Tafakari ya Pasaka

Dr Adam Francis

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
479
Reaction score
716
[Zab130:3] BWANA, kama Wewe ungehesabu maovu, nani angesimama?

[Zab51:3] Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima

[Zab51:4]Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, Na kufanya maovu mbele za macho yako.

[Zab51:5]Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani.

[Rum7:19]Lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo.

[Rum7:24]Ole wangu, maskini mimi! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?

[Ayu9:29]Nitahukumiwa kuwa ni mkosa; Ya nini basi nitaabike bure?

[Ayu9:32]Kwani yeye si mtu, kama mimi, hata nimjibu, Hata tukaribiane katika hukumu.

[Ayu9:33]Na hapana mwenye kuamua katikati yetu, Awezaye kutuwekea mkono sote wawili.

[Ayu33:23]Kwamba akiwapo malaika pamoja naye, Mkalimani, mmoja katika elfu;

[Ayu33:24]Ndipo anioneapo rehema, na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake

[Ayu33:28]Yeye ameikomboa nafsi yangu isiende shimoni, Na uhai wangu utautazama mwanga.

[Omb3:21]Najikumbusha neno hili,
Kwa hiyo nina matumaini.

[Ombo3:22]Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.

[Ombo3:23]Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wake ni mkuu.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…