πŸ“’ Story za gawio

Joined
Aug 26, 2022
Posts
64
Reaction score
119
| Leo Tujifunze kwa Mfano Halisi πŸ’°πŸ“ˆ

Juzi CRDB Bank PLC wameanza kutoa gawio (dividends) kwa wanahisa wake! πŸ¦πŸ’΅ Gawio la mwaka huu ni Tsh 65 kwa kila hisa – na guess what? Wanafunzi wangu wa darasa la uwekezaji (kwenye group langu la WhatsApp πŸ“²) waliowekeza kwenye hisa za CRDB wameanza kupokea gawio lao live and direct! 😍

πŸ” Wakaanza kushare SMS za magawio yao, kila mmoja kwa kiasi chake alichowekeza.

Na wote hawa hawajafanya kazi yoyote leo – pesa imeingia tu!

πŸ’­ Hapo ndipo wengine (ambao bado hawajachukua hatua) wakaanza kuuliza:
β€œMbona mimi sijapata? πŸ€”β€
β€œHivi huwa inakuaje mtu anapewa pesa na benki? πŸ¦β€
β€œAaah! Bora ningesikia mapema ningeanza zamani πŸ˜©β€

🧠 Sasa Hebu Tuelewe: GAWIO ni Nini?
πŸ“Œ Gawio ni sehemu ya faida ambayo kampuni inaamua kuigawa kwa wanahisa wake, kulingana na hisa walizonazo.
Mfano: Ukiwa na 1,000 za hisa za CRDB, na kampuni imetangaza gawio la 65 Tsh kwa kila hisa, basi unapata:
πŸ‘‰ 1,000 x 65 = 65,000 Tsh

πŸ“ŒNa Makampuni mengine Yanaendele kutoa Gawio Mwaka Huu.

πŸ“Œ SOMO LA LEO:
Wekeza Leo ili Kesho Upokee Bila Kuvuja Jasho. πŸ’ͺπŸ’Ό
Pesa unayoitafuta kila siku kupitia biashara au ajira – sehemu yake ipange iende kwenye uwekezaji.
Usisubiri uwe na milioni, anza na kile kidogo ulicho nacho leo.

⏳ Baada ya miaka michache, utakua miongoni mwa wale wanaopokea gawio la mamilioni – bila kuandika invoice wala kukodisha fremu.

GODFREY DENIS
Millennium Investors Community Co-founder
0763721523
 
Hii kitu imeniumiza kichwa sana...kwamba nawezaje kuinvest kidogo changu kwenye hisa...msaada mkuu
 
Hisa yenyewe ni shilingi ngapi?
Inategemea na hisa za kampuni husika.

Mfano: hisa moja ya CRDB sokoni kwa sasa ni Tsh 790, NMB ni 3600, AFRIPRISE ni 320 n.k.
na kwa sasa unaweza kuanza na hisa moja.

Ni vema kupata maarifa kabla ya kuwekeza β€” ujue faida za kuwekeza kwenye soko la hisa, changamoto zake, na jinsi ya kuchagua kampuni sahihi kabla ya kuwekeza.
 
Hisa za CRDB zipo vizuri
Naam zipo vizuri.

Kampuni inafanya vizuri kibiashara β€” hii utaiona ukipitia taarifa zake za kifedha. Lakini pia hata valuation metrics (PE na PB ratio) zake ziko vizuri.
 
Inategemea na engo uliyopo, vipi kama hisa moja inauzwa milioni?
Dah itakuwa shughuli hiyo mkuu.
Kwa hisa za crdb kwa sasa ni kama 790 kama sijakosea.

So si uwekezaji mbaya sana kama umeweka fedha yako kwa malengo.

Ila kama umeweka kama sehemu uwekezaji wa faida kubwa utakuwa umepoteza
 
Inategemea na engo uliyopo, vipi kama hisa moja inauzwa milioni?
Hakuna kampuni ambayo kwenye soko la hisa la Dar-es-Salaam (DSE) ina hisa yenye bei ya Tsh Million 1.

Hisa yenye bei ghari ni ya kampuni ya TCC ni Tsh 17000 tu.
 

Attachments

  • Screenshot_20250605-151751_Chrome.jpg
    297.8 KB · Views: 32
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…