Taifa Stars – tatizo ni Kim Poulsen?

Taifa Stars – tatizo ni Kim Poulsen?

Sibonike

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2010
Posts
17,297
Reaction score
18,046
Taifa Stars – tatizo ni Kim Poulsen?
Taifa Stars imetolewa na tayari wadau wanatoa sababu mbalimbali hasa ikizingatiwa katika siku za karibuni ilionekana kufanya vema kwenye mechi za kujipima nguvu dhidi ya Zambia na Cameron. Moja ya sababu ambayo imeandikwa kwenye gazeti la Mwananchi ni wachezaji kutojituma. Wametajwa akina Chuji, Bocco na Sure Boy. Kama hayo yanayoelezwa ni ya kweli basi huenda kocha wa timu yetu, Kim Poulsen ana matatizo ya “Man Management” Tofauti za siku za nyuma wakati wa FAT ya akina Ndolanga, sote tunajua wachezaji hawakuwa na motisha ya kuchezea timu ya taifa, labda kwa ajili ya uzalendo tu. Viongozi pia walichangia sana kwa kutoa vitisho na kuwapiga maarufu baadhi ya wachezaji kuchezea timu ya taifa. Ilikuwa kama timu binafsi ya Ndolanga. Sasa wakati huu kuna wadhamini wa uhakika na kambi za maandalizi za kiwango kizuri, kwa nini wachezaji wasitake kuchezea timu ya taifa?. Angalau Chuji alieleza sababu za msingi maana alijiona ni mtu wa kukamilisha namba tu lakini hakuwa na matumaini ya kucheza. Hali kama hii ilimtokea Michael Carrick wa Uingereza akaamua kujitoa japo sasa karejea baada ya kuhakikishiwa uwezekano wa kucheza. Sababu za Sure Boy na Bocco bado ni kitendawili . Yote hayo yanaashiria kuna walakini katika namna Kim Poulsen anavyohusiana na wachezaji (Man management). Imefika mahali wengine wanajiona hawana thamani kwenye timu na hilo ni kosa kubwa sana kwa kocha. Mwalimu lazima awe na uwezo wa kuwaweka sawa hata wale wasiopata namba ili wajione ni sehemu ya timu. Ndiyo moja ya siri ya mzee Alex Ferguson. Inaelekea Kim Poulsen tayari ana kuwa na watu wake hata kama wengine watafanya bidii ya namna gani ni kazi bure tu. Tunajua alikuwa na malengo hasa ya kuwandaa vijana kwa siku za usoni, lakini ili kupita vigingi kwa wakati huu alihitaji sana kutumia uzoefu wa akina Chuji kuelekea huko. Mchezaji akiona hayumo katika hesabu za mwalimu zaidi ya kukamilisha namba, matokeo yake ndiyo hayo tuliyopata dhidi ya Uganda. Kwa jinsi hali ilivyo, tuna njia mbili tu. Ama Poulsen abadilike na aambiwe kabisa na viongozi wa TFF, au kama hilo litakuwa gumu kwake, aachie ngazi aje mwalimu mwingine. Kama Poulsen ataondoka, ni vyema tukatumia kocha mzalendo wakati tunatafakari mustakabali wa siku za usoni. Akina Marsh lazima waendelee katika bench la ufundi ili kuwe na mwendelezo. Nawasiliasha
 
Unaongea kama uko kambini vile, huwezi kujua siri ya huyo fagasoni maana benchi lake lina karibu watu kumi. Fergie anaongoza klabu wakati kim yuko na timu ya taifa ambayo inaweza kubadiilika wakati wowote. Nahisi maneno yako hayana tafiti za kuyapa uzito.
 
Unaongea kama uko kambini vile, huwezi kujua siri ya huyo fagasoni maana benchi lake lina karibu watu kumi. Fergie anaongoza klabu wakati kim yuko na timu ya taifa ambayo inaweza kubadiilika wakati wowote. Nahisi maneno yako hayana tafiti za kuyapa uzito.

Wakati mwingine utafiti ni pamoja na kusoma taarifa toka vyanzo mbalimbali. Hayo ya Ferguson yapo wazi hata kwenye mahojiano yake na vyombo mbalimbali vya habari. Wataalam wengine wa soka pia wameliongelea hilo kuhusu mafanikio ya Ferguson. hatuhitaji utafiti wa kitu kilichowazi. Usemi kwamba usiongee bila utafiti si wa kuuchukulia kama kasuku tu
 
Hivi kwanini watanzania hawataki kukubali kuwa watanzania hatujui kucheza mpira?Kwa nini hatukubali kuwa ni lazima tupande halafu ndio tuvune?Je tunawachezaji wanaoweza kucheza vikombe vya afrika chini ya U17,U20 na U23?Lini tumeshiriki mashindano hayo?Kidato cha kwanza hukufika unataka degree?Tuache pa mlomo mpira ni weledi sio kusema!!
 
