Tanzania 2005-2020: Kipindi kigumu cha Mpito

Pius Kafefa

Member
Aug 9, 2011
88
20
Wadau nimeamua kuandika haya kutokana na ukweli wa hali inayoelezea kipindi tunachopitia Watanzania. Kipindi hiki kilianza wakati wa awamu ya nne ya utawala chini ya Rais J. M. Kikwete, na kitaendelea hadi mwaka 2020. Tukiitazama Tanzania kabla ya mwaka 2005, ni wazi tutaona jinsi ilivyokuwa tofauti kisiasa, kiuchumi, na kijamii na Tanzania iliyoko kwenye kipindi cha mpito.

Sababu za Tanzania kuingia kwenye kipindi cha mpito:
  1. Utawala wa kisiasa ulioshika dola kuanzia mwaka 2005 ulibadili mfumo wa kiutawala ili kuweka watu waliokuwa wakiuunga mkono uongozi huo. Kipindi hiki ndicho kilichoshuhudia utawala ukilaumiwa kwa kuweka watu kwenye system kishkaji. Waliokuwa kinyume na status quo walipoteza nafasi zao. Kipindi hiki kimeshuhudia mnyukano mkali na wa wazi ndani ya chama tawala kiasi cha kukaribia kumeguka kufuatia kuibuka kundi lililokuwa likipinga ufisadi, huku wanachama wengi wa chama tawala wakiona hakukuwa na tatizo. Hadi leo, mambo ndani ya chama tawala hayajatulia kutokana na harakati za kisiasa kuelekea 2015.
  2. Vyama vya upinzani vilivyokuwa vimebadili uongozi viliweka watu wapya waliokuja na mbinu mpya za kufanya siasa. Siasa ya upatanisho na dola au chama tawala ilikoma na kuingia siasa ya kushambuliana kupitia kashfa mbalimbali kama za wizi wa EPA, mikataba ya kifisadi, wizi wa fedha za halmasauri, na wizi wa kura wakati wa uchaguzi. Uchaguzi mkuu wa 2010 umeshudia Chadema ikiongeza wabunge kutoka 5 (2005) hadi 44 (2010) huku ikionywa na chama tawala na wachambuzi wengine iachane na siasa za kiharakati.
  3. Kutikiswa kwa umoja wa kitaifa. Kwa mara nyingine ufa kwenye muungano wa Tanganyika na Zanzibar umekolezwa kutokana na uwepo wa maridhiano ya CCM na CUF. Maridhiano hayo yamewafanya Wazanzibari kuwa na sauti moja linapokuja suala la maslahi ya Zanzibar, hali iyopelekea kutokea kwa hoja ya kurudisha serikali ya Tanganyika wakati wa mchakato wa kuandika katiba mpya. Umoja wa kitaifa umetikiswa pia na vuguvugu za kidini ambapo wakristo na waislamu wamepungukiwa na uvumilivu. Tayari kuna mauaji yameshatokea kutokana na hili, na hakuna juhudi za kuridhisha zinazofanywa kushughulikia tatizo la kidini.
  4. Kadhalika, siasa za kizazi kipya zimebadili mfumo wa uendeshaji wa harakati za kisiasa ambapo vyama vya siasa vinalazimika kuwa na mtandao wa vyombo vya habari kwa ajili ya kufanya propaganda. Kwa sasa imekuwa vigumu kuamini moja kwa moja taarifa zinazopashwa kuhusu chama fulani kwani vyombo vingi vya habari (pamoja na waandishi wake) vinaegemea kwenye maslahi ya kisiasa. Hili linathibitika kirahisi kwa kupitia 'headlines' kwenye magazeti ya kila siku au kila wiki.
Kwa kuzingatia dondoo chache hapo juu; siasa za visasi ndani ya chama tawala, siasa za kiharakati kwenye vyama vya upinzani, ufa wa muungano, ufa wa kidini, na siasa za kupakana matope kupitia vyombo vya habari zitapelekea Tanzania iendelee kukumbwa na matatizo ya kisiasa na kijamii hadi itakapoanza kuimarika baada ya 2020. Na ili hali iimarike mapema yafuatayo yanatakiwa yawepo:
  • Vyama vya upinzani viendelee na siasa za kiharakati bila kulala (vikilala kitafuata kipindi kigumu cha maangamizi ya wafuasi wake).
  • Chama tawala kianze kujipatanisha na tabaka la maskini ambao ndio wengi katika nchi hii. Kisipofanya hivi kitaendelea kukataliwa na kutegemea mbinu muflisi za kupakana matope.
  • Watu wote maarufu wa nchi hii waheshimiwe bila kujali itikadi au mitazamo yao katika baadhi ya mambo yanayotokea katika nchi hii.
  • Maoni yenye mtazamo wa kisiasa yaheshimiwe pale yanapotolewa na Watanzania ambao hawaishi kwa kufanya siasa. Watnzania hawa wanaweza kuwa ni wanafunzi, wafanyakazi, wanataaluma, wamachinga, madereva wa bodaboda, n.k.
  • Baada ya uchaguzi mkuu wa 2015 chama kitakachotawala kiendelee na ujenzi wa taifa jipya lenye amani na watu wenye upendo, utulivu, na mshikamano bila kujali itikadi zao za kisiasa, kidini na tabaka atokalo mtu.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Acha uongo wewe, kipindi kigumu ndo nini? Ni kipindi cha opportunities kwa kila developmental areas including political arena
 
