Sitta awasimamisha Watendaji watano TRL

Dotto Mnzava

R I P
Joined
Mar 6, 2014
Posts
864
Reaction score
427
Waziri wa Uchukuzi, Samweli Sitta. amewasimamisha watendaji watano wa Kampuni ya Reli Tanzania akiwemo Mkurugenzi mtendaji, Kipallo Kisamfu, ili kupisha uchunguzi wa ununuzi wa mabehewa ambayo mengi yanadaiwa kuwa ni mabovu na kufanya malipo ya manunuzi kinyume na makubaliano.

Aidha, Sitta amemrudisha Idara ya utumishi aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, TPA, Madeni Kipande, baada ya kumsimamisha kazi ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizokuwa zikimkabili za uendeshaji mbovu wa bandari.
================= CHANZO: NIPASHE(17th April 2015)
 
Aiseee! Mwaka huu kila mtu anapanga na kupangua karata zake.Mwaka wa uchaguzi ni mwaka wa kujionea mengi.
 

Weka chanzo cha habari yako
 
Mkuu waliosimamishwa ni TPA au TRL?
 
Sidhani kama kuondolewa au kusimamishwa kwa watu hawa kuna tija yoyote kwa Taifa. Dawa ni kuwafilisi tu. Wa kuwafilisi simuoni.
 
Yeye mwenyewe Sitta wakati anavuruga bunge la Katiba na kula posho ya wabunge waliotoka bungeni nani alimsimamisha kazi?? Sitta ni nyoka tu
 
.... Yumo Meneja, Mhasibu Mkuu Na Vigogo Wengineo. Wamesimamishwa Na Waziri Wa Uchukuzi Mh Sitta. Chanzo Ni ITV
 
Waziri wa Uchukuzi Mh.Samwel Sitta amewasimamisha viongozi mbalimbali ndani ya shirika la reli kutokana na tuhuma za upotevu wa vitu vyenye thamani ya mabilioni.
 
Hongera Samuel Sitta. Hakika wewe ni mzee wa speed and standard
 
aiseee sitta hata afanye lipi jema hataonekana tena..
kakera wananchi walimuamin hapo kabla.
yan afanye tu kaz zake bt akumbuke kaharb katiba yetu nzuuuri ya mzee wa ukwel...mzee warioba
 
Yeye mwenyewe Sitta wakati anavuruga bunge la Katiba na kula posho ya wabunge waliotoka bungeni nani alimsimamisha kazi?? Sitta ni nyoka tu

Ndio nashangaa lini amekuwa msafi kuwaona wenzie wachafu.
 
Nchi hii imeshindikana,yaani nilivyomuamini Mwakyembe sikutegemea kama hili lingetokea chini yake na hakuchukua hatua zaidi ya kujisifia kuwa anaimarisha shirika!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…