Tafakari kidogo

Tafakari kidogo

Kitimbwisi

Senior Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
155
Reaction score
72
HEBU CHUKUA DAKIKA KADHAA KUTAFAKARI KUHUSU HILI.

Kila Siku Tunaingia Kwenye Maduka Makubwa Ya Nguo Na Supermarkets Na Tunalipa Bei Ileile Iliobandikwa Pale Kwenye bidhaa husika. Lakini Cha Ajabu Tunapopita Mitaani Kununua Ndizi, Mchezo Wetu Wa Kuomba Kupunguziwa Bei (Bargaining) Hauna Kipimo. Mjane Masikini Mwenye Watoto 12 Wanaomtegemea Anakwambia Ndizi Moja Ni 200,

Anajaribu Kukueleza Ni Jinsi Gani Ilivokuwa Ngumu Kununua Hizo Ndizi, Anakueleza Jinsi Gani Hali Ya Maisha Ilivo Ngumu Saivi, Lakini Tunalazimisha, '' Usiponiuzia Kwa Sh. 100 Sichukui'', Na Kwa Jeuri Unaamua Kuondoka Zako. Lakini Kwa Kuwa Kwake Nusu Ya Mkate Ni Afadhali Kuliko Kutokuwa Na Kitu, Analazimika Kukuita Na Kukuuzia Kwa Bei Ndogo Au Bila Faida Kabisa. Moyoni Mwake Analia, Ana Wasiwasi Ni Jinsi Gani Ataweza Kuishi Wa Wanawe. Kimyakimya Anajipa Moyo, Ipo Siku Mungu Atamfungulia Njia Huku Wewe Ukiimega Ndizi Kwa Majigambo.

Hebu Chukua Mda Kidogo Tafakari Kuhusu Hili. Tusipende Ku Bargain Sana Na Watu Kama Hawa. Wanafanya Hizo Biashara Sio Kwa Ajili Ya Kununua Nguo, Viatu Au Magari Ya Kifahari Bali Ni Kwa Ajili Ya Kuishi Na Kulisha Watoto Wao.
 
ni kawaida ya binadam kusahau alipotoka akipata nafasi, kuna mdau humu juzi kasema hawezi fanya kazi mwezi mzima akisubiria vipande vyekundu vya fedha ambavyo havifiki hata mia
 
HEBU CHUKUA DAKIKA KADHAA KUTAFAKARI KUHUSU HILI.

Kila Siku Tunaingia Kwenye Maduka Makubwa Ya Nguo Na Supermarkets Na Tunalipa Bei Ileile Iliobandikwa Pale Kwenye bidhaa husika. Lakini Cha Ajabu Tunapopita Mitaani Kununua Ndizi, Mchezo Wetu Wa Kuomba Kupunguziwa Bei (Bargaining) Hauna Kipimo. Mjane Masikini Mwenye Watoto 12 Wanaomtegemea Anakwambia Ndizi Moja Ni 200, Anajaribu Kukueleza Ni Jinsi Gani Ilivokuwa Ngumu Kununua Hizo Ndizi, Anakueleza Jinsi Gani Hali Ya Maisha Ilivo Ngumu Saivi, Lakini Tunalazimisha, '' Usiponiuzia Kwa Sh. 100 Sichukui'', Na Kwa Jeuri Unaamua Kuondoka Zako. Lakini Kwa Kuwa Kwake Nusu Ya Mkate Ni Afadhali Kuliko Kutokuwa Na Kitu, Analazimika Kukuita Na Kukuuzia Kwa Bei Ndogo Au Bila Faida Kabisa. Moyoni Mwake Analia, Ana Wasiwasi Ni Jinsi Gani Ataweza Kuishi Wa Wanawe. Kimyakimya Anajipa Moyo, Ipo Siku Mungu Atamfungulia Njia Huku Wewe Ukiimega Ndizi Kwa Majigambo.
Hebu Chukua Mda Kidogo Tafakari Kuhusu Hili. Tusipende Ku Bargain Sana Na Watu Kama Hawa. Wanafanya Hizo Biashara Sio Kwa Ajili Ya Kununua Nguo, Viatu Au Magari Ya Kifahari Bali Ni Kwa Ajili Ya Kuishi Na Kulisha Watoto Wao.
tumekuelewa sana,mentally slave imetu`addict,tukijitambua tutaenda sawa mkuu...ila pameuma!
 
Hao ni wengi sana na hawajihurumii wenyewe, ikifika wakati wa uchaguzi ni hao hao wanaoipigia kura ccm, na ikishinda inawatimua maeneo wanayofanyia biashara, waache waisome namba
 
Back
Top Bottom