kazi kwenye kompyuta.” “Ndiyo, lakini”, Tenet

alisema “je, watu wa kituo cha kupokelea majina Duniani (Global Response Center)

Alikuwa akimaanisha watu wanane waliokuwa katika sehemu ya uchunguzi

katika ghorofa ya sita karibu sehemu ya juu ya jengo hilo, ambao walikuwasehemu

wakipokea na kufuatilia habari mpya za ujasusi kuhusu ugaidi duniani kote

“watakuwa katika mazingira ya hatari.” “Hilo ndio suala lenyewe itabidi tuwaache

waendelee kukaa sehemu hiyo “Sawa, lakini ni lazima tuwaondoe watu haohiyo.”azima

kutoka sehemu hiyo ,” Tenet alisisitiza .“Hapana, bwana ni lazima tuwaache pale

kwani wana kazi muhimu ya kufanya katika mgogoro kama huu. Ndio maana

tuna kituo cha GRC.” “Wanaweza kufa.” “Mheshimiwa kama ni hivyo basi

lazima wafe.”Tenet alikaa kimya.

Mkurugenzi huyo wa CIA alikuwa ni kama baba mlinzi wa maelfu ya watu

waliokuwa wakifanya kazi hapo. Katika imani ya watu wengine kwa watu wengi

mjini Washington, CIA ilikuwa taasisi iliyomegeka na isiyokuwa ya lazima kwana

maneno ya wazi zaidi ilikuwa ni chombo ambacho kilikuwa kinakaribia kutoweka.

35


BUSH ALIZUNGUMZA KWA KUBABAIKA

“Tuko vitani,” Bush alisema na kumwambia Cheney kuueleza uongozi wa Baraza la

Congress maelezo mafupi. Rais huyo alikata simu aliwageukia baadhi ya maofisa

wake katika ndege hiyo ambaowalikuwa wamemsikia akizungumza na Cheney.

“Vijana hiyo ndiyo kazi inayotupatia mkate”, Inatubidi tulishighulikie jambo hili

na tukiwapata walofanya hivi, hawatanipenda kabisa nikiwa Rais.

Lazima apatikane mtu atakayejuta kwa kufanya hivi.” Muda mfupi Cheney alipiga

simu tena kwa Rais huyo akimtaka aidhinishe ndege za Marekani kuziangusha

ndege zozote zaidi za abiria ambazo zilikuwa mikononi mwa watekaji nyara

ilikuwa ni silaha. Ungekuwa ni uamuzi muhimu lakini Cheney ambaye kwa

kawaida huwa mwangalifu, alisisitiza kwamba kuwaidhinisha marubani kuzipiga

ndege za abiria hata kama zingekuwa zimejaa raia, ilikuwa ndiyo hatua pekee ya

kufanya. “sawa” Bush alisena na akatoa idhini hiyo.

Saa 4.30 asubuhi Cheney alimpigia tena simu Bush katika ndege yake ambayo

ilikuwa njiani kwenda Washington. Ikulu ilikuwa imepata tishio likisema

kwamba malaika (Angel) ndiye atakayekufuata kwa vile neno Angel ilikuwa jina

la siri la ndege ya rais, hilo lingemaanisha kwamba magaidi hao walikuwa

wanafahamu habari za ndani za serikali “lazima tumpate aliyefanya hivi” Bush

alimwambia Cheney na watatutambua. Card aliripoti kwamba bibi Laura Bush

alikuwa mahali pa usalama na maofisa wa usalama walisema kwamba mabinti zake

walikuwa wamehamishiwa katika maeneo ya usalama zaidi.

Dakika chache baadaye Cheney alipiga simu tena akimtaka rais huyo asirejee

Washington. Habari mbalimbali za kijasusi na taarifa za aina zote zilikuwa zinaingia

kwa wingi. Kutokana na kilichokuwa kimetokea, yaani utekaji wa ndege nne,

haikuwa vyema kurejea Washington Cheney alifikiria uwezekano wa magaidi hao

kujaribu kuikata kichwa serikali kwa kuwaua viongozi wake. Alisema walikuwa

na wajibu wa kuilinda serikali na viongozi wake.Bush alikumbuka baadaye na

kusema, “ alikuwa ndiye mtu aliyeniambia kwenye simu, usirejee Washington”

Rais huyo alikubali na kuelekea kwenye kituo cha jeshi la Anga cha Barksale huko

Louisiana. Muda mfupi baadaye wale waliokuwa kwenye ndege hiyo walihisi

jinsi ilivyopinda ghafla kushoto na kuelekea magharibi.

Saa 4:45 Bush alizungumza na mkewe. Ulikuwa ni wakati wa matatizo na

mikanganyiko ambavyo vilikuwa vimejionyesha katika hati mbali mbali za

kiserikali siku hiyo, nyingine zikiwa za wazi na nyingine zikiwa za siri. Hati mbali

mbali zilikuwa zinasema Bush alikuwa amewasili Luoisiana kwenye saa 5:48

asubuhi 5:57 asubuhi,6:05 mchana na 6:15 mchana ambacho ni kipindi

kinachojumuisha dakika 28 Kunako majira ya mchana ndege hiyo ya rais ilitua

huko Barksale huko kukiwa na ulinzi mkali. Saa 6:36 kamili, Bush alitoa taarifa

nyingine mbele ya waandishi wa habari wa televisheni.

Ilikuwa ni zaidi ya masaa matatu tangu rais huyo au kiongozi mwingine wa ngazi

za juu kuzungumza mbele ya watu. Macho ya rais huyo yalikuwa yamebadilika na

kuwa mekundu wakati anaingia sehemu hiyo alionekana kuwa amechanganyikiwa.

Alizungumza kwa vituo na maneno mengine alikuwa anayatamka vibaya wakati

36


akisoma taarifa yake. Alionekana kupata nguvu mwishoni mwa taarifa yake hiyo

yenye maneno 219 na akaahidi kuchukuwa hatua thabiti, “lakini ni lazima

mfahamu wazi kwamba tutaushinda mtihani huu.”alisema.

Alimwambia Card , “nataka kurejea nyumbani haraka. Sitaki kuona kwamba mtu

aliyefanya kitu hiki ananilazimisha nisirejee Washington.” Lakini maofisa wa

usalama walisema kwamba hali ilikuwa ya mashaka mjini Washington, na Cheney

alisema kwamba hali ilikuwa bado haijawa ya usalama. Jambo sahihi ni kusubiri

kwanza mambo yatulie,” Card alisema. Bush alikubali shingo upande na kupanda

tena ndege yake ambayo muda mfupi baada ya saa 7:30 ilikuwa katika anga

ikielikea magharibi wakati huo ikiwa inaelekea katika kituo cha jeshi la anga cha

Offutt huko Nebraska.

Kituo cha Offut ndicho kituo cha uongozi mkuu wa mikakati ya kijeshi ambacho

husimamia silaha za nyuklia za Marekani ambapo kituo kina vyombo vya kutoa

ulinzi kwa rais. Huko angeweza pia kukutana na Baraza lake la usalama wa taifa

kwa kutumia mawasiliano ya njia ya video. Akiwa katika ndege hiyo Bush aliweza

kuwasiliana kwa simu na waziri wake wa ulinzi Donald H. Rumsfeld. “Lo,!

ilikuwa ni ndege ya abiria ya kimarekani ambayo ilijibamiza Pentagon rais huyo

alisema kwa mshangao “Ni siku ya janga la kitaifa na itabidi tusafishe vurugu yote

hiyo na mpira utakuwa katika eneo lako na eneo la Dick Myers, Jenerali Richard

B. Myers wa jeshi la Anga mtu mrefu na mtaratibu ambaye siku mbili ambazo

zinge fuata angeukwaa unaibu wenyekiti, cheo cha juu zaidi katika jeshi la

Marekani.

37


NYOTA YA RUMSFELD

Rumsfeld mtu mwenye umbo dogo na uso wa kijana, rubani wa zamani wa jeshi la

maji ambaye hakuonekana umri wake wa miaka 69 kuwa mkubwa katika kipindi

cha mgogoro, alikuwa anasubiri amri kutoka kwa Rais huyo kwaajili ya

majukumu. Mwanzoni mwa mwaka wakati Rumsfeld alikuwa katika majadiliano

kuhusu kuwa waziri wa ulinzi wa Bush alifanya mazungumzo na rais mteule

huyo, alimwambia Bush kwamba, wakati kwa miaka minane ya Clinton muundo

wa asili uliendelea kuwa ni wa kutumia tahadhari na usalama. Na chaguo la

silaha kwa upande wa Clinton lilikuwa ni kombora lenye kuongozwa kwenye

lengo.

Rumsfeld alimweleza wazi Bush kwamba iwapo muda ungefika kama ilivyokuja

kutokea ukafika kweli kwamba Marekani inakabiliwa na tishio yeye akiwa

waziri wa ulinzi angemshauri rais kutumia jeshi. Bush alikuwa amejibu wazi wazi

makadirio ya Rumsfeld kwamba hivyo ndivyo hasa alivyokuwa anataka. Rumsfeld

aliamini kwamba walikuwa na msimamo wa wazi na wa pamoja. Rumsfeld alikuwa

mmoja wa nyota zinazo ng’ara zaidi ndani ya chama cha Repblican, mnamo miaka

ya 1960 na 1970 akiwa na sifa kama za John F. Kennedy mwenye sura nzuri

mkakamavu, msomi, mwenye busara, mcheshi na mwenye tabasamu la kudumu.

Watu wengi katika chama hicho akiwemo Rumsfeld mwenyewe walikuwa

wanafikiri kwamba njia yake ilikuwa inamwelekeza kwenye urais .Lakini kamwe

hakuweza kupata sifa ua umaarufu au sura ya kuwa na msimamo wa ukorofi

dhidi ya watu waliokuwa chini yake kikazi. Isitoshe alijikuta akiwa adui wa

mmoja wa nyota wa chama hicho aliyekuwa akiibuka, yaani George W. Bush

ambaye alikuja kuufikia urais.

Kuibuka kwa Rumsfeld hadi kufika katika ngazi za madaraka ya ndani ni habari

inayotokana na mapito magumu, juhudi binasfsi na majungu. Na habari mnamo

1962 akiwa na umri wa miaka 30 zinasema, Rumsfeld alichaguliwa katika vipindi

vinne katika baraza la Congress akiwa mwakilishi wa vitongoji vya ufukwe wa

kaskazini wa Chicogo ambako alikuwa amekulia, Alijiuzulu kutoka Congress

mwaka 1969 na kuwa mkurugenzi wa Ofisi ya Fursa za kiuchumi taasisi yenye

kupiga vita umasikini ambayo ilikuwa ni cheo cha uwaziri katika utawala wa

Nixon cheo ambacho ni maarufu na chenye kuonekana sana.

Mnamo 1973-74 alikuwa Brussels akiwa balozi wa Marekani katika Umoja wa

kujihami wa nchi za Magharibi (NATO) na hivyo kuweza kukwepa kashfa ya

Watergate. Kwa mujibu wa kitabu cha simulizi ya maisha ya Nixon, mnamo Julai

1974, “Donard Rumsfeld alipiga simu kutoka Brussels akitaka kujiuzulu akiwa

balozi wa NATO na arejee kusaidia kazi dhidi ya kufunguliwa mashitaka kwa

washirika wake wa zamani. Nixon alijiuzulu mwezi uliofuata na Rumsfeld

aliombwa kuwa mwenyekiti wa timu ya kusimamia kipindi cha mpito kabla ya

mshirika wake wa zamani Gerad Ford kushika nafasi hiyo. Ford alimwomba

Rumsfeld kuwa mnadhimu wa Ikulu lakini Rumsfeld alitaka kubakia NATO.

Rumsfeld alikubali wakati Ford alipoahidi kuzipanga upya safu za wafanyakazi

na kumpa Rumsfeld madaraka kamili.

38


Baada ya mwaka mmoja akiwa Ikulu, Ford alimwambia kwamba alikuwa na

mpango wa kumwondoa waziri wa ulinzi, James Schlesinger hivyo Rumsfeld

angehamia katika wizara ya ulinzi na Mkurugenzi wa CIA William Colby nafasi

yake ilikuwa ichukuliwe na George Bush mkubwa ambaye wakati huo alikuwa

mwakilishi wa Marekani nchini China. Katika faragha, Rumsfeld alikiita cheo

hicho cha China kuwa ni kazi ya ovyo na isiyokuwa na uhusiano wowote na siasa

mbele ya nyuso za wamarekani,

Alikuwa anapinga majukumu hayo mapya kwa Bush na yeye mwenyewe,

alimwambia Ford kwamba, kuwaweka pembeni watu hao kungesaidia katika

kuwatumia wakati wa kampeni ya kugombea urais ikifika. Alisema kwamba

wao walikuwa ni watu wawili pekee ambao wangetoa hotuba thabiti za kisiasa

katika uchaguzi ambao ungefuatia katika mwaka wa uchaguzi wa 1976. Lakini

Rumsfeld alikubali na kuchukua wizara ya Afya.

Bush mkubwa alikuwa anaamini kwamba Rumsfeld alikuwa anamwondoa kwa siri

kutoka katika CIA ilikummaliza kisiasa. Wakati huo ilionekana kwamba mkuu wa

ujasusi na mwenye kupanga njama chafu nchi za nje asingeweza kuwa rais. Rais Ford

wakati huo alimpandisha cheo naibu wa Rumsfeld Bw. Dick Cheney kuwa mnadhimu

wa Ikulu. Wakati huo pakiwa na manung’uniko kuhusu kuingiza siasa katika CIA,

baraza la Seneti lilikuwa linakataa kumthibitisha Bush mkubwa kuwa mkurugenzi

hadi hapo Ford aahidi kutomchagua kuwa makamu mgombea mwenza wake

katika uchaguzi ambao ungefuata, Rumsfeld aliwambia Ford na Cheney kwamba

rais asikubali shinikizo la Seneti. Hatimaye Ford na Bush walipata ahadi hiyo

kwa Seneti, Rumsfeld alimlaumu Cheney kwa sehemu fulani akimwambia kwa

maneno mengi kwamba Umevuruga mambo katika jambo ulilofanya

Mnamo katikati ya mwaka uliofuata 1976, paliibuka aina ya upinzani kati ya waziri

wa Ulinzi Bush mkubwa na Rumsfeld,Rumsfeld alikuwa amemwomba Bush

kuwa mtu mwepesi mwenye kupendelea urafiki na uhusiano na watu wengi katika

maoni yake, Bush mkubwa alikuwa anaepuka migongano isiyokuwa yalazima katika

maeneo ya Ikulu.

39


MAJENERALI WAFOKEWA

Hoja za Rumsfeld zilizofuata zilikuwa za ajabu, kila mara alikuwa akinukuu kitabu

cha Pearl Habour Warning and Decision kilichoandikwa na Robert Wohlstetter.

Alikuwa akiweka msisitizo katika utangulizi wa kitabu hicho ulioandikwa na

Thomas Schelling ambaye alikuwa akitoa hoja kwamba tukio la Pearl Harbour

lilikuwa ni kosa la kawaida ambalo linaweza kufanywa na serikali. Katika mipango

yetu kuna tabia ya kuchanganya mambo mageni na yale ambayo hayawezekani,

hatari yenyewe imo katika mapungufu ya matarajio, chuki za kawaida pamoja na

hatari kadhaa ambazo huwa za kawaida.

Mipango ya Rumsfeld katika kuleta mabadiliko ilikabiliwa na upinzani kadhaa

miongoni mwa safu za askari. Ofisa mmoja mwenye cheo cha nyota nne ambaye

alikuwa akifanya naye kazi alimwelekeza Rumsfeld kama jamaa mmoja mjanja

ambaye huonyesha sura isiyokuwa yake. Mwingine alimwelezea kwamba iwapo

mtu atapingana na Rumsfeld basi ajue hali hiyo ni ya hatari, ofisa huyo alisema.

Nilikuwa napanda kwenda katika ofisi ya Rumsfeld katika ghorofa ya tatu na

ikitokea tulikuwa hatukubali nilimweleza wazi kwamba nilikuwa sikubaliani naye

kuna nyakati alikuwa anafurahia hali hiyo na kuna nyakati alikuwa hafurahii hali

hiyo. Kuna nyakati Rumsfeld alikuwa anawafokea majenerali ofisini mwake

akiwaambia njoni mtoe maelezo ya mambo ambayo mnayafahamu. Wakati

mnazungumza matatizo yalikuwa yanawapata maofisa ambao walikuwa wanatoa

maelezo yasiyokuwa na ufumbuzi thabiti kwa Rumsfeld kwani alitaka kujua

walivyofikia maamuzi na sababu kamili za kufanya hivyo. (Kwamujibu wa Colonel

G. Dster)

Hali hii iliwachanganya maofisa wa ngazi za juu Na Rumsfeld alikuwa akiwakabili

na maswali magumu baadhi ya maswali hayo yalikuwa ni: Ni nini unafahamu

kuhusiana na suala hilo?, Unafikiri ninapaswa kukuuliza nini?, Hiyo ndiyo njia

pekee ambayo nitaielewa hali halisi. Alikuwa anasema na kuongeza kwamba na

hakika hiyo ndiyo njia pekee ambayo na wewe utajifunza mambo! Alionekana

kujiamini mno na kutowaamini watu waliokuwa chini yake jeshini akiwa anafanya

kazi na kikundi chenye kuwasiliana kwa karibu. Kikundi ambacho washiriki wake

wengi wao walikuwa ni raia. Kilikuwa ni kama kioja kwa watu wengine katika

jengo hilo, jopo la pamoja la wanadhimu na wakuu wa jeshi la kawaida, jeshi la

majini la anga na askari wa miavuli. Rumsfeld hakupenda kuchanganya mambo.

Hakutaka kufanya mambo yasiyotimia alikuwa kila mara anaipanga upya mipango

mbali mbali na kuifanyia marekebisho alikuwa anachukia lugha za kijinga

Neno “Combone” lilikuwa daima mdomoni mwa Rumsfeld kila alipokuwa akitaka

kupata habari au kufanya jambo fulani alimtumia Steve Cambone mwenye urefu

na mwenye utaalamu wa hali ya juu katika mambo ya ulinzi aliyewahi kufanya

kazi kwenye tume za ulinzi katika anga za juu za makombora, tume ambayo

Rumsfeld alikuwa amewahi kuiongoza Alikuwa ni raia msaidizi maalum kwa

waziri huyo na alikuwa kielelezo kikubwa cha uhusiano kati ya Rumsfeld na

wafanyakazi wenzake katika wizara ya ulinzi. Combone alikuwa ndiye chombo

alichokitumia Rumsfeld katika kuwafikia maofisa wa ngazi za juu jeshini.

40


Jenerali Henry B. Hugh Shelton, mwenyekiti wa jopo la wanadhimu tangu 1997

hakupendelea sana uongozi mpya wa kiraia ambapo alikuwa akiwajulisha wenzake

migongano na Rumsfeld. Katika tukio moja Rumsfeld alipendekeza kwamba

Shelton alilazimika kutoa ushauri wake wa kijeshi kwa rais kupitia kwake. Shelton

alilazimika kusema kwamba sheria imemfanya kuwa mshauri mkuu wa mambo

ya kijeshi kwa rais na aliamini kwamba ushauri wake ni lazima utolewe kwa rais

moja kwa moja.

