Tanzania is among top 10 Fastest growing Economies in the World

Mkuu Felix, mimi nimeweka mada pengine nikiwa na kutoamini kwa kile nilichokisikia na kukiona. Ndo maana nikaomba wataalam wa uchumi waje kutusaidia kulielewa hili jambo.
Hiyo picha niliyoweka nilipiga mwenyewe kutoka kwenye tv wakati kipindi kilikuwa live kikiendelea.
Kuhusu address, nadhani ukienda msnbc.com ukatafuta kipindi cha 'last word' au ukatafuta jina la mwenye kipindi 'Lawrence O'Donnell' utaipata.
 
Kama Bigurube alivyopsema hapo juu takwimu hizo hazina uhalisia. Zinatokana na template za kukokotoa uchumi wa nchi (GDP) zinazotolewa na World Bank na IMF kwa nchi za dunia ya tatu. Hizo zinajumuisha uzalishaji ghafi (Gross Income) hata kama sehemu kubwa ya uzalishaji huo unaishia nje ya nchi. Kwa mfano, ukuaji wa uchumi wa Tanzania unajumuisha ule wa madini ambao zaidi ya 80% unatoka nje na kunufaisha nchi za 'wawekezaji'. Mfano wa pili, ni mabenki ya kigeni ambayo asilimia mia (100%) yanamilikiwa na wageni. Ukuwaji wake unajumuishwa katika takwimu za Tanzania lakini matunda yake (faida) yote yanaishia nje. Hiyo ndiyo sababu ya kuambiwa uchumi unakuwa na wakati huo huo umasikini unaongezeka.

Kwa maoni yangu tatizo ni wataalamu wetu, hasa wachumi, ambao wanazipokea nadharia hizo na 'template' za WB na IMF kama Sala ya Bwana. Hawahoji hata kidogo mantiki ya nadharia hizo. Tunapaswa kuwa na takwimu zetu ambazo ni 'capital/profit-flight adjusted' (nimelibuni tu) ili takwimu zetu ziwe halisi kwa kujumuisha kile tu kinachounufaisha uchumi wa ndani wa Tanzania. Kama WB na IMF wanataka za kwao kwa template zao tuwape lakini taarifa na mipango yetu ya ndani itokane na takwimu zetu wenyewe.

Siku za karibuni nchi ya Ghana imekuwa ikisifiwa na nchi za magharibi kuwa ni mfano wa uchumi unaopaa barani Afrika. Lakini jana nimeona kwenye taarifa ya habari ya chombo kimojawapo cha habari cha magharibi kuwa pesa ya Ghana imepoteza aslimia arobaini (40%) toka mwaka huu unanze, mfumuko wa bei ni wa kutisha na sasa inakwenda IMF kukopa ili iweze kudhibiti thamani ya sarafu yake (Cedi). Sasa ajabu ni kwamba Ghana ni mzalishaji wa kwanza au wa pili wa dhahabu barani Afrika, mwaka jana walianza kuzalisha (ndiyo, kuzalisha na siyo kugundua) mafuta na ni mzalishaji mkubwa wa zao la Cocoa. Inakuwaje iwe na matatizo ya kiuchumi namna hiyo na huku tunaambiwa uchumi wake unakuwa kwa kasi? Hapa kuna nafasi kwa vijana wetu kupata shahada za uzamili na uzamivu kama watafanya tafiti za kweli na ku-challenge dogma za wachumi wa magharibi badala ya kukaririshwa. Wapo hao?
 
Digits should be translated into the growth in people's pockets. Not otherwise.
 
Due to abundant natural resources found in developing countries, especially those of sub saharan African countries, it can be very true that their economic growth, can be among the fastest economic growth in the world.

But the main problem in these countries is there is no fair of distribution of the National cake.

That means that, only those big shots from the ruling party are enjoying that economic growth, but for the majority, ordinary citizens, they are struggling even to get their daily meals!!
 
huyo. masopakyindi tangu lini wahindi wakawa na nia njema na uchumi wa nchi hii wao fursa zote wakipata wanazikimbiza nje ya nchi.....
 
Last edited by a moderator:
What is happening does not reflect peoples life,how can be proud of something that does gaves positive impact to peoples life?
 
*g.n.p=0
*g.d.p=0
*supplus export=0

uchumi umekuwaje hapo fiksi tu....wengine hatujui uchumi kihivyo ila we are not that stupid ukatudanganya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…