Napenda kuwapa tahadhari Dr Slaa na Mbowe vurugu zote zinazoendela hapa mtandaoni walengwa wa kuu ni nyie. Mzee wa Pembe za ndovu anapambana kufa na kupona baada ya kugundua kuwa chama chake kipo kwenye hali mbaya kabisa hasa baada ya kutambua kuwa hakiwezi kupambana tena na CHADEMA kwa hoja. Huyo jammaa ametengeneza kukundi kidogo cha kupambana na CHADEMA mitandaoni kwa kujisajili kwa ID mbalimbali. Kikundi hicho kimepewa kazi ya kushinda JF kujenga hoja za kuichafua CHADEMA. Lengo kuu la huyu strategist wa magamba ni kuhakikisha mmoja wenu anaingia kwenye malumbano na Mtu wao waliomtengeneza ili kuipunguza nguvu CHADEMA, kwa hiyo mkakati wao ni wa long term kupambana mpaka 2014 kuhakikisha mnaoingia kwenye mgogoro wa kurushiana maneno na huyo mtu wao. Naomba mjiulize mtu huyu alishasema hatagombea uongozi wowote ndani ya chama hata nje ya chama lakini wao wanampamba kuwa anachukiwa kwa kuwa anautaka U/nyekiti, upi huo na alishasema hagombei.Kuelekea 2014 jiandaeni kisawasawa mtapitishwa kwenye tanuru la moto kuliko hivi sasa. Jipeni moyo kwa kuwa mkipita hapo ukombozi ndio utakuwa umekaribia. Pale Makoa Makuu msimwamini yeyote mbinu zinazotumiwa ni za hali ya juu katika kuwanunua viongozi wenu kuweni na utaratibu wa kutilia shaka kila dalili zinapojitokeza ni wakati wa kukesha bila hivyo mtakatwa ki-dizaini mzee wa pembe za ndovu si mchezo.