Pamoja na mikwaruzo aliyokuwanayo Rumsfeld na maofisa wengine bado

waliheshimu kwa akili katika utaalam wake. Jenerali mmoja mwandamizi aliwahi

kusema “Namheshimu sana kwa umahiri kwamba nimependa unyonge wake ni

kutaka kila kitu akifanye”

Akiwa ameyafahamu mashambulizi dhidi ya kituo cha kimataifa cha biashara,

Rumsfeldalikuwaakishughulikiamamboyakeyakilasiku

habari za kijasusi ofisini mwake zilisema ndege ya tatu iliyokuwa imetekwa

ilijibamiza kwenye eneo la magharibi la jengo la makao makuu ya wizara ya ulinzi

alihisi kuchanganyikiwa akakimbia kwenda dirishani lakini mahali alipokuwa

hakuweza kuelewa hasa kimetokea nini. Alitoka nje na kufuata eneo lililokuwa

na moshi uliokuwa ukisambaa angani kutoka mahali ndege hiyo ilipojibamiza

akaanza kushiriki katika kazi ya uokoaji kabla ya ofisa mmoja wa usalama

alipomwambia aondoke eneo hilo.

“Nakwenda ndani” Rumsfeld alisema na haraka akaenda katika kituo cha taifa

cha mipango ya kijeshi ambacho ni chumba kimoja kikubwa chenye wafanyakazi

wengi. Katika jengo hilo chumba kilikuwa kimejaa moshi hivyo yeye na wenzake

walikwenda katika chumba maalum cha mawasiliano kilichokuwa kinaitwa “

Cables” ambapo hewa ilikuwa nzuri kidogo.

Jenerali Myers alimtaka Rumsfeled aondoke moshi unazidi kuzagaa kila mahali,

alisema kuna watu wengi wanaohangaika kutoa misaada huko hali ni mbaya zaidi

kuliko hapa, wengine wasingeweza kuondoka kama Rumsfeld alikuwa bado

yupo hapo.

“Mnaonaje tukiondoka hapa?” Sawa Rumsfeld alisema, lakini akaendelea kufanya

kazi. Jeshi ambalo lilionekana kuwa na mipango mbali mbali isiyotegemewa ilikuwa

Afghanistan kituo cha Bin laden na mahali penye kutayarishwa mipango yake.

Hapakuwa na hati yoyote ambayo ingeweza kusomwa angalau kupata picha yoyote

kuhusiana na tukio hilo. Jambo hili halikuwa la kushangaza kwa waziri huyo wa

ulinzi. Alimgeukia Myers na kusema, “kila nilipotaka kuona mipango kadhaa

nimekuwa sifurahi yale niliyokuwa nayaona ni wazi mipango hiyo ni ya zamani na

imekuwepo katika makabati ya hati kwa muda mrefu mno, Sijaifurahia hali hiyo

bado tuna mambo mengi ya kufanya inabidi kulifahamu hilo”, “Nafahamu, bwana”

Myers akajibu.

41




NDEGE ZOTE HAZIKURUHUSIWA KURUKA

Hatimaye Rumsfeld aliondoka katika chumba cha mipango ya vita akaenda ofisini

kwake na kuanza kulifanyia kazi tatizo hilo. “Huu ndiyo wakati wa kuchambua hali

halisi” aliwaambia wasaidizi wake wa ngazi za juu akiwa ni Combone msaidizi

wake wakijeshi na mshauri wake. “Rais atarejea mjini” alisema na ninataka

kujitayarisha kuzungumza naye wakati akiwasili. Ni mambo gani ambayo rais

anataka kuyafikiria? Rumsfeld aliuliza Ni nini rais anahitaji kuwaeleza raia? Alianza

kuandika mambo mbali mbali. Alitaka mawazo kutoka kwa kila mtu na dhana fupi

fupi za matatizo mbali mbali.

Cambone alikuwa ametinga katika mawazo akiichambua hali ilivyokuwa. Victoria A

Torie naibu waziri wa ulinzi katika masuala ya Jumuiya alikuwa anapanga hati

mbali mbali kuhusu mambo ambayo ofisi yake ilikuwa inayafahamu mambo

ambayo yangeshughulikiwa mara moja na mambo ambayo yangeshughulikiwa

muda ujao. Tutalipangaje suala hili kwa rais? Rumsfeld aliuliza aliona ni jukumu

lake kufikiria hali halisi kwa niaba ya rais, ilibidi pawepo na fikra thabiti na

sahihi. Ni kwa sababu alisema mkutano kamili wa kwanza wa Baraza la Usalama

wa Taifa utakuwa ni muhimu sana katika kupanga mambo yatakavyobidi

yafanyike hati mbali mbali zilishughulikiwa.

Baada ya masaa kadhaa Rumsfeld alikuwa ameyaweka mambo yote katika

ukurasa mmoja wa karatasi ambapo kila kitu kilikuwa kimekamilika na kikiwa safi

bila ya maneno kukosewa au kutumia lugha ya ovyo yoyote ile kwa ajili ya kwenda

nayo kwenye mkutano wa rais huko Ikulu. Katika kituo cha kijeshi cha Ofutt huko

Nebraska Rais Bush aliitisha mkutano wa kwanza wa Baraza la Usalama la Taifa

kwa ajili ya mgogoro wa ugaidi saa 9.30 jioni.

Tenet alitoa ripoti akielezea karibu kwa uhakika kamili kwamba Bin Laden

alikuwa ndiye aliyepanga mashambulizi hayo orodha za abiria ziliwaonyesha

watu watatu wanaofahamika kuwa wanaharakati wa Al Qaeda ambao walikuwa

katika safari namba 77 katika ndege ya shirika la American Airlines ambayo

ilikuwa imejibamiza kwenye jengo la wizara ya Ulinzi mmoja wao alikuwa

Khalid al Midhar aliyekuwa amefahamika kwa CIA mwaka wa nyuma huko

Malaysia.Jasusi wa kulipwa wa CIA alikuwa amegundua kwenye mkutano wa

Al Qaeda uliofanyika huko Malaysia.Shirika la upelelezi la FBI lilikuwa

limejulishwa na kuorodheshwa miongoni mwa watu wa kufuatiliwa nyendo zao

lakini alijipenyeza na kuingia Marekani na kukwepa kufuatiliwa na shirika hilo.

Al Qaeda ilikuwa ni kikundi pekee cha kigaidi chenye kuweza kufanya

mashambulizi hayo makubwa na yaliyopangwa vyema, alisema habari za kijasusi

zilikuwa zimenasa idadi kadhaa ya washiriki wa Bin Laden wakipongezana baada

ya mashambulizi hayo. Habari zilizokuwa zimekusanywa hapo nyuma na sasa

zikiwa zinafanyiwa kazi zilionyesha kwambawatu kadhaawaliokuwa

wanazifahamu njama hizo sehemu mbali mbali duniani walikuwa wanategemea

tukio kubwa kutokea.

43


Hakuna aliyeelezea siku, wakati na mahali au jinsi ya kufanya shambulio hilo.

Ilionekana wazi kwamba palikuwa na aina fulani ya uzembe kwamba FBI na CIA

kweli zilikuwa zinakaribia kutoweka katika uso wa taifa la Marekani. Changamka!

Bush alimwambia Tenet alisema kwamba kwa vile mashambulizi yote

yamefanyika kabla ya saa nne asubuhi hiyo hali ilivyoonesha ni kwamba

pasingekuwepo na mashambulizi mengine siku hiyo lakini hapakuwa na njia ya

kuwa na uhakika.

Mkurugenzi wa FBI Robert S. Mueller, ambaye alikuwa ameanza kazi kwa muda

wa wiki moja tu, alisema walikuwa hawajui ni vipi wateka nyara hao walikuwa

wamezikamata ndege hizo. Kama hali ya tahadhari ndege zote katika anga la

Marekani zilikuwa zimesimamishwa kwa muda usiojulikana. Rais alisema alikuwa

anataka kuruhusu safari za ndege zianze tena. Tunataka kufahamu usalama kwenye

viwanja vya ndege kabla ya ndege kuanza kuruka tena Tenet alitahadharisha.

Lilikuwa ni pendekezo la busara lakini lilionekana kulihamishia tatizo hilo katika

uzembe wa shughuli za kijasusi ambazo zilisababisha watekaji hao kuingia na

kuishi nchini Marekani kwa miezi kadhaa kabla ya kutekeleza njama zao.

Nitatangaza hatua zaidi za usalama alisema rais, lakini tusiwe kama mateka na

akazidi kusema safari za ndege zitaanza kesho mchana. Ingekuwa siku tatu kabla

ya safari za ndege za abiria kurudia ratiba zake ambapo zilikuwa zimepunguza.

“Magaidi wanaweza kushambulia wakati wowote, Rumsfeld alisema Wizara ya

ulinzi itaanza kazi kesho”. Mkurugenzi wa makachero Brian L. Stafford alifanya

mazungumzo na rais, “msimamo wetu ni kwamba usiondoke hapo ulipo”

alisema mkurugenzi huyo hali si salama. Staford alifikiri alikuwa akitimiza

wajibu wake. Bush alifahamu kwamba alihitaji uthibitisho wa usalama kamili kwa

asilimia mia moja lakini iwapo rais angeweza kumpatia uthibitisho wa usalama

wa hali ya juu na wapo angepuuza mapendekezo yao basi hilo lisingekuwa suala

lao. “Ninarejea” Bush alisema, Stafford akashangaa. Kwenye saa 10:30 jioni rais

alimpigia mkewe simu “Nitakuona badae, nenda nyumbani nakupenda”!

Kwenye makao makuu ya CIA James L Pavitt naibu mkurugenzi wa uendeshaji

(DDO) ambaye alikuwa anasimamia shughuli za siri za shirika hilo alitaka kutuma

ujumbe wake binafsi kwa majeshi yake. Pavitt, mwenye umri wa miaka 55 alikuwa

ni mtu aliyebobea katika mambo ya ujasusi. Ujumbe wa Pavit ulipewa jina la DOSB

ukiwa ni ujumbe wa siri kwa kurugenzi zote za stesheni na vituo vya Uendeshaji

( DOSB) Marekani imeshambuliwa tena na maadui wake wakubwa katika kujitoa

mhanga ili kutekeleza nia zao za kigaidi.

Ninategemea kila kituo na kila ofisa kuzidisha mara dufu juhudi za kukusanya

habari mbalimbali kuhusiana na janga hilo Kituo cha kupambana na ugaidi ndiyo

lengo maalum katika kupatikana kwa habari kuhusiana na suala hili na

tunategemea kwamba asilimia kubwa ya habari kuhusiana na mashambulizi haya

na watu walioyafanya zitapatikana katika muda wa masaa 48 yajayo. Walilazimika

kupata habari hizo kabla mambo hayajaharibika alisema ni lazima wawe

makini na kuzilinda familia zao pia ninawaombea nyote kuungana nami katika

sala za kimya kimya kuwaombea maelfu ya watu walioangamia leo na wapenzi

wao ambao wamebakia wapweke.

44


Bush alitaka kutoa hotuba usiku huo kwa taifa katika televisheni na mwandishi

wake mkuu wa hotuba Michael Gerson alikuwa ametayarisha muswada wa hotuba

hiyo. Ilikuwa na sentensi za hiki ni kitendo cha vita haya yalionesha jinsi Bush

alivyokuwa akilieleza kwa siku nzima Baraza la Usalama la Taifa na wafanyakazi

wake. Ziondoe sentensi hizo Bush amwamuru Karen Hughes, “jukumu letu ni

kuwaliwaza wananchi”. Alikuwa anafanya hivyo kwa kuwaondolea watu wasi wasi

uliokuwa umewakumba.

“Sikutaka kuwaongezea wasi wasi wananchi wa Marekani”, Bush alisema katika

mahojiano. Baadaye alitaka kutokea kwenye televisheni na kuonyesha msimamo wa

nguvu aonyesha dhamira aliyokuwa nayo ya kuyalinganisha mambo ikiwa ni

pamoja na kuwaliwaza wananchi na kuonyesha kwamba serikali ilikuwa ikifanya

kazi na kulionyesha taifa kwamba rais wao yupo hai na imara. Hiyo ilitokana

na wasi wasi kwa vile alikuwa ameitumia karibu siku yote akifikiri kutoka Kituo

cha jeshi la Anga kimoja hadi kingine.

Hatimaye rais alirejea Ikulu saa 12:30 jioni akiwa anashughulikia muswada wa

hotuba yake katika chumba kidogo cha kusomea. Akiwa anatayarisha hotuba ya

kampeni ya urais mwaka 1999 kwenye chuo cha jeshi cha the Cidael, Gerson

alikuwa ameandika kwamba katika kukabiliana na ugaidi Marekani isingeweza

kuwa tofauti kati ya wale wanaopanga vitendo hivyo na wale wanaowadekeza au

kuwachochea magaidi, ambayo Gerson aliyarejea tena kwenye muswada huo.

“Hiyo haieleweki vizuri” Bush alilalamika kuhusu maneno hayo akipendekeza

neno liwe “kuwafadhili” hivyo katika taarifa ya mwisho ambayo baadaye ilikuja

kuitwa itikadi ya Bush.

“Hatutatofautisha kati ya wale wanaopanga vitendo hivi”, ilikuwa ni dhamira

kuu ya kuwasaka magaidi na wale wanaowafadhili badala ya kuwa na lengo tu la

kutaka kulipiza kisasi mahali penye kuhusika. Uamuzi huo ulifanywa bila ya

kuwasiliana na Cheney Powell au Rumsfeld. Mshauri wake wa usalama wa taifa

Condoleezza Rice alishangaa iwapo azimio hilo lenye sera ya kuliliwaza taifa

ambalo lilikuwa limekumbwa na janga hilo kubwa, “unaweza kuyasema sasa au

unaweza kupata fursa ya kuyasema baadaye, Rice alimshauri rais. Hivyo ndiyo

ilikuwa namna yake ya ushauri iwapo rais hakuweka shinikizo.

Lakini hatimaye Rice alikubali taarifa hiyo isomwe kama ilivyo usiku huo kwa

sababu alifikiri kwamba maneno huwa yana uzito zaidikuliko kitu chochote.

“ufanye hivyo sasa” Bush alisema. Hiyo ndio sera yake aliyokuwa anainyemelea

kwa muda hivyo aliona inafaa kuisema. Katika kitengo cha magharibi cha Ikulu

kulikuwa na mjadala iwapo rais alilazimika kutoa azimio la wazi wazi kwamba

mashambulizi hayo yalikuwa yametangaza vita.

Rais Bush alizungumza na taifa kwa dadika saba kutoka katika ukumbi wa Oval

alitangaza sera yake ya kuwasaka magaidi na wale wanaowafadhili. “Hakuna kati

yetu atakayesahau siku hii lakini bado tutaendelea kutetea uhuru na yote yaliyo

mema na haki duniani”. Baada ya hotuba hiyo Bush aliongoza mkutano wa Baraza

la Usalama la taifa ambalo ulijumisha watu wengi zaidi hivyo kwenye saa 3.30

usiku aliwakusanya katika chumba maalumu cha chini ya ardhi katika Ikulu

washauri wake karibu wote na waandamizi wa masuala ya usalama taifa walifika.

45


“Huu ni wakati wa kujilinda” alisema rais huyo, hapo hali ilionyesha kuwa

mambo yalikuwa hayajatulia na walikuwa wakikutana katika chumba hicho si

kwa vile palikuwa pazuri bali kwa vile hali ilikuwa bado ya hatari kwani bado

ilikuwa haijafahamika ni nini kilikuwa kimetokea au kingefuatia; nini na jinsi ya

kujibu matukio hayo. “Tumeamua kuwaadhibu wote magaidi na wale watu

wanaofanya ugaidi wenyewe” aliwaambia.

Rais, Rice, Hughes na waandishi wa hotuba walikuwa wameanzisha moja ya

maamuzi muhimu ya sera ya mambo ya nje ambayo haijawahi kutokea katika

miaka mingi na waziri wamambo ya nje alikuwa hajahusishwa, Powell ndiyo

kwanza alikuwa ametoka Peru. Na sasa alisema, tumeuweka wazi msimamo wetu

kwa nchi za Pakistan na Afghanistan.

46


BUSH NA MKEWE WAFICHWA

Yapata wiki moja kabla ya kuapishwa kwa Bush, Rice alihudhuria mkutano kwenye

jengo la Blair jengo lililo mkabala na Ikulu pamoja na Rais mteule Bush na

makamu wa Rais mteule Cheney, hapa kulikuwa na majadiliano kuhusu siri mbali

mbali kama ilivyoelezwa na Tenet na Pavit. Kwa muda wa masaa mawili na nusu

Tenet na Pavitt walikuwa wameelezea kwa kirefu mema, mabaya na mambo ya

kutisha kuhusu CIA kwa rais huyo mteule ambaye alikuwa amesikiliza kwa

makini.

Walimwambia kwamba Bin Laden na mtandao wake walikuwa ni tishio kubwa

ambalo la shughulikiwa mara moja. Ilikuwa ni dhahiri kwambaBin Laden

angechukua hatua nyingine dhidi ya Marekani, walisema lakini haikuwa dhahiri

ni lini wapi na vipi, Bin laden na mtandao wake walikuwa ni wajanja na

wagumu kuwanasa Rais Clinton alikuwa ameidhinisha amri tano za kipekee

zenye kuhusisha ujasusi ambapo aliidhinisha kuchukuliwa kwa hatua za kisiri

kummaliza Bin Ladeen na mtandao wake kuziharibu na kuziwahi njama zao za

kigaidi, hapakuwepo na idhini ya kumwua Bin Laden.

Tenet na Pavitt walimwelezea Bin Laden kama moa ya matishio makubwa zaidi

matatu yaliyo kuwa yanaikabili Marekani . Matishio mengine mawili yalikuwa ni

kuongezeka kwa silaha za maangamizi makubwa yaani silaha za kikemikali

kibaiolojia na za nyuklia pamoja na kuibuka kwa nguvu za China kiuchumi,

kijeshi na mambo mengine.

Mnamo Aprili kamati ya wajumbe wa Baraza la Usalama la taifa likiwa

linajumuisha wakuu wawili wa juu wa kila idara na wakala lilipendekeza kwamba

Rais Bush aanzishe sera ambayo itahusisha juhudi kubwa za kuwapatia silaha

wapiganaji wa Nothern Alliance mbao ulikuwa ni muungano hafifu wa mabwana

wa vita nchini Afghanistan ambao ulikuwa unapinga utawala wa Taliban ambao

ulikuwa unamhifadhi Bin Laden.

