Tatizo la watanzania si Katiba ya CCM

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
21,443
40,537
Pamoja na kukataza kuonesha Bunge Mubashara, leo tumeshuhudia kundi zima la walishadadia bunge kutokuoneshwa Mubashara wakiwa na bashasha kwa Mkutano wao Mkuu kuoneshwa Mubashara. Kwa maana nyingine wao wanaona vikao vya chama chao ni muhimu sana kuliko vikao vya Bunge letu ambalo linamuhusu kila mtanzania.

Lakini hicho walichotaka kioneshwe Mubashara si kitu au jambo la muhimu sana kwa watanzania wote. Chama cha siasa kubadili katiba yake ni mambo ya chama husika na kulifanya kama ni jambo la maana sana kwa nchi basi hao wenye mawazo hayo wana mawazo mufulisi!!

Mkwamo kwa nchi yetu hausababishwi na Katiba ya CCM ikoje, bali unatokana na Katiba ya nchi yetu ikoje. Katiba iliyotungwa katika mfumo kwamba nguzo zote za utawala zinawajibika kwa mtu mmoja tu Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania ndiyo inayotakiwa kubadilishwa na wala si ya chama cha siasa ambacho kinaweza kuondolewa madarakani kwenye uchaguzi wowote huru na wa haki.

Watanzania hawana ajira za uhakika, hawana masoko kwa mazao yao, hawana huduma za kuaminika za Afya, huduma za maji ni dhahama,Uchumi wa familia zao umeyumba, mambo mengi yameparaganyika, hata Katiba ya CCM ifutwe kabisa haitaathiri maisha yao bali kinachoathiri maisha yao ni Katiba ambayo pamoja na kuchukia baadhi ya mambo hawana cha kufanya kuyaondoa zaidi ya kusubiri "Rais aamue".
 
Lets be honest....Tatzo la TAIFA hili si KATIBA MPYA.....maana kama mnapata katiba mpya afu viongozi ni AINA YA HAO WANAONGOZA hapo UFIPA wanaoshindwa kusimamia hata hizo katiba za CHAMA ni vipi wataweza simamia KATIBA ya NCHI?????
Kila siku tunasema CDM ndio walitakiwa wawe mfano mzuri sana kupita CCM kwenye uendeshaji wa CHAMA CHAO KUPITIA katiba vilivyo bila kuwa na hata chembe chembe za kupindisha KATIBA.....na pia kuwa ni chama ambacho hakihusishwi na MAKANDO KANDO YA KIPUUZI kama vile ufisadi..ukwepaji kodi...MATUMIZI Mabaya ya ruzuku...kutokujali thamani ya WAFUASI wake wanaokipigani CHAMA mfano BEN....SERIOUS wangekuwa vizuri kwenye haya UHITAJI WA KATIBA mpya tungeupigia KELELE IPASAVYO maana MAFUNDI wa kusimamia KATIBA tumepata.......LAKINI sasa mpaka sasa hao WANOTAKA katiba mpya YA KWAO TU NDANI YA CHAMA imewashinda kuisimamia YA nchi MTAWEZA vipi?????ebu msitudanganye hii ya kulilia KATIBA mpya kila siku ni kujificha kwenye kichaka cha kufuja MALI ZA CHAMA.....
NI UPUUZI KUWAAMINI HAWA NDIMI MBILI.....
Ukweli mchungu siku ikaja tokea na sijui ni lini CDM mkashika nchi hii ndani ya miezi miwili tu WATANZANIA watapiga miano na kusema mara mia CCM.....UNLESS OTHERWISE SI HIKI KIZAZI CHA UONGOZI ULIOPO HAPO UFIPA.......
 
Kwa mtazamo wangu inabidi tupitie upya sheria nyingi za nchi hii, mpaka hivi sasa bado tuna sheria nyingi zingine zilitungwa na mkoloni kwaajili ya mkoloni na nyingine zilibadilishwa lakini haziemdani na dunia ya mawasiliano huru. Sheria za mirathi, sheria za umiliki wa ardhi, sheria za watoto na haki ya kila raia hizi na zingine nyingi lazima zifanyiwe "complete overhaul". Tutaletewa katiba mpya na masheria yakawa haya haya, tutajikuta tuna katiba mpya inayo wapendezesha watawala kuliko wananchi kwa ujumla.
 
Back
Top Bottom