Tengeneza mkakati leo kwa ufanisi wa biashara yako

The Consult

JF-Expert Member
Jan 20, 2017
220
252
teacher.png

Kuwa na mpango mkakati (strategic plan) katika biashara/kampuni yako ni jambo la msingi sana, hii hupelekea ufanisi na uhai mrefu wa biashara yako. Kwa mfano, katika makampuni 100 yenye mafanikio yaliyoorodheshwa na jarida la Forbes mwaka 1917 (Forbes 100) ni makapuni 3 tu yameweza kubaki sokoni mpaka dakika hii, hii ni kutokana na kuwa na mipango mkakati ambayo imeiwezesha makampuni haya kukabiliana na changamoto za kimasoko.

Tafiti pia zinaonyesha kwamba kampuni zinazojiendesha kimpango mkakati hufanya vizuri sokoni kuliko zile zisizojiendesha kimpango mkakati, hii hutokana na ubadilikaji wa mazingira katika soko pia ushindani katika biashara; ambao huongezeka kadiri siku zinavyozidi kwenda. Bain&Company mwaka 2007 walifanya mahojiano na watendaji wakuu 1,221 wa makampuni (global executives), 88% ya waliohojiwa walikiri kutumia na kutegemea mipango mkakati kama silaha (tool) katika uendeshaji wa kampuni zao.

Uandaaji wa mpango mkakati wa kampuni/biashara huweza kufanywa kwa njia (models) mbalimbali, lakini njia maarufu ni hii yenye kujumuisha hatua 4 zifuatazo;
  • Kufanya uangalifu yakinifu wa mazingira (environmental scanning) hapa unapaswa kufanya ufuatiliaji (monitoring) na utathmini (evaluation) wa visababishi (factors) vyenye kuathiri utendaji wa kampuni yako (internal factors), ambavyo hujumuisha; rasilimali, utamaduni wa kampuni, miundombinu n.k. Kisha utaangali visababishi vipatikanavyo nje ya kampuni yako vyenye kuathiri utendaji wa kampuni yako (external factors) ambavyo hujumuisha; washindani wako, hali ya kiuchumi, taratibu za kisheria, hali ya soko n.k. Kimsingi hali zote hizi huathiri ufanisi wa kampuni yako. Njia maarufu itumikayo kufanya zoezi hili huitwa SWOC/T Analysis
  • Uundaji wa mkakati (Srategic formulation), hapa utapaswa kuanza na kauli ya utume ya kampuni yako (mission statement), hii kauli itapaswa kuonyesha ni nini kampuni yako inafanya sasa (What's your organization now?). Baada kuwa na kauli ya utume, utapaswa kutengeneza malengo mahsusi (specific objectives), malengo haya yawe yametokana na (strategic issues) ulizoibua katika mchakato wa kwanza wa uangalifu yakinifu wa mazingira. Malengo yako mahsusi yanaweza yakagusa maeneo kama; ukuaji katika soko(market share/leadership), uongezekaji wa faida (profitability), ukuzaji wa hadhi ya kampuni (reputation), wajibu wa kampuni kwa jamii (taxes paid, participating in charities) n.k. Baada ya kuwa umetengeneza malengo yako; utapaswa kutengeneza mbinu (strategies) za kufikia hayo malengo (Utengenezaji wa mbinu utategemea na ngazi katika kampuni; ambazo ni corporate level, business level na functional level, hivyo kutapaswa kuwe na corporate strategy, business strategy na functional strategy). Baada ya kuwa na mbinu za kufikia malengo; utapaswa kutengeneza sera (policies) ambazo zitawaongoza wafanyakazi wa kampuni yako katika majukumu yao ili utekelezaji wa majukumu hayo umepelekee kufikia malengo ya mpango mkakati.
  • Utekelezaji wa mpango mkakati (Strategy implementation),mpango mkakati hutekelezwa kwa kutumia njia (tools) mbalimbali ambazo hujumuisha; programs/projects, malengo makubwa (overall objectives/goals) ya programs/projects hizi yatapaswa kurandana na malengo mahsusi ya mpango mkakati kama tulivyoyaona hapo juu. Pia bajeti ya kampuni hutumiwa kama chombo cha kutekelezea mpango mkakati wako.
  • Tathmini na udhibiti (Evaluation and control) hapa utapaswa kufanya ulinganifu kati ya matokeo baada ya utekelezaji wa mpango na malengo yaliyowekwa katika document ya mpango mkakati, ikiwa kutaonekana makosa katika utekelezaji; basi mashihisho yatapaswa kufanywa. Shughuli hii itapaswa kufanywa na mameneja wa ngazi zote za kampuni yako.
KUMBUKA: Mpango mkakati hushauriwa kuwa wa miaka 3 au 5 ili kuleta ufanisi kiutekelezaji.

