Taasisi ya urais ijiepushe na sifa katika kesi za jinai

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
40,432
73,078
Akizungumza na Wakuu wa mikoa na wilaya wapya Mtukufu Rais alisema tena kwa dhati kuwa wamemkamata mfanya biashara aliyekuwa anaiba milioni 7-8 kila dakika na kuwa keshatuibia matrilioni na kuwa yuko mikono salama sasa hivi.

Hilo ni tangazo la Rais kwa umma. Leo vyombo vinavyo husika vimesema jina la mtu huyo na kuwa ni jumla ya kama bilioni 29 ndio zimeibiwa tofauti na tangazo la matrilioni la Rais.

Kwa vile Rais ndiye akiyetangaza basi vyombo vya habari vilimsifia yeye kuwa kakamata wezi hao na mafisadi wakubwa (ingawa kiasi kina walakini na uhalisia)na kuwa hizo ni juhudi zake.

Hofu yangu ni kuwa, hayo ni makosa ya jinai na yalipaswa yatangazwe na vyombo husika kwanza kisha yeye afanye rejea katika hotuba zake kwani hizi kesi za jinai zaweza kuja kukosa ushahidi wa kutosha na serikali kushindwa na picha itakuwa Rais kashindwa kesi.

Ndio yaweza kuwa habari kama hiyo inaleta sifa kwa Rais kisiasa lakini awe makini na sifa za aina hiyo. Hatutaki kuona baadae anaaibika.
Kwanza kwa taarifa yake kuwa wizi wa milioni 7-8 kwa dakika na kuwa ni matrilioni ulishaleta taharuki lakini pia umemuaibisha mtukufu Rais wetu kuwa alitoa taarifa ya uongo.

Aachie wahusika wayatangaze wao.
 
Acha zako, unadhani Rais hajui hicho kiasi? unajua ni makampuni mangapi hadi dakika hii yamegundulika?

Mimi nipo kitengo maalumu tulieni, Rais yupo sahihi, tulieni baada ya muda vyombo husika vitatoa tena taarifa.

Cha msingi tuungane kwa pamoja kujenga nchi yetu, hili si swala la Rais pekee, tumsaidie Mh. Rais tafadharini
 
yani kila anapofungua kinywa chake tu lazima utokee mkanganyiko,rais wangu uwe mfalme Suleiman japo kwa baadhi ya matukio tu.
 
Acha zako, unadhani Rais hajui hicho kiasi? unajua ni makampuni mangapi hadi dakika hii yamegundulika?

Mimi nipo kitengo maalumu tulieni, Rais yupo sahihi, tulieni baada ya muda vyombo husika vitatoa tena taarifa.

Cha msingi tuungane kwa pamoja kujenga nchi yetu, hili si swala la Rais pekee, tumsaidie Mh. Rais tafadharini
Hicho kitengo maalumu kama watu wake ni aina yako basi picha tumeipata kwa nini haya yanatokea
 
Kweli shule ni tatizo, hivi kweli ukisikiliza vizuri hiyo hotuba ya Rais kuna sehemu kasema huyo mtu alikuwa anaiba izo milioni kwa dakika? kwa ukichwa maji wako transaction na wizi na ukwepaji kodi ni kitu kimoja enh? na kama sio kitu kimoja umeandika ivyo kwa lengo lipi?
 
Akizungumza na Wakuu wa mikoa na wilaya wapya Mtukufu Rais alisema tena kwa dhati kuwa wamemkamata mfanya biashara aliyekuwa anaiba milioni 7-8 kila dakika na kuwa keshatuibia matrilioni na kuwa yuko mikono salama sasa hivi.

Hilo ni tangazo la Rais kwa umma. Leo vyombo vinavyo husika vimesema jina la mtu huyo na kuwa ni jumla ya kama bilioni 29 ndio zimeibiwa tofauti na tangazo la matrilioni la Rais.

Kwa vile Rais ndiye akiyetangaza basi vyombo vya habari vilimsifia yeye kuwa kakamata wezi hao na mafisadi wakubwa (ingawa kiasi kina walakini na uhalisia)na kuwa hizo ni juhudi zake.

