Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 14,176
- 25,919
Imefikia mahali ambapo viongozi wa upinzani, viongozi wa kidini, taasisi za kijamii za ndani na nje, ofisi za ubalozi, watu binafsi mmoja mmoja au kama vikundi, nk, wakatamka jambo lolote kama mashauri au kukosoa kuhusu mustakabali wa uongozi nchini Tanzania wenye kuboresha haki, uongozi bira na usawa, jibu la viongozi wetu ni moja tu "tutawashughulikia kwa nguvu zote wanaotaka kuvunja amani yetu"
Tangu lini mapendekezo ya kuboresha utawala bora na haki na usawa katika taratibu za uchaguzi vikawa ni tishio kwa amani ya nchini, isipokuwa kwa mtu au chama cha Makaburu weusi nchini?
Na ni mtu mpumbavu tu ndani ya Tanzania ambae hadi sasa hataelewa kwamba pendekezo la badiliko lolote lenye kuleta usawa ambalo litaonekana ni tishio la kuleta ukosefu wa amani nchini! Hata kuwakosoa viongozi wa nchi siku hizi wanapoendesha nchi hii kinyume cha asili ni kutishia amani ya nchi.
Tumefikia mahali tuna Makaburu weusi ndani ya Tanzania, ambao kama ilivyokuwa kwa Afrika Kusini, wananchi kudai uboreshaji wa demokrasia na usawa imekuwa ni kutishia amani ya nchi,. Na kama ilivyokuwa Afrika Kusini, watu wanauwawa ndani ya Tanzania au kufungwa jela kwa ajili ya hilo. Makaburu walimfunga jela Mandela kwa miaka 27 kwa kudai tu mabadiliko ya katika ya Afrika Kusini ili kuleta usawa kwa kila mtu. Leo hii makaburu wa Kitanzania wanaofanana na wale wa Afrika Kusini ni hawa watu wanaojiita viongozi wetu, hususa ndani ya CCM, ambapo pia wako tayari kuwafunga jela na hata kuwaua wananchi wanaodai turekebishe mifumo ya usawa ndani ya nchi yetu kwa faida yetu wenyewe.
Wewe kama Mtanzania mwenye kuona mbele, unafikiri tunaelekea wapi kama nchi? Kama tuliwasaidia Afrika Kusini, Angola, Msumbiji, Namibia, Zimbabwe nk kuondokana na Makaburu waonezi na wauaji, wakandamizaji waovu wa demokrasia wenye mikono iliyajaa damu, na kuwa tayari kupambana vita ya ukombozi, kwa nini tunashindwa kujisaidia wenyewe ndani ya Tanzania? Kwa nini tuliyachukia yaliyofanywa na Makaburu wa Afrika Kusini kwa Waafrika Kusini, na tukajitoa muhanga kuwasaidia, lakini leo tunashindwa kuwaondoa Makaburu weusi wa ndani ya Tanzania, kwa ajili yetu wenyewe?
Tangu lini mapendekezo ya kuboresha utawala bora na haki na usawa katika taratibu za uchaguzi vikawa ni tishio kwa amani ya nchini, isipokuwa kwa mtu au chama cha Makaburu weusi nchini?
Na ni mtu mpumbavu tu ndani ya Tanzania ambae hadi sasa hataelewa kwamba pendekezo la badiliko lolote lenye kuleta usawa ambalo litaonekana ni tishio la kuleta ukosefu wa amani nchini! Hata kuwakosoa viongozi wa nchi siku hizi wanapoendesha nchi hii kinyume cha asili ni kutishia amani ya nchi.
Tumefikia mahali tuna Makaburu weusi ndani ya Tanzania, ambao kama ilivyokuwa kwa Afrika Kusini, wananchi kudai uboreshaji wa demokrasia na usawa imekuwa ni kutishia amani ya nchi,. Na kama ilivyokuwa Afrika Kusini, watu wanauwawa ndani ya Tanzania au kufungwa jela kwa ajili ya hilo. Makaburu walimfunga jela Mandela kwa miaka 27 kwa kudai tu mabadiliko ya katika ya Afrika Kusini ili kuleta usawa kwa kila mtu. Leo hii makaburu wa Kitanzania wanaofanana na wale wa Afrika Kusini ni hawa watu wanaojiita viongozi wetu, hususa ndani ya CCM, ambapo pia wako tayari kuwafunga jela na hata kuwaua wananchi wanaodai turekebishe mifumo ya usawa ndani ya nchi yetu kwa faida yetu wenyewe.
Wewe kama Mtanzania mwenye kuona mbele, unafikiri tunaelekea wapi kama nchi? Kama tuliwasaidia Afrika Kusini, Angola, Msumbiji, Namibia, Zimbabwe nk kuondokana na Makaburu waonezi na wauaji, wakandamizaji waovu wa demokrasia wenye mikono iliyajaa damu, na kuwa tayari kupambana vita ya ukombozi, kwa nini tunashindwa kujisaidia wenyewe ndani ya Tanzania? Kwa nini tuliyachukia yaliyofanywa na Makaburu wa Afrika Kusini kwa Waafrika Kusini, na tukajitoa muhanga kuwasaidia, lakini leo tunashindwa kuwaondoa Makaburu weusi wa ndani ya Tanzania, kwa ajili yetu wenyewe?