Tanzania bado tuko nyuma sana katika mambo ya muhimu kama elimu,afya na technologia... kuweka nguvu nyingi kuhamasisha nchi ya viwanda naisi si wakati sahihi kufanya ilo,,,, bado tunatakiwa kuimarisha elimu, sekta ya afya na kukuza nchi katika technologia na ubunifu apo tutakuwa kwenye nafasi nzuri ya kuwa nchi ya viwanda kwa nguvu zetu wenyewe bila kutegemea wawekezaji kutoka nje. Kwa wakati huuu kama nchi hatuna technologia na watu wenye uzoefu wa kuviendesha ivyo viwanda,,, the only option itakuwa kuzinunua kwa garama ya juu na kuajiri watu wenye uzoefu kutoka nje na kuwalipa garama kubwa ili waweze endesha ivyo viwanda. Pili dunia sasaivi imekuwa kama kijiji ... competition ni kubwa sana,, je tuna uakika vitu tutakavyo zalisha apa nchi vitaweza kushindana na bidhaa kutoka mataifa mengine yenye uzoefu na technologia ya hali ya juu. Mwisho wa siku ivi viwanda vitakufa na tutakuwa tumetumia pesa nyingi ambazo tungewekeza kwenye elimu afya na ukuaji wa technologia baada ya miaka kadhaa tungekuwa kwenya nafasi nzuri ya kuviendesha ivi viwanda kwa garama nafuu .
Kwa sasa serikali inachoweza kufanya ni kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na uzalishaji,,,,, kupunguza kodi za viwanda ili kuwashawishi wenye viwanda kuhamishia production zao tanzania.,,, kama wakipiga mahesabu na kuona uzalishaji ukifanyika tanzania unakuwa wa garama nafuu watakuja tu kujenga ivyo viwanda. Apo kama nchi tutafaidika kwa kuwapatia ajira vijana wengi wanaolalamika kila siku kukosa ajira na pili serikali itapata kodi kutoka kwa waajiriwa,,, pili tutapata nafasi ya kupata uzoefu na kujifunza technologia mbali mbali zinazotumika katika uzalishaji . Baada ya miaka kadhaa tutakuwa kwenya nafasi nzuri ya kuwa nchi ya viwanda . The only way ya kuwa nchi ya viwanda kwa sasa ni kuweka mazingira mzuri ya wawekezaji., ambapo ni kwa kumake sure production cost zao zinakuwa chini ili kuwavutia kuja.