Tahadhari BAVICHA

Tahadhari BAVICHA

kailakarama

Member
Joined
Aug 30, 2014
Posts
73
Reaction score
30
Vijana ndiyo moyo wa chama ila moyo huu ufa pale chama kinapopata Mwenyekiti wa vijana aliyepwaya.

Kitengo cha vijana wa NCCR chini ya Mwenyekiti Deo Meck kimekufa kabisa ni ukweli usiopingika hakuna mtu anahamu ya kujiunga nao na Kama siyo kina Kafulila chama hiki tungekuwa tumekisahau kabisa.

Jumuiya ya vijana ya CUF chini ya Mwenyekiti Katani A Katani nayo iko taabani imepoteza dira na haina muelekeo ni Kama vile Lipumba ndiyo Mwenyekiti wa kila kitu CUF maana hao vijana hawapo kabisa.

Umoja wa vijana wa CCM chini ya Mwenyekiti Sadifa Hamisi Juma nayo imepwaya mno na pia imepoteza mpaka mvuto unaweza sema bora rizwan ndiye angekuwa Mwenyekiti wao
Nawapa tahadhari CHADEMA mnaenda kuchagua Mwenyekiti wa Bavicha makosa mliyofanya 2009 msiyarudie tena:-
1. mkachague Kijana siyo mnachagua Mzee halafu mnalazimisha kuwa ni kijana
2.kiukweli Daniel Naftal na Philipo Mwakibinga ni wepesi sana kiuwezo ila kazi Kwenu
3.kachagueni Mwenyekiti wa vijana na siyo kipenzi cha viongozi wa makao makuu kufanya hivyo mtarudia yaleye ya 2009.
Ngome ya vijana wa ACT chini ya Mwenyekiti Grayson Manyori Nyakarungu (Brigedia) ni moto wa kuotea mbali bado sijaona Mwenyekiti anayemfikia japo kwa 50%.
 
Ulitaka kutoa ushauri mzuri,ulipoingiza mambo ya ACT umekuwa ni umbeya na si ushauri tena.
 
Ulitaka kutoa ushauri mzuri,ulipoingiza mambo ya ACT umekuwa ni umbeya na si ushauri tena.

Hata mimi nimeshituka. Alikuwa anakuja vizuri, lakini ghafla akapotea alipoleta mambo ya ACT Tanzania chama cha siasa ambacho kiukweli sidhani hata kama kimepata usajili wa kudumu!!

Halafu baadaye nikaangalia tarehe aliyojiunga hapa JF katika jukwaa hili, hilo pia likaithibitisha hofu yangu kabisa kuwa iko sahihi......ni wiki moja iliyopita, Tarehe 30/8/1014!!
 
Kama roho imekuuma kusikia neno ACT basi we utakua ni mgonjwa wa akili.

Mtoa mada kawapa ushauri mulua kazi kwenu kusuka au kunyoa. Kama adui yako kajipanga vizuri hupendi kusikia akipewa sifa? Tete te hte teh teh.... bavicha kwa wivu hamtofautiani na wanawake.
 
Hata mimi nimeshituka. Alikuwa anakuja vizuri, lakini ghafla akapotea alipoleta mambo ya ACT Tanzania chama cha siasa ambacho kiukweli sidhani hata kama kimepata usajili wa kudumu!!

Halafu baadaye nikaangalia tarehe aliyojiunga hapa JF katika jukwaa hili, hilo pia likaithibitisha hofu yangu kabisa kuwa iko sahihi......ni wiki moja iliyopita, Tarehe 30/8/1014!!

Uko makini sana mkuu! Dah
 
Greson Manyori Nyakarungu ana kitu gani zaidi ya usaka tonge. Hopeless. ...
 
Umejitahidi kutuzuga,na kwabahati mbaya umewaharibia hata hao wagombea ulowataja!Naona unakaharufu ka usaliti na umewanukisha na hao wenzio.
 
Huu uzi ulilenga kuviponda vyama vingine na kuwapromoti wazee wa miba ACT.
 
Huyo daniel naftali kwakweli ataua chama. Maneno mengi bila utekelezaji. Hafai hafai hafai
 
Umeanza vizuri ila ulipofika mwisho umeongea kama umekatwa kichwa!!!!
 
Back
Top Bottom