Tabora: Wapiga ramli chonganishi 27 wakamatwa

kirerenya

JF-Expert Member
Aug 27, 2013
1,696
2,253
ramli.png

Kufuatia matukio ya ukatili dhidi ya wazee vikongwe kuongezeka mkoani Tabora, yanayosababishwa na imani za kishirikina, Jeshi la polisi mkoani humo limeazimia kuyamaliza, kwa kuwakamata wapiga ramli chonganishi ambapo tayari wamekamatwa wapiga ramli 27 wakiwa na matunguli na madawa mbali mbali yanayotumika kwa shughuli hizo.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari mkoani Tabora kamanda wa polisi mkoani humo,Kamishina Msaidizi Mwandamizi Willbroad Mtafungwa amesema kuwa, baada ya kufanyika msako huo na upelelezi dhidi yao waganga hao wengine wamebainika kupiga ramri chonganishi na wengine kufanya shughuli hizo bila kibali.

Aidha katika hatua nyingine Kamanda wa polisi amesema kuwa,kumezuka vikundi vya vijana waarifu ambao wamekuwa wakiwapora wananchi mali zao huku wakiwajeruhi kwa vitu vyenye ncha kali wanaojiita changia dogo,ambapo wamekamatwa viijana wapatao 17,watafikishwa mahakamani kutokana na kukiri makosa yao.

Chanzo: ITV
 
Back
Top Bottom