Hofu yangu ni kuwa, hayo ni makosa ya jinai na yalipaswa yatangazwe na vyombo husika kwanza kisha yeye afanye rejea katika hotuba zake kwani hizi kesi za jinai zaweza kuja kukosa ushahidi wa kutosha na serikali kushindwa na picha itakuwa Rais kashindwa kesi.

Ndio yaweza kuwa habari kama hiyo inaleta sifa kwa Rais kisiasa lakini awe makini na sifa za aina hiyo. Hatutaki kuona baadae anaaibika.
Kwanza kwa taarifa yake kuwa wizi wa milioni 7-8 kwa dakika na kuwa ni matrilioni ulishaleta taharuki lakini pia umemuaibisha mtukufu Rais wetu kuwa alitoa taarifa ya uongo.

Aachie wahusika wayatangaze wao.

unataka ashindwe mara ngapi? ..kwani sukari aliifanyaje?
 
Kweli shule ni tatizo, hivi kweli ukisikiliza vizuri hiyo hotuba ya Rais kuna sehemu kasema huyo mtu alikuwa anaiba izo milioni kwa dakika? kwa ukichwa maji wako transaction na wizi na ukwepaji kodi ni kitu kimoja enh? na kama sio kitu kimoja umeandika ivyo kwa lengo lipi?
Umepiga mvinyo SAA hizi? Kesho ukishakunywa supu soma tena ulicho andika kama utakielewa
 
Acha zako, unadhani Rais hajui hicho kiasi? unajua ni makampuni mangapi hadi dakika hii yamegundulika?

Mimi nipo kitengo maalumu tulieni, Rais yupo sahihi, tulieni baada ya muda vyombo husika vitatoa tena taarifa.

Cha msingi tuungane kwa pamoja kujenga nchi yetu, hili si swala la Rais pekee, tumsaidie Mh. Rais tafadharini
Upo kitengo gani maalum wakati kuandika kwenyewe shida? Tuache kudanganyana hapa JF jamani.
 
Wewe ni ******** sana, tatizo lako ni uchama ndo unakusumbua tu, watanzania tuache mambo ya uchama, tutafika mbali sana, tumuunge mkono Rais.
Ona zoba huyu! Ni uchama gani uko kwenye andiko hili? Kumshauri MTUKUFU Rais ajiepushe na kutangaza yeye hizi kesi za jinai anbazo hazijulikani mbeleni zitakuwaje nayo ni makosa?
Pole sana, unahitaji maombi wewe ndio tiba yako
 
Acha zako, unadhani Rais hajui hicho kiasi? unajua ni makampuni mangapi hadi dakika hii yamegundulika?

Mimi nipo kitengo maalumu tulieni, Rais yupo sahihi, tulieni baada ya muda vyombo husika vitatoa tena taarifa.

Cha msingi tuungane kwa pamoja kujenga nchi yetu, hili si swala la Rais pekee, tumsaidie Mh. Rais tafadharini


Hivi watu kama nyie huwa wanakuwa ni wananchi wa Tz au wanatoka wapi?? Yani kama vile hawaoni hali halisi, ngekushauri ujitafakari tena kama wew ni mtanzania na hakuna any hidden string juu ya wew na maisha yako
 
Unaunga mkono kipi kutoka kwa huyu dikteta!? Bomoa bomoa? Kufukuza wanafunzi 8,000 wasio na hatia yoyote kisha kuwadhalilisha kwa kuwaita vilaz.a!? Kubaka demokrasi nchini ikiwemo ya Wabunge wa upinzani ndani na nje ya Bunge? Kuzuia vyama vya upinzani kufanya shughuli zao mwa miaka mitano? Kuwakingia kifua mafisadi wa lugumi, UDA, Pride, Escrow, Mv Dar, Nyumba za Serikali etc? Kwa Watanzania wanaojitambua huyu hastahili kuungwa mkono kwa sababu ni JANGA KUBWA LA TAIFA. Hakustahili na wala hana sifa ya kuiongoza Tanzania.

Wewe ni ******** sana, tatizo lako ni uchama ndo unakusumbua tu, watanzania tuache mambo ya uchama, tutafika mbali sana, tumuunge mkono Rais.
 
Back
Top Bottom