Suala la Lissu: Serikali tumeisikia, sasa familia ichukue jukumu lake

twahil

JF-Expert Member
May 31, 2011
4,100
2,793
Salaam wana bodi,

Tangu Mheshimiwa Tundu Lissu adhuriwe huko Dodoma na hatimaye kupelekwa Mjini Nairobi-Kenya, kumekuwepo na mijadala, mivutano na malumbano mengi sana juu ya namna suala hili linavyoshughulikiwa.

Kwa siku za hivi karibuni CHADEMA imekuwa ikiongeza kasi ya kuhamasisha watanzania kuchangia matibabu ya Mheshimiwa Lissu huko Nairobi. Sababu ambazo zimekuwa zikitolewa ni kuwa gharama za matibabu ni kubwa kwani kwa siku ni takribani Milioni 10 za kitanzania. Mchungaji Msigwa wakati akihojiwa na kituo cha televisheni cha Azam alisema kuwa jumla ya Shilingi Milioni 150 zimekwishatumika na bado fedha nyingi zinahitajika.

Kwa hakika matibabu ya Mheshimiwa Lissu yataendelea kutafuna fedha nyingi na kwa kutegemea kupitisha bakuli la michango kila siku kwa watanzania haitawezekana. Sasa kwakuwa Serikali kupitia Waziri wa Afya Ummy Mwalimu imetoa tamko lake kuwa inayo nia ya dhati kabisa kugharamia matibabu ya Mheshimiwa Lissu, basi ni vema Serikali ikaachwa igharamie matibabu hayo na familia yake ichukue jukumu la kuwa msemaji na "role" ya wanasiasa wenzake wa CHADEMA walioko huko Nairobi ipungue kwa wao kuacha kutoa matamko ambayo bado hayamsaidii mgonjwa zaidi ya kumuweka katika "position" ya kutokuwa na uhakika wa matibabu yake kutokana na makusanyo ya fedha za matibabu kuwa "unpredictable".

Ni wakati sasa familia ndio iwe msemaji wa matibabu ya Lissu na familia ndio iwe na maamuzi na sio hawa wanasiasa ambao kwao ni kuona suala la Lissu linatumiwa kukipa umaarufu chama chao.
 
Tangu lini Serikali iliyokuwa ikimkamata hovyo hovyo ikamtakia mema, acheni unafiki wa kidananda.

Sizonje Kalimwa barua ya Onyo Kali toka Uingereza, ndio mnajitekenya tekenya.
Wananchi tutachanga, tutakopa na ikibidi kuuza mali zetu Lissu apone.

Kama mnania kweli, Serikali ichange kama tunavyochanga sisi. After all hata hizo pesa za Serikali ni zetu sisi walipakodi.

Sisi tumeamua kumchangia Lissu, nyinyi kajengeni Ukuta Mererani kwa kodi zetu.
 
Serikali imegundua hawa jamaa hawapo kwa ajili ya lisu..wapo kwa ajili ya chama..wanaitumia hii fursa..bahati mbaya familia ya lisu imetulia tu..ila mwisho wa siku wao ndio watakaolia..

Na ndio maana serikali inataka tamko la familia ili kumuondoa lisu kwenye mikono ya wanasiasa.. Na katika hili tayari wanasiasa wameibuka na matamko yao..

Kiukweli lisu kama atapona matibabu yake yatachukua hata miezi sita ku recover..chadema pesa wanayo..ila hawakuandaa kutumia pesa yao kwenye masuala kama haya..angekufa kwao ingekuwa rahisi sana..isingefika hata mil 10..ila hili la kumuuguza lisu na kutumia mamilion kwa siku limekuwa pigo kubwa sana kwao..kumbuka hakuna posho za safari za nje kama zamani..hakuna posho za ushiriki wa vikao kwenye mashirika ya uma..mianya ya ukwepaji kodi imebanwa..kila mtu anaitolea macho pesa ya ruzuku..ni shida
 
