St. Joseph University- Arusha na TCU

St. Joseph University- Arusha na TCU

mshipa

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2015
Posts
12,355
Reaction score
23,084
Habari za jumapili wana JF
Hiki chuo cha st.joseph campus ya arusha mwaka jana walipokea wanafunzi wa mwaka wa kwanza ngazi ya shahada (education) kama walivyopangiwa na TCU. Sasa cha kushangaza wanafunzi hao baadae walipata taarifa kuwa wao hawasomei shahada bali ni stashahada tofauti kabisa na udahili wao unavyoonesha na hii imepelekea mgomo kwa wanafunzi hao wa mwaka wa kwanza wakitaka kujua hatima yao ambao ulipelekea kusimamishwa masomo kwa mda. Na hv navyoandika uzi huu wamepewa notes ya kurudi chuoni lkn kati ya wanafunzi 600 waliosimamishwa wamerudi 147 tu ambao wamekubali kusoma hyo stashahada.
Sasa najiuliza ilikuwaje tcu wapeleke wanafunzi kwenye chuo ambacho wanajua hakitoi shahada?
Na je wanafunzi wa stashahada wanaomba kupitia tcu?
Alafu hawa wanafunzi wanapewa mkopo na bodi ya mikopo, je bodi ya mikopo siku hzi inawakopesha wanafunzi wa stashahada?

Karibuni tujadiane kuhusu hili mm binafsi linanichanganya
 
Ni dili kati ya TCU na BODI YA MIKOPO,na baadhi ya maofisa wa serikali
 
Sio chuo kile m nashangaa watu wanakishobokea tu m hata tcu wanipange siendi Ng'o.
 
Wanafunzi karibu ya 400 hawajui waende wapi na tayari wapo kwenye system ya bodi ya mikopo na naskia kuomba upya inabidi alipe 25% ya mkopo ambao tayari ameutumia ....mbona hii wizara ya elimu imekuwa legelege hv
 
Sio chuo kile m nashangaa watu wanakishobokea tu m hata tcu wanipange siendi Ng'o.


Mbona kama unajitekenya na kucheka mwenyewe?.
kipindi cha nyuma ulishasema unasoma hapo leo unakiruka ndo ninyi mloenda bungeni na kuambiwa muingie darasani?.
Hivi Dodoma mlifuata nini?.
Kwa nini msitii maelekezo ya PM na Kawambwa ya kuwataka muingie darasani?.

mi mdogo wangu yuko hapo mwaka wa pili ila kaniambia wakati wakiwa likizo Kawambwa alikuja na kuwaomba muingie darasani ninyi wa mwaka wa kwanza na matatizo yatashughulikiwa mkiwa mnaendelea na masomo,ila ninyi mkagoma mlitaka nini na tayari mamlaka husika zimeshawapatia majibu?.
 
Upinzani noma ww hujui kinachoendelea st joseph ndo maana unamfaliji huyo mdogo ako acha amalize kisha aje kuwa dereva wa sahani mezsn ndo utajua km ni degree au co

Tcu wenyewe wanasema hawajui nn kinafundishwa hapo ww unajfalij tu

Chuo kikuu hakiwez kuwa chuo bila ya prospectus,curriculum bora ma lecturer wazr na miundombinu mzr
 
Back
Top Bottom