Simulizi: Nice guy of century

Simulizi: Nice guy of century

Asaelofficial

Member
Joined
Sep 5, 2017
Posts
30
Reaction score
35
[9/16, 11:27] : NICE GUY OF CENTURY

SEHEMU YA 01

Ni katika supermarket moja alionekana Baba akiwa mke wake pamoja na mtoto wao mdogo wa mwisho katika uzao wao,mke alikuwa alilalamika kuwa hela hawana halafu mmewe amemleta sehemu ya gharama supermarket kununua keki ya birthday ya mtoto wao mkubwa wa kiume Asael,mtoto ambaye hana hata kazi tangu amalize masomo yake hakuwa ameajiriwa mpaka muda huo bado tegemezi nyumbani,
Baba alichukulia busara hakutaka kubishana na mke wake alimwambia...
"Mke wangu huyu ni mtoto wetu hata kama kwa sasa hana kazi ni tegemezi kwetu itafika tu wakati naye atapata kazi,na kuhusu kutumia pesa hata iliyobaki ya matumizi yetu nyumbani kumnunulia keki ya gharama mtoto wetu ambaye hana hata msaada kwetu kwa sasa sioni kama ni tatizo huyo ni mwanawetu hivyo ikiwa leo ni siku ya kuzaliwa kwake acha tutumie hata kidogo tulichonacho kuhakikisha mtoto wetu anapata furaha,ikiwa sisi tupo hai ni jukumu letu hili"
Hayo yalikuwa maneno ya mzee baada ya mkewe kulalamika kuhusu kijana wake kukosa kazi ya msingi tangu amalize masomo yake kutokana na tatizo la ajira kwa sasa.
Mkewe alimuangalia mmewe kisha akasema...
"nilijua tu utamtetea tu kijana wako,haya nunua hiyo keki twende"
aliongea mkewe,
mzee akajua huyu tayari nimeshamshinda ujanja,hayo yalikuwa ni maneno ya hapa na pale ya familia wakati wakiwa katika supermarket...
mara mtoto akaona mkate akamunyoshea mkono baba ake amnunulie...
Baba akawa anataka kumnunulia mtoto wake kwa siri ili mkewe asijue maana alijua tu lazima mkewe angemsema tena kuwa kawadekeza watoto wake....
Mzee alikuwa na tabia ya kutokukubali mtoto wake apate shida au ateseke ikiwa yeye anauwezo wa kumsaidia...

Walifika nyumbani walianza maandalizi ya kuandaa siku ya kuzaliwa ya kijana wao mpendwa walipanga kumfanyia surprise/mshitukizo hawakumpa taarifa,yeye mwenyewe haikuwa rahisi hata kuikumbuka hata siku yake ya kuzaliwa maana muda mwingi alikuwa akiutumia kufanya kazi ndogondogo mtaani akisubiri ajira kiufupi maisha hayakuwa sawa kabisa yalikuwa ya dhiki mtindo mmoja...

Wakati wao wakiandaa surprise aliyekuwa akiandaliwa hiyo surprise ndio kwanza wakati huo alikuwa akikabidhi guta alilokuwa akitumia kujiingizia kipato kwa boss wake,alikabidhi akapewa ujira wake kutokana na kazi aliyoifanya kwa siku hiyo,maana alikuwa akilipwa kwa kutwa,sasa alishangaa siku hiyo kulipwa nusu ya mapato yake alipohoji akaambiwa nusu ingine ilikuwa ibaki ili kukarabati guta alilokuwa akitumia,
Hakuwa na jinsi ilibidi tu akubaliane na matokeo alinishauri boss wake akaondoka....
Taratibu alikuwa akitembea kurejea nyumbani moyoni alijiuliza mateso na unyanyasaji huo uliokuwa ukimkumba ungeisha lini kazi ngumu mshahara mdogo,mtaani anadhaurika kuwa kasoma bure kaishia kuuza maji hakika hizo ndio zilikuwa changamoto kubwa kwake...
Aliingiza mkono mfukoni akatoa simu yake,alipotazama saa ilikuwa saa mbili usiku kama na dakika tano hivi alijiona amechelewa aliongeza mwendo akaendelea kukatiza katika vichochoro....

Nyumbani maandalizi yalikuwa tayari familia ilikuwa na furaha tele licha ya hali ya uchumi kutokuwa nzuri tangu Baba mwenye nyumba afukuzwe kazi katika kampuni alikuwa akifanya kazi kutokana na kuongoza wafanyakazi katika kudai haki zao kampuni lilichukua uamuzi wa kumfuta kazi na kumpa haki zake zote ili kuepusha asisambaze sumu iliyokuwa katika moyo wake ya kutetea wafanyakazi wenzake ili wapate haki zao za msingi hivyo alijikuta alifukuzwa kazi akarudi katika kazi yake ya kilimo cha mbogamboga za majani mpaka wakati huu....
Mama alianza kupata hofu akasema mbona kijana wake hakuwa na tabia ya kuchelewa nyumbani hivyo labda huko alipo alikumbwa na matatizo,
Mme akamsihi asiwe na hofu kijana wao angefika tu muda sio mrefu hivyo waendelee tu kumsubiri....

Upande wa pili ni kweli kijana wao Asael hakuwa kabisa na kumbukumbu kuhusu siku yake ya kuzaliwa,aliendelea kutembea ili awahi nyumbani....

Sasa wakati akiwa anatembea katika jengo moja alisikia kama kuna watu walikuwa wakiongea na vishindo vya hapa na pale ilimuwia vigumu kupita hilo eneo tena la mtaani kwake asijue nini hasa kiliendelea wakati huo,,,
Taratibu alijisogeza katika jengo hilo,aliamini wazi alikuwa sahihi kwa alichokusudia kuchunguza wakati huo kwa yeye alisomea masuala ya uwandishi wa habari sasa alitaka kujigeuza naye kama mwandishi halisi wa habari aliyekuwa akipeleleza habari kwa kina!
Rahasha kumbe haikuwa hivyo yeye akitokea katika kazi za guta hakuwa ameajiriwa kwa wakati huo licha ya kuwa kweli alikuwa na ujuzi huo...

Taratibu kabisa alipata upenyo akapenyeza jicho lake la kushoto bado ilionekana hajaridhika,alizidi kupepesa macho kwa harakaharaka aligundua kulikuwepo na makundi mawili ya watu ambayo yalisimamiana wima,alipotazama kwa umakini zaidi kiongozi mmoja wa kundi alimtambua,alikuwa ni Mr chalima mfanyabiashara mkubwa kabisa wa madini aliyejulikana sana hakuelewa kwa harakaharaka nini walikuwa wakikifanya usiku ule...
Baada ya muda gari iliingia mpaka eneo hilo gari ilikuwa imefunikwa turubai juu,Taratibu Mr chalima alisogea katika gari hilo akatoa amri vijana wafungue aone kilichokuwa ndani vijana walifanya hivyo...

Zilikuwa ni pembe za Ndovu aise!!!

Moyo wa Asael ulijawa na hofu sana kwa muda huo,hakuwahi kufikiria kuwa mtu kama mr chalima alikuwa akisifika kwa kutoa misaada katika jamii angesubutu kufanya biashara ya hatari kiasi kile tena wakishirikiana na maafisa wa polisi!!
mr chalima kwa wakati huo alikuwa na furaha sana hakuwa na wasiwasi kwa alitendalo...
ni wazi alikuwa ni mwenyeji na biashara hiyo,
Taratibu mwili ulimsisimka Asael akaitoa simu yake mfukoni aliona ni bora angebaki na ushahidi yeye kama mwandishi wa habari...
Alirekodi tukio hilo kwa simu yake ya mkono wakati mr chalima akikabidhi pesa kwa maafisa wale wa jeshi la polisi...
akajiona mshindi hakuta kuishia hapo alitaka apige na picha!!!

Nyumbani Bado alikuwa akisubiliwa
na familia yake ili waje kusherehekea siku yake ya kuzaliwa
mdogo wao wa mwisho alianza kulilia ile keki mama akaamua kumkatia kidogo..

Huku Asael akafanikiwa kupiga picha mbili za mwanzo,ila tayari alishaonekana mwanga wa simu ulimponza!!!

