Tafsiri sahihi ya uzalendo kwamba ni Kuilinda nchi yetu Tanzania dhidi ya serikali hii ya CCM

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,242
34,903
Mabingwa wa kutukana matusi mitandaoni, vijana wa Chama cha mapinduzi CCM, mngeanza kujitukana wenyewe leo basi, kabla hamjaanza kumshangilia Rais Magufuli kwa kumuondoa kazi aliyekuwa waziri wa nishati na madini Pro. Muhongo (Mb).

Wapinzani tulipoisukuma serikali wakati wa sakata la Escrow, kwamba imuwajibishe Pro. Muhongo, mlikaza mishipa ya shingo kumtetea na kumsifu kwamba ni Jembe, mzalendo msomi na mchapa kazi. Leo mmekuwa kama Bendera fuata upepo.

Uundaji wa kamati za ...kuchunguza wizi kuhusu madini tumelisema sana, lakini CCM imekuwa na kiburi kuliko hata ibilisi. Hotuba mbalimbali zilizowasilishwa na wasemaji wa kambi ya upinzani bungeni zimekuwa zikikataliwa kwa kisingizio kwamba zina uchochezi, uchochezi kwasababu tu zimeandika ukweli wa wizi katika sekta ya madini, lakini watanzania walikuwa wanaona. Leo tunashuhudia yale yale yaliyopiganiwa na wapinzani miaka mingi, tunampongeza na kumtukuza mtu mmoja kama kwamba mambo haya ni mapya.

Laiti kama ushauri wetu ungelikuwa unasikilizwa na kufanyiwa kazi, nchi hii ingefika mbali sana, lakini tumefika hapa kwasababu ya kiburi cha serikali ya CCM, na ushabiki wa wabunge wa chama hicho na wanachama wake wanaodumisha fikra za Mwenyekiti wao.

Watanzania lazima wafahamu kwamba, serikali inaweza kuyakusanya madini, kama ilivyofanya kwenye makusanyo ya mapato, ikajilimbikizia yenyewe, na wananchi wasinufaike hata kidogo, na umasikini ukaendelea kushamiri.

Nawakumbusha tena tafsiri sahihi ya UZALENDO, kwamba ni; Kuilinda nchi yetu Tanzania dhidi ya serikali hii ya CCM.
 
Kuna kitu nilikisema na leo narudia tena, tatizo kuu ,adui mkubwa kuliko maadui wote katika hii nchi ni CCM. Hata kama tutaondoa mawaziri wote hatuwezi kupiga hatua kama kuna mdudu ccm. Utafukuza Muhongo bado utateua kina makonda na Gambo. Ukombozi wa kweli ni kuondoa ccm madarakani na kuchagua watu wengine makini hata akiwa mgombea binafsi. Ila bora JPM anafanya mengine ambayo hata maccm hawayapendi kwa manufaa ya taifa.
 
Mkuu Mwanahabari Huru naunga mkono hoja yako. Ifikie wakati sasa watanzania wajitambue na waanchane na ushabiki wa kisiasa waangalie maslahi ya taifa zaidi. Sio mara moja tu kambi ya upinzani imekuwa ikiimamba kuna uozo katika sekta ya madini. Ni mara nyingi wapinzani wameshatoa matamko kuwa waziri muhongo hatakiwi pale, toka enzi za awamu ya nne. Sasa cha kushangaza watawala wetu waliamua kuunda ‘tume’ kufuatilia kinachoitwa usafirishaji wa michanga kwenda nje ya nchi. Hili la kusafirishwa michanga sio geni kwa hapa Tanzania. Limekuwepo kitambo tu. Hii tume iliyoundwa sijaona ilichokifanya zaidi ya kutekeleza tu matakwa ya kisiasa. Kama kungekuwa na weledi katika utendaji nchini Tanzania haikuwa na haja ya kuunda tume, utekelezaji ungeshafanyika kitambo.

Kwa upande wangu naona ni sinema tu linachezwa, watawala wanacheza kwa nguvu na madaha ili watazamaji wawashangilie na kusema “hapa sasa tumepata wachezangoma mahiri kabisa”.
 
Mabingwa wa kutukana matusi mitandaoni, vijana wa Chama cha mapinduzi CCM, mngeanza kujitukana wenyewe leo basi, kabla hamjaanza kumshangilia Rais Magufuli kwa kumuondoa kazi aliyekuwa waziri wa nishati na madini Pro. Muhongo (Mb).

Wapinzani tulipoisukuma serikali wakati wa sakata la Escrow, kwamba imuwajibishe Pro. Muhongo, mlikaza mishipa ya shingo kumtetea na kumsifu kwamba ni Jembe, mzalendo msomi na mchapa kazi. Leo mmekuwa kama Bendera fuata upepo.

