Tafakuri ya leo

Mungu alimuumba Adam kisha akampulizia pumzi ya uhai.

Hivyo alianza kuumba mwili kisha ndio aka upa uhai ambaye ni roho.

Roho hukaa mwilini na siyo moyoni.

Inasema Mungu alisema na tumuumbe mtu kwa mfano wetu na wakamuumba Adam, kisha wakampulizia punzi wakampa uhai naamini mwili ni utupu bila pumzi ya Mungu.

Sijui Adam ni jina la ubatizo au ndio jina la asili ila twende hivyo hivyo.

Na ile pumzi ndiye roho na ndio uhai utwaliwao na kuucha mwili mauti yanapofika.
 
Askofu anasema kwamba kwa mujibu wa masomo ya theology Roho ilikuwepo kabla ya mwili kwa hio kilichoanza kwenye uumbaji wa Mungu ni Roho sio Mwili

Askofu anasisitiza zaidi watu tusiishi kwa matendo ya kimwili bali tuishi kwa matendo ya kiroho maana Mungu anaishi Rohoni sio Mwilini

Sijasema mimi amesema Askofu
 
Mwili uliumbwa kwanza kisha ukapuliziwa uhai, uhai uliopuliziwa ndiye roho.

Inaonekana roho au uhai hauwezi kuishi kwenye utupu bali mwilini.

Kama roho anaweza kuishi lwenye utupu basi sijui tafsiri ya uhai ni nini kwa binadamu.
 
Mwili uliumbwa kwanza kisha ukapuliziwa uhai, uhai uliopuliziwa ndiye roho.

Inaonekana roho au uhai hauwezi kuishi kwenye utupu bali mwilini.

Kama roho anaweza kuishi lwenye utupu basi sijui tafsiri ya uhai ni nini kwa binadamu.
Askofu anasema, huo Uhai ulikuwepo kabla ya Mwili kuumbwa baada ya huo Uhai Mungu akaumba mwanadamu mwenye mwili ndani ya mwili ikafungiwa Roho ndani ila Roho ilikuwepo kabla ya Mwili kuwepo yenyewe ilikuwepo tu

Sijasema mimi amesema Askofu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…