mabereng'ombe
Member
- Nov 22, 2013
- 70
- 18
Kuna watu wanalalamika kwamba kampuni ya simu Tanzania inakufa lakini hawajui sababu. Sasa hivi ukiwa na simu yako Landline inachezewa ili isifanye kazi. Ukipiga simu Huduma kwa Wateja wanakupa namba za mafundi.
Hao mafundi ukiwapigia wanakwambia Lunch yangu leo iko kwako. Maana yake hapa ni kwamba wanazichezea simu za baadhi ya wateja kwa makusudi ili wawape rushwa. Mchezo huu uko ofisi ya TTCL Nyerere Road na kuna fundi mmoja anaitwa Tesha huyu ndiye kinara wa mchezo huu.
Shirika lenyewe linakufa kutokana na kukosa wateja halafu hao wachache waliopo badala ya kunyenyewa wanazidi kuumizwa. Naomba Takukuru wapitie malalamiko haya!!
Hao mafundi ukiwapigia wanakwambia Lunch yangu leo iko kwako. Maana yake hapa ni kwamba wanazichezea simu za baadhi ya wateja kwa makusudi ili wawape rushwa. Mchezo huu uko ofisi ya TTCL Nyerere Road na kuna fundi mmoja anaitwa Tesha huyu ndiye kinara wa mchezo huu.
Shirika lenyewe linakufa kutokana na kukosa wateja halafu hao wachache waliopo badala ya kunyenyewa wanazidi kuumizwa. Naomba Takukuru wapitie malalamiko haya!!