Panthera 1
Member
- Dec 30, 2014
- 50
- 9
Habari zenu ndugu zangu,
Ashukuriwe Mungu muumba mpaka hapa tulipofika. Mimi ni kijana wa miaka 26 ambae leo nimeamua kuja kuomba ushauri kwenu kwani nipo njia panda na sielewi kipi cha kufanya. Nilikuwa na mpenzi wangu mmoja ambae nilimpenda kwa moyo wote, nilimuonyesha mapenzi yote lakini leo hii ameamua kunisaliti na kwenda upande mwingine huku tayari tulikuwa katika ahadi za kuoana.Siku chache zilizopita kuna rafiki yangu ambae alinieleza kuhusu mambo ya mpenzi kuwa ni msaliti.
Lakini sikutaka kumkubalia hilo. Rafiki huyo aliendelea kunisisitizia kuwa mpenzi wangu siyo muaminifu lakini nami nilikataa ila leo nimeamini baada ya kushuhudia hayo niloelezwa. Mpaka sasa moyo wangu unauma, najihisi kuwa mgonjwa kabisa kwa kuwaza kilinitokea, sina raha na ninaona dunia nzima ni chungu. Ila nako katika hali ya kushangaza sikuchache baada ya mpenzi wangu kunisaliti, alitokea msichana mwingine mzuri tu na kudai ananipenda.
Ukweli mimi simpendi ingawa ni mrembo na anapesa. Mpaka muda huu sijampenda msichana huyo wala sikuwahi kumpenda. Je nimpende kwa sababu nimesalitiwa au nimpende kwa ajili ni msichana mwenye hela? Kweli sijampenda wala sitaki kutumia pesa zake hata kidogo, ila yeye ananipenda. Nipo njia panda, nakumbuka hata familia yangu iliwahi kunambia kuwa mpenzi wangu hafai lakini mimi nilimng'ang'ania kwa kuwa tulipendana tangu utoto.
Nifanyaje ndugu zangu?
Ashukuriwe Mungu muumba mpaka hapa tulipofika. Mimi ni kijana wa miaka 26 ambae leo nimeamua kuja kuomba ushauri kwenu kwani nipo njia panda na sielewi kipi cha kufanya. Nilikuwa na mpenzi wangu mmoja ambae nilimpenda kwa moyo wote, nilimuonyesha mapenzi yote lakini leo hii ameamua kunisaliti na kwenda upande mwingine huku tayari tulikuwa katika ahadi za kuoana.Siku chache zilizopita kuna rafiki yangu ambae alinieleza kuhusu mambo ya mpenzi kuwa ni msaliti.
Lakini sikutaka kumkubalia hilo. Rafiki huyo aliendelea kunisisitizia kuwa mpenzi wangu siyo muaminifu lakini nami nilikataa ila leo nimeamini baada ya kushuhudia hayo niloelezwa. Mpaka sasa moyo wangu unauma, najihisi kuwa mgonjwa kabisa kwa kuwaza kilinitokea, sina raha na ninaona dunia nzima ni chungu. Ila nako katika hali ya kushangaza sikuchache baada ya mpenzi wangu kunisaliti, alitokea msichana mwingine mzuri tu na kudai ananipenda.
Ukweli mimi simpendi ingawa ni mrembo na anapesa. Mpaka muda huu sijampenda msichana huyo wala sikuwahi kumpenda. Je nimpende kwa sababu nimesalitiwa au nimpende kwa ajili ni msichana mwenye hela? Kweli sijampenda wala sitaki kutumia pesa zake hata kidogo, ila yeye ananipenda. Nipo njia panda, nakumbuka hata familia yangu iliwahi kunambia kuwa mpenzi wangu hafai lakini mimi nilimng'ang'ania kwa kuwa tulipendana tangu utoto.
Nifanyaje ndugu zangu?