The Palm Tree
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 7,951
- 12,535
Unawalaumu Yanga SC bila kufikiria shida iko wapi...Nimeona msemaji wa Yanga anayejulikana kama Bumbuli, akitaja mechi zilizobaki katika premier kuwa ni nne tu huku alisema wao yanga hawatambui mechi ya tarehe 3.
Jambo hili kama kweli litatokea, itakuwa ni dharau kwa TFF, serikali ambayo waziri wake alishiriki kwenye kuahirishwa kwa mechi ile na alishiriki kikao cha usuluhishi, pia ni dharau kwa wapenzi wa soka ambao walianza kurudisha mapenzi na soka la nchi hii. Na ninaamini hata mdhamini wa ligi hawezi kufurahishwa na tabia hii wanayotaka kuonesha yanga,ijapo mpaka sasa hivi naamini ni mbinu ya kumzubaisha mpinzani ili a relax halafu siku hiyo imshitukize kama mwivi.
Natoa rai kuwa sasa ndio muda sahihi kwa TFF kuwachukulia hatua kali .wote wanaoendekeza uswahili
Tujifunze kuheshimu sheria na kanuni tulizojiwekea wenyewe...
Kosa ni la TFF kwa kukubali kutumiwa na wanasiasa kuharibu mchezo huo...
Mimi nakubaliana na Yanga SC kwa msimamo wao ili wawafundishe TFF kuelewa namna njema ya kuuendesha na kuusimamia soka la Tanzania...
TFF waache ubababishaji. Waende wakacheze wao na Waziri aliyeshiriki hicho kikao...