Tanzania leo

Arcad Atmos

Member
Joined
Apr 18, 2013
Posts
33
Reaction score
0
Tanzania katiba sio tatizo.iliyokuweko ilikua inatosha sana hadi kwa wakati huu.Tatizo ilikosa usimamiaji wa kweli kiasi kwamba kikatokea kipengele maarufu (hekima) kwakuficha uovu au kuipindisha katiba na sheria.
Kama wazanzibari hawataki muungano kwanini Tanganyika inawang'ang'ania?
Kama mtu kaamua kuchukua Uraia wa nchi nyingine kwanini aendele Kuwa Mtanzania?
Kama mtu anashindwa kuendana na matakwa ya chama,anawezaje kuendana na katakwa ya wananchi ambao hao ndio wenye vyama vya siasa.kumbe mgombe binafsi ni hatari,hafai anaweza kuuza nchi bila hata Kuwa na wakumpinga.
Napata mgagasiko tonapoitaka katiba mpya kwanguvu kiasi kwamba tunashindwa kuona mambo mengine ya maana kama ile Sera yetu ya kilimo kwanza,au kushindwa kufwatilia mfumo mbovu wa elimu ambao sasa tuna Big result now(BRN).ufaulu wa Makaratasi bila chochote kichwani.Yaani haiingi akilini ufaulu kuongezeka kwa kiasi kikubwa ndani ya mwaka mmoja.

Huku jana tu jeshi la polisi na jeshi la wananchi wa Tanzania wakipigana duu.
Yaani usalama wa nchi kama hii ni majanga.askari hawana nidhamu,chombo chakulinda amani kinawatu wasioelewa nafasi yao ktk jamii.Sijui hii ni nchi ya namna gani?

Sasa wewe kaa vijiweni na mitandao yakijamii ukijadili katiba mpya huku wenzako wakipiga hela.Kwani inamaana siku hizi tembo hawauliwi,madawa ya kulevya je hayasafirishwi?
Vyombo vya habari vyote vipo bungeni kwenye michezo ya kuigiza huku watu wakifanya yakwao.

Nachukua fursa hii kuwaambia watanzania wenzangu msikubali kuwa mafala kiasi hichi,
Amka wewe ni mtu muhimu sana ktk nchi hii.
Fanya kitu sahihi kwaajili yako na Tanzania

Ni mimi Mtanzania mwenzako Arcad.
 
Tunaona mbwa akiona chatu sikuzote anamkimbilia kwa kumlilia,lkn kumbe ndiyo mwisho wake wa uhai,chatu akiona hivyo ananyamaza tu anakuwa mpole anasubiria hatima ya kujipatia kitoeo,ni kweli mbwa hanaga la kufanya kwachatu,zaidi kusubiri hukumbu ya kuvunjwavunjwa na kumezwa kabisa,Chama kilichoko madarakani na mfumo wake uliyopo,kinafananishwa na mbwa anapomuona chatu,hivyo matukio tunayoyaoba ya mapungufu makubwa ya maadili kwa kutimiza matakwa binafsi kwa viongozi na mmfumo mzima,ni dalili za kumezwa na busara za wachache wenyeiwezo ws hoja na tafsiri ya utawala bora kwa raia wa Tanzani na vizazi vijavo,na ni kwamba hili haliepukiki mfumo wao ni mmbovu,wanatumia sasa mamlaka hata kunyanyasa raia kupora fedha kwa nguvu barabarani,kwa madereva wa magari yote na bodaboda,wakijua ni Daresalaamu tu,kumbe sumu hii inaenea kwa wa watu wote wanaohitajika kukipa chama nafasi,na kukinyima pia,kazi ni moja jamani tuvumilie kazi imeisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…