kibunange
Senior Member
- Feb 18, 2015
- 165
- 148
Habari za leo wananzengo!?
Ni matumaini yangu wote ni wazima wa afya. Leo ningependa kutoa mtazamo wangu wa kiroho juu ya taifa hili teule la Mungu. Taifa lenye misingi ya utu na umoja. Taifa lililobarikiwa kwa kila aina ya baraka, ardhi, watu wapole, mimea, madini, mito, wanyama, milima, maji n.k..
Kuna maswali mengi ambayo nimekuwa najiuliza sana kuhusu taifa hili. Baba wa taifa alifuta laana ya taifa hili kwa kutokumwaga damu za watu wake na hivyo aliondoa unajisi kwenye nchi yake, aliondoa dhulma, ubaguzi, ubinafsi nk. Na kuwafanya watanzania wamoja na ndio maana leo hii taifa hili haliwezi kutumbukia kwenye hila za maadui wawe wa nje au wa ndani kwani mkono wa Mungu upo na wananchi wa tanzania.
Taifa hili ni taifa mama limechagiza ukombozi wa nchi nyingi za bara la Africa, limekuwa kimbilio la wanyonge na wote waliokimbia makazi yao sababu ya vita na dhiki mbalimbali na hivyo Mungu analiangalia taifa hili kwa jicho la huruma na upendo na hivyo kamwe hatoliacha taifa lake teule liangamie.
Amen!
Ni matumaini yangu wote ni wazima wa afya. Leo ningependa kutoa mtazamo wangu wa kiroho juu ya taifa hili teule la Mungu. Taifa lenye misingi ya utu na umoja. Taifa lililobarikiwa kwa kila aina ya baraka, ardhi, watu wapole, mimea, madini, mito, wanyama, milima, maji n.k..
Kuna maswali mengi ambayo nimekuwa najiuliza sana kuhusu taifa hili. Baba wa taifa alifuta laana ya taifa hili kwa kutokumwaga damu za watu wake na hivyo aliondoa unajisi kwenye nchi yake, aliondoa dhulma, ubaguzi, ubinafsi nk. Na kuwafanya watanzania wamoja na ndio maana leo hii taifa hili haliwezi kutumbukia kwenye hila za maadui wawe wa nje au wa ndani kwani mkono wa Mungu upo na wananchi wa tanzania.
Taifa hili ni taifa mama limechagiza ukombozi wa nchi nyingi za bara la Africa, limekuwa kimbilio la wanyonge na wote waliokimbia makazi yao sababu ya vita na dhiki mbalimbali na hivyo Mungu analiangalia taifa hili kwa jicho la huruma na upendo na hivyo kamwe hatoliacha taifa lake teule liangamie.
Amen!