Makini
Senior Member
- Dec 23, 2014
- 154
- 59
Katika harakati za kufatilia kinachoendelea Hollywood Marekani, nimegundua kuwa Mastaa wengi katika tasnia za filamu na muziki wamekua sehemu ya maisha yetu hasa kwa vijana waliopo katika mashule ya sekondari na vyuo. Vijana wengi wanawachukulia hawa ‘celebs' kama ni Miungu watu, wanawaamini sana na kuona hawawezi kukosea.
Tunachoshindwa kugundua ni kwamba mastaa hawa wanatuletea hasara zaidi ya faida kwenye jamii zetu. Mitindo ya mavazi wanayokuja nayo, yaani kila kukicha afadhali ya jana, ni kama wanashindana nani ataonesha mwili zaidi ya mwingine au nani atatoa video chafu zaidi ya muziki.
Kingine ambacho hivi sasa nimegundua kuwa ni tatizo kubwa, ni movie za hollywood zinazotufundisha mbinu za ujambazi na ubabe huku zikijificha chini ya mwavuli wa ‘Action'. Vijana wengi wa kike na wa kiume wanawatizama mastaa kama mashujaa na watu wa kuigwa.
Rihanna aliwahi kusema yeye si mfano wa kuigwa kutokana na yale anayoyafanya. Mtazamo wangu ni kwamba si yeye tu bali mastaa wengi wanafanya mambo yasiyostahili kuigwa kabisa. Nahisi huu ni muda wa kubadilika na kuhakikisha vijana tunakuwa makini na vitu tunayotizama na tunayoamua kuiga kutoka kwa mastaa.