The Consult; +255 (0) 719 518 367
Dar es Salaam
Tanzania

Kwa huduma za

  • Uandaaji wa michanganuo ya miradi (project proposals) na mipango mkakati (Strategic plans)
  • Utoaji wa mafunzo (trainings) na ushauri (consultancy) katika maeneo ya usimamizi wa miradi (Project management) na mipango mkakati (Strategic Management)
Karibu Sana
Your Success is My Desire
 
...

[*]Uundaji wa mkakati (Srategic formulation), hapa utapaswa kuanza na kauli ya utume ya kampuni yako (mission statement), hii kauli itapaswa kuonyesha ni nini kampuni yako inafanya sasa (What's your organization now?). Baada kuwa na kauli ya utume, utapaswa kutengeneza malengo mahsusi (specific objectives), malengo haya yawe yametokana na (strategic issues) ...

The Consult; +255 (0) 719 518 367
Dar es Salaam
Tanzania


Hongera kwa kurahisisha elimu ya 'Strategic Planning' (Mpango Mkakati) japo hugusia husiano wake na 'Project Management' (Usimamizi Mradi).

Makampuni yaliyofanikiwa kibiashara yameoanisha faida za 'Strategic Planning' na 'Project Management'.

Haitoshelezi tu kuwa na Mpango Mkakati kama malengo mahsusi (strategic objejectives) hayatafsiriwi katika dhana ya mradi (converting them into projects).

Uzoefu ni muhimu kuliko kuishi kinadharia.
 
Haya mambo yako vyuoni huko na kwenye consultation industry.

Mabadiriko ya haraka na makubwa yanayotokea kwenye tasnia ya teknologia ya mawasiliano yanatoa challenge kubwa sana kwenye dhana nzima ya strategic planning.

Umuhimu wake uko overrated in literatures.
 
Unakuaje na mission bila vision??..nafikiri baada ya kubaini mission unatakiwa pia kutengeneza vision itakayopelekea kufikia mission yake..ukishamaliza hapo there comes strategic objectives kama ulivyobainisha..ni mtazamo wangu tu..lkn targets ni muhimu pia otherwise utakua na mkakati usio na shabaha ikiwa strategic objectives zako hazina targets
 
Haya mambo yako vyuoni huko na kwenye consultation industry.

Mabadiriko ya haraka na makubwa yanayotokea kwenye tasnia ya teknologia ya mawasiliano yanatoa challenge kubwa sana kwenye dhana nzima ya strategic planning.

Umuhimu wake uko overrated in literatures.
Mkuu
Ni kweli mabadiliko yatokeayo katika "Industry" ya technolojia na mawasiliano yanaleta changamoto katika SP.
Ni vyema ikafahamika kwamba STRATEGY maana yake ni namna taasisi au kampuni inafanya maamuzi juu ya matumizi ya rasilimali zake (resource utilization) kwa lengo la kujihakikishia utendaji mzuri (good performance) na hatimaye kuwa na sifa ya kiushindani (competitive advantage) dhidi ya washindani wake ndani ya soko/"industry".

Hivyo kwa maana hii bado mabadiliko ya teknolojia na mawasiliano hayafanyi kampuni zikakosa kuwa na SPs. Na hapa ndipo huja kukuta kuna INTENDED na EMERGENT STRATEGY, aina hizi mbili hutokana na hali ya mabadiliko katika mazingira ikiwemo TEKNOLOJIA YA MAWASILIANO n.k,

Kitu cha muhimu katika mazingira-badilika kampuni au taasisi inapo-andaa SP, ni vyema ikazingatia mambo 4;
Mosi; Kipi ambacho mabadiliko ya kimazingira yanahitaji?
Pili: Kipi kampuni inapaswa kutoa kuitikia mabadiliko hayo?
Tatu; Kipi ambacho kampuni inahitaji kwa hakika (real need)
Nne; Kipi ambacho mazingira itatoa kwa kampuni.