Serikali imegundua hawa japo hawapo kwa ajili ya lisu..wapo kwa ajili ya chama..wanaitumia hii fursa..bahati mbaya familia ya lisu imetulia tu..ila mwisho wa siku wao ndio watakaolia..
Na ndio serikali inataka tamko la familia ili kumuondoa lisu kwenye mikono ya wanasiasa.. Na katika hili tayari wanasiasa wameibuka na matamko yao..
Kiukweli lisu kama atapona matibabu yake yatachukua hata miezi sita Ku recover..chadema pesa wanayo..ila hawakuandaa kutumia pesa yao kwenye masuala kama haya..angekufa kwao ingekuwa rahisi sana..isingefika hata mil 10..ila hili la kumuuguza lisu na kutumia mamilion kwa siku limekuwa pigo kubwa sana kwao..kumbuka hakuna posho za safari za nje kama zamani..hakuna posho za ushiriki wa vikao kwenye mashirika ya uma..mianya ya ukwepaji kodi imebanwa..ni shida
Lissu tunamhitaji ila wanasiasa wanaweka wingu juu ya matibabu yake hali ambayo inamuweka pabaya na kuweka pabaya familia yake. Wanasiasa wanafanya kila hila kuhakikisha Serikali haigharamikii matibabu ya Lissu ili ile propaganda kuwa Serikali ndo imehusika kumdhuru ibaki bila kuangalia hali ya mgonjwa ikoje.
 
Lissu tunamhitaji ila wanasiasa wanaweka wingu juu ya matibabu yake hali ambayo inamuweka pabaya na kuweka pabaya familia yake. Wanasiasa wanafanya kila hila kuhakikisha Serikali haigharamikii matibabu ya Lissu ili ile propaganda kuwa Serikali ndo imehusika kumdhuru ibaki bila kuangalia hali ya mgonjwa ikoje.
Sasa kama haijahusika, mbona haijasema nani mmiliki wa Gari alilolitaja Lissu, kama haijahusika mbona hakuna updates zozote za kiitelijensia zaidi ya kukamata wakimbizi uchwara eti kwa taarifa za kiitelijensia pamoja na kumkamata Zitto Airport kwa mbwembwe. Acheni unafiki, muwe na aibu.
 
Wasubiri bili siku anaruhusiwa, au wanataka wamsaidie kwa utaratibu upi?
 
Tangu lini Serikali iliyokuwa ikimkamata hovyo hovyo ikamtakia mema, acheni unafiki wa kidananda.

Sizonje Kalimwa barua ya Onyo Kali toka Uingereza, ndio mnajitekenya tekenya.
Wananchi tutachanga, tutakopa na ikibidi kuuza mali zetu Lissu apone.

Kama mnania kweli, Serikali ichange kama tunavyochanga sisi. After all hata hizo pesa za Serikali ni zetu sisi walipakodi.

Sisi tumeamua kumchangia Lissu, nyinyi kajengeni Ukuta Mererani kwa kodi zetu.
.
 
Lissu tunamhitaji ila wanasiasa wanaweka wingu juu ya matibabu yake hali ambayo inamuweka pabaya na kuweka pabaya familia yake. Wanasiasa wanafanya kila hila kuhakikisha Serikali haigharamikii matibabu ya Lissu ili ile propaganda kuwa Serikali ndo imehusika kumdhuru ibaki bila kuangalia hali ya mgonjwa ikoje.
Kuna michango mingi sana..mingine inaingia kinyemela kutoka taasisi na makampuni na watu wazito hata serikalini..hii unaweza kuta inaingia kimya kimya kwenye mifuko ya kina mbowe..hivyo kuwanyang'anya mgonjwa ni kuwapora ulaji..ndio maana wimbo wa endeleeni kuchangia umekuwa wimbo mwepesi sana kwa viongozi hawa..this is worse..
 
Kuna michango mingi sana..mingine inaingia kinyemela kutoka taasisi na makampuni na watu wazito hata serikalini..hii unaweza kuta inaingia kimya kimya kwenye mifuko ya kina mbowe..hivyo kuwanyang'anya mgonjwa ni kuwapora ulaji..ndio maana wimbo wa endeleeni kuchangia umekuwa wimbo mwepesi sana kwa viongozi hawa..this is worse..
Serikali imewastukia na kuona itibue mipango yao ovu...
 
Nadhani kaka yake ambaye ni mwanasheria aingilie kati...
Unafikiri Kaka yake na Tundu Lissu, Wakili Mughwai na mke wa Lissu nani anapaswa kuwa na sauti juu ya Tundu kuhusu matibabu yake?

Jibu lako angalia usifunue upu..mbavu wako. (Kayasome yale maneno ya Invisible)
 
Sasa kama haijahusika, mbona haijasema nani mmiliki wa Gari alilolitaja Lissu, kama haijahusika mbona hakuna updates zozote za kiitelijensia zaidi ya kukamata wakimbizi uchwara eti kwa taarifa za kiitelijensia pamoja na kumkamata Zitto Airport kwa mbwembwe. Acheni unafiki, muwe na aibu.
Je ukiombwa kuisaidia polisi kutoa USHAHIDI namna Serikali ilivyohusika na kushambuliwa kwa mh. lissu utasemaje?
 
Kuna michango mingi sana..mingine inaingia kinyemela kutoka taasisi na makampuni na watu wazito hata serikalini..hii unaweza kuta inaingia kimya kimya kwenye mifuko ya kina mbowe..hivyo kuwanyang'anya mgonjwa ni kuwapora ulaji..ndio maana wimbo wa endeleeni kuchangia umekuwa wimbo mwepesi sana kwa viongozi hawa..this is worse..
 
Serikali imegundua hawa jamaa hawapo kwa ajili ya lisu..wapo kwa ajili ya chama..wanaitumia hii fursa..bahati mbaya familia ya lisu imetulia tu..ila mwisho wa siku wao ndio watakaolia..
Na ndio maana serikali inataka tamko la familia ili kumuondoa lisu kwenye mikono ya wanasiasa.. Na katika hili tayari wanasiasa wameibuka na matamko yao..
Kiukweli lisu kama atapona matibabu yake yatachukua hata miezi sita ku recover..chadema pesa wanayo..ila hawakuandaa kutumia pesa yao kwenye masuala kama haya..angekufa kwao ingekuwa rahisi sana..isingefika hata mil 10..ila hili la kumuuguza lisu na kutumia mamilion kwa siku limekuwa pigo kubwa sana kwao..kumbuka hakuna posho za safari za nje kama zamani..hakuna posho za ushiriki wa vikao kwenye mashirika ya uma..mianya ya ukwepaji kodi imebanwa..kila mtu anaitolea macho pesa ya ruzuku..ni shida

Ndugu walikuwepo mbona hawajaenda Nairobi? Kwani lazima mpaka serikali iwaambie? Mbona Nyalandu Zito Lema jsji mstaafu si wamrkwenda wenyewe su wamepelekwa na serikali.hii ni wiki ya pili sasa huyo mgonjwa critical angekuwa anasubiri mpaka baada ya siku mbili ndiyo waseme ndugu watume maombi wao watahudumia.

Mimi anajua ni kwa nini,kwasababu wameambiwa hali yake siyo nzuri kwa hiyo wanategemea muda wowote Mungu atamuita kwa hiyo wajisafishe wsseme tukimtoa ofa ya matibabu popote duniani lakini ndiyo hovyo walipo lala wao ndiyo wenzao waliyo amkia
 
Lissu tunamhitaji ila wanasiasa wanaweka wingu juu ya matibabu yake hali ambayo inamuweka pabaya na kuweka pabaya familia yake. Wanasiasa wanafanya kila hila kuhakikisha Serikali haigharamikii matibabu ya Lissu ili ile propaganda kuwa Serikali ndo imehusika kumdhuru ibaki bila kuangalia hali ya mgonjwa ikoje.
Nafikiri hawajasema mgonjwa wamesimamisha huduma huduma zinaendelea kama kawaida na mke wake yuko
 
Serikali imesubiri weee kutangaza breaking news kwamba Mh. Tundu Lissu hayuko tena duniani lakini Mwenyezi Mungu kutokana na maombi ya waja wake kawasikia na kafunga break. Serikali inahaha, jaribio linaelekea kubuma na wengine serikalini wanaanza kuonja machungu ya laana na kuanza kujikokongojakongoja mradi twende. Jemadari Lissu, pona haraka urudi tuendeleze mapambano dhidi ya malimbukeni, washamba na madikteta uchwara walioparamia madaraka, a luta continua...!
 
Back
Top Bottom