Akashangaa anaguswa kwa nyuma,akageuka mapema sana akafanikiwa kumtoroka huyo mtu ila aligundua ameshafamika alilaumu kimbelembele chake alijiona tayari ameiongoza familia yake matatani kwa muda wowote yule mtu angeweza kufika nyumbani....
akazunguka upande mwingine kusikia nini kingejili baada ya yeye kuonekana....

Alisikia kabisa mr chalima akitoa amri kwa kujiamini kabisa....
"kama amesikia haina budi sisi kumfunga mdomo asiongee mpaka mwisho,
na njia sahihi zaidi ya yeye kutunza siri ni kufa tu kabla hajafika nyumbani aeleze hili akiwatangulia kufika basi mmalize familia nzima siri izidi kuwa siri"
hii sauti Asael Alijisikia waziwazi kabisa kifo chake na cha familia yake kikipangwa na mr chalima....

Moyoni aliona ni bora awahi nyumbani akaiondoe familia yake mapema kabla wauaji hawajafika....

Wazazi wakiwa wamezubaa zubaa ghafla mwanao alifika akiwa na hofu iliyopitiliza
"baba,mama yatupasa tuondoke eneo hili mara moja wauaji wanakuja muda sio mrefu sitaki mniulize maswali kwa sasa nitawaeleza mbele ya safari"

Aliongea huku jasho likimtoka kama alitokea katika riadha marathon...

fataki zilianza kufyatuka picha yake mbele ndipo akakumbuka ilikuwa siku yake ya kuzaliwa!!

Alijilaumu sana kuwa na kiherehere...
walitoka akawasindikiza yeye akawahaidi kukutana mbele amalizie kuchukua vitu ndani....

Wakati tu anarudi kabla hajafika alishuhudia wauaji wakiingia ndani katika nyumba walipoishi wao....

Huu ni utangulizi tu wa mkasa huu...
[9/16, 11:35] : SEHEMU YA 02

...ilipofika
Baada ya kijana mdogo Asael kuingilia mambo ya wakubwa kwa kujitia mwandishi wa habari na kuamua kupiga picha biashara za watu,anajikuta katika wakati mgumu hata familia yake kuitia matatani

Sasa endelea....
Baada ya wale wauaji kuingia ndani na kukosa mtu walijua moja kwa moja walizidiwa akili,walijilaumu kuchelewa kufika hapo,
wakapiga simu kwa mr chalima kumjulisha habari hizo...
Baada tu ya watu hao kuondoka katika nyumba ya akina Asael,kwa umakini mkubwa Asael akaingia ndani naye akapita mpaka katika chumba alichokuwa akilala akainama katika uvungu wa kitanda akatoa kisanduku kidogo,akaamua kukivunja,kilikuwa ni kibubu chake alichokuwa akihifadhi pesa,baada ya kukipasua akazitia zile pesa mfukoni kwa upesi upesi akatoka....

Sasa familia yake baba,mama na wadogo zake wawili wakiume na wakike walifanikiwa kufikia kwa ndugu,baba mdogo wa Asael/mdogo wake na baba wa Asael(Mr kiwila).
Cha ajabu Ndugu akakataa hata kuwaruhusu kulala akidai hawezi kukaribisha matatizo kwake,wakabaki nje wasijue hatima yao ni nini usiku ule hakika usemi wa ndugu ni ndugu wakati wa raha tu au unapokuwa umefanikiwa tu na kuja kuomba misaada ukiwa na shida unapambana na hali yako ukiwa peke yako ama na familia yako...
Waliendelea kukaa hapo kwa muda baadae mtoto wao,

Asael akafika naye,alijisikia mkosaji kila alipowaangalia wazazi wake katika hali ile wakati muda mchache tu uliopita familia ilikuwa katika furaha tele chanzo cha matatizo yote alikuwa yeye....

Hawakuwa na jinsi waliingia jikoni hapohapo kwa ndugu yao,Asael aliwaomba radhi wazazi wake kwa kilichokuwa kimetokea,mwisho aliamua kuwaeleza nini kilitokea mpaka wao wakafikia katika hali ile...

Mr chalima akiwa amelala na mke wake nyumbani usingizi haukuwa karibu kwake kwani alikuwa anahisi usalama wake ulikuwa mdogo tayari ushahidi kuhusu biashara zake haramu sasa ulikuwa mikononi mwa mtu fulani!!
Mkewe alimuuliza kuhusu hilo ila hakuweza kumuweka wazi alisema hakuwa na usingizi tu...

Hakutaka kuzungusha kichwa sana kwa mara zote alikuwa akiamini hakuna linaloshindikana mbele ya pesa,sheria aliishikilia mkononi kila alilotatizwa alimwaga pesa na kulifukia bila shida...
iweje leo kijana mdogo mwenye kiherehere tu eti amnyime usingizi??

kakijana tu ambacho hakajafunzwa vyema nyumbani kanaingilia vitu vya wakubwa,Mr chalima alimbeza Kijana mdogo Asael aliyejitia kimbelembele mbele ya biashara zake...
Alijiuliza Ni mara ngapi nimekuwa nikipambana na wanasheria waliosomea na wanaujuzi nawashinda??
Hizo ni rekodi zake alikuwa akizikumbuka....

Alipiga simu katika kituo cha polisi na kuwataarifu familia ya mr kiwira iangaliwe kwa umakini popote itakapoonekana ajulishwe...
mpaka hapo aliamini ameua mchezo.

Asael baada ya kueleza kilichotokea ,walimshauri tu asiumie sana kuwa amewaingiza matatani yote hiyo ni mipango ya mungu tu,
aliwambia wajiandae kusafiri kesho tayari alishaanda usafiri watoke kabisa katika mji wa Arusha waende Morogoro wakaishi huko, aliwambia asingependa aendelee kuitia doa familia na kuhatarisha usalama wao yeye ageenda sehemu nyingine akaanze maisha mapya...

Asubuhi na mapema gari ilifika,Waliagana mama alimsihi mwanaye awe makini na anapoenda Asael alihaidi kufanya hivyo mzee alimkumbatia mwanaye akampiga piga mgongoni kumfariji "take care my son" mzee aliongea...

Gari iliondoka,Asael aliishuhudia tu gari kwa mbali ikipotelea,
moyoni alipatwa na furaha familia kuondoka bila kudhurika yeye aliona kwa upande wake ilikuwa rahisi kujiokoa...

Mr Chalima leo alifika katika kanisa kubwa ambalo pia lilikuwa likijihusisha na kulea watoto yatima,mr chawala alikuwa anatumia nafasi hiyo kila alipokuwa akitoa misaada katika kituo hicho cha kulelea watoto yatima aliita wandishi wa habari,
Habari zilikuwa zinatangazwa na yeye kuzidi kujizolea sifa kuwa ni mfanyabiashara mwema,kumbe nyuma ya pazia ni nyoka....

Hivyo kupambana na mtu kama yule aliyekuwa akikubalika na wengi haikuwa rahisi,

Aliongea machache na kiongozi wa kituo kile,hata father alikuwa chini ya mamlaka ya Mr chalima,

Waliongea mengi kuhusu malezi ya watoto,
Mwisho Mr Chalima akamuuliza "vipi wangapi wamekomaa kutuingizia pesa kwa kipindi hiki nimetumia pesa nyingi sana hadi sasa kuwagharamia hawa watoto"

Father aliangalia kulia na kushoto kuhakiki kama hakuna alikuwa akiwasikiliza....

ilikuwa ni kauli tata sana ya mr chalima haikuwa rahisi kuielewa kwa upesi...

je anamaanisha nini usikose sehemu 03
[9/16, 11:36] : NICE GUY OF CENTURY

SEHEMU YA 03

Mtunzi Asael Samwel

...ilipofika
Familia ya Mr kiwila imefanikiwa kuondoka salama mji wa Arusha,kuepuka unyama uliopangwa na Mr chalima Mfanyabiashara mkubwa jiji la Arusha,Asael bado hajaondoka bado yupo Katika jiji moja na hasimu wa Mr Chalima....

Sasa endelea...
Baada ya mkuu wa kituo cha kulelea watoto yatima kuulizwa swali ni Mr Chalima,kuwa ni wangapi walikuwa wamekomaa kuwaingizia pesa kwa kipindi hicho mkuu wa kituo,

Mkuu wa kituo akiangalia huku na kule kuhakikisha hakuna aliyekuwa akiwasikia alimnong'oneza...