Mtoto ksbls ys kuzaliwa akina mama wanapata uchungu mkubwa. wala usishangae kwani mafisadi watang'oka kwa kishindo kikubwa maana walishaweka mizizi mirefu.
 
Acha uongo wewe, kipindi kigumu ndo nini? Ni kipindi cha opportunities kwa kila developmental areas including political arena

Mimi nakiita ni kipindi kigumu kwa sababu toka tupate uhuru tulikuwa tunajivunia amani (utulivu?). Sasa ni kilichopo ni kero inayotokana na harakati za kujinasua kwenye utawala wa chama kimoja cha CCM. Wananchi wanapotaka chama mbadala, by virute wanaanza kuingia kwenye kipindi cha mpito, chenye kulia na kusaga meno kwa wale wasioweza kupata hizo opportunities unazosema zipo kwa wingi.
 
Mtoto ksbls ys kuzaliwa akina mama wanapata uchungu mkubwa. wala usishangae kwani mafisadi watang'oka kwa kishindo kikubwa maana walishaweka mizizi mirefu.

Mkuu Chikaka Sumuni Hakika kipindi cha ujauzito ni kipindi cha mpito. Wazazi (akina mama?) wanakuwa na matamanio ya kupata mtoto aliyekamilika, mwenye afya ya akili na mwili. Tanzania ijayo (kuanzia 2020) yaweza kuwa njema iwapo tutang'oa mazalia yote yanayoyutia machungu leo.
 
Mkuu Chikaka Sumuni Hakika kipindi cha ujauzito ni kipindi cha mpito. Wazazi (akina mama?) wanakuwa na matamanio ya kupata mtoto aliyekamilika, mwenye afya ya akili na mwili. Tanzania ijayo (kuanzia 2020) yaweza kuwa njema iwapo tutang'oa mazalia yote yanayoyutia machungu leo.

Nchi ya ahadi yenye maziwa na asali ndo hiyo inakaribia, vitendo vya hawa jamaa ni kama wanatuaga, si unajua madaraka yakiwalewesha watu. CCM ni chama ambachokingeweza kuwarudisha vijana wenye umahiri mkubwa walioko nje kwa ajili ya kupata ueledi wao wawasaidie kujenga chama makini, lakini kama wanakosa watu mpaka wanawachagua Nape, mwiguli, Makamba - Baba, Mukama na wanawarudish ten akina Mang'ula, Kinana nk ujue wamechoka.

Zawadi pekee ambayo watanzania wanastahili kuwapa ni kuwaweka kando ili wajifunze wkiwa upinzani.
Hekima inasema kwamba " Katika ujenzi wa nyumba yoyote, wapo mafundi waliobobea katika maeneo na hatua mbalimbali za ujenzi, mfano wapo wataalamu wa kuandaa eneo-kiwanja, wapo mafundi wa kuchimba na ujenzi wa msingi, wapo wajenzi wa ukuta, paa na finishing,halafu ndo mwenye kuja kukaa ndani ya nyumba"

Kazi ya TANU na baadae CCM walitujengea msingi na utaifa, lakini wanaendelea kung;nga'ania wao tena ndo waishi humo humo haiwezekani maana wao walikuwa mafundi wa awali tu, na kazi yao walishamaliza. Sasa kitendo cha watanzania kuwachelewesha kuwafukuza Ikulu ndo maana wanataabika na propoganda na sasa mauaji ya wananchi wasiokuwa na hatia yoyote dawa yako ni kuwaondoa tu 2015.