Uundaji wa kamati za ...kuchunguza wizi kuhusu madini tumelisema sana, lakini CCM imekuwa na kiburi kuliko hata ibilisi. Hotuba mbalimbali zilizowasilishwa na wasemaji wa kambi ya upinzani bungeni zimekuwa zikikataliwa kwa kisingizio kwamba zina uchochezi, uchochezi kwasababu tu zimeandika ukweli wa wizi katika sekta ya madini, lakini watanzania walikuwa wanaona. Leo tunashuhudia yale yale yaliyopiganiwa na wapinzani miaka mingi, tunampongeza na kumtukuza mtu mmoja kama kwamba mambo haya ni mapya.

Laiti kama ushauri wetu ungelikuwa unasikilizwa na kufanyiwa kazi, nchi hii ingefika mbali sana, lakini tumefika hapa kwasababu ya kiburi cha serikali ya CCM, na ushabiki wa wabunge wa chama hicho na wanachama wake wanaodumisha fikra za Mwenyekiti wao.

Watanzania lazima wafahamu kwamba, serikali inaweza kuyakusanya madini, kama ilivyofanya kwenye makusanyo ya mapato, ikajilimbikizia yenyewe, na wananchi wasinufaike hata kidogo, na umasikini ukaendelea kushamiri.

Nawakumbusha tena tafsiri sahihi ya UZALENDO, kwamba ni; Kuilinda nchi yetu Tanzania dhidi ya serikali hii ya CCM.

Still shifting the goal post! Mwanzo ilikuwa tunaibiwa, sasa report imetoka mnaweza santuri nyingine kuwa shida ni CCM!
Ushauri, tatizo ni kutojua unasimamia nini.
 
Mabingwa wa kutukana matusi mitandaoni, vijana wa Chama cha mapinduzi CCM, mngeanza kujitukana wenyewe leo basi, kabla hamjaanza kumshangilia Rais Magufuli kwa kumuondoa kazi aliyekuwa waziri wa nishati na madini Pro. Muhongo (Mb).

Wapinzani tulipoisukuma serikali wakati wa sakata la Escrow, kwamba imuwajibishe Pro. Muhongo, mlikaza mishipa ya shingo kumtetea na kumsifu kwamba ni Jembe, mzalendo msomi na mchapa kazi. Leo mmekuwa kama Bendera fuata upepo.

Uundaji wa kamati za ...kuchunguza wizi kuhusu madini tumelisema sana, lakini CCM imekuwa na kiburi kuliko hata ibilisi. Hotuba mbalimbali zilizowasilishwa na wasemaji wa kambi ya upinzani bungeni zimekuwa zikikataliwa kwa kisingizio kwamba zina uchochezi, uchochezi kwasababu tu zimeandika ukweli wa wizi katika sekta ya madini, lakini watanzania walikuwa wanaona. Leo tunashuhudia yale yale yaliyopiganiwa na wapinzani miaka mingi, tunampongeza na kumtukuza mtu mmoja kama kwamba mambo haya ni mapya.

Laiti kama ushauri wetu ungelikuwa unasikilizwa na kufanyiwa kazi, nchi hii ingefika mbali sana, lakini tumefika hapa kwasababu ya kiburi cha serikali ya CCM, na ushabiki wa wabunge wa chama hicho na wanachama wake wanaodumisha fikra za Mwenyekiti wao.

Watanzania lazima wafahamu kwamba, serikali inaweza kuyakusanya madini, kama ilivyofanya kwenye makusanyo ya mapato, ikajilimbikizia yenyewe, na wananchi wasinufaike hata kidogo, na umasikini ukaendelea kushamiri.

Nawakumbusha tena tafsiri sahihi ya UZALENDO, kwamba ni; Kuilinda nchi yetu Tanzania dhidi ya serikali hii ya CCM.

"Nampenda sana Prof Mhongo lakini pia ni rafiki yangu, lakini kwenye hili, ajifikirie..." Hayo ni maneno aliyotamka leo Rais John Magufuli wakati wa kupokea ripoti ya mchanga. Kama Rais Magufuli angewasikiliza vizuri wapinzani walipokuwa wanapinga uteuzi alioufanya, kumrejesha Prof. Mhongo kwenye wizara ya Madini na Nishati wakati tayari alikwishashughulikiwa na Bunge katika serikali ya awamu ya nne, kwa hoja na ushahidi, na kama angekuwa anaheshimu maamuzi hayo ambayo naye alikuwemo kama waziri wa Ujenzi, basi kusingekuwa na haja ya kutamka maneno hayo hapo juu leo hii. kwamba anampenda sana Prof. Muhongo, kwamba ni rafiki yake, inawezekana hizi pekee ndio zilikuwa sababu za kumrejesha "mheshimiwa" huyu ambaye tayari alishaonekana hafai. Muhongo alikuwa hafai katika awamu ya nne, na bado hafai hata hivi sasa, ila ushosti na kiburi ndio vilimfanya aendelee kumng'ang'ania.