"Mkuu kwa sasa kuna mabinti kama watatu tu ambao wanafaa kuuzika katika soko letu subiri kwa muda waongezeke...

Aliongea mtu huyo kwa utulivu kabisa,
Mr Chalima akamwambia....
"nimeshatumia kiasi kikubwa cha pesa kuwekeza katika kituo hiki cha kulelea hawa watoto hivyo kwa sasa nataka nipate faida pia wakifika angalau 10 unijulishe"

Aliongea Mr Chalima akainuka na kuanza kutoka kutoka katika kanisa hilo walipokutana kufanya mazungumzo yao...

Ni kwa muda mrefu sasa Mr chalima alikuwa akitumia mgongo wa kutoa misaada katika kituo hicho kama msamalia mwema,kumbe alikuwa anatumia nafasi hiyo kama kuwekeza kwa watoto hao kila walipofikia umri fulani hasahasa mabinti alikuwa akiwachukua na kuwauza nchi za nje hasahasa huko uarabuni na kujipatia pesa wakishirikiana na mkuu wa kituo hicho cha kulelea watoto yatima...

Asael hakuwa mbali na eneo hilo,ni wazi kwa sasa alishaamua kumfuatilia hatua kwa hatu Mr Chalima,Mara tu baada ya kugundua huyo mtu hakuwa mwema licha ya kujivika ngozi ya kondoo kwa kujifanya msamalia mwema ili kuficha uhalisia wa unyama wake,
Aliyasikia mazungumzo hayo,lakini hakufanikiwa kuyaelewa hasa yalilenga nini maana walizungumza kwa ufupi sana na kwa mafumbo mengi,aliamini kuna wakati ungefika angeelewa tu hakuwa na shaka alitoweka hilo eneo...
Nyumbani kwa Mr Chalima
Mke wake alikuwa na Mama yake (mama mkwe wa Mr chalima)
Mama alikuwa anamlalamikia mtoto wake ni kwa muda gani angeendelea kumdanganya mmewe kuwa anaujauzito wakati hakuwa na ujauzito...
Mke wa Mr chalima alimtazama mama yake akamwambia,
"mama usijali kila kitu kitakuwa sawa tu mtoto atapatikana na mimi nitatoa haya matambara nitamfanya huyo mtoto ni wangu na mchezo utaishia hapo"
Aliongea mke wa Mr chalima kwa kujiamini sasa...
Mke wa Mr chalima tangu aolewe hakuwahi kupata mtoto,na mmewe kila mara alikuwa akimpigia kelele kuwa anataka mtoto atakayekuwa mrithi wa mali zake hivyo ikamlazimu yeye kutengeneza ujauzito feki ili kulinda ndoa yake na kumlizisha mmewe...

Mama aliendelea kuhoji,
je huyo mtoto utamtoa wapi?
Hujui kama hii ni hatari siku moja mmeo akija ajue ukweli?
Mama aliuliza maswali kwa mfululizo sana kuonyesha alikuwa na wasiwasi sana kwa alichokuwa akikitenda binti yake...
Bintiye(Mke wa mr chalima)
Alimwambia asihofu hayo yote yasingetokea.

Upande wa pili Asael aliamua kurudi katikati kazi yake ya guta ili kudunduliza pesa zimsaidie kuondoka katika mji huo kama alivyokuwa amemhaidi mama yake hataishi hapo te ataondoka,
Akiwa amekaribia kufika kazini kwake,akaangalia kwa umakini eneo hilo aligundua Vijana wa Mr chalima bado walikuwa wakimtafta hivyo walijitega makusudi katika eneo lake la kazi wakitambua wazi lazima tu angerudi kazini na wao wangempata kiurahisi...

Alijua tayari eneo hilo halikuwa salama tena kwake,alihairisha kwenda...

Ulikuwa ni wakati wa kupata chakula cha mchana,familia nzima ya Mr chalima ilikuwa pamoja mezani wakipata chakula cha mchana...
Mr chalima alikuwa anakula huku akiendelea kupiga story za hapa na pale..
"mke wangu mimi huwa napenda sana kula nyama ya paja iliyo kaushwa vizuri hasahasa na mke wangu"
Mr chalima aliongea kwa masihara,
familia yote ikaishia kumcheka...

akaendelea kuongea,
"mke wangu natumaini hata mtoto wangu junior alizaliwa atakuwa anapenda kula kama baba yake nilivyo"
Mamamkwe akashituka sana baada ya kusikia maneno hayo kwani alijua wazi kilichokuwa kikiongelewa halikuwepo kabisa,mke wa mr chalima hakuwa na ujauzito...
akajifanya amepaliwa na chakula ili kuipotezea ile hali ya yeye kushituka...

"ooh samahani jama tatizo dogo nakuja"
Aliongea Mama akatoka nje...

Asael sasa aligeuka mtu wa kujificha ficha tu sehemu ya kula hakuna kazi hana,pesa zote za akiba alishatumia kuisafirisha familia yake alibaki akizurura tu mtaani...
Aliingiza mkono akatoka na 2000 pesa ya kitanzania pesa ambayo isingemtosha hata kwa siku mbili mbele,Giza lilianza kushika hatamu hakuwa na sehemu ya kulala...
Aliwaza angefika vipi hata kama angeamua kuondoka mji Wa Arusha wakati hakuwa na pesa wakati huo kula kwenyewe ulikuwa mtihani?
Alijisogeza uchochoroni kwa bahati akaona walalahoi hoi wamejipumzisha kwenye uvungu wa gari bovu bovu,naye akaona ingemfaa kulala kwa siku hiyo ili kesho aone pakuelekea....

Alivuta usingizi wa bila shuka,Sasa kipindi akiwa amelala kumbe aliingilia dili za watu aisee...
Kumbe katika wale walalahoi waliolala pale,mmoja hakuwa mlalahoi alitumia tu njia ya kujifanya mlalahoi kumbe moyoni alikuwa akiwaza vingine,
Aliamka kipindi wenzake wakiwa wamelala fofofo taratibu,akashika begi lake dogo akalifungua kwa umakini mkubwa alitoa sindano akaiweka sawa akaitia dawa aliyoijua yeye taratibu alianza kumwendea Asael lengo amdunge hiyo sindano katika bega lake....

2017 Asael Samwel

Sijui huyo mtu analenga nini kuamua kumdunga sindano Asael,
Je atafanikiwa kutimiza???
[9/16, 11:37] : SEHEMU YA 04

...ilipofika
John anajikuta katika wakati mgumu hana kazi,pesa,mji mzima anatafutwa hana makazi anaamua kujumuika na walalahoi wa mtaani ili angalau alale siku ipite anangukia katika mikono ya mtu anayetaka kumdunga sindano...

Sasa endelea....
Mtu huyo alikuwa tayari kabisa kudunga sindano lakini bahati haikuwa ya kwake siku hiyo,ghafla Asael akajigeuza kujikinga na baridi maana alilala bila hata kujifunika kitu cha kumkinga na baridi ya usiku...
Hicho ndio kilimsaidia ila akapata wasiwasi juu ya mtu huyo japo hakuiona sindano,alijifanya hakuelewa chochote alihitaji kujua lengo hasa la mtu yule aliendelea kulala...
Huyo aliyeshika sindano akajua hakuonekana,akashukuru lahasha hakujua kuwa tayari alishaonekana akaona huo ndio muda mwafaka wa kutimiza lengo lake akamuendea Asael kwa mara nyingine tena,

Taratibu akaiangalia sindano yake ilikuwa sahihi,Asael aliogopa baada ya kugundua huyo mtu alikuwa na lengo la kuwadunga sindano....

Alimvizia wakati anapeleka tu mkono begani akaudaka!!
Wakaanza kinyang'anyana sindano wakiwa humo uvunguni mwa gari hilo bovu...
Walisumbuana sana mwisho,Asael akafanikiwa kumdhibiti huyu mpuuzi...