Mungu ibariki Tanzania wape moyo wa subira wote walipoteza ndugu zao, wape ahueni waliopata majeraha, lakini pia MUNGU tunaomba uwaadhibu hao waliopanga, kuwatuma na waliotekeleza uhalifu huu mkubwa na uwaweke hadharani mapema iwezekanavyo.....
 
Mimi nakiita ni kipindi kigumu kwa sababu toka tupate uhuru tulikuwa tunajivunia amani (utulivu?). Sasa ni kilichopo ni kero inayotokana na harakati za kujinasua kwenye utawala wa chama kimoja cha CCM. Wananchi wanapotaka chama mbadala, by virute wanaanza kuingia kwenye kipindi cha mpito, chenye kulia na kusaga meno kwa wale wasioweza kupata hizo opportunities unazosema zipo kwa wingi.
Kwa mtazamo wangu hicho kipindi cha amani na utulivu ndo kilikuwa kigumu na ndo maana tupo hapa, tumeishi kwa mawazo yaliyokufa kwa muda mrefu. By now tupo kwenye kipindi kizuri kwani watu tunajua haki zetu, tupo tayari kuzipigania na tupo tayari kufa kwa mawazo yanayoishi..!
 
Kwa mtazamo wangu hicho kipindi cha amani na utulivu ndo kilikuwa kigumu na ndo maana tupo hapa, tumeishi kwa mawazo yaliyokufa kwa muda mrefu. By now tupo kwenye kipindi kizuri kwani watu tunajua haki zetu, tupo tayari kuzipigania na tupo tayari kufa kwa mawazo yanayoishi..!

Nadhani mtazamo huo unawakilisha kiwango cha juu sana cha ufahamu. Hiyo ni sifa nyingine iliyochelewa, lakini ndiyo inayohitajika zaidi kipindi hiki cha mpito kuelekea kubadilisha utawala uliopo.
 
Kwanza kabisa niweke wazi naongea nikiwa sio mwanachama wa chama chochote!!!! Bali mtanzania mwenye kuipenda nchi yangu.
Kwanza sikubaliani na kauli ya mh pinda aliyoitoa jana kwamba wasiofuata sheria wapigwe hii kauli ni kali sana hasa ktk nchi ambayo inafuata misingi ya demokrasia,na katika kipindi hiki ambacho watz wana/tunajazba za wenzetu waliokufa kutokana na mlipuko wa mabomu huko arusha,na mauaji ya soweto yaliyosababishwa na polisi.
nasema yamesababishwa na polisi kwa sababu wao ndio walikuwa wa kwanza kupiga mabomu kuwatawanya watu,kutoka ktk mkusanyiko waliouita co wa halali!!!,hapa napata maswali mengi ya kujiuliza polisi,je madhara ya kuacha ule mkusanyiko uendelee hata kama sio halali ni kubwa mpk kufikia kuwatawanya kwa nguvu?? Kama jibu ni ndio basi ningependa kujuzwa kivipi?? Na kama jibu ni sio basi polisi wana makosa na wanapaswa wachukuliwe hatua,kwa kusababisha mauaji na fujo(vurugu) zisizokuwa na ulazima,
ifike kipindi. Serikali nikijumuisha polisi na viongozi wa kisiasa kuona kwamba maisha ya mtanzania yanathamani kubwa kuliko vyama vyao vya siasa na mabosi wao waliowaajiri/kuwatumikia,alafu kibaya zaidi hawa polisi we2 ambao ndio 2nawash2mu ndio 2naokaa nao ktk nyumba za kupanga na wengne ni rafiki na ndugu zetu tena wa damu,sasa haya mazingira ya chuki 2nayojengewa baina ya sisi na polisi yananitiliamashaka huko mbeleni 2nakokwenda,
Ombi langu:polisi watumie busara katika kutawanya watu mikusanyiko. Isiyo ya halali hasa tukizingatia madhara yanayosababishwa na kutumia nguvu ni kubwa kuliko kama yangeachwa yaishe kwa amani alafu kutoka hapo sasa zinaweza kuchukuliwa sheria za kufanya mkusanyiko bila kibali,kama huo wa soweto polisi wangepata mara 1 uthibitisho kutoka kwa AICCP. Kama walivyodai wakati wanawataka viongozi wa chadema kuvunja mkusanyiko huo,
Kwa kifupi kuna mengi ya kuongea ila kwa leo ningependa niishie hapa ili na wengne watakaopata bahati ya kusoma uzi huu waweze kuchangia.
 
