Nilitegemea hii TBC 2 ingekuwa bonge la burudani lakini wapi upuuzi mtupu,Hivi CAF si wanawapa haki au kulipia kiasi kidogo kuonyesha mashindano yao,TV station zote za Taifa!,sasa nini kiliwashinda hawa TBC?..
Kituo cha TBC2 kiliponzishwa nilidhani huko ndiko yatapatikana mambo motomoto kama mipira live, bunge live, nk ili kupisha TBC1 ushughulike na mambo mengine ya kitaifa. Hii imesababisha king'amuzi cha starTimes kupoteza mvuto hasa kwa vijana
Hata yakitokea mashindano ambayo kuna mtanzania anashiriki mfano juzi yule aliyeshinda huku india , lakini TBC 2 kuanzia asubuhi mpaka kukicha ni miziki tuu , sasa sijui iliundwa ya nini bora ibaki ile TBC 1 PEKE YAKE