Akamtoa nje ya uvungu akamvuta katika uchochoro uliokuwa karibu...
Akaamua kumhoji kwa amani kwanza kabla ya shuruti,
"hizi sindano zilikuwa za kazi gani"
Asael aliuliza...
akarudia swali mara kadhaa bila ya majibu kutoka kwa mtu yule,
akafikiri huenda alitumwa

"nani amekutuma hii kazi?"
bado kimya kiliendelea,

Asael aliwaza kwa sekunde chake,
akajisemea moyoni...
"nikiendelea kumbembeleza huyu mtu hatutafika popote mimi sina ofisi ya mahojiano mimi mwenyewe sina hata sehemu ya kulala...
alimpa onyo huyo mtu,
"nahesabu mpaka tatu usipojibu tutajua cha kufanya"

Aliongea Asael kama alikuwa na masihara vile...

Kwa mwili wa Asael ulivyoonekana mdogo yule bwana alijua huyu hana cha kunifanya cha msingi ananitisha tu hakujua udogo wa mwili haukuwa sababu ya yeye kujiamini,
Asael alianza kuhesabu...

1......

2......

3.......
mpaka alifika tatu bila ya kusikia yule bwana akinyanyua kinywa chake...
Hasira ilimshika aligundua alidharaulika....
Alimpiga goti akamkandamiza kwa kiwiko,
akaugulia maumivu
"nitakueleza"
kauli ilimtoka yule bwana
"sawa ongea"
Asael aliongea..

"Mimi nimetumwa na boss wangu wa gang fulani na siko peke yangu kuja huku mtaani kupanua soko la biashara yetu ya madawa ya kulevya"
kupanua soko kivipi?
Asael aliuliza
Nyumbani kwa Mr Chalima,
usiku akiwa amelala aliota ndoto Mtu amejitokeza mbele ya vyombo vya habari na kutoboa kila aina ya biashara na vitu vyake haramu"

Ghafla akaamka kwa mshituko...
Hapana!!
alipiga kelele akisema "hapana"
mpaka mke wake akaamka
"nini mme wangu"
mkewe akamhoji
"usijali mke wangu ni ndoto tu lala"
Mr chalima alimsihi mkewe asiwe na hofu wakalala...

Moyoni Mr chalima alijiapia "lazima nimkamate kijana huyu lasivyo atanitia kizuizini kabla sijamtia mimi ili nibaki salama"
aliweka nadhiri ya kumkamata Asael ili aishi kwa amani...

upande wa pili yule mtu akaendelea kumweleza Asael,

"Tunapanua soko kwa kuwadunga watu hasa vijana madawa ya kulevya,baada ya hapo wanaathiriwa,wanageuka mateja basi sisi tunapata soko la kuuza madawa yetu ya kulevya,
hata leo ningefanikiwa kujifunga ile sindano lazima ungenitafta tu ili nikuuzie madawa ungekuwa mtumwa wetu moja kwa moja"

Asael alijikuta akinyong'onyea baada ya kusikia hayo maneno...
yule mtu alipata upenyo akakimbia...

Asael akarejea katika uvungu akachukua kile kibegi,ndani akakuta mabomba kibao na sindano vichupa vya madawa ya kulevya na pesa,akachukua pesa maana alikuwa na tatizo la pesa akatokomea kutoka hilo eneo....

Mke wa Mr Chalima alifika hospitali akashuka kutoka katika Gari yake akiwa na mama yake,moja kwa moja akaingia katika hosipitali,alikuta wagonjwa wakisubiri huduma,
kwa kiburi na dharau yeye akaingia moja kwa moja....

Alifika mpaka ndani,akaongea na nesi mkuu kwa muda mchache,mwisho akaulizwa vipi umekuja kiliniki mama?
"hamna ninamaongezi na wewe naomba wamasiliano na wewe"
aliongea mke wa mr chalima,
nesi hakuwa na neno akampa namba ya simu ya mkononi....

Asael alifika kituo cha mabasi,alikuwa anatafuta tiketi mwisho alipata lengo lilikuwa ni kwenda mwanza,Aliambiwa gari itaondoka jioni aliondoka akasubiri muda ufike...
Alitazama mkononi alikuwa bado amebaki na pesa kiasi flani alizozipata jana katika begi lile la mtu yule aliyemweleza kuwa anapanua soko alikimbilia kwa mama ntilie ili apate angalau hata chai....
Mke wa Mr chalima leo alimuita yule nesi ili wapate chakula cha mchana pamoja apate nafasi ya kueleza shida yake,
Wakiwa wanaendelea kupata chakula Mrs chalima aliona huo ndio wakati mwafaka wa kueleza shida yake...

"nesi mimi nashida....
nataka unitaftie mtoto"

Nesi alishituka "nikutafutie mtoto kivipi?"
Nesi alihoji kwa mshituko mkubwa
"usijali nesi wewe huwa unahusika na uzalishaji hapo hospitali hivyo sioni kama ni kazi kupata mtoto"
aliongea kwa kujiamini
Nesi alisema...
"sipo tayari kwa ujinga kama huo mtafute mtu mwingine"
Aliongea Nesi kwa kwa kujiamini na kuanza kuondoka...

"Subiri"
Aliongea mke wa Mr Chalima,

Nesi akageuka,

"unajua kuwa mme wangu anaasilimia 60 ya umiliki wa hiyo hospitali,ukifanya mchezo kazi utakosa tunza hili akilini Nesi,kazi lazima ufanye"
Aliongea mke wa mr chalima kwa vitisho na kujiamini

Akaitaka mhudumu akamlipa pesa ya aliyotumia kupata huduma hapo akaondoka....

Asael alikuwa katika basi tayari kwa safari ya kwenda Mwanza, Haikuchukua muda safari ikaanza taratibu alianza kuuacha miji aliokulia,
moyoni hakuwa na kinyongo aliamini kule alipokusudia kwenda angeishi kwa amani huku akiendelea na mipango yake...

2017 Asael Samwel

je Asael atafika salama?
vipi kuhusu mipango ya mke wa Mr chalima?

Usikose sehemu ya 05
 
NICE GUY OF CENTURY

SEHEMU YA 05


....ilipofika
Mke wa Mr Chalima amemtia mkwara Nesi ili atimize matakwa yake,
Safari ya Asael kwenda Mwanza imeanza Rasmi,Mr chalima ameweka nadhiri ya kumteketeza Asael kijana aliyeshikilia ushahidi juu ya biashara zake haramu....

Sasa endelea....
Mr chalima alikuwa anatoa misaada katika kituo chake alichokidhamini katika kanisa kuu la R.C,kama ilivyo kawaida yake alialika pia wandishi wa habari,
alileta chakula mavazi na vitu vingine vidogovidogo vilivyokuwa vikiwahusu ukuaji wa watoto...
Watu walikuwa na furaha sana huku wakimsifu Mr chalima kuwa hakuna mtu mwema kama mr chalima anasaidia na anajali jamiii yake,hiyo ndio njia aliamua kuitumia Mr chalima kuwapumbaza watu kwa kutoa misaada midogomidogo ili aendelee kuaminika zaidi asishitukiwe juu ya maovu yake aliyokuwa akiyatenda....

Hilo tukio lilikuwa likiruka hewani Asael alilishuhudia akiwa bado yupo safarini katika basi alilosafiria,
"yaani huyu mwanaharamu bado tu anawapumbaza watu kwa kutoa vimisaada vyake vidogovidogo huku nyuma yake ni simba mla watu anatenda kili aina ya uharamia!!!"
alijiongelesha Asael peke yake huku ikionyesha wazi hasira zilimpanda kweli kweli,
shiiiiit...
alipiga ngumi kiti cha mbele kutoka alipokaa,dada mpaka aliyekuwa amekaa mbele kwenye kiti hicho akajisemea moyoni,
"haki ya mungu hapa nimekaa na machizi zamu inayofuata nitapigwa mimi na si kiti tena"

Anyway hakuwa na jinsi aliacha tu mwenye nguvu atawale kwa wakati huo,aliamini siku moja atakuja amuumbue tu huyo mpuuzi mr chalima binadamu asiyekuwa na haya hata kidogo...

Huku Mr chalima alikuwa amemaliza kutoa misaada na kila kitu sasa alikuwa akihojiwa na wandishi wa habari,
Wandishi walikuwa wakimuuliza hasa kwanini yeye amekuwa alijitolea zaidi kutoa misaada tofauti na wafanyabiashara wengine?
Alijibu "kwasababu naipenda jamii yangu inayonizunguka"
alijibu bila wasiwasi hata haya,
Mwandishi mwingine aliuliza...

