Mkuu umeandika idadi ndeefu ya unaowadhania kuwa watakuwa miongoni mwa majina ambayo yapo mfukoni mwa Mwenyekiti Mbowe. Lakini sasa unapokuja kwenya kwenye sifa naona umewalenga Lowassa na Sumaye tu basi. Na kwa jinsi mambo yalivyo sioni Lowassa akipewa hayo madaraka hivyo basi lengo lako limejikita kwa Sumaye. Japo hapo pia kuna tatizo kwa kuwa siamini kama Mwenyekiti atakubali kuwa na Katibu ambaye ni maarufu kuliko yeye na ambaye ni kama mkimbizi aliyekimbilia Chamani toka kwa mahasimu; anaaminika?