Karibu Mkuu.
 


Hongera kwa kurahisisha elimu ya 'Strategic Planning' (Mpango Mkakati) japo hugusia husiano wake na 'Project Management' (Usimamizi Mradi).

Makampuni yaliyofanikiwa kibiashara yameoanisha faida za 'Strategic Planning' na 'Project Management'.

Haitoshelezi tu kuwa na Mpango Mkakati kama malengo mahsusi (strategic objejectives) hayatafsiriwi katika dhana ya mradi (converting them into projects).

Uzoefu ni muhimu kuliko kuishi kinadharia.
Mkuu
Nakubaliana nawe kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya SP na PROJECT/PROGRAM.
Kwa maana ya kwamba SP inakuwa realized kupitia PROJECTS na PROGRAMS zinazotekelezwa na taasisi husika.

Na ndio maana katika andiko langu; hususani katika hatua ya IMPLEMENTATION nimetambua PROJECTS/PROGRAMS kama tools kwa ajili ya kutekeleza SP

Ahsante kwa mchango wako Mkuu.
 
Unakuaje na mission bila vision??..nafikiri baada ya kubaini mission unatakiwa pia kutengeneza vision itakayopelekea kufikia mission yake..ukishamaliza hapo there comes strategic objectives kama ulivyobainisha..ni mtazamo wangu tu..lkn targets ni muhimu pia otherwise utakua na mkakati usio na shabaha ikiwa strategic objectives zako hazina targets
Uko vyema Mkuu.
Dhima na Uono katika taasisi au kampuni hutoa muelekeo na namna ya kuelekea.

Shukrani kwa mchango wako Mkuu.
 
Naomba mawasiliano ya huyo mdada kwenye hiyo picha..nina jambo la business nataka anishauri
 
The Consult...napenda na kuadmire Consulting yako...nami nahisi kupitia article zako naboresha sana ufahamu Wangu and much better my skills ...I like Consulting services...I am surely trying since 2011:
 
The Consult...napenda na kuadmire Consulting yako...nami nahisi kupitia article zako naboresha sana ufahamu Wangu and much better my skills ...I like Consulting services...I am surely trying since 2011:
Mkuu IPILIMO
Nashkuru sana kwa remark yako.
Consultancy inamtaka mtu kila siku kujifunza jambo jipya.
Vile ujifunzavyo kupitia kwangu, nami nina mengi nahitaji kujifunza kutoka kwako.
May Almighty God Bless Our Esfuerzo/Endeavor
 
teacher.png

Kuwa na mpango mkakati (strategic plan) katika biashara/kampuni yako ni jambo la msingi sana, hii hupelekea ufanisi na uhai mrefu wa biashara yako. Kwa mfano, katika makampuni 100 yenye mafanikio yaliyoorodheshwa na jarida la Forbes mwaka 1917 (Forbes 100) ni makapuni 3 tu yameweza kubaki sokoni mpaka dakika hii, hii ni kutokana na kuwa na mipango mkakati ambayo imeiwezesha makampuni haya kukabiliana na changamoto za kimasoko.

Tafiti pia zinaonyesha kwamba kampuni zinazojiendesha kimpango mkakati hufanya vizuri sokoni kuliko zile zisizojiendesha kimpango mkakati, hii hutokana na ubadilikaji wa mazingira katika soko pia ushindani katika biashara; ambao huongezeka kadiri siku zinavyozidi kwenda. Bain&Company mwaka 2007 walifanya mahojiano na watendaji wakuu 1,221 wa makampuni (global executives), 88% ya waliohojiwa walikiri kutumia na kutegemea mipango mkakati kama silaha (tool) katika uendeshaji wa kampuni zao.