"mheshimiwa kunafaida yoyote unayoipata kutokana na misaada inayotoa?
hakujibu hilo swali aliharakia kuondoka kwa kigezo alikuwa na mkutano mwingine aliwahaidi kuwa angejibu maswali yao kwa wakati mwingine,
alipanda gari akaondoka...

Sasa wandishi wa habari wakachukia hicho kitendo,

"yaani mtu ametualika sisi wandishi wa habari ili tuandike habari yake halafu hajibu kwa ufasaha maswali yetu kila mara amekuwa akitualika kwenye mambo yake cha ajabu kila ukifika muda wa kuuliza maswali amekuwa akitukimbia sasa tutaandika nini wakati hataki mahojiano"
Alisikika mwandishi mmoja wa habari akilalamika sana huku akiongea maneno hayo...

Father wa kanisa hilo alimsikia barabara taratibu akatoa simu yake ya mkononi akampiga picha huyu mwandishi wa habari alijua,
halafu akasema...

"ukiona katika kundi lako la ng'ombe unaowachunga kuna mmoja anakimbelembele sana kuliko wengine fanya upesi kumuondoa lasivyo hiyo sumu atawaambukiza na wengine katika kundi lako,

sijui alimaanisha nini father kuongea maneno hayo,
alianza kutembea kuondoka hilo eneo...

Asael akiwa ndani ya basi,alisikia kondakta akitangaza kuwa muda si mrefu wataingia jiji la Mwanza,alishtuka!

Moyoni alitamani safari ingeendelea tu,maana hakujua ataanzia wapi baada ya kushuka hapo stendi hakuwa na ndugu wala hakuwahi kufika huko kabla,alijiweka sawa kwa kohozi la kinafiki na tisheti jezi yake ya simba sport club na koti lake tangu avae mwanzo wa safari kama mlinzi wa zamu,
Alimuangali binti aliyekuwa mbele taka akajisemea moyoni...
"huyu ndio atakuwa mwenyeji wangu"
akaanza uchokozi
"samahani dada unashuka wapi"

aliuliza kama wanafahamiana kumbe hawakujuana hata majina yao,
"hapo mbele kaka angu"
akapumua kwa sekunde kadhaa
"ok ok sawa"

moyoni akasema kumbe huna nyodo hahaha wewe ndio utanipa ramani nianzie wapi...

Nesi sasa aliyetishiwa na mke wa Mr Chalima leo alikuwa kazini akiwahudumia akina mama wajawazito waliokuja kiliniki kutazama afya za watoto wao,akiwa anaendelea kuwafanyia vipimo kwa bahati sasa kuna mama alionekana anaujauzito wa mapacha,akatulia tu hakumwambia huyo mama kuhusu hilo na kwa jinsi mama alivyoonekana wa hali duni,
moyoni aliamini asingeweza kutoka hapo akaenda hospitali nyingine kupima tena afya yake,

Hivyo yeye angeitunza hiyo siri mpaka siku ya kuzaliwa watoto ili mmoja ampe Mke wa Mr chalima kulinda ajira yake,kwani aliambiwa asingeweza kufanya hivyo kila kitu angepoteza...

Mwanza
Basi lilifika salama abiria wakashuka Asael naye akiwemo,akamuangalia binti alikuwa na mizigo kibao,akajiangali yeye hakuwa na mzigo wowote hata chupa ya maji mkononi,
Akaona hiyo ndiyo njia ya kumuingilia binti,
akamfuata...
"Naomba nikusaidie kubeba mizigo"
kwa utulivu kabisa Asael aliongea,
No problem
Naomba unisaidie
Binti aliongea...

Walitembelea kwa mfupi binti akaanzisha story...
"Unaitwa nani"
Binti aliuliza
"haa nani mimi"
Asael alijikuta akijibu swali hilo bila umakini
"ndio jina lako"

"Naitwa Asael"

Asael alijibu kwa utulivu mara hii

"ooh Asael jina zuri unique sana ni la kipekee"

aliongea Huyo mdada

"na wewe unaitwa nani dada"

Asael aliuliza

"naitwa Jenifer au jen"

"hata jina lako zuri pia"

Asael alimsifia jen,

"Asante"
jen alishukuru kwa aibu tele

Sasa story zikanoga,jen akawa anajiuliza sasa huyu mtu mbona hasemi hata amefika toka tushuke kule nyegezi...
uvumilivu ukamshinda ikabidi aulize....

"Hivi kaka unaenda sehemu gani"

uuuuh!
Asael alishituka akajua wazi alikuwa mbioni kuumbuka hakuwa anajua hata mitaa ya huko angesema nini sasa?

2017 Asael Samwel

Asael sasa yupo jiji la Mwanza,unafikiri atayamudu maisha ikiwa hajui A wala B hajui aelekee wapi?

umewahi kufika sehemu halafu hujui hata mitaa yake na mwenyeji huna! lengo ikiwa ni kutafuta maisha?

usikose muendelezo.....
 
mkuu hebu toa kwanza muhtasari wa stori yako, main theme / dhamira kuu ni nini!!!.., main character ni nani....., ina sehemu/episodes ngapi...,,!! ili tujue kama itatufaa au vipi
 
mkuu hebu toa kwanza muhtasari wa stori yako, main theme / dhamira kuu ni nini!!!.., main character ni nani....., ina sehemu/episodes ngapi...,,!! ili tujue kama itatufaa au vipi
Episode zote hizo tano hujaelewa tu
 
mkuu hebu toa kwanza muhtasari wa stori yako, main theme / dhamira kuu ni nini!!!.., main character ni nani....., ina sehemu/episodes ngapi...,,!! ili tujue kama itatufaa au vipi
Ambacho hujaelewa ni nini hapo jamaan mbona kila kitu kinajieleza
 
Episode zote hizo tano hujaelewa tu
mkuu nadhani haujanielewa.
Ambacho hujaelewa ni nini hapo jamaan mbona kila kitu kinajieleza
Na wewe pia mkuu,..., nime- request kitu cha maana tu,
unajua maana ya muhtasari?
unajua maana ya main theme?
unajua maana ya idadi ya episodes?
.............. Nimeukiza kwa nia njema tu, mfano stori inaweza ikaanza na mahadhi ya kijasusi hivi kumbe main theme ni love, sasa hii kuigundua kwa kusoma tu hizo epds 5 haiwezi kutoa taswira kamili.

Ndio maana hat kwenye movies, kabla movie haijatoa huwa inaaza Trailer , lengo ni kumfahamisha tu mteja kuwa hii movie itahusu nini hasa..., trailer ndio muhtasari wa movie...
But it is your choice, kama unaona haina umuhimu we potezea tu
 
mkuu nadhani haujanielewa.

Na wewe pia mkuu,..., nime- request kitu cha maana tu,
unajua maana ya muhtasari?
unajua maana ya main theme?
unajua maana ya idadi ya episodes?
.............. Nimeukiza kwa nia njema tu, mfano stori inaweza ikaanza na mahadhi ya kijasusi hivi kumbe main theme ni love, sasa hii kuigundua kwa kusoma tu hizo epds 5 haiwezi kutoa taswira kamili.

Ndio maana hat kwenye movies, kabla movie haijatoa huwa inaaza Trailer , lengo ni kumfahamisha tu mteja kuwa hii movie itahusu nini hasa..., trailer ndio muhtasari wa movie...
But it is your choice, kama unaona haina umuhimu we potezea tu
Maisha/familia
Siasa
Unyanyasaji
Kujitolea
Mapenzi
in short ina maudhui nyingi tu
 
NICE GUY OF CENTURY

SEHEMU..............06

Mtunzi: Asael Samwel

......ilipofika
Asael amefika Mwanza salama,Kutokana na kutokuwa na mwenyeji huko anaamua kumgeuza msafiri mwenza Jen kuwa mwenyeji wake kwa kujipendekeza kumbebea mizigo yake,Nesi ameamua kumficha ukweli mama mwenye ujauzito mapacha ili kutimiza matakwa ya mke wa Mr chalima....