Hivi kwanini watanzania hawataki kukubali kuwa watanzania hatujui kucheza mpira?Kwa nini hatukubali kuwa ni lazima tupande halafu ndio tuvune?Je tunawachezaji wanaoweza kucheza vikombe vya afrika chini ya U17,U20 na U23?Lini tumeshiriki mashindano hayo?Kidato cha kwanza hukufika unataka degree?Tuache pa mlomo mpira ni weledi sio kusema!!

Timu ikifanya vizuri mechi kadhaa hakuna anayeona U17, U20 na U23. Tatizo liko hapo. Hii timu iliyopo huo ndiyo msingi wake. Wengi ni vijana na ndio maana akina Chuji wanawekwa benchi na akina Domayo. Hata ukiwa na hizo U.. uongozi pia una umuhimu wake, mbinu za mpira, nani acheze na timu ipi kwa sababu gani, lini kubadili mbinu kutegemeana na timu pinzani. Kocha lazima awe na namna ya kuwafanya wachezaji wengi wafurahie kucheza chini yake. Wale wanaopata namba na wengine. Kutokuwepo wachezaji wawili, watatu isiwe sababu. Katika mpira kuna kuumia. Hapo option inakuwa nini?
 
Ilo la kusema eti wako kwenye mfungo wa Radhaman nadhani hapo ni kosa kubwa sana. Ijulikane kuwa mashindano ya kuwakilisha nchi ni sawa na vita. Huwezi kushindwa kupigana vita na adui yako akakushambulia kisa eti umefunga, mpira hivyo, unajua kabisa nguvu yako ndio ushindi halafu unafunga na mwisho wa yote unakosa pumzi na adui yako anakupiga, nashindwa katika mfungo wako utakuwa umekosa suna mbele ya Mwenyezi Mungu.
 
Bila kuwekeza kuanzia chini kila kocha tutamuona hafai,na pia baadhi ya wachezaji wetu awajitambui kabisa,hiyo yote ni kwa vile wamekosa malezi ya kisoka!
 
Taifa Stars – tatizo ni Kim Poulsen?
Taifa Stars imetolewa na tayari wadau wanatoa sababu mbalimbali hasa ikizingatiwa katika siku za karibuni ilionekana kufanya vema kwenye mechi za kujipima nguvu dhidi ya Zambia na Cameron. Moja ya sababu ambayo imeandikwa kwenye gazeti la Mwananchi ni wachezaji kutojituma. Wametajwa akina Chuji, Bocco na Sure Boy. Kama hayo yanayoelezwa ni ya kweli basi huenda kocha wa timu yetu, Kim Poulsen ana matatizo ya "Man Management" Tofauti za siku za nyuma wakati wa FAT ya akina Ndolanga, sote tunajua wachezaji hawakuwa na motisha ya kuchezea timu ya taifa, labda kwa ajili ya uzalendo tu. Viongozi pia walichangia sana kwa kutoa vitisho na kuwapiga maarufu baadhi ya wachezaji kuchezea timu ya taifa. Ilikuwa kama timu binafsi ya Ndolanga. Sasa wakati huu kuna wadhamini wa uhakika na kambi za maandalizi za kiwango kizuri, kwa nini wachezaji wasitake kuchezea timu ya taifa?. Angalau Chuji alieleza sababu za msingi maana alijiona ni mtu wa kukamilisha namba tu lakini hakuwa na matumaini ya kucheza. Hali kama hii ilimtokea Michael Carrick wa Uingereza akaamua kujitoa japo sasa karejea baada ya kuhakikishiwa uwezekano wa kucheza. Sababu za Sure Boy na Bocco bado ni kitendawili . Yote hayo yanaashiria kuna walakini katika namna Kim Poulsen anavyohusiana na wachezaji (Man management). Imefika mahali wengine wanajiona hawana thamani kwenye timu na hilo ni kosa kubwa sana kwa kocha. Mwalimu lazima awe na uwezo wa kuwaweka sawa hata wale wasiopata namba ili wajione ni sehemu ya timu. Ndiyo moja ya siri ya mzee Alex Ferguson. Inaelekea Kim Poulsen tayari ana kuwa na watu wake hata kama wengine watafanya bidii ya namna gani ni kazi bure tu. Tunajua alikuwa na malengo hasa ya kuwandaa vijana kwa siku za usoni, lakini ili kupita vigingi kwa wakati huu alihitaji sana kutumia uzoefu wa akina Chuji kuelekea huko. Mchezaji akiona hayumo katika hesabu za mwalimu zaidi ya kukamilisha namba, matokeo yake ndiyo hayo tuliyopata dhidi ya Uganda. Kwa jinsi hali ilivyo, tuna njia mbili tu. Ama Poulsen abadilike na aambiwe kabisa na viongozi wa TFF, au kama hilo litakuwa gumu kwake, aachie ngazi aje mwalimu mwingine. Kama Poulsen ataondoka, ni vyema tukatumia kocha mzalendo wakati tunatafakari mustakabali wa siku za usoni. Akina Marsh lazima waendelee katika bench la ufundi ili kuwe na mwendelezo. Nawasiliasha

