Sonona gonjwa hatari sana

Sonona gonjwa hatari sana

Dr leader

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2016
Posts
1,041
Reaction score
1,294
Wasiseme sikuumwa.

Usiku wa saa nane ,imepigwa hii simu
Ni kwasababu ya mane, nimeridhi kunywa sumu
Nimeishi kama bene , sikuwa na umuhimu
Wasiseme sikuumwa, Abuu hili liseme

Sikulala miezi sita, mawazo yaniumiza
Hadi macho yalisita, yalivyo nisheheneza
Chakula hakikupita, hata ningajiliwaza
Wasiseme sikuumwa, Abuu hili liseme

Nje 'likuwa mzima, kwa ndani kulishakufa
Nikabakia hamuma, bongo likapata ufa
Isitokee husuma, Abuu andaa dhifa
Wasiseme sikuumwa, Abuu hili liseme

Waambie niliumwa, sonona imeniua
Hakika sijasukumwa, meafiki kujiua
Nimezidi mkaumwa, munifanyie adua
Wasiseme sikuumwa, Abuu hili liseme

✍️Abuuabdillah
 
Back
Top Bottom