Tatizo la siasa za Tanzania

Tatizo la siasa za Tanzania

mayange

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2013
Posts
701
Reaction score
198
Ndugu wana Jf,

ni ukweli usiopingika kwamba wapenzi na wafuatiliaji wa siasa hapa tanzania mawazo yao walio wengi yamekuwa yakifuata upepo kulingana na mazingira yaliyojitokeza. Hili linamaanisha kuwa watu wamekuwa watumwa wa mawazo (fikra). Haya yote nayasema kwa sababu nimekuwa nikiona hata humu jf watu wana comment kulingana upepo wa siku hiyo ila kesho wanabadili mawazo kwasababu nani kaongea.

Wengi wanachama wa chadema tumekuwa na mapenzi makubwa sana na baadhi ya viongozi wetu wa kitaifa na kudhani kwamba wao hawakosei, na ikitokea mtu akaja na hoja tofauti za kukosoa viongozi wetu basi huyo ataonekana ni wa ccm mwenye nia mbaya na chadema. Ila ikumbukwe kwamba hata hawa viongozi ni binadamu wanamakosa yao ambayo yanahitaji ushauri.

Ninaimani hata wajumbe wa kamati kuu wapo watu wa namna hii wa kuangali hiki kimesemwa na nani nikubali hata kama ni uongo au nikatae hata kama ni ukweli. Ukweli wa haya ni pale kwenye kikao cha tarehe 22 kulikuwa na pande mbili zinazokinzana.

kuhusu swala la zitto na kitila akitoke mtu wa kuwa na mawazo tofauti na walio wengi ya kumtetea zitto ataonekana mwana ccm sasa uhuru wa mawazo uko wapi?

watu wamekuwa wakimuandama zitto kabwe kuwa ni msaliti na kumuonyeshea chuki hadharani tena bila ushahidi ila sijawahi kusikia kupitia vikao vya chama hawa watu wameshugulikiwa, mfano Lema kamchafua zitto kuwa anakataa posho huku akila rushwa kuto ccm kaambiwa alete ushahidi hana sasa na huu tuuite usalti?.

kuna viongizi walishiriki kusambaza ripoti ya siri ya zitto na baada ya kuoneka ni ya uongo mbona kwenye kikao hawakushugulikiwa? Au zitto hakuwa kiongozi anayechafiliwa? Au anayechafuka ni mbowe na slaa tu?.

Makundi nani ya chama ni kitu cha kawaida sana na ule mkakati ulikwa wa kujiimali kwa watakaokuwa wapinzani wao, sasa mlitegemea waanze kuwasifia kama si kuainisha mapungufu ya watakaokuwa wapinzani wao?.

kama baada ya kugundua mkakati huo mkaona si vyema mbona hamjachukua jukumu la kuwaita na kuwakanya huko huko bila ya kuleta mazara kwa wananchi kama yanayotokea huko kigoma, rukwa, tabora na shinyanga pamoja na kuleta sintofahamu kwa wananchi nchi nzima?

hata kama tatizo ni huo waraka mbona ulikuwa haujamfikia zitto na kutoa maoni yake? Kama alilengwa ila hajui sasa tatizo liko wapi au kuna mengine yaliyojificha?

Naheshimu busara za zitto alizoonyesha akiwa na kitila. Chama kimeona sasa ni kazi yenu kurudisha imani kwa wanachama walioguswa na hili mfano wanaoendelea kunguza kadi na kubomoa mashina ya chadema.

Msigwa nakuheshimu hufanani na mipasho kama kweli unaona mwenzio kakosea mshauli na sio mjungu utaendelea kubomoa kwa wale wanaomini unachokiongea.
Kwa mwanachama wa kweli hawezi kushabikia majungu huku chama kinatekea.
 
Umetumwa kumfagilia Zitto? CDM haina tatizo na Zitto isipokuwa undumilakuwili wake! Hao unaowasema wanachoma kadi za CDM muulize Mwigulu Nchemba atakuambia wanaratibiwa na nani!
 
Suala la uwajibikaji ni lazima liwe la kipaumbele sana ,juu ya watu AMA mtu anayekuwa kinyume na misingi ya Chama,pasipo kujari,ushawishi wake, jina ,cheo wala pesa,hata hapa binafsi naona ni uamuzi sahihi sana KAMA KWELI Zito na wenzake wamekiuka utaratibu wa Chama.

Sio kweli kuwa vijana wengi wameingia CHADEMA kutokana na ushawishi wa Zito Kama inavyofikiliwa na kuenezwa na wachangiaji wengi wa jukwaa hili,Washawishi ndani ya ChADEMA ni wengi sana na wanafanya ushawishi kweli kweli Zito pia ni miongoni mwa hao,ambao wengi wao hata hawana majina makubwa,na wengi wao hata si wana chama kabisa bali ni wapenda maendeleo hivyo wanaamini katika mabadiliko.Binafsi na wengine wengi hatukushawishiwa na Zito, Bali kilichotushawishi ni Matumaini hasa kutokana na sera,utendaji,mikakati na maono ya mbele juu ya chama kwa Tanzania yetu.