Sasa endelea...
Jen aliuliza swali ambalo lilikuwa gumu sana kwa upande Asael,
Asael alitafakari kwa muda kabla ya kulijibu swali hilo,aliona akiendelea kuwa muongo asingeweza kupata msaada wowote kutoka kwa jen ambaye kwa sasa alishamchukulia kama mwenyeji wake,
Jen alimgusa begani wakati akitafakari nini ajibu...
akashituka kidogo,

"aaaah mimi,mimi kiukweli maeneo haya ni mgeni hii ndio mara yangu ya kwanza kufika nimekuja kutafuta maisha tu hivyo kwasasa siwezi kukudanganya kwamba naishi sehemu flani"
Asael aliongea Kwa uwazi kabisa...
Jen alimtazama kwa sekunde kadhaa bila kuongea kitu,
Asael akahisi labda binti alimsuta....

Maana Jen mwenyewe kwa kiasi flani alionekana wa matawi ya juu,
Sasa mabinti kama hao wenye nafasi kiasi fulani kumsikiliza boy tena asiyekuwa na makazi kama alivyokuwa Asael kwa Dunia ya sasa ni mtihani sana,
Asael alihisi na jen ni kama wale tu baada ya kumwambia tatizo lake bila kumjibu,
Alijikuta akiachia mizigo ya mlimbwende huyo...

Jen akashindwa kumuelewa....

"mbona unaacha sasa mizigo twende mbele hapo nikuonyeshe sehemu ukaombe kazi au hutaki kazi?"

Jen alimuuliza Asael,

Asael alijibu kwa unyenyekevu...

"please kanionyeshe kazi nataka tena sana"
Aliongea huku akibeba mizigo ya binti yule....

Arusha
Mr chalima Alikuwa kwenye kikao cha bodi ya kampuni yake ya ujenzi,Alikuwa akilalamika sana kwa kuwashutumu wafanyakazi wake wazembe,kuna mradi walipewa oda wajenge sasa mpaka sasa ilikuwa miezi mitatu imepita bila hata msingi kuanzishwa,
Meneja alisimama akasema,
"Boss sisi hatuna tatizo,tatizo ni kwamba wamiliki wa viwanja wamekataa kuhama maeneo yao wanadai mpaka walipwe fidia,na kampuni haina uwezo wa kulipa fidia ni pesa ndefu sana"

Wafanyakazi wengine wakamuunga mkono mzungumuzaji,
kwa kushabikia kuwa ni kweli wananchi hawataki kuhama maeneo yao,
Sasa hiyo hali ikamfanya Mr chalima kuhairisha kikao ili ashughulikie hilo swala kazi iendelee...

Nesi leo alimualika yeye mke wa Mr chalima ili waweze kupata kinywaji pamoja,Mke wa Mr chalima alishangaa sana kuona hivyo akajiwekea imani kuwa alishamshinda ujanja Nesi yule,
Basi waliendelea kupata kinywaji taratibu,
"nimeshakubali ofa yako nitafanya hiyo kazi"
aliongea Nesi kwa sauti tulivu kuhakikisha walisikilizana wenyewe tu...

"aah kweli!"
alidakia madam

"mtoto wako kwa sasa anakuja kiliniki hivyo jiandae kumpokea"
Madam alifurahi kusikia hivyo...

akasema
"lini atazaliwa ni kumchukua mwanangu jamani,natamani sana kushika mtoto"

Madam alijikuta akiropoka kutokana na furaha iliyokuwa imemjaa hakuwahi kuwa na mtoto tangu azaliwe madam mpaka akafikia umri wa kuzeeka na Mr Chalina alimvumilia tu,

Moyoni nesi alisema...
"yaani unafurahia mtoto ambaye si wako kweli wewe madam hamnazo kabisa,nakufanyia hivi kwasababu umenilazimisha tu sijakusudia kufanya unyama huu"

Licha ya nesi kukubali kufanya hivyo hakulizia kutoka moyoni ni kwasababu mke wa mr chalima/madam alimlazimisha tu,

"ila kuna sharti moja"

Aliongea Nesi kwa kujiamini sana

"nini unataka"

"walibaki wamengaliana kwa macho makavu sana"

"nitakwambia baada ya kukamilisha kazi yako madam"

"sawa rafiki yangu nitakupa chochote unachotaka"

aliongea madam kwa furaha na bashasha za kutosha

"hakuna tatizo madam wewe andaa nguo tu za kijacho ndani ya wiki mbili mtoto anazaliwa wa kiume"

madam baada ya kusikia habari hizo,kwamba mtoto ni wakiume aliibuka kwa furaha akamuaga harakaharaka Nesi akaondoka...

Nesi alimfyonza Madam,

Mwanza
Baada ya kutembea kwa muda mfupi jen alimwambia Asael wamefika hiyo sehemu...

"fuata hiyo barabara ndogo mbele kidogo kwa mkono wa kushoto utakuta hotel jina imeandikwa "YELLOW STAR HOTEL"
ulizia ofisi ya boss sio meneja wa hiyo hoteli utaelekezwa wapi ilipo ni hotel kubwa sana"
yalikuwa ni maelekezo ya Jenifa,

Asael alimshukuru Jen kwa ukarimu wake akashika njia aliyoelekezwa,alitembelea kama hatua nne akasikia jen anamwita...

aligeuka,
"chukua namba za simu uspofanikiwa unitafute nione njia nyingine ya kukusaidia"

aliongea jen akapokea simu toka kwa Asael akaandika namba yake ya simu wakaagana....

Asael akiwa njiani kufuata maelekezo ya jen kwenda mahali alipo onyeshwa akatafute kazi,alikuwa akijilaumu kwa tabia yake ya mwanzo kumshutumu jen ni msichana anayejiona kama alivyokuwa alishuhudia mabinti wengine wa hadhi yake wakiwasuta wanaume wasio na kitu kama yeye,
Huyu hakuwa hivyo aligeuka kuwa msaada kwake mpaka wakati huo,

Alitembea kwa dakika chache,kweli akaona jengo kubwa limeandikwa "YELLOW STAR HOTEL"
bila shaka alitambua wazi ndipo hasa alielekezwa na jen alijiweka sawa akachepuka kutoka katika njia alikua alipokuwa kuifuata hiyo hoteli kwa umakini mkubwa....

Aliingia mpaka ndani ya hoteli hiyo kwa ufupi hakufanania na mazingira ya hoteli hiyo,hoteli ilikuwa ya hadhi ya juu yeye hata mavazi alikua na kitisheti cha simba sport club,
Alipokelewa na wahudumu kwa ukarimu mkubwa,ila aliwambia yeye hakuwa anataka huduma alihitaji kukutana na mmiliki wa eneo hilo maana ofisi yake pia ilikuwepo palepale hotelini,
Wahudumu ilibidi wamcheke maana hakufanania na hadhi ya boss wao,

waliona wasimnyime nafasi wakamuelekeza ofisi yake ilipo,moja kwa moja alitembea kwa mwendo wa kujiamini kuifuata ofisi hiyo,

Secretary alimuuliza kama alikuwa na ahadi ya kukutana na boss alisema hakuwa nayo alimsihi asubiri kwa muda,
secretary aliingia ofisini kutoa taarifa ya ujio huo boss aliruhusu aingie...

Basi secretary alirudi akamwambia Asael aingie...
Aliingia,,

Boss Mr Sam alimuelekeza kiti akae..
"kijana nini kimekulete hapa sikuwa na appointment na wewe"

"samahani mkuu ni kweli nimekuingilia katika shughuli zako"

"bila samahani kijana"

"nilikuwa naomba kazi hapa hotelini"

Mr sam akamtazama kwa sekunde kadhaa bila kusema kitu,
moyoni akasema
"sasa huyu kijana anaomba kazi za hoteli mwili wenyewe mwembamba kiasi hiki ataweza kweli kufanya kazi kiufasaha au ni msumbufu tu"

akiwa anatafakari jambo hilo kabla hajamjibu Asael simu yake ya mkononi iliita....

Alishtuka baada ya kuangalia nani alikuwa akimtafta ilikuwa namba ngeni,
alipokea akaiweka katika sikio lake la kushoto,
Ghafla sura ilibadilika uso wa woga ukamjaa,

"please jamani msimzuru"

hilo ndio neno pekee lilimtoka wakati huo huku wazi akionekana alikuwa na wasiwasi sana....