Uandaaji wa mpango mkakati wa kampuni/biashara huweza kufanywa kwa njia (models) mbalimbali, lakini njia maarufu ni hii yenye kujumuisha hatua 4 zifuatazo;
  • Kufanya uangalifu yakinifu wa mazingira (environmental scanning) hapa unapaswa kufanya ufuatiliaji (monitoring) na utathmini (evaluation) wa visababishi (factors) vyenye kuathiri utendaji wa kampuni yako (internal factors), ambavyo hujumuisha; rasilimali, utamaduni wa kampuni, miundombinu n.k. Kisha utaangali visababishi vipatikanavyo nje ya kampuni yako vyenye kuathiri utendaji wa kampuni yako (external factors) ambavyo hujumuisha; washindani wako, hali ya kiuchumi, taratibu za kisheria, hali ya soko n.k. Kimsingi hali zote hizi huathiri ufanisi wa kampuni yako. Njia maarufu itumikayo kufanya zoezi hili huitwa SWOC/T Analysis
  • Uundaji wa mkakati (Srategic formulation), hapa utapaswa kuanza na kauli ya utume ya kampuni yako (mission statement), hii kauli itapaswa kuonyesha ni nini kampuni yako inafanya sasa (What's your organization now?). Baada kuwa na kauli ya utume, utapaswa kutengeneza malengo mahsusi (specific objectives), malengo haya yawe yametokana na (strategic issues) ulizoibua katika mchakato wa kwanza wa uangalifu yakinifu wa mazingira. Malengo yako mahsusi yanaweza yakagusa maeneo kama; ukuaji katika soko(market share/leadership), uongezekaji wa faida (profitability), ukuzaji wa hadhi ya kampuni (reputation), wajibu wa kampuni kwa jamii (taxes paid, participating in charities) n.k. Baada ya kuwa umetengeneza malengo yako; utapaswa kutengeneza mbinu (strategies) za kufikia hayo malengo (Utengenezaji wa mbinu utategemea na ngazi katika kampuni; ambazo ni corporate level, business level na functional level, hivyo kutapaswa kuwe na corporate strategy, business strategy na functional strategy). Baada ya kuwa na mbinu za kufikia malengo; utapaswa kutengeneza sera (policies) ambazo zitawaongoza wafanyakazi wa kampuni yako katika majukumu yao ili utekelezaji wa majukumu hayo umepelekee kufikia malengo ya mpango mkakati.
  • Utekelezaji wa mpango mkakati (Strategy implementation),mpango mkakati hutekelezwa kwa kutumia njia (tools) mbalimbali ambazo hujumuisha; programs/projects, malengo makubwa (overall objectives/goals) ya programs/projects hizi yatapaswa kurandana na malengo mahsusi ya mpango mkakati kama tulivyoyaona hapo juu. Pia bajeti ya kampuni hutumiwa kama chombo cha kutekelezea mpango mkakati wako.
  • Tathmini na udhibiti (Evaluation and control) hapa utapaswa kufanya ulinganifu kati ya matokeo baada ya utekelezaji wa mpango na malengo yaliyowekwa katika document ya mpango mkakati, ikiwa kutaonekana makosa katika utekelezaji; basi mashihisho yatapaswa kufanywa. Shughuli hii itapaswa kufanywa na mameneja wa ngazi zote za kampuni yako.
KUMBUKA: Mpango mkakati hushauriwa kuwa wa miaka 3 au 5 ili kuleta ufanisi kiutekelezaji.

The Consult; +255 (0) 719 518 367
Dar es Salaam
Tanzania

Kwa huduma za

  • Uandaaji wa michanganuo ya miradi (project proposals) na mipango mkakati (Strategic plans)
  • Utoaji wa mafunzo (trainings) na ushauri (consultancy) katika maeneo ya usimamizi wa miradi (Project management) na mipango mkakati (Strategic Management)
Karibu Sana
Your Success is My Desire
Thanks
 
2.jpg

Mikakati (strategies) katika kampuni/biashara imegawanyika katika sehemu kuu tatu, ambazo ni;
  • Corporate Strategies; hii ni mikakati ambayo hufanyika katika ngazi ya juu kabisa ya kampuni (corporate), mikakati hii hujumuisha Growth Strategy, Stability Strategy na Retrenchment Strategy.
  • Business Strategies; hii ni mikakati ambayo hufanyika katika ngazi ya biashara (business unit), mfano wa ngazi ya biashara ndani ya kampuni ya IPP ni; IPP Media, IPP Bodycare Ltd, IPP Resources, hivyo mkakati wowote chini ya hizi "business units" hujulikana kama " Business Strategies"
  • Functional Strategies; hii ni mikakati ambayo hufanyika katika ngazi ya chini kabisa ya kampuni, ngazi hii hujumuisha; Research & Development department, Marketing department, HR department n.k. Hivyo mkakati wowote chini ya hizi "functional areas" hujulikana kama functional strategies.
Kama kichwa cha habari kinavyojitambulisha hapo juu, ningelipenda kukazia juu ya "Retrenchment strategies" ambayo ni aina ya mikakati ifanyikayo katika ngazi ya juu kabisa ya kampuni.

