Ile simu kali aina ya iPHONE aliyopoteza kijana mdogo injinia wa apple Powel imerudishwa Apple baada ya kuokotwa katika bar ailiyokuwa akilamba lager kijana huyo. Simu hiyo ambayo ilikuwa bado katiika majaribio inasadikika kuwa itakuwa kiboko kingine kutoka Apple-mabingwa wa elektroniki wanaoendelea kutesa mitaani ni kifaa chao hatari cha iPAD! Simu hiyo iliripotishwa katika mtandao maarufu wa gizmodo, nao walimaindi apple waandike barua rasmi ya kuiomba simu hiyo, mzee mzima Bruce alifanya hivyo, na hivyo kuwahakikishia wananchi kuwa hicho kifaa walichokizindua kabla ya muda kuwa ni next iphone haswaa. Haijajulikana mpaka sasa kama Mzee mzima Steve atamuadabisha dogo huyo kwa uzmembe ama la. Kituko hiki kimekuja siku chache baada ya picha za smartphone ijayo kutoka dell kulick mtandaoni kutokea China.
sielewi kwa nn Iphne ina publicity sana. nadhani wana wataalamu wazuri sana wa marketting. Hata hii story ya dogo kupoteza future iphone inaweza kuwa ni njia nzuri ya kuwaweka wateja sawa.
Lakini techincally and features ukilinganisha Iphone na simu nyenza kama Nokia E71, HTC, Blackberry bold utaona Iphone inazidiwa vitu vya msingi au iko sawa na hizi nyingine.
Mfano wa features ni kama FM radio, Camera resolution , signal rececption kwenye majengo marefu au sehemu zisizo na mawasiliano mazuri , Taking time, Standby time nk.