CIA ilikuwa na makisio kwamba majeshi ya Northern Alliance yalikuwa

yanazidiwa mara mbili na yale ya Talliban yaliyokuwa na wanajeshi wapatao 45,000

ikiwa ni pamoja na wapiganaji wa kujitolea ambapo Northen Alliance ilikuwa na

askari 20,000 tu. Mpango wa siri wa CIA wa thamani ya dola millioni kadhaa

ulikuwa mezani kutekelezwa, lakini wasi wasi kuhusiana na Northen Alliance

uliongezeka. Kwanza kundi hilo kwa kweli halikuwa na muungano kwa vile

mabwana wa vita kadhaa wa upande huo wangeweza kufanya jambo lolote,

wengine walikuwa ni wahuni tu, wavunjaji wa haki za binadamu na wauza

madawa ya kulevya. Isitoshe warusi na wairan ambao walikuwa wanawaunga

mkono Northen Alliance kwa kuwapatia fedha nyingi walikuwa na uhusano

mkubwa na baadhi ya mabwana hao wa vita.

Katika utawala wa Clinton Wizara ya mambo ya nje ilikuwa imekataa waziwazi

kuwapatia silaha jamaa hao wa Alliance kutokana na wasiwasi huo. Alikuwa ni

Richard Amrtage naibu, aliyekuwa amewasiliana na Powell ambaye alikubali

kuondoa upinzani huo wa serikali. Armitage alikuwa amewasiliana na Powell

47


ambaye aliyekubali kwamba Bin Laden alikuwa ni tishio tosha la kuhalalisha

kuwapatia silaha Northen Alliance kwa kiwango kikubwa.

Mnamo mwezi Julai kamati ya wajumbe hao ilipendekeza mpango kabambe,si wa

kuivuruga tu Al Qaeda bali kuitokomeza kabisa. Ulikuwa ni mpango wa kuanza

mashambulizi na kuuvunja nguvu utawala wa Taliban. Mnamo August wahusika

wengi wakuu walikuwa hawapo. Ilikuwa ni hadi September 4 ambapo walikubali

na kupitisha mpango ambao ungeipa CIA dola millioni 125 hadi 200 kwa mwaka

kwa ajili ya kuwapatia silaha Alliance. Rice alikuwa na waraka wa Rais wa

Usalama wa Taifa (NSPD) kwenda kwa rais tarehe 10 september. Mlango

ulikuwa umefunguliwa na walikuwa tayari kuupitia waraka huo uliokuwa na

namba 9 ikimaanisha kwamba masuala mengine manane yamepitishwa rasmi na

kukubaliwa na kusainiwa na rais kama sera rasmi kuhusiana na Al Qaeda. Swali

ambalo lingekuwepo kila mara ni iwapo wamechukua hatua za haraka kukabiliana

na tishio hilo lililodhihirishwa na CIA kama moja ya matatizo makubwa matatu

yanayoikabili nchi iwapo matukio ya septembe 11 yalikuwa yanatokana na

kushindwa kwa sera na habari za kijasusi.

Saa 5.08 usiku September 11 maofisa wa usalama walimwamsha Bush na mkewe

na mara moja wakawakimbiza kwenye handaki maalum. Ndege moja isiyojulikana

ilionekana kuelekea Ikulu Rais alikuwa amevaa bukta na fulana aina T-Shirt bibi

Bush alikuwa katika nguo zake za usiku bila ya miwani yake ya kuonea, Mbwa

wao Spot na Barney walianza kuhangaika katika njia ndefu ya chini ya ardhi

yenye kuelekea kwenye handaki maalum, walikutana na Card Rice na Stephen J.

Hadley naibu mshauri wa usalama wa taifa ambao nao walikuwa wakikimbia.

Ndege hiyo ambayo ilikuwa imekosea njia ilifahamika lakini maofisa usalama

walimtaka alale huko huko kwenye handaki Bush alikitazama kitanda kidogo

kilichokuwepo na akatangaza kwamba alikuwa anarudi kwenye makazi yake.

Rice alikuwa na maelezo ya maofisa Usalama ambayo alipewa na ofisa mmoja

alisema kwamba hawakutaka aende nyumbani usiku huo kwenye makazi yake

ya Watergate, Nafikiri ni lazima ukae hapa alisema ofisa huyo Rice alikubali

kulala kwenye handaki hilo. Hapana, rais alisema twendeni kwenye makazi yetu.

Kama alivyokuwa baba yake wakati akiwa Ikulu, rais huyo alikuwa anaweka

kumbukumbu za siku hiyo aliyaweka hayo kwa kusoma imla, “Pearl Harbour ya

karne ya 21 imetokea leo”alisema.

48


AL QAEDA NA TALLIBAN HAWATAPATA

PAKUJIFICHA

Utawala wa Talibani nchini Afghanistan ambao ni kundi la wanamgambo wa

kiislam wenye imani kali waliotwaa madaraka mwaka 1996, ulikuwa

unawafadhili magaidi wa Al Qaeda ambao kwa upande wake ulikuwa unapewa

fedha na Bin Laden, vyombo vya kijasusi katika nchi jirani ya Pakistan(ISI)

ndivyo vilivyoshiriki kwa kiwango kikubwa katika kuiunda Taliban na kuiweka

madarakani. Utawala huo wenye msimamo makini ambao uchambuzi wake

makini wa sheria za kiislamu na sheria za manyanyaso vilisababisha udhalimu

kwa wanawake, njaa iliyowakumba watu wengi na watu wapatao millioni moja

kukimbilia nchi za nje ulishutumiwa sana kimataifa kwa kuharibu sanamu kubwa

zilizojengwa karne nyingi zilizopita za wafuasi wa dini ya Buddha huko Bamian.

“Hii ni fursa kubwa” alisema Bush. Ulikuwa ni wakati wa kuimarisha uhusiano

hususani na mataifa makubwa kama vile Rusia na China. Wajumbe wa baraza la

vita na mawaziri walikuwa na maswali mengi, Rumsfeld akiongoza kwa wingi wa

maswali hapo katika karatasi yake, alikuwa na mswali ambayo alifikiri rais na

wengine wangetaka kuyazungumzia na hatimaye kuyatafutia jibu, Nani

walengwa? Tunahitaji ushahisi kiasi gani kabla ya kuanza kupambana na Al

Qaeda? Tuanze kufanya hivyo lini?

Rumsfeld alisema katika kuchukua hatua hizo mapema, wananchi wangeweza

kuziunga mkono zaidi kama pakitokea madhara ya kujumuisha pande

zisizokuwemo. Alikuwa anataka kuwa makini kwa vile jeshi halikuwa na

mipango na majeshi katika eneo la karibu na lengo lililofikiriwa alitaka kuyafanya

matumaini yasiwe makubwa sana, aliwaambia kwamba baadhi ya mashambulio

makubwa yangeweza kuchukua hadi siku 60 katika kuyatayarisha.

Hivyo wazo la kusubiri siku 60 kuanzisha jambo hilo kubwa ikiwa ni hadi

November 11 lilitawala katika chumba cha mkutano. Rumsfeld alikuwa na maswali

mengine.Powell aliwaona wajumbe katika mkutano huo kwamba walikuwa ni

wajanja wa kutoa hoja lakini wakiwa wanakwepa kuchukua misimamo. Rumsfeld

aliwataka wengine kujibu hoja zake ambapo Powell aliona mbinu hiyo aliyokuwa

anaitumia Rumsfeld ilikuwa nzuri.

Bado maswali yalikuwa mazuri na Rumsfeld aliendelea je, kuna malengo

ambayo yako nje ya mipaka? Je, ni lazima kuwashirikisha maswahiba wa Marekani

katika mashambulizi yoyote ya kijeshi?. Mwishowe waziri huyo wa ulinzi alisema

ni lazima kuweka sera ya kutangaza maazimio kuujulisha ulimwengu

tunachokifanya.

Cheney alisema kwamba, Afghanistan ingetoa changamoto ya kweli ikiwa ni nchi

ambayo iko nyuma kimaendeleo na iko umbali wa maili 7,000 kutoka Marekani

pamoja na idadi ya watu milioni 26 ni nchi ambayo ukubwa wake nisawa na

jimbo la Texas, jimbo la nyumbani kwao Bush lakini ikiwa na mabarabara

machache na miundo mbinu kidogo sana katika kutafuta malengo ya kuyapita

ingekuwa ni jambo gumu.

49


Rais alirejea suala la magaidi wa Al Qaedakwenye maficho yao nchini

Afghanistan. Tangu bin Laden alipohamia huko kutoka Saud mnamo Mei 1996

utawala wa Taliban ulikuwa umeiruhusu Al Qaeda kuanzisha makao makuu

pamoja na kambi za mafunzo nchini humo.

“Ni lazima tuhakikishe al Qaeda hawapati mahali pa kujificha”. Tenet alisema

“waambieni Taliban tumechoka nao”. Taliban na al Qaeda kilikuwa ni kitu

kimoja .

Rumsfeld alisema kwamba si lazima watumie jeshi tu, bali sheria, fedha,

diplomsia na shirika la ujasusi CIA. Tenet alisema kwamba Al Qaeda japokuwa

ilikuwa na makao makuu nchini Afghanistan, ilikuwa inaendesha shughuli zake

dunia nzima katika mabara yote. Hivyo tuna tatizo linalohusu nchi 60 alisema.

Tuanze kuzishughulikia moja baada ya nyingine rais alisema. Rumsfeld ambaye

hakutaka kushindwa katika kuelezea matatizo alisema suala lilikuwa si Bin Laden

na Al Qaeda tu, bali nchi nyingine ambazo huunga mkono ugaidi. “Ni lazima

tuzilazimishe nchi hizo kufanya chaguo, alisema Bush. Mkutano uliahirishwa Rais

huyo ambaye alikuwa hajapata mtihani wala mafunzo kuhusiana na usalama wa

taifa alikuwa aanze kuelekea katika vita bila kuwa na ramani yoyote.

Condoleezza alikwenda kwenye ofisi ya mshauri wa kitaifa iliyokuwa kwenye

kona ya Tawi la magharibu la Ikulu baada ya mkutano. Mwanamke huyo

ambaye aliwahi kuwa profesa wa sayansi ya siasa katika chuo kikuu cha Stanford

na kisha kuwa mhadhiri, alikuwa amefanya kazi katika Baraza la Usalama la

Taifa, akiwa mtaalam wa mambo ya Russia wakati wa rais Bush mkubwa. Rice

mwenye umri wa miaka 46 katika kipindi cha mgogoro huu, huenda alikuwa ni mtu

pekee miongoni mwa watu wa ngazi za juu wa Bush katika timu ya usalama wa

taifa ambaye alikuwa ni mpweke zaidi, mama yake amekwisha fariki na baba

yake alikufa mwaka mmoja liopita .

Baada ya mashambulio asubuhi hiyo aliwapigia simu watu pekee wa familia yake

shangazi yake na mjomba wake wanaoishi Birminghan Alabama na kuwajulisha

kwamba alikuwa salama. Akiwa ameanzia katika kampeni ya urais wakati akiwa

mshauri mkuu wa sera ya nchi za nje, Rice alikuwa ameendeleza uhusiano wa

karibu sana na Bush. Akiwa mrefu mwenye tambo la kuvutia mwendo wa kuvutia

na tabasamu pana alijijenga miongoni mwa watu wa rais na mkewe na walifikia

kuwa kama familia moja.

Usiku huo alijiona kwamba alikuwa ametahayari. Alijaribu kufikiria ni mambo gani

yangefanywa siku ili yofuata. Mambo yote yalielekea kwa bin Laden na Al Qaeda –

lakini kulikuwa na tatizo jingine katika muda mfupi au baadaye pangetokea

maswali kuhusu ni nini utawala wa Bush ulikuwa unafahamu kuhusiana na Bin

Laden, ni lini ilifahamu hivyo na nini kilikuwa kimefanywa kuhusiana na jambo

hilo.

50
 
WANADHANI HATUNA MAADILI?.

Bush alikuwa na kumbukumbu mbili, kwanza hii ilikuwa vita ambayo watu wengi

wangekufa, Pili hakuwa na utaalam wa mambo ya kijeshi. Alilifahamu hilo na

alitegemea ushauri na maelezo ya Rumsfeld, Shelton, Myers na Tenet. Sasa alikuwa

ni rais anayetawala katika kipindi cha vita. Askari na wananchi duniani kote

wangeyaona mambo aliyopanga kuyafanya, nguvu na uthabiti wa maoni yake.

Dhana iliyokuwa imeenea kwamba alikuwa ni mtu mwenye moyo mwepesi

asiyefuata maelekezo, anayejikweza na hata kuwa mjinga ingekomeshwa. Alikuwa

na kazi nyingi za kufanya. Makamo wa Rais Dick Cheney, ambaye alikuwa mtu

thabiti na shupavu akiwa nyuma au pembeni mwa Rais Bush wakati wa miezi

minane ya kwanza ya utawala wake, alitegemea kuwa na jukumu kubwa katika

mgogoro huo.

Akiwa mtu mwenye tambo kubwa nywele zikianza kupungua kichwani mwake,

kichwa chake chenye kubenuka kila wakati na mwenye tabasamu la dhihaka,

Cheney alikuwa mwenye umri wa miaka 61 wakati wa masaibu hayo, mhafidhina

mwenye msimamo mkali na katika maisha yake yote alikuwa akielekeza

katika vita kama hii. Sifa zake katika fani hiyo zilikuwa za kuvutia akiwa na umri

wa miaka 34, alikuwa ni mnadhimu wa Ikulu chini ya Rais Ford, akawa mjumbe

wa Congress kutoka Wymoming kwa muda wa miaka 10, akapanda cheo na kuwa

mtu Namba 2 Bungeni akiwa kiongozi wa chama cha Republican, akawa waziri

wa ulinzi kwa Rais Bush wa kwanza wakati wa vita vya Ghuba. Cheney alikuwa

amejaribu kutaka kugombea urais mwaka 1999 lakini alighairi baada ya kugundua

matatizo yake ikiwa ni pamoja na matatizo ya kupata fedha kwa ajili ya kampeni

na uchunguzi mkubwa uliofanywa na vyombo vya habari dhidi ya wagombea

katika majira ya machipuko mwaka 2000.

Bush alikuwa amemwomba Cheney kuwa mgombea mwenza wa nafasi ya

makamu wa rais kwa kumwambia maneno kwamba “iwapo mambo yatakuwa

mema nitahitaji kupata ushauri wako, lakini kama mambo yatakwenda vibaya

tukiwa tunaugulia maumivu basi kusimamia migogoro ni sehemu muhimu sana ya

kazi hiyo”. Asubuhi ya tarehe 12 September jumatano, Cheney alikuwa kwa muda

na Bush peke yao. “Je, mtu mwingine awe mwenyekiti wa kikao cha kujadili vita

kwa niaba ya viongozi wakuu”? Alisema Cheney kwa kicheko. Jambo hilo

lingeweza kufungua maoni mengi zaidi kwa masikio na mboni za wamarekani na

dunia kwa ujumla.

“Hapana!!, Bush alisema, “nitakuwa mwenyekiti mimi mwenyewe kwenye

mikutano hiyo”. Yeye ndiye aliyekuwa mkuu wa majeshi kulingana na kazi yake,

kazi ambayo asingeweza kukabidhiwa mtu mwingine kwa muda. Pia alitaka

kueleweka ni kwamba ni yeye ndiye aliyekuwa nyuma ya dhamira hiyo

alidhamiria kuendelea kuwa mwenyekiti wa mikutano yote ya Baraza la Usalama

wa Taifa na Rice angeendelea kuwa mwenyekiti wa mikutano mingine ya

viongozi wa husika iwapo yeye (rais) angekuwa hahudhurii. Cheney ndiye

angekuwa mshauri mkuu zaidi, akiwa mtu mwenye ujuzi na msomaji mzuri wa

habari za kijasusi, angeweza kama ilivyokuwa katika siku za nyuma kuuliza

maswali muhimu sasa na kuyafanyia kazi. Akiwa hana wizara au idara kama vile,

Mambo ya nje, Ulinzi au CIA, Cheney alikuwa ni waziri asiye na wizara maalum.

51


Lilikuwa ni jukumu lenye uzito mdogo kuliko alivyotegemea, lakini yeye kama

walivyokuwa wengine alizifahamu na kupokea amri.

Rais Bush kama wajumbe wake wengi wa timu ya usalama wa taifa, aliamini kuwa

jibu la utawala wa Clinton dhidi ya Osama Bin Laden na ugaidi wa kimataifa,

hususan tangu kulipuliwa kwa balozi (za Marekani nchini Tanzania na Kenya)

mwaka 1998 lilikuwa ni dhaifu mno kiasi kwamba lilikaribisha dhamira nyingine

ya kuitwanga tena Marekani kwa ugaidi. Dhamira ya kupiga kombora lenye lengo

lililopimwa (cruise missile) katika hema la mtu fulani ni utani, Bush alisema

baadaye katika mahojiano “Nina maana kwamba watu walikiona kitendo hicho

kama unyonge wa Marekani.

“Ninaamini kuwa kunadhana kuwa watu wa nje kwamba Marekani tunapenda sana

anasa kiasi kwamba hatuna maadili na kwamba tukipigwa hatuwezi kujibu” Buash

alisema. Ilikuwa ni wazi kwamba Bin Laden alijihisi kupata nguvu na dhana hiyo

na hakuona kama kulikuwa na tishio kutoka Marekani . Hata hivyo hadi tarehe 11

September Bush alikuwa hajaiweka dhana hiyo katika vitendo na wala alikuwa

hajashinikiza lolote kuhusu suala la Bin Laden japokuwa Rice na wengine

walikuwa wanapanga mpango wa kuiangamiza Al Qaeda, hapakuwepo na mipango

yoyote iliyopendekezwa ili kutolewa kwa rais.

“Najua kulikuwa kuna mpango unapikwa, sifahamu mpango huo umefikia wapi”.

Bush alisema, alisema kwamba mpango kamili ungeletwa kwenye meza yake

September 10 “labda ulikuwa tarehe nzuri ingekuwa ajabu mpango huo kuletwa

September 10 kwani nilikuwa Florida siku hiyo ya September 10, hivyo sidhani

kama wangenifuata na kunitaarifu hayo nikiwa Florida”. Alikiri kwamba Bin Laden

hakuwa lengo lake au lengo la timu yake ya usalama wa taifa. “Alikuwa na tofauti

kubwa katika msimamo wangu baada ya September 11, Sikuwa na uhakika lakini

nilifahamu alikuwa ni tatizo, Najua ndiye mhusika au tulihisi alikuwa amehusika

kwa ulipuaji mabomu (wa nyuma) ambao uliua wamarekani), Nilikuwa niko tayari

kutazama mpango ambao ungekuwa mpango thabiti ambao ungemleta mbele ya

sheria na ningetoa amri ya kutekeleza jambo hilo, Nilisisitiza kufanya lolote katika

kumtafuta lakini sikuwa na papara hiyo, nilitaka mambo yaende taratibu”.

Bush alisema katika mahojiano kupitia kitengo maalumu cha Ikulu ambacho

hutumiwa na rais kuongea na raia yeyote kila siku.