Ni taarifa gani amezipata Mr Sam,Mmiliki wa Yellow Star Hotel?
ungana na mimi sehemu inayofuata.....

2017 Asael Samwel

NICE GUY OF CENTURY

SEHEMU...............07

....ilipofika
Arusha
Nesi amekubali kufanya kazi ya kumuibia mtoto mke Wa Mr Chalima,upande wa Mr Chalima mambo hayako sawa kabisa kampuni imeshindwa kuendelea na ujenzi wananchi hawataki kuondoka katika maeneo yao bila kulipwa fidia kupisha mradi unaotekelezwa na kampuni ya Mr Chalima,
Mwanza Asael ameonana na boss wa Yellow Star Hotel kazi hajapata bado....

Sasa endelea....
Simu ilikatwa Mr Sam alikuwa na hofu sana,
"nipitie secretary mara moja"

Asael alitumwa,

"sawa boss"

Alitoka nje akaingia na secretary....

"wapigie simu vijana wangu wafike hapa mara moja kuna tatizo limetokea"

"sawa boss"

secretary alijibu,
"Boss nini kimekusibu?"
Asael alihoji

Mr sam akawaza hata kama angemwambia huyo bwana mdogo na kaumri chake kadogo na mwili pia angeweza kumsaidia nini sasa....
alisema
"nipo sawa ni mushkeli ndogo tu kijana"

Aliongea Mr Sam

Simu ilipigwa tena,Alipokea upesi hii ilimshtua zaidi woga ukazidi zaidi hata kiti kiligeuka cha moto zamu hii alisimama,
Simu ilikatwa tena.

Zamu hii aliona bora hofu yake amshirikishe na jirani ingawa jirani mwenye alikuwa mgeni...

"kijana binti yangu mpendwa ametekwa,hapa nilipo sijui hata kama yupo salama au vipi"

Asael alishtuka,
"Ametekwa"

Nani amemteka?

"kijana swala sio nani amemteka mimi nahofia usalama wa binti yangu"

"nikusaidie vipi sasa mimi niko tayari kukusaidia"

Mr Sam alimwambia "kijana sizani kama una ujasiri wa kunisaidia maana naona hata huna ujasiri wa kufanya hivyo ila unaongea ongea tu"

Aliongea Mr Sam kwa kumdharau Asael,
Asael hakuwa na haraka kwakuwa yeye alikuwa mgeni pale ni lazima tu asingeaminika alishalala nje kama wiki 2 hivi hivyo hata afya yake haikuwa wima ililenga lega kwa kiasi fulani...

Waliingia kama vijana sita hapo ndani,vijana walioaminika kwa MR SAM,Hakutaka kuwaficha chochote aliwambia hali halisi jinsi ilivyokuwa ikiendelea...

kuwa "Binti yake katekwa na gang flani la wahuni na sharti wapeleke milioni 20 tasilimu bila kuhusisha polisi ndani ya masaa matatu (03)
lasivyo bintiye anapoteza uhai wake"

Mzee aliongea kwa hofu sana,"
Sasa cha kufanya andaeni utaratibu mzuri pesa zipelekwe mara moja"

Alisisitiza "wewe Idris Wahi mara moja ukatoe pesa benki"

Alimtuma mmoja kati vijana wake aliowaamini sana,

Muda wote huo Asael alikaa kimya tu hakuwa na la kufanya kwani Boss kwa wakati huo alikuwa na presha za mtoto wake kuwa hatarini asingeweza kumsikiliza yeye....
Mr Chalima aliendelea kuzunguka zunguka tu hapo ofisini bila kukaa wako akiendelea kumsubiri Idris alete fedha ili wazipeleke wakamkomboe binti yake...

Arusha
Baada ya Madam/mke wa Mr Chalima kupata habari kitikadi kwa nesi kuwa mtoto alikuwa mbioni kuzaliwa,
Leo alimleta mmewe supermarket kununua mahitaji ya mtoto wao walikuwa wakitegemea kumpokea siku sio nyingi,
Katika hilo Mr chalima hakika alikuwa kipofu hakuweza kutambua kuwa mkewe alikuwa na mimba bosheni tu alitia matambara tu ili kuzuga,
Hizo nguo na mahitaji mengine walioenda kununua hayakuwa ya mtoto wao,
mtoto alitegemewa wa kuibwa...

Mr chalima alichagua kila kilichokuwa kikimhusu mtoto ili kutimiza wajibu wa baba wa mtoto hakujua kilichokuwa nyuma ya pazia,
licha ya kuwa nyemela mtu hatari lakini bado mkewe alimchezea tu changalamacho...

Walifika nyumbani baada ya kutoka huko supermarket,
Mr Chalima akawahi kuwasha runinga,

Bahati nzuri ilikuwa taarifa ya habari....

sasa katika kuifuatilia taarifa hiyo ya habari,
Mr chalima akasikia mwandishi wa habari ameuwawa na mwili wake kutekelezwa,ikabidi aweke umakini kufuatilia habari hiyo,

Baada ya kuona picha ya mwandishi huyo wa habari ndipo akamkumbuka,

"aaah ni yule yule aliyekuwa amenibana maswali kule kituo cha kulelea watoto yatima"

alimkumbuka
moyoni aliona ni moja ya faida kwake maana huyo mwandishi alizidi ushilawadu,sasa alijiuliza nani alifanya hiyo kazi?
jibu hakuwa nalo...
Ghafla simu yake ikaita,
Alipoangalia,Alikuwa ni father wa kanisa lile linalojihusisha pia na uleaji wa watoto yatima,
Father alisikika akisema
"nimeshusha mbuyu ulioanza kumeya katika yetu mkuu"
simu ilikatwa
Mr chalima alimuelewa father nini alimaanisha.....

Mwanza
Idris alifikisha pesa baada ya kuzitoa Benki,Mr Sam alishukuru kwa hilo upesi alishika simu yake akawapigia watekaji,
"tafadhali naomba niongee na binti yangu"
aliongea Mr chalima

upande wa pili majambazi wakamfungua binti mdomo aongee na baba yake...
Hali yake haikuwa nzuri,hakuwa amepata chakula kwa muda mrefu hata kuongea alisumbuka,
aliishia tu kuita "baba"

Mzee hofu iliongezeka,

"niambieni sehemu gani tukutane niwapatie pesa mnikabidhi binti yangu"

alipewa maelekezo sehemu ya kukutana....

Sasa ilibaki tu kupatikana mtu wa kupelekea pesa hizo,hilo mzee hakuhofia sana alijua Idris angefanya hiyo kazi kwani alikuwa akijigamba mara kwa mara kuwa anampenda binti yake anahitaji kumuoa,
walipanga mikakati jinsi ya kwenda hilo eneo,
Mwisho mzee akauliza swali la makusudi akijua wakwanza kujibu atakuwa Idris,

"nani atabeba hili jukumu la kwenda kufanya mabadilishano sasa ili awahi mapema sehemu ya makutano"

cha kushangaza sasa wote walikaa kimya na kurudi nyuma hakuna mtu aliyekuwa tayari kuharisha maisha yake katika jambo hilo hata idris alimkana mzee alirudi nyuma mzee akabaki mwenyewe tuu,
mzee hakuamini kilichotokea...
aliwatazama wote waliinamisha vichwa chini kwa aibu...

Mzee alisema

"Nitaenda mwenyewe kumkomboa binti yangu"

kimya kikatanda kwa muda

Ghafla
Sauti ikasikika ikisema....

"usijali boss mimi nitaenda kukuletea binti yako"

Alikuwa ni Asael ameropoka!

watu wote wakamtumbulia macho kwa mshituko,maana kamwili chenyewe alikuwanacho kadogo mabaunsa wenyewe akina Idris walikataa hiyo mission....

Mr Sam alimshamgaa sana kijana mdogo Asael,kujana ambaye hakuwa hata akilini mwake,hakuwa anajua hata kama bado yupo ndani maana mwanzo alikuja kuomba kazi tuu.

Je Asael ataenda? Atafanikiwa kumleta binti salama?

majibu yote yapo sehemu inayofuata....