Kampuni hufanya uamuzi wa kutekeleza aina hii ya mikakati kipindi ambacho kampuni husika ipo katika nafasi dhaifu ya kiushindani (weak competitive position) katika baadhi ya bidhaa "business units" zake au zote na hatimaye kuwa na ufanisi hafifu sokoni (poor performance) ambayo husababisha mauzo kushuka na hatimaye faida kupungua.
Hivyo katika hali kama hii, kampuni/biashara husika hupaswa kutumia "retreachment strategies" kwa lengo la kuongeza ufanisi na kukabiliana na madhaifu ambayo yanaweza kuiyumbisha kampuni husika.

"Retreachment strategies" hujumuisha;
  • Turnaround Strategy; mkakati huu hufanyika kipindi ambacho matatizo yanayoikumba kampuni husika hayajawa makubwa "critical". Mkakati huu hujumuisha " Contraction" ambacho ni kitendo cha kupunguza gharama za uendeshaji wa kampuni, pia kupunguza "size" ya kampuni husika, mara nyingi hili huendana na upunguzaji wa wafanyakazi (jobs elimination), kufunga baadhi ya vinu au vifaa vya uzalishaji (plants/facilities closing) n.k. Njia hii pia hujumuisha "Consolidation" ambacho ni kitendo cha kampuni kupunguza gharama zisizo za lazima (unnecessary overhead costs), kitendo hichi kisipofanyika kiungalifu huenda kikapoteza "best people" ndani ya kampuni.
  • Captive Company Strategy; kampuni ambayo iko katika nafasi dhaifu ya kiushindani (weak competitive position) inaweza isifanya "turnaround" kwa kiasi kikubwa kama tulivyoona hapo juu, ila ikaamua kuwa "captive company", hapa kampuni husika itapunguza/kuhamisha baadhi ya shughuli zake kama "marketing" n.k kwa kampuni nyingine yenye ufanisi sokoni kwa mkataba maalum , hivyo kampuni tekwa itapata asilimia fulani ya mauzo/faida ya shughuli iliyohamishwa kutoka kwa kampuni teka "captor" , kwa kufanya hivi, kampuni tekwa itakuwa imepunguza gharama za uendeshaji pia itaweza kujihahakikishia kubaki sokoni. Kwa mfano kipindi fulani kampuni ya Simpson Industries ya Birmigham iliingia mkataba na General Motors GM, ambapo GM walitoa timu maalum kwa ajili ya ukaguzi wa vifaa, utunzaji wa kumbukumbu na uajiri ndani ya kampuni ya Simpson Ind kwa makubaliano maalum.
  • Sell-out/ Divestment Strategy; ikiwa kampuni husika imeshindwa kufanya "captive company strategy" basi uongozi unaweza kufanya uamuzi wa kuiuza kampuni nzima (sell-out) au kuuza "business line/unit" ambayo haifanyi vizuri kwa kampuni nyingine (divestment).
  • Liquidation strategy; hii hutokea kipindi ambacho kampuni huwa katika hali mbaya zaidi kiushindani na imekosa mvuto wa kununulika. Katika hali hii uongozi wa kampuni husika utaamua kusitisha uwepo wa kampuni (company elimination), kisha "assets" zote za kampuni zitauzwa kisha kiasi cha pesa kitakachopatikana baada ya kulipia madeni ya kampuni kitagawiwa kwa wanahisa (shareholders).
Ahsante

Adverts

Africa Energy Ideas Competitions (Deadline 20th May ,17)

https://www2.fundsforngos.org/envir...ply-for-2017-africa-energy-ideas-competition/

Call for Capacity building & Institutional Development Projects (Deadline 30 May, 17)
https://www2.fundsforngos.org/envir...ply-for-2017-africa-energy-ideas-competition/


The Consult; +255 719 518 367
Dar es Salaam

Project Management, Strategic Management, Brand Management.

Choose It, Embrace It, Love It.
 
Back
Top Bottom