Tunaweza pia kusema hayo hayo kwa mtu anayeitwa Albert Bashite. bado naisubiri siku ambayo Magu atatamka, iwe ni kimoyomoyo, au hadharani, kwamba "Nampenda sana Paul Makonda lakini pia ni rafiki yangu, lakini kwenye hili, ajifikirie..."
 
Still shifting the goal post! Mwanzo ilikuwa tunaibiwa, sasa report imetoka mnaweza santuri nyingine kuwa shida ni CCM!
Ushauri, tatizo ni kutojua unasimamia nini.
Hakuna kusogeza magoli bado bao halijafungwa ndio kwanza match inaanza. Yes amegundua kulikiwa kuna wizi, nini kinafuata? Nini kitawazuia wengine kufanya wanavyotaka kama walio kuwepo hawajafanywa chochote?
 
Still shifting the goal post! Mwanzo ilikuwa tunaibiwa, sasa report imetoka mnaweza santuri nyingine kuwa shida ni CCM!
Ushauri, tatizo ni kutojua unasimamia nini.
Ni hivi, ni kweli tunaibiwa. sasa ukiuliza kwa nini tunaibiwa miaka nenda miaka rudi, hapo ndio jibu zuri kabisa linakuja: CCM. tatizo hasa sio kuibiwa. mtu yeyote anaweza kuibiwa. nchi yoyote inaweza kuibiwa. tatizo ni kuibiwa miaka nenda miaka rudi, huku wote: anayeiba, anayeibiwa, na watazamaji, wote wanajua kwamba wizi unafanyika, lakini bado mwizi anendelea kuiba, na anayeibiwa bado anaendelea kuibiwa, na watazamaji nao wanaendelea kuangalia. hapo ndio jibu la CCM linakuja, na hapo ndio pa kuanzia kupata ufumbuzi wa kweli. maana hizi zote ni sinema tu. Kama Muhongo alionekana kapiga hela na hana ufanisi wakati wa awamu ya nne, na Magu akishuhudia vikao vile vya bunge, na kushiriki pia, inakuwaje alipopata urais tu akamrejesha? halafu leo anamwondoa tena, sisi tupige makofi? si tutaonekana wote hatuna akili? asiye na akili, asiye na uzalendo, mwizi, chanzo cha matatizo yote, ni CCM.
 
"Nampenda sana Prof Mhongo lakini pia ni rafiki yangu, lakini kwenye hili, ajifikirie..." Hayo ni maneno aliyotamka leo Rais John Magufuli wakati wa kupokea ripoti ya mchanga. Kama Rais Magufuli angewasikiliza vizuri wapinzani walipokuwa wanapinga uteuzi alioufanya, kumrejesha Prof. Mhongo kwenye wizara ya Madini na Nishati wakati tayari alikwishashughulikiwa na Bunge katika serikali ya awamu ya nne, kwa hoja na ushahidi, na kama angekuwa anaheshimu maamuzi hayo ambayo naye alikuwemo kama waziri wa Ujenzi, basi kusingekuwa na haja ya kutamka maneno hayo hapo juu leo hii. kwamba anampenda sana Prof. Muhongo, kwamba ni rafiki yake, inawezekana hizi pekee ndio zilikuwa sababu za kumrejesha "mheshimiwa" huyu ambaye tayari alishaonekana hafai. Muhongo alikuwa hafai katika awamu ya nne, na bado hafai hata hivi sasa, ila ushosti na kiburi ndio vilimfanya aendelee kumng'ang'ania.

Tunaweza pia kusema hayo hayo kwa mtu anayeitwa Albert Bashite. bado naisubiri siku ambayo Magu atatamka, iwe ni kimoyomoyo, au hadharani, kwamba "Nampenda sana Paul Makonda lakini pia ni rafiki yangu, lakini kwenye hili, ajifikirie..."
Hata akitoa its tooo late kachelewa sanaaa
. Acha ccm ni adui mkubwa
 
Ahaaa.......kumbe..ivi muhongo ndo nan?.....[HASHTAG]#tanzania[/HASHTAG] ya viwanda tunaibiwa mabilioni tunabakisha vyerehani tunaita viwanda
 
Back
Top Bottom