2017 Asael


NICE GUY OF CENTURY

SEHEMU.............08

....ilipofika
Mwandishi wa habari ameuwawa na watu wasiojulikana,baadae tukasikia father akimwambia Mr chalima "nimeshusha mbuyu ulioanza kumeya katikati yetu"
Hatimaye Mr chalima amefanya maandalizi ya kupokea kiumbe kijacho,
Asael ameweka nadhiri ya kumrudisha binti wa mr sam/Rais wa Yellow Star Hotel salama kutoka katika mikono ya watekaji je atafanikiwa?....

Sasa endelea.....
Asael alikuwa kwenye hekaheka za kumkomboa binti wa Mr Sam baada ya kumhaidi kufanya hivyo Mr Sam,
Alikuwa na briefcase iliyosheheni pesa za kwenda kufanya mabadilishano katika mkono wake wa kushoto,
mkono wa kulia alikuwa anautumia kushika simu iliyokuwa na mawasiliano na watekaji...

Alifika katika dustbin aliloelekezwa akaitia hiyo briefcase ndani alihakikisha hakuna aliyeshuhudia hilo,kama alivyokuwa akielekezwa na watekaji hao....
akaambiwa asogee mbele kwenye njiapanda asubiri kwa muda wa dakika 5-10
binti angefikishwa hapo alifanya hivyo...

Baada ya kuweka hizo pesa kwenye pipa la taka alisogea mpaka kwenye njiapanda aliyoambiwa akasubiri mateka aletwe,
Majambazi yalifanikiwa kuzichukua zile pesa kwenye pipa la taka halafu wakatokomea nazo,
walipofika mbali kidogo waliangalia ndani wakakuta zipo sahihi...

wakapiga simu,

"aisee mpelekeni binti hajakiuka masharti pesa tayari tunazo"

simu ilikatwa,

Asael bado alikuwa akiendelea kusubiri tu ilikuwa mida ya jioni jioni kila mtu akiendelea na pilikapilika ili awahi kwenda nyumbani baada ya kazi,
Ghafla Gari ndogo ilisimama mbele yake akaamuliwa apande akapanda...

Ndani sasa alikutana na binti amechoka sana moja kwa moja alijua ni huyo alikuwa akimsubiri aletetwe,akamhoji yule jamaa alikuwa akiendesha hiyo gari...
"bro tunaenda wapi sasa hela tayari nishawakabizi sasa unataka nini zaidi?"

yule jamaa kwa kiburi na jeuri akaambiwa "tulia wewe mtoto wa mama"

akaona hapa lazima atumie akili ili kumkomboa binti,

Aliiikunja ngumi yake taratibu kabisa bila woga akamshindilia moja safi katika shingo yule mpambe akapoteza fahamu...

Gari ikaanza kuyumba baada ya kukosa dereva,
waliishia kugonga mti ulikuwa pembeni ya barabara...

Asael hakuumia sana baada ya ajali,alikurupuka upesi,akamtoa binti katika gari hiyo mpaka nje,akapiga simu kwa Mr chalima ili apate msaada....

moyoni alijisemea

"huyu mpuuzi katumwa amlete mateka kwangu halafu yeye anajifanya mjanja anataka kula dili mara mbili hana akili kweli"

Ni kweli huyo jamaa aliambiwa amelete binti amekabidhi kwa Asael kama walivyokubaliana pesa zilishaletwa na Asael,sasa yeye kwa tamaa zake akataka awateke tena akipatiwa pesa nje na mpango wa Boss gang wao aliyemteka binti mwanzo....

Haikuchukua muda gari ilifika binti akawahishwa hospitali,

Hospital
Idris,Mr Chalima na Asael walikuwa nje wakisubiri majibu toka kwa madaktari,
Mr Chalima alikuwa na hofu sana,Alimuuliza Asael kama aliumia popote naye apate matibabu,lakini Asael alijibu hajaumia alipata mikwaruzo midogomidogo tu,
"kijana nenda kapumzike mimi nitamwekea umakini mwenyewe binti yangu tutaonana kesho"
Mr Chalima alimwambia Asael,

Asael akabaki kutoa macho tu hakuwa na sehemu ya kulala sasa angeenda wapi?,

"Boss mimi sina makazi ndio kwanza tu nimefika mwanza leo hivyo......"

Asael hakumalizia kuongea mr chalima akamkatiza,

"usihofu kijana wewe nenda hapo hotelini nitaongea na meneja atakupa chumba cha kulala mengine tutaongea kesho"

"nashukuru boss"
Asael alijibu kwa heshima zote

"haya usiku mwema"

Mr Sam alimuaga.

Haikuwa mbali kutoka hospitalini mpaka hotelini hivyo Asael alitembelea tu kwa miguu,
Baada ya muda alifika akajieleza kwa meneja,
Meneja alimwambia tayari taarifa zake alishazipata kutoka kwa Boss...
Hivyo moja kwa moja alipelekwa mpaka kwenye chumba kilichokuwa wazi hakina wateja,
Alimshukuru meneja kwa hilo.

Aliingia ndani akajipumzisha kwa muda kitandani,
Ghafla simu yake iliita kutazama kwa umakini alikuwa ni mama yake!
Alitabasamu kuona hivyo alisha mmiss mama yake akaipokea simu...
Alimuamkia
Mama akamuuliza "bado upo Arusha"

"Hapana mama"

"Umeenda wapi"

"Nipo Mwanza mama"

"Lini ulifika huko?
Ulifikia kwa nani huko mwanangu,upo salama kweli?"

Mama alikuwa na hofu sana kuhusu mama yake hiyo ilimfanya aulize maswali mfululizo bila hata kumpa nafasi ya kujibu mwanaye,

"Usijali mama mimi mtoto wa kiume,nitakosaje sehemu ya kufikia nipo salama"

Asael aliongea kwa kujiamini ili kumtoa wasiwasi mama yake,ingawa alikuwa na maumivu kutokana na hekaheka za muda mfupi uliopita wakati akipambana kumuokoa binti wa Mr Sam,hakutaka kueleza hilo,

"Vipi nyie mlifika salama huko?"

"Ndio mwanangu,Baba yako,Maria mdogo wako na Bright pia wote wazima wanakusalimia tu"

Mawasiliano yalikatika,

Asael alijua tu salio lilimwishia mama yake...

Haikuchukua muda baada ya simu kukatika...

Ujumbe mfupi ukaingia...

"Salio limeisha mwanangu tutaongea kesho,cha msingi kuwa makini usijiingize kwenye magenge ya kihuni tu kuwa makini nakupenda sana son"

Asael alifurahia sana kusoma huo ujumbe...

Akaamua apunguze nguo ili aoge alale sasa maana alichoka sana,

Mara simu ikaita tena...

Alikuwa Jen,

"Vipi umepata kazi?"

"Ndio nakushukuru sana"

"Aaah hamna bhana usinishukuru mimi mshukuru mungu maana ndiye kakuwezesha mimi sio kitu"

Jen aliongea..

"Ok sawa"

"Umepata sehemu ya kulala pia?"

"Ndio"

"Usiku mwema,mimi nipo hospitali namuangalia rafiki yangu hapa kapata matatizo"

Aliongea jen,

"Haya poleni nitakuja kukuona kesho"

Asael alijibu maongezi yakaishia hapo,Asael akaelekea kuoga....

Arusha
Madam/mke wa Mr chalima alikuwa akitandika kitanda chake taratibu tumbo likiwa limefura kama kweli ni mjamzito...
Ghafla simu yake ikaita,
Alikuwa ni yule nesi wake.
Akaangalia huku na kule kuhakikisha hakuna aliyemuona kisha akaipokea...

"Madamu leo ndio mtoto anazaliwa hivyo jiandae,kesho asubuhi uhakikishe unakuja,kuwa makini mimi ndio naingia wodini kwenda kumzalisha"

Simu ilikata...

Hizi habari zilikuwa njema kwake,aliruka ruka kitandani kwa furaha,

"Hatimaye sasa mikono yangu inaenda kushika mtoto siamini!"

Aliongea

Ghafla mmewe akaingia......

Unajua nini kitafuata usikose

[HASHTAG]#ToaMaoni[/HASHTAG]
[HASHTAG]#Like[/HASHTAG]

Facebook: Asael Samwel


instagram: @asaelsamwel
 
Story Nzuri ila inakosa ubunifu kias
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom