Teknolojia ni Yetu sote
JF-Expert Member
- Apr 28, 2020
- 1,221
- 2,425
Kampuni ya TECNO inayotoa matoleo mbalimbali ya simu za kisasa smartphone, imetangaza kuimarisha Uhusiano wake na shirikisho la Soka (CAF) kwa kuwa mshirika Rasmi wa kimataifa wa TotalEnergies CAF itayofanyika Morocco pamoja na Kenya, Uganda na Tanzania kwa Mwaka 2025 na 2027.
TECNO ilikuwa mdhamini wa kipekee wa simu za kisasa kwa mashindano ya CAF mwaka 2023, sasa yamerudi Tena kwa mwaka huu 2025.
Makamu wa Rais wa Transsion Holdings , Benjamin Jiang alisema " ushirikiano huu mpya ni uthibitisho wa uaminifu mkubwa na mafanikio ambayo TECNO wamejenga na CAF. Kupitia Ushirikiano wao wa awali uliweza kuonyesha jinsi mapinduzi ya Teknolojia zinavyoendeshwa na AI yanaunganisha mamilioni ya watu barani Afrika.
Ushirikiano baina ya TECNO na CAF ni hatua muhimu katika Maendeleo ya soka na teknolojia.