What I can say is this: Hata waje YESU na Mtume Mohamed wawe makocha, we will never make it: BECAUSE we are unteachable!
 
poulsen is not to blame....blame the public who dnt understand the game. many were happy with the results against cameroun na zambia but those wer frendlies. in frendlies the focus is on experimenting...tactics formations player combination not winning. so never judge a team by frendlies. hilo ndio tatizo la public that knows lettle abt this game. we therefore created false hope concerning our teams ability.

our true ability was shown during the cecafa competition. i wrote extensively abt our matches and the main issue was our inability to compete in central midfield especially in a 3 v 3 situation.

credit has to go to poulse for recognizing that and the way stars plays is a reflection of that weakness. kiemba is fielded as w wide attacker but playes central thus making it 4 central midfielders. this is wat has contribute heavily to stars dominating possession in some of the matches. knowing that most team play a 4231 formation a 3v 3 situation is inevitable so that was poulsen way of overcoming his midfielders inability to compete in midfield tho it did create a false impression of dominance. the natural effect was that it created a weakness down the ryt handside as the fullback nyoni had to play as a wingback and ivory coast exposed this weakness with their rapid transitions. so poulsen has nor fault with regards to the tactics since he cnt do match abt players inability. this is largely down to our league that still is fixcated with the 442 or 4132. so playerz arent accustomed to the scenarios they face in international competition.

with regards to man msnagement...i cnt comment much because no day to day working with him but his decision to drop chuji for domayo was correct.

the issue to fully understand here is that IN INTERNATIONAL COMPETITION WHERE FEILDING THREE CENTRAL MIDFIELDS IS THE NORM STARS INABILITY TO COMPETE IN A 3 V 3 SITUATION DUE TO TECHNICAL AND TQCTICAL UNDERSTANDING WILL ALWAYS BEEN ITS DOWNFALL. UNTIL WE ARE ABLE TO PRODUCE QUALITY MIDFIELDERS WE SHULD FORGET ABT WINNING. POINT NOT THE FINGER AT POULSEN BUT AT THE COACHES THAT COACH IN THE LEAGUE.
 
Hivi kwanini watanzania hawataki kukubali kuwa watanzania hatujui kucheza mpira?Kwa nini hatukubali kuwa ni lazima tupande halafu ndio tuvune?Je tunawachezaji wanaoweza kucheza vikombe vya afrika chini ya U17,U20 na U23?Lini tumeshiriki mashindano hayo?Kidato cha kwanza hukufika unataka degree?Tuache pa mlomo mpira ni weledi sio kusema!!

wee umenena...sisi hatujui mpira. hizo competitio ulizotaji kila leo first round elimination
 
kifupi hatuna kocha na kinachosikitisha zaidi kocha hakupewa target kama kocha anafanya vibaya kuliko wa nyuma yake kwa nchi nyingine ni direct fire!!!! hata kwa uwezo mdogo tulionao kocha kama marcio marximo alitufikisha chan ilitakiwa na huyu atupeleke na twende mbele zaidi sio kushangilia kushinda mechi za majaribio!!! fire this guy bring back marcio marximo
 
mbona sababu haziishagi kwenye sekta ya michezo watanzania?
 
"Katiba ijayo lazima sasa iondoe kinga kwa marais ili mtu yeyote aweze kumshtaki Rais na hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa," Mateo Qaresi.
 
Back
Top Bottom