Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,999
- 1,187
Baada ya kuwasilisha maombi yao rasi Ewura, mamlaka hiyo nayo imetoa tangazo lifuatalo:
TANGAZO KWA UMMA
WITO WA KUKUSANYA MAONI YA WADAU KUHUSU OMBI LA TANESCO LA KUPANDISHA BEI YA HUDUMA YA UMEME
Kulingana na Kifungu Na.19 (2) (b) cha Sheria, Sura 414 ya Sheria za Tanzania, EWURA imeanza mchakato wa kukusanya maoni ya wadau kuhusu uhalali wa ombi lililowasilishwa na TANESCO. Ili kufikia malengo hayo, EWURA inawakaribisha wananchi wote kuhudhuria na/ama kuwasilisha maoni yenu katika mikutano itakayofanyika katika mikoa na tarehe mtakayojulishwa baadaye.
Kulingana na kifungu Na. 10(1) cha Mwongozo wa Uwasilishaji Maombi ya Bei wa Mwaka 2009 (Tariff Application Guidelines of 2009), wanachi wote wanaotaka kuweka pingamizi kuhusiana na ombi tajwa wanatakiwa kujiandikisha EWURA kabla ya saa 11:00 jioni siku ya Jumatano tarehe 14 Julai 2010. Wale watakaojiandikisha watapewa fursa ya kuwasilisha maoni yao katika mikutano husika. Wadau wengine ambao hawatajiandikisha pia watapewa fursa ya kutoa maoni yao papo kwa papo katika mikutano hiyo. Ndani ya kipindi cha wiki mbili baada ya mikutani husika, wadau watapewa fursa ya kuwasiliasha maoni yao kwa maandishi kuhusiana na maombi husika wakati wowote kabla ya saa 11:00 jioni.
Pamoja na nakala ya ombi husika kupatikana bure katika tovuti ya EWURA (www.ewura.go.tz), isipokuwa nyaraka za siri zilizowasilishwa EWURA na mwombaji kulingana na kifungu cha 25 cha Sheria, Sura 414; nyaraka nyingine zote zilizowasilishwa zinapatikana katika ofisi yetu katika annuani hapo juu kuanzia saa tatu (3) asubuhi mpaka saa 11:00 jioni. Hata hivyo wadau watakaohitaji nakala za ombi hilo wanaweza kupata kwa kulipa kiasi cha TZS 25,000 ikiwa ni gharama za kudurusu nakala hizo. Pia, unaweza kusoma maombi hayo bure wakati wa kazi katikq ofisi za EWURA.
Kwa maelezo zaidi tuandikie kwa anuani hapa juu.
Imetolewa na:
MKURUGENZI MKUU,
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Nishati na Maji
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Nishati na Maji