52


BOSI WA FBI AANZA KUELEZEA UCHUNGUZI

Mkurugenzi wa FBI Mueller alinza kuelezea uchunguzi uliokuwepo ili kuwatambua

watekaji wa ndege zilizohusika, alisema ilikuwa muhimu kutovuruga ushahidi

wowote ili washiriki wote wanaokamatwa wawekwe hatiani. Mwanasheria mkuu

John D. Ashcoroft aliingilia, “Tuyaache majadiliano haya” alisema “lengo kuu la

utekelezaji wa sheria za Marekani ni kuzuia shambulizi jingine na kuwakamata

maswahiba wa magaidi kabla hawajatupiga tena”. Iwapo tunaweza kuwafikisha

mbele ya sheria basi na iwe hivyo. Rais alikuwa amemweleza wazi Ashcroft

katika mazungumzo ya hapo nyuma kwamba alitaka kuhakikisha mashambulio

kama yale yaliyofanywa dhidi ya pentagon na kituo cha biashara cha kimataifa

kamwe hayatokei tena.

Ilikuwa ni muhimu kufikiria mambo katika hali ambayo si ya kawaida. Sasa

Ashcroft alikuwa anasema, nadharia ya FBI na wizara ya Sheria lazima ibadilike

kutoka kuendesha mashitaka na kuelekezwa katika kuzuia kwa matukio yenye

kusababisha mashitaka jambo ambalo ni kubwa katika vipaumbele vyake. Baada ya

kumaliza mkutano wake na Baraza la Usalama la Taifa Bush aliendelea kukutana na

watu maarufu ambao walihusika katika baraza la vita ambapo wengi wao walikuwa

hawana manaibu na wasaidizi wao. Powell alisema wizara ya mambo ya Nje ilikuwa

tayari kutekeleza ujumbe wa rais kwamba aidha mko pamoja nasi au la kwa

Pakistan na Talban. Bush alijibu kwamba alitaka orodha ya madai yatakayofanywa

kwa Taliban. “Kumsalimisha Bin Laden hakutoshi,” alimwambia Powell, alitaka

mtandao wote wa Al Qaeda usalimishwe kwa Marekani au kufukuzwa.

Rumsfeld aliingilia, “ni muhimu sana kuelezea malengo yetu mwanzo, alisema nchi

nyingine zitatoa maelezo kamili”. Je tunaelekeza nguvu zetu kwa Bin Laden na Al

Qaeda au ugaidi kwa mapana zaidi? Rumsfeld aliuliza. Lengo ni ugaidi katika

mapana yake yote, Powell alisema, nadhani ikiwa imeelekezwa kwanza katika

mtandao ambao ulifanya vitendo hivyo itakuwa shwari tutakapotoa maelezo kamili ya

jukumu letu Cheney alisema, ikiwa ni pamoja na wale wanaounga mkono ugaidi.

Tutaanza kushughulika na nchi mbali mbali na ni rahisi kuzitambua nchi hizi

kuliko kumfikia Bin Laden.

“Tuanze na Bin Laden! Bush alisema, jambo ambalo wamarekani wanaliegemea”.

“Na iwapo tutafanikiwa tutakuwa tumetoa pigo kubwa na tunaweza kusonga mbele”.

Aliliita tishio hilo”saratani” na akaongeza kusema, “hatutaki kulielezea suala hilo

kwa mapana mno kwa ajili ya kumwelewesha mtu wa kawaida”. Bush

alimshinikiza Rumsfeld aseme ni lini jeshi linaweza kuchukua hatua mara moja?

“Kwa kweli ni hatua ndogo sana” alijibu waziri huyo. Ijapokuwa Rumsefeld

hakuingia katika maelezo yote, alikuwa na matatizo ya kubuni mipango ya kijeshi

katika meza yake. Jenerali Tommy Franks kamanda (CINC ) wa kituo kikuu cha

majeshi ya Marekani (CENTCOM) ambacho kilikuwa ni kitengo kwa ajili ya

maeneo ya Asia ya Kusini na Mashariki ya Kati alikuwa amemwambia kwamba

ingechukua miezi kadhaa kufikisha majeshi katika maeneo hayo na kuwa na

mipango iliyokamilika kwa ajili ya shambulio kubwa nchini Afghanistan.

53


“Siyo lazima miezi” Rumsfeld alisema. Alimtaka Franks kufikiria kufanya hivyo

katika muda wa siku au wiki kadhaa. Franks alitaka vitu kadhaa na mambo

mengine. Afghanistan ilikuwa iko katikati ya eneo la dunia, Al Qaeda ulikuwa

mtandao wa wapiganaji wa msituni ambapo watu wake waliishi katika mapango,

wakipanda punda na kuendesha magari makubwa na kubeba zana mbali mbali katika

kuhofia shambulio la kijeshi la Marekani, kambi zao za mafunzo zilikuwa hazina

kitu Rumsfeld alisema, alitaka zana zenye busara ikiwa ni kati ya kurusha

makombora yenye kuongozwa katika malengo yake na operesheni kubwa ya

kijeshi “Hebu tufikirie tena” Rumsfeld alisisitiza.

Bush aliwaambia washauri wake kile alichokuwa amemwambia waziri mkuu wa

Uingereza Tonny Blair asubuhi hiyo katika maongezi ya siri kwamba, kwanza

kabisa alitaka hatua za kijeshi zichukuliwe ambazo zingewaumiza magaidi badala

ya kuwafurahisha tu Wamarekani. Alifahamu haja ya kupanga na kufanya

matayarisho lakini “Nataka mambo yaanze sasa” alisema.

Bush aliamini kwamba kulikuwa na ulazima wa kulishinikiza jeshi la Marekani.

“Ni lazima wapewe changamoto ya kufikiria jinsi ya kupigana vita vya msituni

kwa kutumia mbinu za kisasa” alikumbushia. Walikuwa wametoka katika muhula

wa kupiga malengo kutoka mbali kwa kutumia makombora yenye kuelekezwa

katika malengo yake. Alifahamu kwamba hatua zake za mwanzo kuhusiana na hali

ya hewa duniani pamoja na mikakati ya kitaifa ya kujihami kwa makombora

ilikuwa imewatia wasi wasi maswahiba wa Marekani barani Ulaya.

Marafiki wa Marekani walikuwa na wasi wasi kwamba utawala huo wa Marekani

ulikuwa umeingiwa na fikra mpya za kujifanyia mambo peke yake bila

kuuhusisha ulimwengu hali ambayo taifa lenye nguvu kubwa linavyotegemewa

kufanya. Katika mahojiano Bush baadaye alielezea jinsi alivyoamini ulimwengu

ulivyomwona katika miezi ambayo ilielekea katika mashambulizi ya September 11.

Kabla ya saa 5.00 asubuhi waandishi wa habari waliruhusiwa kuingia katika chumba

cha Baraza la Mawaziri. Akiwa amevaa suti ya rangi ya bluu yenye weusi, shati la

blue lenye ung’aavu na tai yenye mistari ya bluu, Bush alikaa kitini kwake akiwa

ameegemea mbele kidogo, alitaka kuelezea kauli zake za usiku. “Mashambulizi ya

makusudi na yenye maafa ambayo yalifanywa jana dhidi ya nchi yetu yalikuwa ni

vitendo vilivyozidi ugaidi” alisema, vilikuwa ni vitendo vya vita.

Alimwelezea adui kuwa ni yule ambaye Marekani kamwe haijapata kupambana

naye adui ambaye anaendesha vitendo vyake gizani, mwenye kuvizia watu

wasiokuwa na hatia, anayeshambulia na kisha kukimbia kwenda kujificha, siku

zote kuwanasa wahusika tutaushawishi ulimwengu. Tutakuwa na subira, tutakuwa

na malengo, na tutakuwa imara katika mema na mabaya lakini mema yatashinda.

Kazi kubwa ya kulimbikiza nguvu za washiriki wa kimataifa aliachiwa Powell lakini

Bush alimpigia simu Rais wa Russia Vladimir Putin na pia akazungumza na

viongozi wa Ufaransa, Ujerumani, Canada na China.

54


“Nia yangu kwa muda wote ilikuwa ni kwamba iwapo itabidi tuchukue hatua peke

yetu tungeweza kufanya hivyo peke yetu lakini sitaki iwe hivyo” Bush

alikumbushia. Saa 5.30 asubuhi Rais alikutana na viongozi wa baraza la Congress na

kuwaambia “Ndoto ya adui yetu ilikuwa ni kwamba tusiweze kukutana katika

jengo hili wanataka kuiona Ikulu ikiwa imeangamia katika mashambulizi zaidi,

tukio hili si lakipekee alisema, Watu wanaweza kupoteza nadharia na imani kwa

serikali yao”.

Mwezi mmoja kutoka sasa wananchi wa Marekani watakuwa wakitazama maelezo ya

mpira wa miguu katika kombe la dunia lakini serikali itaendelea na vita hivyo kwa

muda usiojulinaka. Adui huyo hakuwa kundi moja tu linalojulikana alisema, bali

maono yenye kuchochea chuki,watu hao wanachukia Ukristo. Wanachukia

mafunzo ya Judanism wanachukia kila ambacho si chao. Mataifa mengine yatabidi

kuchagua. Aliongeza kusema

Kiongozi wa upande wa wawakilishi wengi seneta Thomas A. Daschle mjumbe wa

chama cha Democratic kutoka South Dakota alimtahadharisha rais kuwa makini

katika kauli zake, neno vita ni zito mno alisema. Daschle aliahidi kuunga

mkono juhudi hizo, lakini aliutaka utawala huo kuishirikisha Congress kikamilifu

katika mawasiliano yake katika mkutano wao wa kwanza wa faragha. Baada ya

Bush kutangazwa mshindi, rais huyo mteule alikuwa ameshangazwa na kauli ya

Daschle aliyoisema, “nafikiri kamwe hutanidanganya”. Ilikuwa ni kauli ambayo

iliendelea kuumiza kichwa cha rais huyo hata alipokuwa madarakani.

Karibuni mwisho wa mkutano huo Senet Robert C. Byrd mwakilishi wa West

Virginia mwenye umri wa miaka 83 akiwa kiongozi maalum katika baraza la Senet

alisema na kuelezea mawasiliano yake kumi na marais mbali mbali, alisema

kwamba Bush alikuwa amesema kwamba hakutaka tangazo la vita litolewe na

Congress kwa Lyndon Johnson katika vita vya Vietnam kupitia azimio la Ghuba

ya Tonkin mwaka 1964. Bado tuna katiba alisema akivuta nakala yake kutoka

mfukoni mwake.

Byrd anakumbuka siku ambayo yeye na mkewe walipokuwa wakila chakula jambo

hilo lilinivutia sana, Byrd alisema Seneta huyo alizungumza kuhusu athari mbaya

inayotokana na mambo ya Hollywood katika jamii, “ninakuombea kila la heri” Byrd

alisema.Licha ya mambo ya Hollywood na televisheni, kuna jeshi la watu

wanaoabudu katika maadui mema na muumba. Maneno yake ya mwisho yalileta

ukimya katika chumba hicho; “Simama kidete ulipo alisema. Nguvu kubwa zitakupa

msaada”

Alasiri hiyo Bush alikutana kwa faragha na Bernadine Healy mkuu wa chama cha

msalaba mwekundu cha Marekani ambaye alisema kwamba hapakuwa na damu

ya kutosha iwapo pangetokea shambulio jingine la kigaidi. “Endelea kukusanya

damu”, rais alisema, “unanielewa”? Alisema kwamba asingekuwa anakimbiakimbia

kujificha “Niko katika mikono ya bwana” Healy alisema. Alimwambia Bush kuwa

alikuwa ameambiwa kwamba ndege moja ya abiria iliyokuwa ikipita juu ya mto

Potomac kutoka uwanja wa ndege wa Taifa ingeweza kupindishwa njia na kufika

Ikulu mnamo sekunde 40. Bush alisema kwamba alikuwa analielewa jambo hilo.

55


Huko kwenye wizara ya mambo ya nje Richard Armitage alikuwa akizunguka huku

na kule katika chumba chake kikubwa kwenye ofisi za ghorofa ya saba mithiri ya

kiungo mkabaji wa kibongo Joseph Henry Shindika) akiwa katika himaya yake na

gozi la ng’ombe.

Rais Bush muda mfupi uliopita alikuwa amemuuliza Armitage ambaye alikuwa

anafahamika kwa kupenda kufanya mazoezi ya kubeba uzito kuwa kiasi gani

ambacho alikuwa ameweza kukimudu kubeba Armitage alimjibu “330/6”

akimaanisha paundi 330 kwa kuzinyakua na kuzitua mara sita bila kupumzika

katika kilele cha nguvu zake. Miaka iliyopita Armitage aliweza kunyakua paundi

440. “Kiwango kizuri hicho”. Rais alimjibu, “Mimi nanyanyua paundi 205/6 je,

kiwango hicho ni kizuri kwa rais yeyote”? Aliuliza kwa upole. “Ndiyo” Armitage

alimjibu akifikiria kuwa hivyo ndivyo inavyopaswa kuwa. Sasa ulikuwa ni wakati

wa mawasiliano ya kidiplomasia, Rais alikuwa ametangaza “Itikadi ya Bush” kwa

mapana yote bila ya kujumuisha hisia za wizara ya Mambo ya nje, makao makuu

ya jeshi yalikuwa bado yanaungua hivyo hapakuwepo na muda wa kuwasiliana na

idara au wizara nyingine.

56


RUMSFELD ATOA HOJA JUU YA IRAQ

Jenerali Mahmoud Ahmad mkuu wa shirika la kijasusi la Pakistan (ISI) kwa bahati

nzuri alikuwa mjini Washington alitembelea CIA ambapo alimwambia Tenet na

wasaidizi wake kwamba kiongozi wa Taliban Mullah Mohammad Omar alikuwa

ni mtu mpenda dini mwenye hisia za kupenda utu na si mtu wa vurugu bali mtu

ambaye alikuwa amevurugikiwa mambo yake kutokana na vitendo vya mabwana

wa vita wa Afghanistan.

“Acha Ahmed! Jim Pavitt alisema usiniambie, “Hivi Mullah Omar anataka jeshi

la Marekani liwatwange Taliban?, kwa nini Mullah Omar atake jambo hilo

litokee?, unaweza kwenda kumwuliza”? Alianza kwa kusema kwamba bado ilikuwa

haifahamiki ni nini Marekani ingetaka kutoka kwa Pakistan lakini maombi

yangelazimika kuwepo faragha kubwa. Pakistan inakabiliwa na chaguo la wazi

ama iwe upande wetu au laa, hili ni chaguo la rangi nyeupe na nyeusi bila kuwepo

rangi ya kijivu.

Mahmoud alisema kwamba nchi yake ilikuwa imekabiliwa naugumu katika

kuchagua mambo mbali mbali katika siku za nyuma. Lakini Pakistan haikuwa

taifa kubwa au lenye nguvu. “Pakistan ni nchi muhimu”, Armitage aliingilia.

Mahmoud alirejea katika masuala ya siku za nyuma. “Mustakabali wa siku zijazo

unaanza leo Armitage alisema fikisha ujumbe huu kwa Jenerali Musharraf rais wa

Pakistan- achague kuwa nasi au dhidi uovu”.

Saa10 jioni Baraza la Usalama wa Taifa lilikutana tena. Suala lililoendelea

kujadiliwa ni kiini hasa cha jukumu lililotakiwa kufanywa. Rumsfeld alisisitiza

katikakipengele kimoja alichokuwaanakitaka ambacho ni: Je, tuanze

mashambulizi dhidi ya ugaidi kwa upana zaidi ya kupambana na Al Qaeda?

Je,tunahitaji kuungwa mkono kwa kiwango kikubwa zaidi?. Bush alisema tena

kwamba kwa maoni yake mwanzo ulikuwa uwe dhidi ya Bin Laden. Iwapo

wangetoa pigo dhidi ya Al Qaeda kila kitu ambacho kingefuata kingekuwa rahisi

zaidi.Lakini Rumsfeld alikuwa na wasi wasi kwamba umoja ulioelekezwa

katika lengo la kuiangamiza Al- Qaeda ungeanguka mara baada ya kutekeleza

wajibu huo na kuifanya hali kuwa ngumu zaidi katika kuendelea na vita dhidi ya

ugaidi sehemu nyingine.

Powell akikubaliana na Bush alishauri kwamba ingekuwa rahisi zaidi mwanzoni

kushawishi katika lengo mahususi la kuitwanga Al Qaeda katika kufanya hivyo

wangeungwa mkono na azimio la Umoja wa Mataifa kwa kuelekeza mandhari ya

Al Qaeda. Cheney alizungumzia tena suala la ugaidi wenye kudhaminiwa na serikari

mbali mbali. “Kupambana na ugaidi ni moja kwa moja kunamaanisha kuelekeza

lengo hilo dhidi ya nchi za nje zenye kudhamini ugaidi huo, alisema katika njia

fulani nchi zenye kufanya hivyo ni malengo rahisi zaidi kupambana nazo kuliko

magaidi wenyewe ambao hawajulikani walipo”. Bush aliingiwa na wasi wasi

kuhusu kuyafanya malengo yao ya mwanzo yawe yenye kujumuisha sura nyingi

“Malengo yetu tusiyafanye yakawa hayaendi sambamba na dhamira yenyewe na

yakashindwa kuungwa mkono wa Wamarekani alisema kwamba nchi ilikuwa

imeangukiwa na janga hili kutoka katika mikono ya Al Qauda.

57


Cheney alidai kwamba ushirikiano huo lazima uwe njia ya kuangamiza ugaidi

jambo ambalo wengine walikubaliana nalo. Walikuwa wanataka kuungwa mkono na

mataifa mengine duniani lakini hawakutaka ushirika huo uwawekee vikwazo.

Jukumu lenyewe lazima lielezee ushirika huo na si vinginevyo.

Katika hali hiyo Rumsfeld alisema walikuwa na dhamira ya kuchukua hatua

thabiti na si washiriki wenye kusitasita. Powell alitoa pendekezo ambalo mjumbeowell

mmoja baadaye alilielezea kama hoja tatanishi kuhusu kujenga ushirika. Ushirika

huo lazima uwe mkubwa kiasi kinachowezekana lakini masharti ya ushirikakinachowezekana

yatategemea nchi hadi nchi . Hii ingemaanisha kama Rumsfeld alivyosema ushirika

wa mashirika.

Rumsfeld alitoa hoja kuhusu Iraq “kwa nini tusiitwange Iraq na si Al Qaeda tu”?kwa

Rumsfeld aliuliza. Alikuwa kama anamalizia hoja kwani wakati alipotoa swali hili

naibu wake Paul D. Wolfowitz alikuwa amekamia sera ambayo ingeifanya Iraq

kuwa lengo kuu katika duru la kwanza la vita dhidi ya ugaidi

Kabla ya mashambulizi, Pentagon ilikuwa ikipanga kwa miezi kadhaa mpango wa

kuitwanga Iraq kijeshi. Kila aliyekuwa kwenye meza ya majadiliano aliamini Rais

Saddam Hussein alikuwa tishio kiongozi mwenye dhamira ya kupata na labdatishio,

kutumia silaha za maangamizi. Vita yoyote ya kweli na kamili ni lazima hatimayemaangamizi.

ingeelekezwa dhidi ya Iraq, Rumsfeld alikuwa akielekeza uwezekano kwamba

wangeitumia fursa iliyosababishwa na mashambulizi hayo ya kigaidi katika

kumshambulia Saddam mara moja.