Ifahamike wazi kuwa Migogoro ndani ya chama AMA taasisi yoyote ni lazima itokee maana kumbuka Hilo ni kusanyiko la watu wengi wenye mitazamo tofauti tofauti, na kila mmoja anataka asikike kwa kile anachokifikiria hilo haliepukiki,lakini suruhisho la migogoro ni Kama Hicho kilichotokea kwa ZZK na wenzake hii inaonesha wazi kuwa ndani ya Chama kuna uwajibikaji na wala haionyeshi kuwa Chama ni kichanga ama kidogo kama inavyofikiliwa na wengi

Democrasia,kamwe haihusishi njia ya Mazungumzo kama wengine wanavyofikilia kwamba suala la Zito ndani ya chadema , uongozi ulitakiwa kukaa na Zito na kusuruhisha (huu ungekuwa ni uamuzi wa kujenga wafalme wachache ndani ya Chama cha watu wengi),diplomasia ndio inahusisha mazungumzo juu ya usuruhishi wa jambo.Hapa ni power of the people,panapo jambo watu tunataraji vitendo na sio hadithi,Hasa Kama situation inapelekea kuvuruga Chama .

Suala la udini,Pesa na u kanda (hapa sina cha kuongea maana sijui kuhusiana na hayo na sijui yanafanyaje kazi ktk chama),ila kama yapo na yana kasoro katika uendeahaji wa Chama ,basi wahusika wamesikia mitazamo na ushauri wa watu wengi natumai watachukua hatua katika hayo

Tunapoingia katika kujadili ni vyema tukashiliki kujadili uhalisia wa jambo na si Hisia juu ya Jambo hii itatupeleka moja kwa moja katika suruhisho juu ya jambo, either Kama limetendeka kwa usahihi ama kimakosa.

Hivyo ndivyo utaratibu wa siasa ,na sio tatizo la siasa ya Tanzania Kama unavyoisingizia.
 
wanaoingia CDM huenda ni kwa kuichoka CCM
 
Suala la uwajibikaji ni lazima liwe la kipaumbele sana ,juu ya watu AMA mtu anayekuwa kinyume na misingi ya Chama,pasipo kujari,ushawishi wake, jina ,cheo wala pesa,hata hapa binafsi naona ni uamuzi sahihi sana KAMA KWELI Zito na wenzake wamekiuka utaratibu wa Chama.

Sio kweli kuwa vijana wengi wameingia CHADEMA kutokana na ushawishi wa Zito Kama inavyofikiliwa na kuenezwa na wachangiaji wengi wa jukwaa hili,Washawishi ndani ya ChADEMA ni wengi sana na wanafanya ushawishi kweli kweli Zito pia ni miongoni mwa hao,ambao wengi wao hata hawana majina makubwa,na wengi wao hata si wana chama kabisa bali ni wapenda maendeleo hivyo wanaamini katika mabadiliko.Binafsi na wengine wengi hatukushawishiwa na Zito, Bali kilichotushawishi ni Matumaini hasa kutokana na sera,utendaji,mikakati na maono ya mbele juu ya chama kwa Tanzania yetu.

Ifahamike wazi kuwa Migogoro ndani ya chama AMA taasisi yoyote ni lazima itokee maana kumbuka Hilo ni kusanyiko la watu wengi wenye mitazamo tofauti tofauti, na kila mmoja anataka asikike kwa kile anachokifikiria hilo haliepukiki,lakini suruhisho la migogoro ni Kama Hicho kilichotokea kwa ZZK na wenzake hii inaonesha wazi kuwa ndani ya Chama kuna uwajibikaji na wala haionyeshi kuwa Chama ni kichanga ama kidogo kama inavyofikiliwa na wengi

Democrasia,kamwe haihusishi njia ya Mazungumzo kama wengine wanavyofikilia kwamba suala la Zito ndani ya chadema , uongozi ulitakiwa kukaa na Zito na kusuruhisha (huu ungekuwa ni uamuzi wa kujenga wafalme wachache ndani ya Chama cha watu wengi),diplomasia ndio inahusisha mazungumzo juu ya usuruhishi wa jambo.Hapa ni power of the people,panapo jambo watu tunataraji vitendo na sio hadithi,Hasa Kama situation inapelekea kuvuruga Chama .

Suala la udini,Pesa na u kanda (hapa sina cha kuongea maana sijui kuhusiana na hayo na sijui yanafanyaje kazi ktk chama),ila kama yapo na yana kasoro katika uendeahaji wa Chama ,basi wahusika wamesikia mitazamo na ushauri wa watu wengi natumai watachukua hatua katika hayo

Tunapoingia katika kujadili ni vyema tukashiliki kujadili uhalisia wa jambo na si Hisia juu ya Jambo hii itatupeleka moja kwa moja katika suruhisho juu ya jambo, either Kama limetendeka kwa usahihi ama kimakosa.

Hivyo ndivyo utaratibu wa siasa ,na sio tatizo la siasa ya Tanzania Kama unavyoisingizia.

umenena mkuu ila vipi kuhusu lema kumchafua zitto nae kashugulikiwa?
 
Back
Top Bottom