Na naomba kukupa angalizo tu kwa upendo kuwa;
Mwenye haki ya kuishi na Mke ni mwanaume Mwenye uwezo wa kutunza Mke na familia!
Siyo kwa kuwa unamidevi tu basi unajitongozea!
Mbona watoto walaini kukamatika kama unafunga mlango wa jikoni vile,
Sema ndo hvo, kama umekulia kilolo, mtitu, dabaga, Magome, utahenya sana watoto wa town kuwapata,
Sijui ninakasumba gani mimi, nimahiri kwenye kutongoza lakini kukataliwa ni suala la kawaida sana japo kuwa mimi ni kijana handsome na mwenye sifa zote.
Kwa usawa huu hakuna mwanamke anaangalia uhandsome pesa mbele mengine ndo yanafuata mwanamke akishakuona tu anajua tu we unazo au hauna fuata ushauri unaopewa hapa cha muhimu ni kukaza roho zaidi ya watu 90% wanakwambia utafute pesa
Mkuuu mi nna sura mbaya mtaa mzima
Sina pesa naungaunga Lakini sitongozagi demu huwa naweka trap na kujifanya sina habari kisha huingia mtegoni wenyewe.
Wanawake hawapendi sura but kile kilicho ndani yako kama ucheshi,, upole uchangamfu na kikubwa kuwajari hata pasipo kutumia pesa wao hueshimu vitu vidogo sana na kujenga upendo na trust
We utakua kauzu dagaa, halafu unanata Kwa kujiona Hb,, mambo hayako ivo create field of attraction from sasa utawakimbia mwenyewe.
Ila usitumie mbinu hii Kwa ajiri Ya uzinzi.
Watu mnapenda Sifa aisee wengine inabidigi tu tuwasifie Maana mnapenda Sifa kweli, kiuhalisia ni wa kawaida tu ila Kwa vile Tunawajua ni mibaba misifa yanapenda Sifa sio zenu, Wanaume wazuriii wala hawajisemagi wala kutaka wasifiwe
Mshukuru Mungu umeepukana na mengi, kupendwa na wanawake haikutajwa popote kwenye vitabu kama ni sifa ambayo mwanamme anastahili awe nayo. Kama huna mapungufu yoyote tafuta mke uoe ndie anae stahili akupende. Wala usijitie harama kwamba lazima upendwe ukifika muda wako watakupenda lakini sio kwa njia iyo unayoitaka wewe sasa ivi ya kufanya zinaa.