kuna msg inatembea whatsapp hii hapa labda itatoa mwangaza...
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)
TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA UMEME KWA MIKOA ILIYOUNGWA KWENYE GRIDI YA TAIFA.
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu wateja wake wa Mikoa waliounganishwa kwenye grid ya Taifa kuwa kimetokea tatizo la kiufundi kwenye GRIDI ya Taifa hivyo kupelekea wateja wetu kukosa umeme kuanzia majira ya saa 11:37 alfajiri.
HATUA ZILIZOCHUKULIWA
Mafundi wanaendelea kufanyakazi ili kuhakikisha umeme unarejea mapema iwezekanavyo
MAENEO YANAYOATHIRIKA
Wateja wote waliounganishwa kwenye GRIDI ya Taifa.
Tafadhali usishike wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka.
Toa taarifa kupitia namba za simu zifuatazo:-
namba za kituo cha miito ya simu 2194400 na 0768 985100
Mitandao ya jamii
www.facebook.com/tanescoyetu/ltd, www. twitter.com/tanescoyetu
Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza.
Imetolewa na:OFISI YA UHUSIANO
TANESCO MAKAO MAKUU