58


Powell ,baadaye alipinga kuishambulia Iraq katika wakati huo, alisema kwamba

walikuwa wanalenga dhamira yao dhidi ya Al Qaeda kwa vile watu wa

Marekani walikuwa wameelekeza kila kitu kwa Al Qaeda. Kitendo chochote

kinachohitaji kuungwa mkono tu na jumuiya ya kimataifa ni kile ambacho

wananchi wa Amerika wanataka tuchukue hatua dhidi ya Al Qaeda. Bush

alisema wazi kwamba muda wa kuliamua suala hilo ulikuwa bado ,alisisitiza tena

kwamba lengo lake kuu lilikuwa ni kutoa mpango wa kijeshi ambao ungewaumiza

kikweli kweli na kuwaangamiza magaidi.

“Sitaki vita vya kuigiza” aliwaambia. “Nataka kitu cha kweli na orodha ya wahuni

ambao watakuwa malengo yetu” “kila mtu alikuwa akilifikiria kuhusu vita vya

Ghuba, alisema jambo ambalo halikustahili kulinganishwa”. Wananchi wa

Marekani wanataka pigo kubwa alisema, Ni lazima ni wahakikishie kwamba hii ni

vita ambayo itapiganwa katika hatua nyingi. Alikuwa akimaanisha Vietnam ambako

jeshi la Marekani lilipigania uhuru wa msituni, baadaye alisema kwamba

alifahamu moja kwa moja kwamba alitakiwa kila mmoja awe na fikra zake tofauti

kuhusu jinsi ya kupigana na magaidi. Mbinu za kijeshi zilikuwa zichukue muda

kabla ya kuanza kutumika alisema, nilijihisi kubanwa nisijue la kufanya.

Badaye alasiri hiyo Pavitt alituma simu ya pili ya siri kutoka makao makuu ya CIA

kwa vituo vyote duniani ikiwa na kichwa cha habari “Hatua zinatakiwa

kuchukuliwa, Maoni yenu tafadhari”. Shirika hili lilikuwa linaendelea na jukumu

lake dunia nzima kuwapata waliofanya mashambulizi ya September 11, aliandika

Pavit. CIA pia inaandaa na kuanzisha mpango mpya na mkubwa wa siri wenye

lengo la wazi la kuwashambulia na kuwaangamiza wadhamini na waungaji

mkono wa ugaidi wa waislamu wenye msimamo mkali duniani kote.

Pavitt aliwashinikiza maofisa wake wa siri katika kurugenzi ya uendeshaji walio

mitaani kwenye kusukwa mipango yenyewe kutumia fikra zao mahiri na bora zaidi

katika kuendesha harakati kubwa za kuwasaka magaidi. Hapakuwa na vizuizi

vyovyote. “Tumieni njia zote mpya na zenye busara katika kufanikisha jukumu

hili, alisema mpango huu wa chini chini utajumuisha harakati za sura ya kijeshi,

mikakaati ya kijeshi, sura ya vita vya kisaikolojia, pamoja na ujasusisimu hiyo

ilisema. Katika maneno mengine hapakuwepo na vipingamizi vyovyote. Kurugenzi

ya uendeshaji ikaanza kazi mara moja. Saa 3.30 asubuhi Alhamisi September 13, rais

alikutana na Baraza la Usalama wa Taifa katika chumba cha Situation Room Ikulu

kilicho ghorofa moja chini ya ofisi ya mnadhimu mkuu katika kona ya kusini

magharibi mwa Tawi la magharibi. Tenet alimleta mkuu wa kupambana na ugaidi

Cofer Black ili atoe maelezo zaidi kuhusiana na mapendekezo ya CIA.

Dhana ya Tenet ilikuwa ni kukusanya nguvu kubwa zaidi za habari mbali mbali

za kijasusi za teknolojia ya hali ya juu za timu ya utaalamu wa mambo ya kijeshi na

makundi ya upinzani nchini Afghanistan ili kuendesha harakati za siri.

Vyote hivyo vingejumuishwa na nguvu za jeshi la Marekani na majeshi maalum

kuwa nguvu kubwa yenye kuleta madhara makubwa kwa lengo la kuiangamiza

mitandao yenye kujificha magaidi.

59


Tenet alisema dhana kuu ilikuwa ni kutoa fedha na kuwachochea wapiganaji wa

Northen Alleance. Wapiganajiwa Alliancewaliokuwa 20,000, walikuwa

mchanganyiko wa askari waliokuwa wanamilikiwa na makundi matano ambayo

kwa kweli yalikuwa ni makundi madogo madogo 25. Ulikuwa ni muungano wa

maslahi ambapo wakati mwingine yalikuwa yakipingana .

Mauaji siku mbili kabla ya mashambulizi ya September 11 ya kiongozi wake

mashuhuri Ahmed shd Massoud, lilikuwa pigo kubwa likiwaacha Northen

Alliance wakiwa wamevurugika zaidi. Lakini kwa kutumia CIA na mafungu

makubwa ya fedha wapiganaji wa Alliance wangeweza kurejeshwa na kuwa nguvu

kubwa ya kuendesha mapigano, Tenet alisema.

Vikundi vyenye utaalam wa mambo ya kijeshi vya shirika hilo (CIA) vilikuwa mara

nyingi vimekutana kwa siri na viongozi wa Alliance mnamo miaka minne

iliyopita. Tenet alisema angeweza kupenyeza vikundi vyenye utaalam wa mambo

ya kijeshi nchini Afghanistan kwa mabwana wa vita ikiwa ni pamoja na

wanajeshi maalum kutoka jeshi la Marekani wangekuwa macho ya ardhini kwa ajili

ya mashambulio ya jeshi la Marekani, ingeweza kuwapa Northern Alliance nguvu

ya ziada.

Cofer Black alifuatia, Black alikuwa amegundua katika mikutano hii na maofisa wa

ngazi za juu zaidi kwamba kulikuwa na mwelekeo wa kujumuisha mambo.

Hapakuwepo na kauli zilizokuwa zimelengwa moja kwa moja katika jambo fulani.

Lakini aliamini kwamba alifahamu kile walichokuwa wakikitaka. Alikuwa na uwezo

mkubwa wa kujieleza na kuelezea. “Bw. Rais, alisema tunaweza kulifanya hili,

Sina wasi wasi wowote kichwani mwangu, Tuyafanye mambo haya kama

tulivyoyapanga, tutalipanga jambo hili ili yasije kuwa mapigano yasiyokuwa ya

haki kwa jeshi la Marekani”.

Black alimkabili Bush ambaye alikuwa katika ncha ya meza. “Lakini lazima

ufahamu kwamba watu watakufa, na kitu kibaya zaidi ni kwamba,Bw. rais

wamarekani pia watakufa washirika na marafiki zangu. Hivyo ni lazima

ifahamike wazi kwamba jambo hili litakuwa ni jambo la umwagaji damu”. “Hiyo

ni vita, Bush alisema, lazima tukubali kwamba tutapoteza watu katika suala hili,

Wangapi sijui, Wanaweza kuwa wengi”. Sawa Rais, alisema “tuendelee, hiyo ni

vita, Hicho ndicho kimetuleta hapa ili kushinda.”

Black alionyesha mbwembwe za kisanii wakati akielezea athari za mipango ya

chini chini. Kila mara alikuwa akijimwaga huku na kule katika kiti chake wakati

akielezea hoja zake, akatupa makaratasi huku na kule wakati akielezea kuteremsha

majeshi nchini Afghanistan, mithiri ya mpinga mchakato wa utakatifu wa baba wa

taifa Mwalimu Julius K. Nyerere, Mch. Christopher Mtikila.

Black alitaka kujuahili lianze mara moja. Alikuwa na uhakika kwamba

lingefanikiwa, “tupe maelekezo alisema tutawapata”. Akirejea lugha ya wazi ya

Rais kuhusu kuwanasa magaidi kutoka mapangoni mwao alisema “ Tutawang’olea

mbali”.

60


Sasa alisema, lengo kuu ni kuwanasa Al Qaeda na kuwafikisha mbele ya sheria ili

haki iweze kutendeka. Hata hivyo alisikitika kugundua kwamba Al Qaeda huwa

hawawezi kusalimu amri, na kwamba hawawezi kufanya majadiliano yoyote.

Kiongozi mkuu wa Northen Allince, hayati Massoud, kuna wakati alimwambia

“tumekuwa tukipigana dhidi ya jamaa hawa kwa miaka minne na kamwe sijawahi

kumkamata hata mmoja wa washenzi hawa”. Sababu ni kwamba wakati wowote

kundi lao likizidiwa nguvu basi hushikamana pamoja na kujilipua na bomu la

mkono. “Hivyo jukumu litakuwa ni kuwaua Al Qaeda”, Black alisema.

“Tukishawamaliza watajikuta mainzi yakitembea juu ya mboni za macho yao

alisema. Hivyo ilikuwa ni sura ya kifo ambayo ilibakia katika akili za idadi

kadhaa ya wajumbe wa baraza la vita. Black alianza kufahamika miongoni mwa

Bush kama bwana mainzi juu ya mboni za macho. Black alisema pia kwamba

walilazimika si kuwatwanga Al Qaeda peke yao, bali na Taliban kwani pande zote

mbili hizo zilikuwa ni kitu kimoja . CIA ilikuwa imeshindwa kutoa mpango kwa

upana zaidi au fedha ili kuwabana Taliban na hivyo kutoa mwanya wa kuwatwanga

Al Qaeda. “Je, tunawafahamu kibinafsi kwa kiwango gani viongozi wa Alliance”?

aliuliza Bush.

Black alitoa maelezo kadhaa, nakisha akaelezea baadhi ya udhaifu uliokuwepo pia

katika kuonyesha kwamba shirika hilo halikuwa limefanya kazi kikamilifu kwani

jenerali mmoja maarufu wa Alliance Abduirrashid Dostum, alikuwa anatumiwa na

kulipwa na kila mtu ikiwa ni pamoja na Russia na Pakistan. Bush aliuliza ni

muda gani ungetumiwa katika kuwaingiza majasusi wenye kujua mbinu za kijeshi

nchini Afghanistan.

“Haraka iwezekanavo”, Black alisema lingekuwa jambo la mfululizo kiasi kwamba

kundi moja likiingia, la pili lingefuata kirahisi na kuendelea. “Itachukuwa muda

gani”? Rais aliuliza alimaanisha ushindi, Black alisema “tukishaanza mapigano,

yataendelea kwa majuma”. Hakuna mtu katika chumba hicho akiwemo Tenent

aliamini kwamba jambo hili lingewezekana. Hata hivyo majadiliano hayo yalikuwa

ni yenye kukumbukwa na yalikuwa naathari kubwa kwa rais. Kwa muda wa siku

mbili Bush alikuwa ameelezea kwa uwazi zaidi uwezekano wa dhamira yake ya

kuwasaka na kuwaangamiza magaidi waliohusika. Sasa kwa mara ya kwanza

alikuwa anaambiwa wazi kwamba kulikuwa kuna njia ya kufikia jambo hili

kwamba hakulazimika kusubiri ji la CIA litoe mpango kuhusu sula hilo.

Ari ya Black ilikuwa na athari yake, japokuwa ni wazi ilikuwa na matumaini mema,

Lingekuwa ni jambo ambalo kamwe lisingekuwa jepesi au rahisi kama ilivyokuwa

inaonekana lakini wakati huo hicho ndicho rais alitaka kukisikia, pia palionekana

kuwa na busara katika kuitumia CIA, Northern Alliance na jeshi la Marekani katika

mpango huo. Powell kwa upande wake aliona kabisa kwamba Bush alikuwa

amechoka na maneno Rais huyo alitaka kuua mtu. Ilionekana wazi kwamba

tungeweza kupigana vita tofauti na ile waliyopigana Warusi, Bush alisema

baadaye. “Kuivamia Afghanistan kwa kutumia jeshi la kawaida kama

walivyofanya Warusi na wakashindwa mnamo miaka ya 1980 hilo lisingekuwa

chaguo la jeshi la Marekani, Nilifurahishwa na jinsi CIA ilivyokuwa inalifahamu

61


eneo hilo, Tulikuwa na mali zetu mbali mbali huko kwa muda mrefu. Kazi yote

ilifanywa na kuchambuliwa ipasavyo” Cond alisema.

Muda mfupi kabla saa 5.00 asubuhi wasaidizi wa Ikulu waliwaingiza waandishi wa

habari katika ofisi ya Oval kwa ajili ya mkutano na Meya wa New York, Rudolph

W. Guiuliani na Gavana wa New York George E. Pataki. Siku ya nyuma yake

kundi la mawasiliano la Ikulu yaani Hughes na wenzake walikuwa wameamua

kuyaonyesha mazungumzo hayo moja kwa moja katika televisheni.

Walitaka rais aonekane akiwasiliana na familia ya maelfu ya watu waliokumbwa

katika janga hilo na kufa wakati minara ilipoanguka pamoja na waokoaji

waliokkuwa wakishughulika muda wote katika kuwatafuta watu walionusurika.

Kwa vile Bush hakupanga kwenda New York wiki hiyo , Mkutano huo wenye

kuonyeshwa kwenye televisheni ulionekana kuwa ni ishara bora zaidi katika

mazingira hayo. Hata hivyo alipopatikana kwenye simu, Bush aliwambia meya na

gavana huyo kwamba angekwenda New York alasiri ya siku iliyofuata, mara tu

baada ya sala kwenye kanisa la Taifa la Washington.

62


RAIS ATIRIRISHA CHOZI

Bush alionekan kutotulia akiwa na wasi wasi wakati akiongea kwenye televisheni.

“Natamani ningefanya ziara hii katika mazingira bora zaidi alisema akimalizia,

Lakini nafikiri hii itakuwa ni fursa ya sisi sote watatu kuwashukuru

kuwakumbatia na kulia na wananchi wa eneo hili lenu zuri”. Baada ya shughuli

hiyo kwisha Bush aliamua kupokea maswali kutoka kwa waandishi ambao

walikuwa wamesimama futi chache kutoka alikokuwa. “Bw. Rais! moja aliuliza,

unaweza kutueleza kuhusu aina ya sala unazofiria na wapi moyo wako uliko

wakati unawaliwaza wamarekani?. “Sasa hivi sijifikirii mwenyewe” Bush alisema

na ilionekana wazi kwamba alikuwa anahangaika kujizuia na jazba, “Ninafikiria

familia!! familia mbali mbali na watoto”. Aligeuza kichwa chake na macho yake

yakiwa yamejaa machozi

“Mimi ni mtu mwenye upendo alisema akianza kutulia, lakini kwa kiasi fulani tu

na pia mimi ni mtu fulani ambaye nina wajibu wa kufanya kazi fulani na

nimedhamiria kuifanya kazi hiyo na hiki ni kipindi cha matatizo makubwa”.

“Lakini nchi hii haiwezi kutulia hadi tumejiokoa sisi na wengine kutokana na

janga hili la kutisha ambapo limeikumba Marekani”. Akiwa bado ana machozi

machoni, Bush alimaliza kikao hicho kwa kuinamisha kidogo kichwa chake na

waandishi wa habari wakasindikizwa kutoka nje. “Marais kwa kawaida huwa

hawapendi kulia mbele ya raia wa Marekani hususani katika Ofisi ya Ovel lakini

mimi nililia” Bush alisema baadaye. Lakini aliamini hali yake ilionyesha katika njia

nyingi.

Machozi hayo aliyoyatoa hadharani labda yalikuwa ni muhimu sana. Kwa muda wa

siku mbili Bush alikuwa akiitikia akiwa kama rais, lakini katika hali halisi

alitegemea kufanya hivyo katika hulka ya kirais. Huenda hali hiyo ilikuwa ni ya

pekee na yenye mazingira mabaya. Alichokuwa anakisema hakikuonekana kama

kilikuwa kinatoka kwake. Alikuwa amekubali na kujitwisha jukumu na wajibu wa

urais. Akiwa amesimama katika Ofisi ya Ovel upande wa kulia, alionyesha wazi

kwamba hisia za kibinadamu huzidi hata nguvu za ofisi ya rais.

Kabla ya alasiri Bush aliondoka na Mke wake kwenda kuzuru kitengo cha watu

walioungua kwenye kituo cha Hospitali ya Washington ambako baadhi ya watu

walionusurika kutokana na mashambulizi ya Pentagoni walikuwa wakitibiwa,

wanaume kwa wanawake walikuwa wamepakwa madawa na kufungwa mabendeji

wengine walikuwa karibu hawatambuliki. Walioungua sehemu kubwa zaidi za

miili yao walisimulia jinsi walivyojiburuza wakipita katika kituo cha biashara cha

kimataifa (WTC)

Ulikuwa ni wakati mwingine wa mshituko kunako saa 6.30 mchanagari lake

lilirejea Ikulu. Hakutaka vurugu yoyote kabla hajatoka, Andy Card aliinua mkono

wake akimwashiria rais kurejea katika kiti chake. “Bw.Rais, Card alisema, “rudi

kwenye kiti chako kwa dakika moja kuna jambo nataka kukueleza”. Alipanda

katika kiti cha nyuma kando ya Bush na kufunga mlango. “Tumepata tishio jingine

dhidi ya Ikulu mnadhimu huyo mkuu alisema hatulipuuzi”, CIA ilikuwa imetuma

ripoti ya tahadhari kutoka katika vyombo vya kijasusi vya India ikisema kwamba

63


watu wenye kuendesha jihadi yaani Waislam wenye msimamo mkali walikuwa

wakipanga shambulio dhidi ya Ikulu.

“Kwa nini unanieleza hapa” Bush alijibu haraka akiwa amechukia kwa Card

kumweleza jambo hilo hapo bila ulazima wowote wakati akijua kwamba hali hiyo

ilikuwa inaonekana wazi mbele ya vyombo vya habari katika eneo hilo la

barabara, “ungesubiri hadi niingie katika ofisi ya Oval” . Bush alitoka kwenye gari,

pamoja na Card moja kwa moja wakaelekea kwenye ofisi ya Oval ambako

mkurugenzi wa vyombo vya upelelezi Stafford na mkuu wa vyombo binafsi vya

upelelezi vya Bush walikuwa wakiwasubiri. “Tunataka tukuondoe hapa” Stafford

alisema. Tishio hilo lilikuwa ni la kweli na likilingana na ripoti zingine za kijasusi

ambazo zilielezea hatari ya ghafla. Vyombo vya kijasusi vya India vilikuwa

vimejichimbia vizuri nchini Pakistan huku vikitiririsha ripoti sahihi. Stafford alitaka

kumchukua Bush na kumpeleka kwenye kituo cha dharura cha kirais, yaani handaki

lililo chini ya Ikulu.

“Siondoki hapa!” Bush alisema alitaka habari zaidi iwapo walikuwa nazo. Kwa sasa

alisema haendi popote, “halafu isitoshe nina njaa”. Alimgeukia Ferdinand Garcia

mpishi wa jeshi la maji aliyekuwa zamu katika tawi la magharibi, “Fredie!

nataka hamburger” (mkate uliopachikwa nyama na viungo vingine katikati).

Card alifahamu kwamba Bush alikuwa ni mtu mwenye hisia za kukubali kila

tukio kwamba ni lazima litokee. Iwapo pangetokea kitu chochote basi

wangefanya alichokitaka, Na kujificha katika handaki halikuwa chaguo lake, Kabla

ya mashambulio Bush alikuwa akila chakula kidogo matunda na vyakula vingine vya

kutia afya ili kupunguza uzito. Baada ya Hughes kusikia kuwa Bush ameagiza

hamburger alisema, “bila shaka utapenda jibini pia”. Rice alikuwa amejiunga na

kundi hilo na wote walikubaliana kwamba hata kama rais hakuwa tayari kuondoka

walikuwa na jukumu kwa wafanyakazi wote wa Ikulu. Wafanyakazi wengi hususan

baadhi ya vijana wasaidizi wa ngazi za chini walikuwa bado wana wasiwasi

kutokana na mashambulizi ya September 11 ambapo wafanyakzi waliihama Ikulu.

Rais na washauri wake waliamua kwamba wawaruhusu wafanyakazi wote

wasiokuwa muhimu kwenda majumbani kwao alasiri hiyo. Card alifikisha habari

hizo kwenye mkutano wa maofisa waandamizi na kutangaza kwamba vyombo

vya upelelezi vingetekeleza hatua za ziada za kulilinda jengo hilo ikiwa ni pamoja

na kupanua wigo wa usalama kuyazunguka majengo ya Ikulu. Alisema makamu wa

rais angehamishiwa katika sehemu ambayo haikutajwa ikiwa ni tahadhari dhidi

ya rais na makamu wake kuwa pamoja, iwapo pangetokea shambulio jingine

juhudi za kuendeleza kuwepo kwa mtu anayetambuliwa na katiba kuweza kushika

hatamu za urais yalikuwa ni mambo yenye kipaumbele sana.

Uamuzi wa kumhamisha Cheney ulikuwa ishara ya wazi zaidi ya jinsi

walivyokuwa wanavichukulia kwa umakini vitisho vya shambulio jingine. Hali

hiyo ingesababisha maswali kuhusu mahali alikokuwa makamu wa rais na afya

yake kwani alikuwa amewahi kupatwa mashambulio manne ya moyo lakini

alisisitiza kutokaa Ikulu wakati vitisho vya mashambulizi vilikuwa vimepamba

moto. Tuna wajibu wa kuhakikisha kwamba serikali inakuwepo, Cheney alimwambia

rais.

64


KIPIGO KITAWASHANGAZA WENGI

Kwenye wizara ya mambo ya Nje Powell na Armitage walikuwa wameelekeza

nadharia yao kwa Pakistan kuwa ni kiungo muhimu kwa mkakati wowote wa

kuwatega na hatimaye kuwashambulia Al Qaeda na Taliban nchini Afghanistan.

Pakistan ilikuwa ni moja ya mataifa ambayo yaliielewa dunia vilivyo na ambayo

yaliitambua Taliban kuwa ndiyo serikali rasmi ya Afghanistan. Chama hicho

chenye msimamo mkali kilikuwa kina wafuasi wengi ndani ya nchi na mipakani

mwa nchi hiyo. Marekani haikuwa na uhusiano mwema na Jenerali Pevez Musharraf

ambaye alikuwa ameshika madaraka kutokana na mapinduzi ya jeshi yasiyokuwa

ya kumwaga damu mwaka 1999 ukiwa ni mwaka mmoja baada ya Marekani

kuiwekea vikwazo Pakistan kwa kufanya jaribio la zana za nyuklia.

Powell alikuwa amemweleza Bush kwamba hata kama akichukua hatua gani

isingewezekana bila kuungwa mkono na Pakistani. Walikuwa ni lazima wajulishwe

viongozi wa Pakistan. Kumbana mno Musharraf lingekuwa jambo la hatari

lakini kutombana kabisa lingekuwa jambo la hatari zaidi. Fanya unachotakiwa

kukifanya Rais alisema, Hebu tupange Powell alimwambia Armitage, tunataka hawa

jamaa wafanye nini?

Walianza kupanga orodha yamikakati. Kwanza wapigeni marufuku wapiganaji

wa Al Qaeda kwenye mipaka yenu, kamateni silaha (zinazowafikia) kupitia

kwenu (Pakistan) na kukomesha misaada yote ya kijeshi kwa Bin Laden. Pili

fuatilieni safari zenye kupita katika anga lenu na kufuatilia haki za ndege kutua

nchini mwenu. Tatu kupewa fursa ya kutumia vituo vyenu vya majini, anga na

mipakani. Nne kupewa mara moja habari za kijasusi na za uhamiaji. Tano kuzuia

dalili zozote zinazo fanana na mashambulizi ya September 11 na kukomesha dalili

zote za ndani za kuunga mkono ugaidi dhidi ya Marekani, marafiki na washirika

wake. Powell na Armitage walifahamu kwamba hilo lilikuwa jambo ambalo

wasingeweza kulifanya hata nchini Marekani.

Sita kufunga njia zote za kuwapatia mafuta watawala wa Taliban na kuwazuia watu

wenye kujitolea kutoka Pakistan kwenda kuungana na utawala wa Talban. Dai

la saba lilikuwa ni lile ambalo Powell alihisi lingewashitua wapakistani na

kumfanyaMusharraf kushituka: Iwapo ushahidiutaonyeshakikamilifu

kumhusisha Osama Bin Laden na mtandao wa Al Qaeda nchini Afghanistan na

iwapo Afghanistan na Taliban wataendelea kumweka mtu huyo na mtandao wake,

Pakistani itavunja uhusiano wa kidiplomasia na serikali ya Taliban na kutusaidia

katika njia tulizozitaja za kumwangamiza Osama Bin Laden na mtandao wake wa

Al Qaeda.

Katika maneno mengi Powell na Armntage walikuwa wanaiomba Pakistan isaidie

kuangamiza kile ambacho mashirika yake ya kijasusi yalikuwa yamesaidia katika

kukiumba na kukilea yaani Taliban. Armitage alimpigia simu mkuu wa shirika la

ujasusi la Pakistan Jenerali Mohmoud ambaye alikuwa amekutana naye siku ya

nyuma na kumkaribisha kwenye Wizara ya mambo ya Nje.

65


“Jambo hili si la kujadiliwa” Armitage alimwambia jenerali huyo akimpa karatasi

moja yenye madai hayo saba. “Ni lazima ukubali madai yote saba. Saa 7.30

alasiri, Powell alimpigia simu Musharraf. Yakiwa mawasiliano kutoka kwa jenerali

mmoja kwenda kwa (jenerali) mwingine alisema, “tunataka mtu katika safu yenu

ambaye atapigana pamoja nasi”. Kwa kusema wazi watu wa Marekani

hawataelewa iwapo Pakistan haitaungana katika mapambano haya na Marekani.

Powell akiwa amepigwa mshangao Musharraf alisema kwamba Pakistani ingeunga

mkono kwa vitendo kufutana na masharti yake saba.

Mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika Pentagon siku hiyo ulifanywa na

Naibu waziri wa Ulinzi Paul Wolfolwitz, aliyekuwa ofisa mwandamizi chini ya

Cheney wakati wa utawala wa Bush mkubwa. Wolfowitz kila mara alikuwa anatoa

maoni ya kundi la wahafidhina waliosema wazi katika baraza la usalama wa taifa

mjini Washington kuwa mapambano yawe dhidi ya Iraq. Wengi wao wakiwa

wakongwe waliopitia katika serikali za Reagan na Bush mkubwa, hawa walikuwa

ni watu walioamini kwamba hapakuwepo tishio kubwa zaidi duniani kuliko Rais

Saddam Hussein wa Iraq na walidai kwamba iwapo rais (Bush) alikuwa

amedhamiria kweli kuwanasa wale wanaowafadhili magaidi alilazimika kumweka

Hussein mwanzoni mwa orodha ya watu hao.

Iraq ilikuwa ni tatizo kubwa kwa rais huyo na kundi lakekama ilivyokuwa

Afghanistan. Walisema iwapo Saddam mtu mjanja na asiyetabirika angeamua

kufanya shambulio la kigaidi au hata pigo la kawaida la kijeshi dhidi ya vyombo

vya kijeshi vya Marekani baada ya September 11 na rais akashindwa kumchukulia

hatua kushitakiana kusingekoma.

Rumsfeld alikuwa ameliibua suala la Iraq wakati wa mikutano ya siku ya nyuma

yake kuhusu usalama wa taifa na rais. Sasa Walfowitz alitaka kutoa tahadhari ya

wazi kwa mataifa ya kigaidi. Ilikuwa ni juhudi nyingine ya kumshinikiza rais

aijumuishe Iraq katika duru yake ya kwanza ya malengo yake. “Si suala la

kuwakamata watu tu na kuwabebesha lawama, bali ni kuangamiza makazi yao,

kuiondoa mifumo yenye kuwasaidia na kuyaangamiza mataifa yenye kufadhili

ugaidi. “Itakuwa ni kampeni kamili na si kitendo cha mara moja na tutawasakama

watu hawa na watu wanaowasaidia hadi kila kitu kikome” Wolfowitz alisema.

Katika hali ya kawaida hata hii ilikuwa hatua yenye kushinikiza zaidi taarifa ya

itikadi ya Bush tangu usiku wa September 11. Wolfowitz alisema hivyo

makusudi kauli yake ingesambaa haraka duniani na kuwashitua washirika wengi

wa Marekani. Kuyakomesha mataifa yanayofadhili ugaidi na kubadilishwa kwa

utawala yalikuwa ni maneno yenye kuhusiana na yale aliyoyasema Bush lakini

hayakusemwa wazi wazi.

66


“Tutawajibika kwako kwa kile ambacho kitakwenda mrama Rumsfeld alisema,Tutawajibikamrama,alisema

mambo ambayo yatavurugika mikononi mwetu kwa mfano kushambulia kambi

ambazo hazina watu”. “Waambieni watu wa Afghanistan kuwa wawanase Al Qaeda”

Bush alisema. “Tunataka tuwaone, bila hivyo tutawatwanga kwa nguvu!

tutawatwanga vibaya kiasi kwamba kila mtu duniani ataacha kushirikiana naanga

Bin Laden, Sitaki kubomoa hema lenye thamani ya dola tano kwa kutumia

kombora lenye thamani ya dola milioni moja”.

Mtu mmoja mwenye kuandika nukuu za mkutano aliandika majadiliano hayoaliandika

ambayo yalikuwa yanatakiwa yakafanyiwe marekebisho ya haraka, Ukosefu waU

mwelekeo maalumu na wingi wa maoni mbali mbali vilishamiri mbele ya meza yao.

“Tunataka maamuzi mapya Rumsfeld alisema. “Hili ni jukumu jipya”. RaisTunatakamapya”Hilijipya

alionekana kukubali, “kila kitu kiko mezani alisema. “Hebu tutazame mambokilamezani”Hebu

tutakayochagua kuyafanya . Pia alisema kwamba Waingereza walikuwa wana niakuyafanya”.

ya kweli ya kushiriki. “Hebu nao wapatieni majukkumu ya kufanya, muda nipatieni

muhimu wakati tukifika Camp David tunahitaji ratiba kamili ya mambo yakati

kufanya lakini nataka kufanya kitu fulani muhimumuhimu”.

67


SIWEZI KUPAZA SAUTI BUSH ALISEMA KWA

KICHEKO

Ilikuwa ni usiku wa manane siku ya tatu tangu mgogoro huo uanze ambapo

hatimaye Rice alirejea nyumbani kwake huko Watergate. Alikuwa ameupitisha

usiku wa kwanza wa mgogoro huo Ikulu kwa usingizi wa kubabaisha. Usingizi

wa jumatano usiku haukuwa mzuri pia alikuwa akiendesha shughuli zake bila

utulivu. Sasa alikuwa na wakati wa kuweka sawa mambo nyumbani kwake,

aliwasha televisheni yake mara ya kwanza tangu mgogoro huo uanze ambapo

aliona mambo ya kawaida ambayo ni kubadilishwa kwa zamu ya walinzi katika

makao ya mfalme mjini London.

Lakini muziki uliofuatia mandhari hiyo ndiyo ulionyesha mshikamano na kuiunga

mkono Marekani ambapo bendi ya Coldstrem Guards ilikuwa inapiga wimbo wa

Taifa wa Marekani wa The star spangled Banner Rice alisikiliza kwa sekunde

chache na kisha akaanza kulia. Mapema asubuhi ya tarehe 14 ijumaa September

afisa wa ngazi za kati kwenye kituo kikuu cha kijeshi cha Taifa (NMCC)

kilichopo katika chumba cha vita cha Pentagon alipiga simu Ikulu akithibitisha

kwamba rais hakutaka ndege yake ya Air Force One isindikizwe na ndege za

kivita wakati akiruka kwenda New York jioni hiyo.

Rice, Steve Hadley na Mnadhimu wa Ikulu Card walifanya majadiliano.

Walikubaliana kwamba yote hayo yangehusiana na uamuzi wa Rumsfeld.

Mazingira ya vitisho yalikuwa hayafahamiki kwa yeyote kwamba nini kingetokea,

iwapo jambo lolote lingetokea kwa sababu hapakuwepo na ndege za kivita

kuisindikiza ndege ya rais Rumsfeld ndiye angelieleza taifa na dunia. Mmoja wa

manaibu wa Rice alipiga simu Pentagon na suala hilo lilipelekwa kwa Rumsfeld

kwamba NMCC walikuwa wamepiga simu Ikulu kuulizia ndege za kivita za

usindikizaji.

Rumsfeld alikasirikka sana “kuna mtu katika jengo langu anazungumza na Ikulu

bila ya mimi kufahamu au kutoa ruhusa? alisema mimi simo humo”!.

Rumsfeld alisema alikuwa hana mipango ya kijeshi na rais, alikuwa anajitayarisha

kuanzisha vita. Utafiti ulianza mara moja kumtambua ofisa aliyepiga simu Ikulu

wakati huohuo Rumsfeld alikataa kulishughulikia suala la iwapo angeweza kutuma

ndege ya kivita kuisindikiza ndege ya rais ya Air Force One

Pentagon walikuwa wanasubiri uamuzi wa Rumsfeld kuhusu iwapo atume ndege za

kivita kumsindikiza rais ambaye katika muda mfupi alikuwa anaondoka kwenda New

York. Waziri huyo alikuwa anasita, aliliona kama suala ambalo lilihusiana naye

sana kimadaraka na sheria. Mawasiliano ya habari kwa kawaida hufanyika kati

ya Pentagon na Ikulu lakini uamuzi wa kupeleka ndege za kivita kumsindikiza

rais ulikuwa ni wake pekee. “mamlaka ya usimamizi wa ulinzi wa taifa ndiyo

jukumu langu, sasa iweje wakaamua kujifanyia maamuzi yao? rais hawezi kuwa

na uhakika kwamba yatakayofanywa yatalingana na yale aliyoyataka niyafanye”.

Na katika hali ambapo watu wanawaambia watu wengine na kisha mtu fulani

akusema oh tutume ulinzi wa kumsindikiza rais au hatua maalum za ulinzi wa

anga au tusifanye au tufanye, hivyo inaweza kuwa kinyume kabisa na kile rais

68


anachokitaka ambacho mtu hutakiwi kutembea nacho. Kiasi cha dakika 15 kabla

ya ndege ya rais kuondoka waziri huyo alitoa amri yake. Kungekuwa na ndege za

kivita kuisindikiza ndege hiyo.

Asubuhi hiyo kikao kizima cha baraza la mawaziri kilichokuwa kinakutana Ikulu kwa

mara ya kwanza tangu mashambulio ya magaidi yafanyike kilisimama na kumpigia

makofi rais alipokuwa akiingia katika chumba cha mkutano. Akiwa amepigwa

na butwaa Bush alishituka kwa muda wa sekunde mbili na kujikuta akigwaya

mbele ya watu wengine. Bush alipenda kufungua kila kikao cha baraza la

mawaziri kwa sala na alikuwa amemwomba Rumsfeld kutayarisha sala moja kwa

ajili ya kikao hicho. Miongoni mwa mambo ambayo Rumsfeld aliomba katika

sala yake ni moyo wa subira wa kupima uchu wa vitendo vyetu.

Powell alikuwa na wasi wasi kuhusiana na hali ya wasi wasi aliyokuwa nayo Bush.

Katika muda mfupi baadaye, rais angekuwa anazungumza kwenye kanisa la

Taifa la Washington na Powell alifikiri kwamba nchi hiyo na dunia vilihitaji

kumwona rais mwenye nguvu. Akiwa amekaa kondo ya rais, Powel alisema,

“nilichofanya wakati ninapotoa hotuba,nimekwepa maneno ninayofahamu

kwamba yataibua jazba kwangu kama vile mauaji au mashambulizi,” kisha akataja

kwa kutumia lugha ya uangalifu huku akisukumiza kikaratasi fulani chenye maneno

ya kuchekesha kwenye meza.

Bush alikiokota kipande kile cha karatasi akakisoma na kutabasamu “hebu

niwaambie ambacho waziri wa mambo ya nje alichoniambia, Bush alisem

akikiinua kikaratasi hicho, “Mpenzi Rais tafadhali usije ukaangua kilio!”

Chumba kililipuka kwa kicheko ambapo Powell na rais pia walijiunga nacho.

Usiwe na wasi wasi hilo sitakuwa nalo Bush alisema. Aliwahakikishia kwamba yeye

na baraza la vita walikuwa wanapanga mipango kwa ajili ya jibu la kijeshi ambalo

lingekuwa la uhakika na kisha akaanza kuuliza maswali kwa watu waliokuwa

mezani hapo ili kupata habari na matukio mapya.

Kisha akaanza kuuhariri muswada wa habari za kijasusi wa siri kubwa ambao CIA

ilikuwa imetaka rais ausaini.Katika maoni yake ulikuwa umetayarishwa

kizembe lugha ilikuwa haifahamiki vizuri na haina melengo, mamlaka yakiwa

makubwa mno na yasiyokuwa na mipaka. Aliiwekea alama nakala yake kuhusu

mapendekezo ya marekebisho na ufafanuzi wa yaliyokuwemo. Mamlaka ambayo

yangebidi yawe ya rais au mkurugenzi wa CIA yalikuwa yanatolewa kwa watu wa

ngazi za chini.

“Je,mnahisi kutatokea jambo fulani”? Hughes aliuliza wakati helkopta iliyokuwa

imebeba wafanyakazi wa Ikulu ilipowasili kutoka New York ikikaribia mwishoni

mwa safari yake, walikuwa kiasi cha maili 20 au 25 kutoka mandhari ya chini ndani

jiji la New York. Wengine walitingisha vichwa waziri wa habari, Ari Flescher

alifikiri jambo hilo linaweza kutokana na helkopta hiyo. Lakini wakitazama nje ya

madirisha yao upande mmoja waliona wingu kubwa la moshi harufu waliyoisikia

ilikuwa ni magofu ya kituo cha biashara cha kimataifa yaliyokuwa yakiwaka.