Kama kwenye chaguzi ndogo za madiwani mambo yamekuwa hivi, sipati picha 2015 wakati wa uchaguzi mkuu mambo yatakuwaje?
Watanzania wenzangu huu ni wakati wa kutibu jeraha kabla halijawa kidonda. Tuombe msaada mapema kwenye umoja wa mataifa watusaidie ulinzi, polisi hawawezi kulinda raia hata kidogo. Naamini wapelelezi wapo, inakuwaje vigumu kupeleleza hilo bomu lilinunuliwa china kiwanga kipi? lilisafirishwaje hadi kuingia nchini? wamiliki wa siraha zilizotumika harusha ni akina nani? Majibu ya maswali hayo yakipatikana tu, basi nchi itakuwa kwenye hali ngumu sana kiusalama.
Mwana JF wasemaje? 2015 tutapona kweli?
 
Kama kwenye chaguzi ndogo za madiwani mambo yamekuwa hivi, sipati picha 2015 wakati wa uchaguzi mkuu mambo yatakuwaje?
Watanzania wenzangu huu ni wakati wa kutibu jeraha kabla halijawa kidonda. Tuombe msaada mapema kwenye umoja wa mataifa watusaidie ulinzi, polisi hawawezi kulinda raia hata kidogo. Naamini wapelelezi wapo, inakuwaje vigumu kupeleleza hilo bomu lilinunuliwa china kiwanga kipi? lilisafirishwaje hadi kuingia nchini? wamiliki wa siraha zilizotumika harusha ni akina nani? Majibu ya maswali hayo yakipatikana tu, basi nchi itakuwa kwenye hali ngumu sana kiusalama.
Mwana JF wasemaje? 2015 tutapona kweli?
hivi kwanini mapadre wanatufungisha ndoa halafu wao hawaoi???
 
Nadhani mtazamo huo unawakilisha kiwango cha juu sana cha ufahamu. Hiyo ni sifa nyingine iliyochelewa, lakini ndiyo inayohitajika zaidi kipindi hiki cha mpito kuelekea kubadilisha utawala uliopo.
Nakushukuru mkuu na pia samahani kwa kukujibu late. Nilikuwa natumikia 5 day ban
 
Kama kwenye chaguzi ndogo za madiwani mambo yamekuwa hivi, sipati picha 2015 wakati wa uchaguzi mkuu mambo yatakuwaje?
Watanzania wenzangu huu ni wakati wa kutibu jeraha kabla halijawa kidonda. Tuombe msaada mapema kwenye umoja wa mataifa watusaidie ulinzi, polisi hawawezi kulinda raia hata kidogo. Naamini wapelelezi wapo, inakuwaje vigumu kupeleleza hilo bomu lilinunuliwa china kiwanga kipi? lilisafirishwaje hadi kuingia nchini? wamiliki wa siraha zilizotumika Arusha ni akina nani? Majibu ya maswali hayo yakipatikana tu, basi nchi itakuwa kwenye hali ngumu sana kiusalama.
Mwana JF wasemaje? 2015 tutapona kweli?

Tutor B,

Kwa uzoefu wangu, uchaguzi wowote mdogo (au kwa ujumla chaguzi ndogo) huwa zilna usumbufu sana kuliko uchaguzi mkuu. Sababu kubwa ni kwamba nguvu nyingi huelekezwa kwenye kushinda katika ngazi moja ya kata au jimbo. Katika mazingira hayo mbinu zote chafu hutumika
  • Kuwarubuni wagombea wa vyama pinzani ili wajitoe
  • Kuwatisha wagombea wa vyama pinzani kwa kuwatumia hata wazazi wao kama iliwahi kufanyika wakati fulani katika kata fulani jimbo la Hai, na hata ilivyotokea kwa ile kata aliyokuwa akigombea kaka yake Tizeba kupitia CDM. Kwangu mimi mbinu hii ya kuwalazimisha wagombea kujitoa kupitia wazazi wao ambao huwatisha kwa kuwaambia kwamba wasipojitoa watawalaani ni mbinu mbaya zaidi kwani tofauti ya itikadi ya kisiasa hupelekea kufa kwa udugu. CCM wanaifahamu vizuri sana mbinu hii ambayo niliisikia kwa mara ya kwanza kwenye kongamano la kumbukumbu ya mwalimu Nyerere ambapo mgeni rasmi alikuwa Job Lusinde, na mtoa mada alikuwa katibu wa wilaya wa CCM, Hai.
 
Ni uchambuzi mzuri ambao hata kama hujagusa mambo yote ambayo taifa linapitia kwa sasa (au kwa kiingereza niseme 'not a very comprehensive and exhaustive analysis), kwa kiasi kikubwa unaonyesha hali halisi tunayopitia kama taifa kwa sasa. Nitachangia mambo mawili kwa kifupi sana.

Moja ni kuhusu muda wa kipindi (timeframe) hiki cha mpito (2005-2020). Maoni yangu katika hili ni kuwa uchaguzi wa mwaka 2015 utakuwa na mchango mkubwa sana katika kubadili hali ya kijamii, kiuchumi na kisiasa (socio-economic and political landscape) ya nchi kuelekea pazuri au pabaya zaidi kutegemea na mchakato wake kama utakuwa huru na wa haki na utakafanyika katika 'mfumo rafiki' kwa kila mpiga kura, mgombea katika ngazi zote za uwakilishi na vyama vyote vya siasa. Rasimu ya Katiba imeanza (anglau kwa sehemu) kuweka baadhi ya mambo yanayohitajika kwenye huo 'mfumo rafiki' ingawa kuna dalili za wazi za chama tawala kuyapinga na hivyo kutia hofu kama kweli tutakuwa na katiba inayoakisi matakwa ya wananchi au katiba ya ccm. Hoja yangu hapa ni kuwa uchaguzi wa 2015 ndio utakaotoa mwelekeo wa hicho kipindi kigumu cha mpito ama kuwa kifupi au kirefu zaidi hivyo kukabiliana na madhara yatokayotokana na mchakato na matokeo ya uchaguzi huo.

Pili, nakubaliana na mapendekezo yako kwenye hizo dondoo zote tano. Hata hivyo, naomba kuongeza chache kwenye hiyo orodha kama ifuatavyo. Moja, vyama vya upinzani vijikite zaidi vijijini ambako ndio kuna wapiga kura wengi ambao kwa kujua (au kutokujua??) wanadanganywa na kuaminishwa kuwa vyama vya upinzani vinaleta vurugu, ugaidi n.k. Pili, chama tawala kifanye shughuli za kisiasa kama vyama vingine, na sio kutegemea polisi na vyombo vingine vya dola kuzuia harakati za kisiasa za vyama vingine. Hili liliwahi kusemwa na mwenyekiti wa ccm lakini naona waziri mkuu ameamua kwa makusudi kupingana nalo (au wamengundua hawawezi kufanya siasa tena???) kwa kuruhusu polisi kupiga na kuua raia. Tatu, asasi za kiraia, wanaharakati, wasomi na makundi mbalimbali ya kijamii yajitokeze hadharani kusema, kukemea, kulaani kila aina ya uonevu unaofanywa na vyombo vyombo vya dola na chama tawala; na kuishauri au hata kuishinikiza serikali (sikivu???) kutatua kero za wananchi na kuheshimu haki za binadamu. Wanaoweza kuifungulia serikali au chama cha siasa mahakamani kama kuna ushaihidi wafanye hivyo, haijalishi kesi itachukua miaka mingapi na kama jaji au hakimu atapokea maagizo kutoka lumumba au magogoni. Safari tuliyonayo ni ndefu lakini mwisho wake u karibu!!!


