Sonona

Sonona

Dr leader

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2016
Posts
1,041
Reaction score
1,294
Sonona
1. Msione wajifia, vijana naso wakubwa
Mawazo nawaambia, akili ndio hukabwa
Fuadi zinaumia, mwili nao dabwa dabwa
Sonona gonjwa hatari

2. Akili inapofeli, mauti yatawasili
Hutaona afadhali, ila ni ubahaluli
Jambo la kutaamuli, vigumu kulikabili
Sonona gonjwa hatari

3. Kazi hutaitamani, itakujaa simanzi
Hutakuwa na amani, kila wakati majonzi
Joto lililo kichwani, halipoagi kwa minzi
Sonona gonjwa hatari

Abuuabdillah
0744 883 353
 
Back
Top Bottom