Helikopta hizo zilitua uwanja wa Wall Street na msururu mrefu wa magari 55

ukiwa ni msururu mrefu zaidi ambao haujapata kuonekana katika makundi ya

69


watu waliokuwa wakishangilia na kupunga bendera hadi eneo la janga la magofu

ya jengo hilo ambalo lilianza kuiwa Ground Zero.

Bush alipoliona eneo hilo kubwa lililokwishakuwa magofu liliacha alama

isiyofutika moyoni mwake, alama ambayo mtu angeiita kuwa ni ya kinyama

sana, japokuwa alikuwa amezungumza na watu wengine kuhusu uharibifu huo

hakuwa ameutayarisha moyo wake kwa yale aliyoyaona, yalikuwa ni jinamizi,

jinamizi la kweli. Pamoja na uharibifu huo mkubwa kuliko aliouona kwenye

televisheni au kuusikia kutoka kwa washauri wake alikutana na kundi kubwa la

wafanyakazi wa uokoaji waliokuwa wamepandwa na jazba kubwa wakidai haki

itendeke katika hilo.

Alipokuwa akitembea na mandhari iliyokuwa imejaa jazba kubwa alisema “siwezi

kuelezea jinsi jazba ilivyokuwa kwa wafanyakazi hao” “lolote na lifanyike!

walikuwa wakipiga makelele”. Mtu mmoja alimwelekeza kidole wakati akitembea

na kupiga kelele akisema “tafadhali usiniangushe! Bush alipigwa butwaa, alifikiri

kwamba maneno na sura aliyokuwa nayo mtu huyo huenda asingevisahau milele

“Tafadhali usiniangushe! Hili ni dai binafsi zaidi” alifikiri. Ilikuwa kama alikuwa

katika eneo la magofu ya zamani. Waokoaji walianza kupiga makelele wakisema

U-S-A, U-S-A,U-S-A. “Wanataka kumsikia akisema”, Nina Bishop mmoja wa

kundi la rais huyo alimwambia Karl Rove wakati rais alipokuwa akipita katika

tukio hilo wafanyakazi wa Ikulu hawakuwa wamejitayarisha na jambo hilo.kwa

vile hapakuwa na mpango wa Bush kuhutubia kundi hilo, hapakuwepo na vyombo

vya kupazia sauti. “Je, Nina, unaweza kutafuta kipaza sauti cha kubebwa?”, Rove

aliuliza.

Kwa karibu Bob Beckwith mzee mmoja dhaifu aliyestaafu kazi ya zimamoto mjini

New York, mwenye umri wa miaka 69 alisimama juu ya lori lililokuwa limevutwa

kutoka katika magofu.Msaidizi mmoja wa Bush alimuuliza iwapo rais

angeweza kulitumia kama jukwaa na iwapo Beckwith aliyekuwa na kinyago cha

picha ya Mwalimu Julius Nyerere kikiwa ninaning’inia shingoni mwake angeweza

kurukaruka juu yake mara chache kuhakikisha iwapo lilikuwa imara. Chini ya

gari la zimamoto kulikuwa na pande kubwa la zege, baadhi ya wasaidizi wa rais

walifikiria kuliondoa lakini waokoaji waliwaambia wasifanye hivyo kwani huenda

kulikuwa na maiti za watu chini yake.

Saa 10.40 jioni mtu mmoja alikuwa na kipaza sauti cha kubeba na kumpa rais na

akamsaidia kupanda juu ya mabaki ya lori hilo. Beckwith alimwomba rais asimame

kando yake. Makelele mengine yakaanza, U-S-A,U-S-A. “Asanteni wote! Bush

alianza, “nataka nyote mfahamu Amerika leo inalia, nawaomba ujasiri tuliorithishwa

na mababu zetu utujenge tuwe imara katika mapito haya magumu,” na lundo kubwa

la watu waliokuwepo walionyesha nyuso za matumaini mbele ya kiongozi wao.

“Hatukusikii! mmoja wa waokoaji alipiga kelele. “siwezi kupaza sauti zaidi ya

hapa” Bush alisema kwa kicheko. “Mimi nakusikia, wale kulenyuma wanakusikia,

walimwengu pia wanakusikia na waliotenda haya wanakusikia, hivyo rejesha moyo

konde, kuwa nami katika haya.

70


Amerika leo hii imepiga magoti ikiwaombea watu waliopotea hapa! Sauti nyingine

ilijitokeza katika kundi hilo “Sikusikii’, Bush alisita kidogo, kisha akiwa amemshika

Beckwith begani, alipaza sauti na kusema, Mimi nakusikia, Walimwengu wengine

wanakusikia, Na watu walioteketeza majengo haya watawasikieni hivi karibuni!.

Hughes aliyekuwa amesimama kando alikuwa akitabasamu, “Huu ulikuwa wakati wa

kushangaza” Hughes alifikiri, ikiwa nitukio lenye mambo mengi, lenye kuonyesha

sura halisi, wakati wa vyombo vya habari kuandika chochote na umaarufu kwa ajili

ya historia alikuwa hahusiki kwa lolote.

Baada ya muda mfupi rais alipata fursa ya kuwashukuru watu waliokuwa wakifanya

kazi katika eneo hilo, msururu wa magari ulielekea njia kuu ya West Side hadi

kwenye kituo cha Jakob K Javits Convertion ambacho kilikuwa kinatumika kama

jukwaa la juhudi za uokoaji. Ratiba ya rais ilimtaka kutumia dakika 30 hadi 45 na

familia za watu waliokumbana na maafa hayo. Hafla hiyo ilibidi kufanyika bila

kushirikisha vyombo vya habari, wapiga picha, na wajumbe wa baraza la Congress

waliokuwa wamefuatana na Bush. Watayarishaji wa ratiba hiyo walikuwa

wametumia vitambaa mbalimbali ili kulifanya eneo hilo lililo kuwa wazi lipate

uficho, na wasaidizi wa Bush walilizunguka eneo lote ili kuweza kutoa fursa ya

faragha kwa kundi hilo.Watu wapatao 250 walikuwa wanamsubili rais, wengi wao

wakiwa wamebeba picha za ndugu za waliokuwa hawafahamiki walipo. Watoto

ambao sasa walikuwa hawana wazazi, walikuwa wamebeba picha za wazazi wao na

vitu vingine vya kumbukumbu.

Watu wa familia hizo walishangilia wakati rais alipofika hapo, kisha ghafla pakawa

na ukimya ambao ulifanya mashine zenye kurekebisha hewa ndani ya eneo hilo

kusikika peke yake. Kilikuwa ni kipindi cha mahangaiko kwa Bush ambaye hakujua

ni vipi aanze kukutana na kuzungumza na familia hizo. Hatimaye, alipenya katikati

ya makundi ya watu, “Hebu niambie unavyojisikia”, alimwambia mtu mmoja, kisha

mtu mwingine na mwingine. Kila mara alisikia maneno yenye kufanana, maneno

ambayo yalimfahamisha kwa kishindo hali halisi. Wote walisema kuwa walikuwa

wanaamini kwamba wapendwa wao walikuwa wangali hai. Walitaka kumbukumbu

ya maandishi na Bush alianza kusaini jina lake katika picha na karatasi mbalimbali

au kwenye vitu mbalimbali vya thamani. Alikuwa akiziambia familia kwa kadri

alivyo kuwa akikumbuka. “Nitawaambia kitu furani, nitasaini hapa namkimwona

Jimy au mkimwona Bil mmwambie kuwa hii ni saini yangu halisi na kwamba

hamkuigushi na kwamba hii ndio njia muhimu ambayo nimeichagua katika kutoa

msaada, utumieni wakati huo ilikuweza kusema, Ninashiliki katika matumaini yenu

pia, na tunaomba Jim atokee”

Watu wengi katika chumba hicho walikuwa wakilia. Rais alikuwa amejawa machozi

wakati akikutana na familia moja hadi nyingine. Mtu mmoja akiwa amebeba mtoto

mikononi mwake, alikuwa amebeba picha ya kaka yake ambae ni mzimamoto ambae

alikuwa amefariki. Mtoto huyo aliinyoshea kidole picha hiyo na kusema: “Baba

mkubwa”. Saa moja baadae akiwa bado sehemu hiyo, Bush alionekana kupata nguvu

zake. Kulikuwa navicheko kadhaa kutoka kwa baaadhi ya wananduguu wakati

akisonga mbele katika shughuli iliyo mchukua muda wa masaa mawili kuwasiliana

nao.

71


Alizungumza na kila familia. Mwishoni mwamatembezi yake hayo, Bush alikutana

na Arlene Howard, mama wa polisi wa Mamlaka ya Bandari aliyekuwa hayuko

zamu , ambaye aliuawa akijaribu kuwaokoa wengine. Mama huyo alikuwa amebeba

ngao ya polisi ya mwanae na alimpa rais akimwomba aipokee kwaajili ya heshima ya

mwanaye, rais aliipokea ngao hiyo huku huzuni ikizidi kutanda usoni pake.aye,kutanda

72


VITA ITAKUWA NGUMU MAMBO YAKIENDA

MRAMA

Wakati ukirejea uwanjani, msururu wa magari ya Bush ulipita katika uwanja wa

Times Square ambao ulikuwa umejaa watu wakiwa wamebeba mishumaa na bendera

za Marekani wakishangilia wakati magari hayo yakipita. Baada yakurejea kituo cha

jeshi cha McGuire Air Force Base huko New Jersey, Bush aliyekuwa amechoka,

aliagana na wafanyakazi wakewaliokuwa wakirejea Washington. “Iwapo

ingewezekana kuishi maisha yote katika siku moja, siku yenyewe ilikuwa leo”,

alisema. Badala yakupanda ndege ya Air Force One, Bush alipanda katika ndege aina

ya C-20 ambayo ilikuwa ndogo kiasi cha kuweza kutua Hangerstown, Maryland.

Kutoka hapo angekwenda Camp David. Picha ya video ya rais huyo akitoka katika

helikopta yake, ilimuonyesha akiwa amechoka vibaya, akiwa anatembea kwa

kutetereka.

Rais alikuwa amewaagiza washauri wake waandamizi wa usalama wa taifa Cheney,

Powell, Rumsfeld na Rice kutangulia Camp David kwaajili ya matayarisho ya

mkutano wa siku iliyofuata. Watu hao walikutana katika chumba cha makamu wa rais

ilikupata mlo wa jioni wa nyama ya nyati, haikuwa na bonde la ufa kipindi hicho

kama nyama za kibongo za mwaka 2007 japo utamu haukufanana na nyati wakule

kwetu Iringa - Ruaha kwani kule wanaishi katika marisho ya majani mabichi katika

himaya ya Mkwavinyika.

.

Chakula hicho kiliwapatia fursa ya kupeana habari mbalimbali katika hali ya utulivu

zaidi, kupashana habari za matukio mapya na kupanga masuala ya kujadiliwa katika

vikao vya siku iliyofuata. Walizungumzia shinikizo la kuchukua hatua za haraka,

urefu wa mapambano yaliyokuwa yanategemewa na tofauti kati ya mgogoro

uliokuwa unatarajiwa na Vita vya Ghuba ya Uajemi ,wakati ambapo palikuwa na

matayarisho makubwa ya muda mrefu na muda mfupi wa mapambano ya kijeshi

ambapo ilichukua siku 38 za ulipuaji mkubwa wa mabomu na siku 4 ya vita vya

ardhini.

Hali ya sasa walivyofikili ingekuwa kinyume, na walivyozidi kuzungumza, ndivyo

walivyotambua jinsi vita hivi vingekuwa vigumu zaidi na jinsi matokeo yake

yangekuwa makubwa wangevipanga vibaya. Powell alielezea kuhusu hatua za

shambulio kwa upande wa kidiplomasia. Kama alivyokuwa rais, Powell aliona

mashambulio hayo kama fursa ya kupanga upya mifumo ya mahusiano duniani

kote, lakini alikieleza kikao hicho. Hii ilikuwa ni hatua ya ushirikiano wenye

malengo ya wazi ya kuzishikilia fedha zote za magaidi na kusaidiana katika

kampeni za kijeshi. “Hili si shambulio dhidi ya Marekani tu, hili ni shambulio

dhidi ya demokrasia” Powel alisema akitoa sauti yenye mamlaka ya kirais.

“Hivi ni vita virefu na ni vita ambavyo ni lazima tushinde, tunaishirikisha dunia,

tunataka kuufanya ushirikiano huu uwe wa muda mrefu”. Katika kipindi cha

asubuhi hiyo Powell alikuwa ametuma simu 35 kwa viongozi mbali mbali duniani

na zingine 12 akazipiga baadaye siku hiyo. Nimefanya kazi chungu nzima mnamo

siku chache zilizopita najisikia mnyonge alisema kwa utani, Waliokuwepo

wakacheka.

73


Rumsfeld alikieleza kikao kuhusu uharibifu uliofanywa Pentagon na akatangaza

kwamba hali ya tahadhari kijeshi imepunguzwa kiwango cha Def Con 4.Tarehe

11 September Pentagon ilikuwa katika tahadhari kwa kiwango cha Def Con 3 kwa

mara ya kwanza tangu vita kati ya kiwango cha juu zaidi. Def Con 1 hutumika

wakati wa vita kamili.

Waziri wa Usafirishaji Norman Y. Mineta alisema usafiri ulikuwa unarudia hali

ya kawaida siku hiyo kwa kiwango cha asilimia 16 ikiwa ni hatua iliyotokana na

mashambulio hayo. Bush alihitimisha hayo kwa kukumbusha kwamba wakati

ukiwa ni kuamua vita dhidi ya ugaidi ni lazima wasipuuze majukumu makubwa ya

nchi kama vile muswada wa elimu, muswada wa haki za wagonjwa na sheria

yenye kumpa madaraka makubwa zaidi ya kuendesha majadiliano kuhusu

mikataba ya biashara. Wakati wa chakula cha mchana msururu wa magari ya rais

uliondoka Ikulu huku mvua kubwa ikinyesha, ulielekea kwenye kanisa la taifa

umbali wenye kuchukua dakika 12

Kundi lisilokuwa la kawaida lilikuwa linasubiri kanisani hapo kwa ajili ya sala.

Wazungumzaji walikuwa ni pamoja na mchungaji wa kiprotestant, kasisi wa

kiyahudi, kadinali wa kikatoliki, shehe wa kiislam na mchungaji Billy Graham.

Marais wa zamani Bill Clinton na Jimmy Carter walikuwepo pamoja na makamu

wa zamani wa rais Al Gore. Wasikilizaji walikuwa ni pamoja na baraza la

mawaziri, wajumbe wa baraza la Seneti, wabunge, mwenyekiti wa shirikisho Alan

Greenspan na maofisa wengine wa ngazi za juu serikalini. Kando ya rais na mke

wake, walikuwa ni baba na mama yake Bush.

Condi Rice alifikiri kwamba safari hiyo ya kwenda kwenye kanisa hilo ilikuwa

kama msururu wa mazishi wakati mwimbaji msanii, Denyce Graves alipoongoza

mkusanyiko huo katika kuimba sala ya Bwana, alifikiri, ni vipi (rais) ataweza

kujizuia katika hali hiyo?

“Tuko hapa tukiwa katikati ya dimbwi letu la masikitiko” Bush alianza “Ni watu

wengi waliokumbwa na madhara na hasara kubwa kutokana na mashambulio hayo

alisema na taifa litayakumbuka majanga haya na kuyatambua na kushiriki katika

kilio cha waliokumbwa nayo, lakini jukumu letu katika historia tayari liko wazi

kuyajibu mashambulizi haya na kuuondolea ulimwengu maovu” Rais alikuwa

akitoa ujumbe wake na wa nchi katika mwanga wa mpango mkuu wa Mungu.

Kuna msemo kwamba matatizo ndiyo hutukumbusha tulipo alizungumzia vitendo

vya ushujaa na kujitolea ambavyo vilionyesha dhamira ya wamarekani katika

kushirikiana na kuipenda nchi yao. “Leo hii tunatambua kile ambacho Franklin

Rooseverlt alikiita nguvu thabiti ya umoja wa kitaifa, umoja ambao utakuwa mvuto

wa huzuni na uthabiti wa kupambana dhidi ya adui yetu”.

74


Kulikuwa na mambo mengi yaliyokuwa na lengo la kuliwaza katika hotuba hiyo

lakini msitari wa kukumbukwa zaidi ambao ulikuwa umetokana na kundi la

waandishi wake wa hotuba na ambao aliusisitiza haraka, ulikuja wakati Bush

aliposema kwa kujiamini kuhusu nini kingefuta. “Mgogoro huu umeanza katika

kipindi muafaka na mazingira ya mambo mengine. Utaisha katika namna na

wakati ambao tutauchagua”.

Hotuba ya vita kutolewa kanisani kilikuwa kitu cha kushitua, na hata kuwa cha

hatari lakini ilitoa ujumbe ambao Bush alitaka. Aliporejea kwenye kiti chake

kwenye safu ya mbele baba yake alinyoosha mkono uliompita Laura Bush hadi

akaufikia mkono wa mwanaye na kuukamua huku macho yake yakilegea akiwa na

fikra za kihafidhina zenye nguvu na zenye kuungwa mkono na mabwana wa vita wa

kiamerika. Mwishoni mwa sala mkusanyiko ulisimama na kuimba wimbo wa vita

wa jamhuri. Rice aliona kanisa lote likiwa limesimama kwa dhamira thabiti.

Wakati kundi la rais lilipokuwa likiondoka mwanga mkubwa wa jua na mbingu

ya bluu vilikuwa vimechomoza.

Bush alikumbuka na kusema kwamba hotuba yake ilikuwa ni kielelezo cha wazi cha

vita kuliko kielelezo cha masuala ya dini. “Niliona wakati huo ulikuwa mwafaka

kuhakikisha natoa liwazo na kusaidia kuwaondoa watu katika maombolezo”

alisema katika mahojiano. “Pia nililiona tukio hilo kwa sura ya kiroho kwamba

ilikuwa ni lazima kwa taifa kusali”. Alikubali kwamba baadhi ya maneno katika

hotuba yake yalikuwa makali sana na akasema kwamba alikuwa nayo lakini

aliongeza kusema “kwangu kipindi hicho kilikuwa na mambo mengi kilikuwa ni

sala ya kweli sikuona kama kuna fursa ya kutayarisha jukwaa kwa ajili ya kutoa

hotuba nyingine baadaye, Niliamini kwamba taifa lilihitaji kusali’.

75


TENET ALITEGEMEA KUPEWA

KUUA

MAMLAKA YA

Mpango huo ulihusu shambulio kamili katika mtandao wa fedha wa magaidi, Ikiwa ni

pamoja na upelelezi wa siri wa kutumia kompyuta na ujasusi wakutumia zana za

elektroniki, kutambua mali za Al Qaeda na makundi mengine ya kigaidi ambazo

zimefichika kupitia katika mashirika mbalimbali ya misaada na zile ziitwazo taasisi

zisizokuwa za kiserikali. Hati nyingine ilikuwa na kichwa cha habari ‘’Nadharia ya

CIA na FBI katika jamii kubwa ya Waafghanistan nchini Marekani.’’ CIA na FBI

zingeshiriki kuwanasa na kuwatokomeza wafuasi wa Bin Laden, jambo ambalo

lilionyesha uzembe wa wazi kabla ya mashambulio hayo. Tenet alielezea kuhusu

juhudi za kusafisha propaganda, akitaja kwamba walikuwa wamefanikiwa kuwapata

Mullah miongoni mwa watu waliokuwa wanawalipa kwa kuwatumia. Kiini cha

pendekezo hilo kilikuwa ni kutaka rais atoe kile Tenet alichokiita ‘’mamlaka

maalum’’ kwa CIA kuitokomeza Al Qaeda nchini Afghanistan na duniani kote.

Alitaka amri yenye habari pana za kijasusi yenye kuiruhusu CIA kuendesha harakati

za siri bila ya kulazimika kurejea kwa ajili ya kutafuta idhini kwa kila operesheni

iliyofanywa. Mkondo wasasa ulikuwa na masuala mengi ya muda, vipengele vya

kisheria, uhakiki wa mambo mbalimbali na majadiliano. CIA ilikuwa inahitaji

mamlaka mapya yenye nguvu ya kuendesha shughuli zake bila vikwazo. Tenet pia

alitaka kuungwa mkono kutoka kwa rais katika kutekeleza majukumu yake. Jambo

jingine muhimu alisema lilikuwa ni kutumia mamlaka maalum ya kuwatia ndani

waendesha shughuli za Al Qaeda duniani kote. Hiyo ilimaanisha CIA ingetumia

vyombo vya kijasusi au njia zingine za kuwatumia watu wengine.

Tenet na wasaidizi wake waandamizi wangepewa mamlaka ya kuidhinisha

operesheni za ‘’ kunyakua’’ watu nchi za nje. Tenet alikuwa ameleta muswada wa

amri ya rais kuhusu ujasusi, ambao ungeipa CIA nguvu za kutumia kikamilifu

vyombo vyake vya kisiri ikiwa ni pamoja na nguvu za mauaji. Kwa zaidi ya miaka

ishirini CIA ilikuwa imebadili tu kanuni hiyo ya kirais katika harakati za kupiga vita

ugaidi. Pendekezo lake jipya, lilitolewa kama marekebisho ya operesheni zakijasusi

katika kuupiga vita ugaidi duniani ambalo lilitiwa saini na Rais Reagan mwaka 1986.

Kama vile likifuta mambo yaliyokuwemo, pendekezo hilo lilichukua nafasi ya amri

iliyo sainiwa na Rais Clinton.

Mkuu huyo wa CIA alifika kwenye ukurasa wenye kichwa cha habari cha “Kutoa

Ruzuku Kubwa kwa Huduma za Mawasiliano kutoka Nchi za Kiarabu.”Alielezea

kwamba pamoja na mamia ya mamilioni ya dola za ziadi kwaajili ya kuendesha

operesheni za siri, CIA ingenunua habari muhimu za kijasusi, kutoa mafunzo, zana

mpya, fedha kwa ajili yamtandao wa mawakala wake kwa chochote kinachotakiwa.

Huduma kadhaa za kijasusi zilikuwa zimeorodheshwa kuwa ni nchi za Misri, Jordan

na Algeria. Zikifanya hivyo kwa niaba ya Marekani, nchi hizo zingeweza kuzidisha

nguvu za kijasusi za CIA na kuwa kundi pana zaidi la mamluki wenye kukusanya

habari za kijasusi. Kama ilivyo katika operesheni nyingi za kisiri duniani, utaratibu

huu huwa na hatari zake. Zingeweza kuiweka Marekani kundi moja na operesheni

zingine za kijasusi zilizo jaa uovu, zikiwemo nchi zenye sifa mbaya dhidi ya haki za

binadamu kama ilivyoelezwa kule mwanzo kuwa kuna nchi ambazo ni mihimili ya

76


ukosefu wa haki za binadamu na kinara mkuu ilikuwa ni Iraq, ambapo sasa usukani

unashikiliwa na Sudan. Nchi yingine zina sifa ya ukatili na hutumia mateso ili kupata

habari kutoka kwa watu. Tenet alikiri kwamba hawa si watu ambao ungekaa karibu

nao kanisani siku ya jumapili. “jamani, watu hawa mimi sina uwezo wa kuwa

simamia” alisema. Bush alisema kwamba alizitambua hatari zilizokuwemo. Tenet

aliongeza kusema kwamba Marekani tayari ilikuwa na kituo kikubwa cha nguvu

mbalimbali katika eneo hilo, hii ni kutokana na kazi ambayo CIA ilikuwa ikifanya

kazi katika nchi zilizo karibu na Afghanistan.

Shirika hilo lilikuwa likitumia vyombo vya anga visivyokuwa na binadamu yaani

ndege zenye kujulikana kama PREDATOR, ambazo zilikuwa zikifanya safari za

uchunguzi wa kijasusi kutoka Uzbekistan kwa zaidi ya mwaka mmoja ilikuweza

kuifahamu sura halisi ya Afghanistan. Ndege ya predator inaweza kuwekewa

makombora aina ya Hellfire ambayo huongozwa na chombo maalumu kutoka mbali

na yanaweza kutumika kwamalengo ya mauaji pia, ikiwa nipamoja na

kuwashambulia Bin Laden na vipemba wake. “Marekani nilazina ihakikishe

inashirikiana na Tajikistan, Turkmenistan na Pakistan Tenet alisema, ilikukwamisha

usafiri wa viongzi wa Al Qaeda nakuwa fungia njia zote za mpakani”. Alipendekeza

kuanzisha mawasiliano yakijasusi na nchi za kiovu kamaLibya na Sirya

ambazo alisema zinaweza kusaidia katika kujaribu kuangamiza Al Qaida, “Ili

CIA iweze kupata habari muhimu dhidi ya magaidi, ni lazima ifanye uovu”

Tenet alirejea katika uhusiano na Afghanistan.Makundi yenye uhasama na

Northem Alliance lakini yakiwa muhimu katika kampeni dhidi ya Alqaida na

serikali ya Taliban. CIA ilikuwa imeshaanza kushilikiana na viongozi wa kikabila

wapatao kumi na mbili sehemu ya kusini mwaka wa nyuma.

Baadhi yao wangejaribu kushiliki katika pande zote, lakini mara vita inapoanza

wangeshawishiwa kwa fedha, chakula ,risasi na vitu vingine mbali mbali kwa ajili ya

kuungana na kampeni yenye kuongozwa na Marekani.

Tanet alifafanua kuhusu maelezo yake yanyuma kwa Rais kuhusu jinsi ambavyo

wange watumia Northn Alliance ambao CIA iliamini wangeweza kuwa nguvu

kubwa hapo baadaye ambayo ilikuwa inahitaji fedha, siraha na habari za kijasusi.

77


TEGEMEO LA U.S.A NI TALIBAN KUMTOSA BIN

LADEN

“Musharraf anafanya jambo la hatari sana!, alisema rais, Tunalazimika kumsaidia

asije kujuta, Lazima tumsaidie kwa mambo kadhaa, ikiwa nipamoja na kuhakikisha

usalama wake dhidi ya silaha za nyuklia, Tayarisheni mambo kadhaa ya kuisaidia

Pakistan”. Hatari nyingine waliyokuwa wakikabiliwa nayo ni kujikuta wakikwama

nchini Afghanistan, kama walivyojikuta Waingereza katika karne ya 19 na Warusi

katika karne ya 20. Rice alikuwa na wasiwasi iwapo hali ingekuwa kama hiyo dhidi

ya Marekani katika karne 21. Wasiwasi wake ulikubaliwa na wengine, hali ambayo

ilileta majadiliano tofauti; Je wafikirie kuanzisha mashambulizi ya kijeshi sehemu

nyingine ikiwa ni sera yakufidia iwapo mambo yangekwenda kombo nchini

Afghanistan? Walilazimika kupata ushindi katika vita vyovyote ilikuweza kuungwa

mkono nyumbani na ulimwenguni.

Ushindi wa haraka wa Marekani katika Vita vya Ghuba mwaka 1991, na watu

kushuhudia ikionyeshwa LIVE katika mtandao wa televishen ya CNN, ulikuwa

umewapa watu matumaini mapya kuhusu vita, hali ambayo mashambulizi ya

makombora ya ‘cruise’ yaliyofanywa wakati wa utawala wa Clinton ilishindwa

kubadili chochote. Rice aliuliza iwapo wangeweza kupanga mashsmbulizi mengine

ya kijeshi baada ya Afghanistan, ambayo ni dhahiri yangefanywa dhidi ya Iraq.

Naibu Waziri wa Ulinzi, Paul Wolfowitz alijitokeza, akiwa mwenye utulivu na sera

za msimamo mkali, Wolfowitz, mwenye umri wa miaka 57 katika kipindi cha

mgogoro, aliamini kwamba kumalizika kwa ghafla kwa shambulio ardhini la Desert

Storm mwaka 1991 lililomwacha madarakani Saddam lilikuwa ni kosa. Tangu

achukue madaraka Bush alikuwa anatafuta njia za kumdhoofisha Saddam ambapo

Wolfowitz alikuwa akishinikiza juhudi za kuyasaidia makundi ya upinzani, na Powell

akipigania kuanzishwa kwa vikwazo vipya dhidi ya nchi hiyo. Wasiwasi uliokuwepo

ni kwamba Saddam alikuwa bado anajaribu kupata na hatimaye kutumia silaha za

maangamizi, na bila ya wakaguzi wa silaha wa Umoja wa Mataifa kuwepo nchini

humo, kulikuwa hakuna njia ya kufahamu hasa aina ya tatizo ambalo USA

walikabiliwa nalo. Mashambulizi ya kigaidi ya septemba 11 yaliipa USA fursa mpya

yakumwangusha Saddam Hussein.

Wolfowitz aliitumia fursa hiyo. Mashambulizi dhidi ya Afghanistan yangekuwa

hayaeleweki kikamilifu. Alikuwa na wasiwasi wa askari 100,000 wa USA kukwama

katika mapigono ya milima ya Afghanistan. Lakini kwa upande mwingine, Iraq

ilikuwa na serikali dhaifu na dhalimu ambayo ingeweza kuanguka kirahisi.

Jambo hilo liliwezekana, alikisia kwamba kulikuwa na kila fursa kwamba kwa

asilimia 10 hadi 50 Saddam alishiriki katika mashambulizi ya septemba11. Marekani

ilikuwa nilazima imtwange baadaye iwapo vita dhidi ya ugaidi vingetiliwa maanani.

Andy Card alifikiri Wolfowitz alikuwa anajisemea tu bila kutoa maelezo au hoja

mpya. Wakati wa mapumziko, Bush alijiunga katika majadiliano ya pembeni ambayo

yalimujumuisha Chenney, mnadhimu mkuu wa Chney, I. Lewis, Scooter Libby na

Wolfowitz. Aliwaambia kwamba alikuwa ameyaona maamuzi kadhaa ya Shelton

kuwa ni yasiyokuwa yakufikirika. Wolfowitz alielezea kuhusu hoja yake jinsi vita

dhidi ya Iraq vingeweza kuwa rahisi zaidi kuliko dhidi ya Afghanistan. Rais aliuliza

kwanini hakuyaeleza kwenye mkutano. “Siwezi kupingana na mwenyekiti wa jopo la

Wanadhimu isipokuwa tu ni pale waziri wa ulinzi akisema hivyo”. Wolfowitz

78


alisema akifahamu kwamba Shelton alikwa anapinga wazo la kuishambulia Iraq.

Kundi hilo lilipokutana tena, Rumsfeld aliuliza: “Je, huu ni wakati wa kuibomoa

Iraq?. Alisema kwamba pangelazimika kuwepo ulimbikizaji mkubwa wa majeshi

katika eneo hilo na alikuwa bado anawasiwasi mkubwa kuhusu kuwepo kwa malengo

mazuri ya mashambulizi nchini Afghanistan. Powell alikataa, “Utayasikia hayo

kutoka kwa washirika wako,” alimwambia rais, Wote wako pamoja nawe kila

mmoja, lakini watakuacha pekeyako iwapo utaamua kuipiga. Iwapo unakila

kinachoihusisha Iraq na mashambulizi ya Septemba 11, basi tukielezee na

tuwatwange wakati unaotakiwa, lakini kwa sasa tuishughulikie Afghanistan kwanza”.

“Tukifanya hivyo, tutakuwa tumeongeza uwezo wetu wa kuifuata Iraq iwapo

tunaweza kuthibitisha kwamba Iraq ilishiliki katika mashambulizi hayo”. Bush

alikuwa na dhamira kubwa kuhusu kuitwanga Iraq, lakini aliyaacha mazungumzo

kuhusu suala hilo yaendelee. Alikuwa anahangaishwa na masuala mawili, aliyosema

baadaye. “Nadharia yangu nikwamba ni lazima tufanye jambo fulani na tulifanye

vyema kiasi kwamba tukithibitisha kuwa tutafanikiwa (nchini Afghanistan), basi

sehemu ya jukumu jingine itakuwa nyepesi zaidi, Tukijaribu kufanya mambo

mengineyo mawili kwa mfano: kijeshi, kutozingatia matokeo yake kutakua nijambo

lenye hatari kubwa.” Wasiwasi mwingine wa Bush ulikuwa ni ule ambao

haukuelezwa kwenye baraza lake la vita lakini baadaye alikuja kusema kwamba

ulikuwa ni kutokana na fikra zake. Alifahamu kwamba katika meza ya mazungumzo

kulikuwa na washauri Powell, Cheney na Wolfowitz ambao walikuwa pamoja na

baba yake wakati wa mazungumzo ya vita vya Ghuba.

“Na moja ya mambo haya ambayo sikutaka litokee ni kwamba hatukutaka ujuzi wao

wa nyumba katika mazingira ya sasa yatie shinikizo katika mkondo wa vita vipya.”

Katika maneno mengine, hakutaka wavitumie vita dhidi ya ugaidi kama kisingizio

cha kumaliza mgogoro wa zamani. Wakonge wa vita vya ghuba, ambao moja kwa

moja walikuwa ni Powell na Cheney walishangazwa na jinsi hali ya kijeshi nchini

Afghanistani iliyokuwa inajitokeza tofauti na lile shambulio la Desert storm

Jumamosi tarehe 4 Agost 1990.

Katika jeshi hilo huko Camp David, Jeneral Norman Schwarzkopf,wakati huo

akiwa kamanda mkuu wa kijeshi wa mamlaka kuu ya kijeshi alikuwa ametoa mpango

mrefu wa mapendekezo ya hatua za kijeshi ambayo alikujanayo mwenyewe.

Pendekezo hilo liliitwa(Mpango wa Operetion 1990—2002) na ndio ulikuwa

mpango mkuu wa kijeshi ambao ungechukuliwa katika muda wa miezi saba ambao

ungefuata kuliondoa jeshi la Iraq kutoka Kuwet. Sasa hapakuwa na mpango wa aina

hiyo, Hivi sasa palihitajika mpango wa haraka kutoka mwanzo kabisa mara tu baada

ya rais kuamua aina ya vita yenyewe, nadhari ya kwanza ya kampeni na uhusiano

kati ya CIA na Pentagon. Kuna wakati mtu mmoja alisema kwamba, hali hii

isingekuwa sawa na maeneo ya Balkan ambako chuki ya kikabila ilikuwa imeujaa

utawala wa Clinton kwa karibu miaka minane. Tungependa hali hii ingekuwa kama

ile ya Balkan, Rice alisema,

Masuala ya Afghanistan na maeneo ya jirani yake yalikuwa ni yenye kutatiza,

alitazama ramani na kufikili, Afghastani iliibua kila aina ya mandhari mbaya; Nchi

iliyo mbali, yenye mawe, miti mingi , ile isiyo na pwani. Bushi alisema kwamba

matokeo halisi ya kampeni hii yangekuwa ni kuwafukuzilia mbali magaidi kutoka

79


katika sehemu kama Afghastani na kufanya hivyo ni kuziomba nchi nyingine

ambazo zilikuwa zinaunga mkono ugaidi katika siku za nyuma kama vile Iraq

kubadili tabia yake. Powell alisisitiza kwamba kila mtu aliyekuwa katika ushilika wa

kimataifa alikuwa tayari kuwasaka Al Qaida, laki kutaka msako huo uenezwe katika

makundi mengine ya kigaidi au nchi nyingine kungezifanya baadhi ya nchi kutoafiki

jambo hilo. Rais alisema kwamba hakutaka nchi nyingine ziweke shinikizo au

masharti kuhusu vita dhidi ya ugaidi. Katika mambo mengine Powell alisema,

“tutajikuta tumebaki peke yetu”

Hilo ni sawa tu kwangu “Sisi ni Amerika” Powell hakujibu. Kuchukua jukumu hilo

kipekee ndicho kitu ambacho hasa alitaka kukikwepa iwapo ingewezekana. Alifikiri

kwamba mipangilio ya rais haikuzingatia halihalisi. Bila ya washirika Marekani

isingeweza kuanzisha vita thabiti hata nchini Afghanistan mbali na vita duniani

kote. Aliamini kuwa rais alitoa kauli hiyo akijua kwamba wasingeweza kuhimili

kufanya uchunguzi mara yapili. Maneno makali yalikuwa ni lazima, lakini

yasichanganywe na sera za nchi. Kinyume chake, Cheney aliyapokea maneno ya

Bush. Aliamini kwamba rais alikuwa amedhamiria aliposema kwamba Marekani

ingeendesha vita hivyo peke yake iwapo ingekuwa lazima. Rumsfeld alizungumzia

tatizo jingine, “japokuwa kila mtu alikubali kuwangamiza Al Qaeda lilikuwa jukumu

la kwanza, maneno yoyote yakumtaja Bin Laden yangempa umaarufu kama

alivyokuwa Rais Sadaam Hussein wa Iraq wakati wa vita vya Ghuba”.

Alisema kwamba jambo baya zaidi ambalo wangeweza kulifanya katika hali kama

hii ilikuwa ni kulitaja vibaya lengo lao. Isingeleta matokeo yoyote ya maana katika

kumwondoa au kumuua Bin Laden au kiongozi wa Taliba Mohammad Omar, bila

yakutatua sababu ya msingi ya ugaidi. Kumshutumu Bin Laden kungeinyima

Marekani uwezo wake wa kudai kwamba hii ilikuwa vita kubwa zaidi. Katika

maneno mengine alama ya “Bin Laden” ambayo ilikuwa katika ukurasa wa maelezo

ya CIA ilikuwa haifai na ilipaswa isirudiwe tena hadharani. Bush aliangalia kwa

nyuma yake juu ukutani, palipokuwa na saa na kisha kuwaeleza wajumbe wake kuwa

azimio la msingi wanaloondoka nalo ni kuibomoa Iraq lakini hawezi kuungwa

mkono bila kutumia mwavuli kwa Afghanistan. Wakongwe wa vita na wahafidhina

wote katika Baraza la Vita walisimama nakupiga makofi wakiwa na nyoyo kunjufu

huku wakiacha pembeni kabisa tafsiri ya vita dhidi ya ugaidi.
 
Back
Top Bottom