Wadau nimeamua kuandika haya kutokana na ukweli wa hali inayoelezea kipindi tunachopitia Watanzania. Kipindi hiki kilianza wakati wa awamu ya nne ya utawala chini ya Rais J. M. Kikwete, na kitaendelea hadi mwaka 2020. Tukiitazama Tanzania kabla ya mwaka 2005, ni wazi tutaona jinsi ilivyokuwa tofauti kisiasa, kiuchumi, na kijamii na Tanzania iliyoko kwenye kipindi cha mpito.

Sababu za Tanzania kuingia kwenye kipindi cha mpito:
  1. Utawala wa kisiasa ulioshika dola kuanzia mwaka 2005 ulibadili mfumo wa kiutawala ili kuweka watu waliokuwa wakiuunga mkono uongozi huo. Kipindi hiki ndicho kilichoshuhudia utawala ukilaumiwa kwa kuweka watu kwenye system kishkaji. Waliokuwa kinyume na status quo walipoteza nafasi zao. Kipindi hiki kimeshuhudia mnyukano mkali na wa wazi ndani ya chama tawala kiasi cha kukaribia kumeguka kufuatia kuibuka kundi lililokuwa likipinga ufisadi, huku wanachama wengi wa chama tawala wakiona hakukuwa na tatizo. Hadi leo, mambo ndani ya chama tawala hayajatulia kutokana na harakati za kisiasa kuelekea 2015.
  2. Vyama vya upinzani vilivyokuwa vimebadili uongozi viliweka watu wapya waliokuja na mbinu mpya za kufanya siasa. Siasa ya upatanisho na dola au chama tawala ilikoma na kuingia siasa ya kushambuliana kupitia kashfa mbalimbali kama za wizi wa EPA, mikataba ya kifisadi, wizi wa fedha za halmasauri, na wizi wa kura wakati wa uchaguzi. Uchaguzi mkuu wa 2010 umeshudia Chadema ikiongeza wabunge kutoka 5 (2005) hadi 44 (2010) huku ikionywa na chama tawala na wachambuzi wengine iachane na siasa za kiharakati.
  3. Kutikiswa kwa umoja wa kitaifa. Kwa mara nyingine ufa kwenye muungano wa Tanganyika na Zanzibar umekolezwa kutokana na uwepo wa maridhiano ya CCM na CUF. Maridhiano hayo yamewafanya Wazanzibari kuwa na sauti moja linapokuja suala la maslahi ya Zanzibar, hali iyopelekea kutokea kwa hoja ya kurudisha serikali ya Tanganyika wakati wa mchakato wa kuandika katiba mpya. Umoja wa kitaifa umetikiswa pia na vuguvugu za kidini ambapo wakristo na waislamu wamepungukiwa na uvumilivu. Tayari kuna mauaji yameshatokea kutokana na hili, na hakuna juhudi za kuridhisha zinazofanywa kushughulikia tatizo la kidini.
  4. Kadhalika, siasa za kizazi kipya zimebadili mfumo wa uendeshaji wa harakati za kisiasa ambapo vyama vya siasa vinalazimika kuwa na mtandao wa vyombo vya habari kwa ajili ya kufanya propaganda. Kwa sasa imekuwa vigumu kuamini moja kwa moja taarifa zinazopashwa kuhusu chama fulani kwani vyombo vingi vya habari (pamoja na waandishi wake) vinaegemea kwenye maslahi ya kisiasa. Hili linathibitika kirahisi kwa kupitia 'headlines' kwenye magazeti ya kila siku au kila wiki.
Kwa kuzingatia dondoo chache hapo juu; siasa za visasi ndani ya chama tawala, siasa za kiharakati kwenye vyama vya upinzani, ufa wa muungano, ufa wa kidini, na siasa za kupakana matope kupitia vyombo vya habari zitapelekea Tanzania iendelee kukumbwa na matatizo ya kisiasa na kijamii hadi itakapoanza kuimarika baada ya 2020. Na ili hali iimarike mapema yafuatayo yanatakiwa yawepo:
  • Vyama vya upinzani viendelee na siasa za kiharakati bila kulala (vikilala kitafuata kipindi kigumu cha maangamizi ya wafuasi wake).
  • Chama tawala kianze kujipatanisha na tabaka la maskini ambao ndio wengi katika nchi hii. Kisipofanya hivi kitaendelea kukataliwa na kutegemea mbinu muflisi za kupakana matope.
  • Watu wote maarufu wa nchi hii waheshimiwe bila kujali itikadi au mitazamo yao katika baadhi ya mambo yanayotokea katika nchi hii.
  • Maoni yenye mtazamo wa kisiasa yaheshimiwe pale yanapotolewa na Watanzania ambao hawaishi kwa kufanya siasa. Watnzania hawa wanaweza kuwa ni wanafunzi, wafanyakazi, wanataaluma, wamachinga, madereva wa bodaboda, n.k.
  • Baada ya uchaguzi mkuu wa 2015 chama kitakachotawala kiendelee na ujenzi wa taifa jipya lenye amani na watu wenye upendo, utulivu, na mshikamano bila kujali itikadi zao za kisiasa, kidini na tabaka atokalo mtu.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Ni uchambuzi mzuri ambao hata kama hujagusa mambo yote ambayo taifa linapitia kwa sasa (au kwa kiingereza niseme 'not a very comprehensive and exhaustive analysis), kwa kiasi kikubwa unaonyesha hali halisi tunayopitia kama taifa kwa sasa. Nitachangia mambo mawili kwa kifupi sana.

Moja ni kuhusu muda wa kipindi (timeframe) hiki cha mpito (2005-2020). Maoni yangu katika hili ni kuwa uchaguzi wa mwaka 2015 utakuwa na mchango mkubwa sana katika kubadili hali ya kijamii, kiuchumi na kisiasa (socio-economic and political landscape) ya nchi kuelekea pazuri au pabaya zaidi kutegemea na mchakato wake kama utakuwa huru na wa haki na utakafanyika katika 'mfumo rafiki' kwa kila mpiga kura, mgombea katika ngazi zote za uwakilishi na vyama vyote vya siasa. Rasimu ya Katiba imeanza (anglau kwa sehemu) kuweka baadhi ya mambo yanayohitajika kwenye huo 'mfumo rafiki' ingawa kuna dalili za wazi za chama tawala kuyapinga na hivyo kutia hofu kama kweli tutakuwa na katiba inayoakisi matakwa ya wananchi au katiba ya ccm. Hoja yangu hapa ni kuwa uchaguzi wa 2015 ndio utakaotoa mwelekeo wa hicho kipindi kigumu cha mpito ama kuwa kifupi au kirefu zaidi hivyo kukabiliana na madhara yatokayotokana na mchakato na matokeo ya uchaguzi huo.

Pili, nakubaliana na mapendekezo yako kwenye hizo dondoo zote tano. Hata hivyo, naomba kuongeza chache kwenye hiyo orodha kama ifuatavyo. Moja, vyama vya upinzani vijikite zaidi vijijini ambako ndio kuna wapiga kura wengi ambao kwa kujua (au kutokujua??) wanadanganywa na kuaminishwa kuwa vyama vya upinzani vinaleta vurugu, ugaidi n.k. Pili, chama tawala kifanye shughuli za kisiasa kama vyama vingine, na sio kutegemea polisi na vyombo vingine vya dola kuzuia harakati za kisiasa za vyama vingine. Hili liliwahi kusemwa na mwenyekiti wa ccm lakini naona waziri mkuu ameamua kwa makusudi kupingana nalo (au wamengundua hawawezi kufanya siasa tena???) kwa kuruhusu polisi kupiga na kuua raia. Tatu, asasi za kiraia, wanaharakati, wasomi na makundi mbalimbali ya kijamii yajitokeze hadharani kusema, kukemea, kulaani kila aina ya uonevu unaofanywa na vyombo vyombo vya dola na chama tawala; na kuishauri au hata kuishinikiza serikali (sikivu???) kutatua kero za wananchi na kuheshimu haki za binadamu. Wanaoweza kuifungulia serikali au chama cha siasa mahakamani kama kuna ushaihidi wafanye hivyo, haijalishi kesi itachukua miaka mingapi na kama jaji au hakimu atapokea maagizo kutoka lumumba au magogoni. Safari tuliyonayo ni ndefu lakini mwisho wake u karibu!!!

Mkuu nakushukuru sana kwa uchambuzi wako. Tuendelee kuwatia matumaini wanaharakati wote wa mageuzi Tanzania ili kesho yetu iwe bora zaidi ya hii iliyopo kwenye kipindi cha mpito, na bora zaidi ya ile ya awamu zilizopita.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom