Tanzania kushindwa kutumia majeshi ya ulinzi na usalama

Uliza_Bei

JF-Expert Member
Feb 17, 2011
3,216
990
Ni kwanini nchi yangu haitumii majeshi na vikosi vya ulinzi na usalama katika vyombo na taasisi zake nyeti?

Nimekuwa nikijiuliza, ukipita barabara kuu ya Mbeya au Mwanza kuja Dar Es Salaam huoni askari na wanajeshi (JWTZ) wa kutosha barabarani.

Pia nimekuwa nikijiuliza kwanini hatuoni katika taasisi mfano: TRA, TPA (Bandari), Maabara zake Kuu, TFDA, TBS, Airport, TANESCO na vitengo vya Hospital kama Muhimbili nakadhalika, n.k.

Hili ni tatizo kubwa sana la kushindwa kutumia majeshi yetu vilivyo.

Katika maeneo haya nyeti, watumishi wasiowaaminifu hupata mwanya wa kuhujumu serikali na nchi kama hawakudhibitiwa na vyombo vya dola.

Tujifunze Ulaya na Marekani waliofanikiwa; hata siku moja hawamwachi mtumishi katika vyombo hivi nyeti ajimwage kufanya kila alitakalo.

Intelijensia yetu hapa haioni ama kwa makusudi imeamua kufumbia macho ili serikali iweze kuhujumiwa.

Natoa wito kwa serikali ya MAGUFULI, kama tunahitaji ufanisi katika haya mambo ni lazima tuige wenzetu wanafanyaje. Taasisi nyeti hazitakiwi kuachwa bila udhibiti.

Kwa kawaida maeneo kama niliyoyataja, serikali inakuwa na vijana wake wa intelijensia waliosoma mambo husika na wanaajiriwa humo.Lakini pia serikali inakuwa na inakuwa na wasiowataalam katika eneo hilo wakibaki kuwa wanajeshi ama askari na unifomu zao kwaajili ya kuangalia kila kinachotendeka.

Mfano, wanaweza kuwa wasindikizaji nyuma kila linapotendeka jambo fulani; watu wa intelijensia wananielewa na mimi sitaki kwenda kwa undani zaidi.

Siingii ndani zaidi kulielezea jambo hili kwavile natambua serikali hata kama itachelewa kulichukua bado huko mbeleni itaamua kulifanyia kazi.

Nimekuwa nchi za wenzetu Ulaya na Marekani na nimeshuhudia hilo. Nimekuwa hapa katika ofisi zetu nyeti kadhaa na sijashuhudia hilo.

Haya majipu mengi yametokea kwa kukosa udhibiti, na yapo mengi na kwavile hayajaanza kudhibitiwa bado tunaona haya yakitokea.

Kwa nia nzuri naomba serikali iweke uangalizi wa kiintelijensia lakini pia wa wazi kiusalama katika maeneo yote nyeti itapunguza uvujaji wa siri na pia wizi na uhujumu unaoweza kudhibitiwa.

Nawasilisha.
 
Huyu ni mlinzi viwanja vya ndege na yuko na silaha tayari kwa lolote
 

Attachments

  • 08292011_5_08292011_5_hires.jpg
    08292011_5_08292011_5_hires.jpg
    333.8 KB · Views: 31
mtoa mada kaz ya JWTZ unaijua vzr kweli? sasa mwanajesh akae barabaran afanye kazi gan? embu jaribu kupitia majukumu ya majeshi yetu vzri kwanza.....!!
mkuu tulipofikia inatakiwa msaada kutoka jwtz.

ww kama porini huko kwenye wanyama watu washakubuhu na kuota mizizi kiasi kwamba ukiwazuia wameamua mpaka kutungua ndege kabisa na wana siraha za kivita je unataka tufanye nini??
si inamaana hiyo ni vita tayari ishatangazwa?!
wakati wao wapo wenye ujuzi huo why wasitumike kutusaidia??
 
Nimefanya uchunguzi wa kutosha wala sibàhatishi
mkuu tulipofikia inatakiwa msaada kutoka jwtz.

ww kama porini huko kwenye wanyama watu washakubuhu na kuota mizizi kiasi kwamba ukiwazuia wameamua mpaka kutungua ndege kabisa na wana siraha za kivita je unataka tufanye nini??
si inamaana hiyo ni vita tayari ishatangazwa?!
wakati wao wapo wenye ujuzi huo why wasitumike kutusaidia??

. Wanajeshi hizi no Nazi zao wala usihofu
 
Sikuhitaji kusoma hadi mwisho kwani nimegundua hata kazi za JWTZ hujui.Hata hivyo tenganisha maana ya intelijensia na JW.INTELLIGENCE ni kitengo maalumu ambacho kinafanya kazi kwa namna ambayo kwa nilivyoona hata kukuelezea ni kazi. Go back to your recruitment class
 
Sikuhitaji kusoma hadi mwisho kwani nimegundua hata kazi za JWTZ hujui.Hata hivyo tenganisha maana ya intelijensia na JW.INTELLIGENCE ni kitengo maalumu ambacho kinafanya kazi kwa namna ambayo kwa nilivyoona hata kukuelezea ni kazi. Go back to your recruitment class

Sina haja ya kuendelea kubishana kwa hilo wenye akili watalifanyia kazi.
 
Serikali imepiga hatua kwa kuanzisha kitngo cha ulizi pale bandarini jana. Ninaamini watafanyia kazi maeneo mengine pia kama tulivyoshauri. Kuna watu hata humu JF hawataki suala la ulinzi kwavile linawanyima nafasi ya kuhujuma ni wazi watajaribu kuleta vikwazo na ngonjera nyingi....ni wa kupuuzwa ili nchi iende mbele kimaendeleo
 
Mtoa mada kwa sehemu uko sahihi. Kuna baadhi ya sehemu kunapaswa kuwa na ulinzi wa jeshi, kama baadhi ya nchi zifanyavyo. Sisi wapo sehemu chache sana. Nadhani walikuwapo chanzo cha maji Ruvu Chini. Inawezekana ni utaratibu wetu, ambao yamkini wafanya kazi vizuri.
 
Serikali imepiga hatua kwa kuanzisha kitngo cha ulizi pale bandarini jana. Ninaamini watafanyia kazi maeneo mengine pia kama tulivyoshauri. Kuna watu hata humu JF hawataki suala la ulinzi kwavile linawanyima nafasi ya kuhujuma ni wazi watajaribu kuleta vikwazo na ngonjera nyingi....ni wa kupuuzwa ili nchi iende mbele kimaendeleo
Kijana unapepesuka, ulinzi wa polisi Bandarini unahusiana vipi na JWTZ kuingia mitaani kulinda raisa na mali zao? Hiyo sio kazi yao mpaka wakati wa emergency. Otherwise utuambie unaona (kwa akili yako, kama unayo anyaway) nchi itangazwe ipo kwenye hatari ya kiusalama.
 
Kijana unapepesuka, ulinzi wa polisi Bandarini unahusiana vipi na JWTZ kuingia mitaani kulinda raisa na mali zao? Hiyo sio kazi yao mpaka wakati wa emergency. Otherwise utuambie unaona (kwa akili yako, kama unayo anyaway) nchi itangazwe ipo kwenye hatari ya kiusalama.
Polisi wameshindwa kulinda mali zetu zinapigwa kila kona(kila polisi ana gari siku hizi kwaajiri ya deal).nafuu wafanye kazi hawa marine force wetu.ukienda ubalozi wa marekani mfano hukutani na polisi.ni army!.
 
Back
Top Bottom