Karibuni sana wapenzi wa simulizi, Leo naitambulisha kwenu simulizi hii iitwayo "MWACHENI AISHI." Ndani ya simulizi hii utakutana na visa, mikasa na matukio ya maisha kwa ujumla, vimbwenga, mapenzi wivu, usalitu, chuki, mauaji, na kadharika. Mwandishi anakukaribisheni kutoa maoni ushauri na mapendekezo usomapo simulizi hii.
Simulizi, "MWACHENI AISHI"
SEHEMU YA KWANZA.
Amini Usiamini lakini hali ilikuwa tofauti na vile wahenga walivyouaminisha ulimwengu ya kwamba "usiku wa deni haukawii kucha" maana licha ya kwamba haukua usiku wa deni lakini kwa maoni yake ni kwamba usiku huu ulikuwa mfupi mno, yaani ni kama jana yake giza lilichelewa kuifukuza nuru duniani, na sasa limeharakisha kuikimbia dunia.
"Aisee, yaani leo ni kama vile sijalala kabisa, yaani kujiegesha kidogo tu tayali kumekucha" aliongea mwanaume mmoja wakati akijiinua kivivu toka kwenye godoro lake ambalo limetandikwa sakafuni pasipo uwepo wa kitanda.
Alijinyanyua taratibu huku akijinyoosha na kupiga miayo kwa mkupuo, aliyafumbua macho yake na kuanza kuangaza huku na kule akitafuta ni wapi simu yake ilipo, kwa hasira aliitazama simu hiyo ambayo mda mchache uliopita ilitoa mlio mkali ulimuamsha mwanaume huyu. Hakuwa na shaka kuhusu muda, kwani ni yeye mwenyewe aliyetega alamu kwenye simu hiyo, hivyo aliamka na kuchukua taulo na baadhi ya zana zake za usafi, akatoka mle ndani kuelekea maliwato ambako angejifanyia usafi wa mwili.
Mawazo mengi yalikuwa yakipita kuchwani mwake, alilikumbuka vema tukio la jana yake usiku lilopelekea mpaka akachelewa kulala, tukio ambalo kwake lilikuwa zaidi senema za kihindi ziaminikazo kuwa na matukio mengi ya uongo. Alipomaliza kuoga aliingia ndani kujiandaa, muda mwingi alikuwa akiitazama simu yake akionekana kutegemea jambo fulani kutoka kwenye simu hiyo. Naam, haukupita mda mrefu simu yake ilitoa mwanga hafifu uliofuatiwa na mlio mkali wa kumfanya mwenyewe aisikie hata awapo katika mazingira ya fujo, aliichukua kisha akabofya kitufe cha kupokea "Vipi jamaa, nimekaribia hapo, fanya haraka, nikukute tayali tuondoke maana mda umeenda sana," ,,,"sawa, " yalikuwa ni maongezi mafupi aliyoyafanya na mtu wa upande wa pili aliyeonekana kuwa mtu wake wa karibu.
Haukupita mda, ulisikika mrio wa pikipiki nje ya nyumba, mwanaume huyu akachukua begi lake dogo la mgongoni na kutokanalo nje ambako alifika na kupanda pikipiki hiyo ya rafiki yake ambaye aliitoa kwa kasi, " Oya Nemes vipi huko utokako, kwema?"> "kunakuwaje kwema jamaa yangu, yaani hapa nangojea leo jioni ifike, lazima yule dogo aondoke, kama kazi imemshinda bora arudi kijijini asijeniletea matatizo mjini hapa" aliongea dereva yule wa pikipiki ajulikanae kwa jina la Nemes. "
Ndiyo mmeafikiana hivyo?" Aliuliza mwanaume huyu ambaye mda huo alikuwa akihangaika kushikilia vizuri pikipiki ile iliyokuwa ikikimbia kwa mwendo wa kasi sana. "Lazima aondoke hilo halihitaji majadiliano yoyote, maana naona kabisa huu ni mchezo ananifanyia, hembu angalia, hii ni wiki ya pili sasa, na bado hali yake ni ileile haibadiliki, wewe unafikiri ni nini kinafatia hapa kama siyo mimi kuanza kumlea kama mtoto mdogo? Hafanyi kazi yoyote, yeye wa kula tu, hata hela aliyokujanayo imeisha kabisa." Nemes alitao maelezo hayo ambayo yalilenga kumshawishi mwenzake "Shida yako unajifanya kutokuelewa nini kinamsumbua bwanamdogo, yule ni mgonjwa kaka, sasa kwanini ulazimishe awe anashiriki kazini, ungekuwa wewe ungeweza? haya ni maisha tu kaka." Yule mwanaume alimjibu Nemes akionesha kutakubaliana na mpango wake.
Safari yao ilikuwa ya kwenda nje kidogo ya mji kwani hata walipofika njia panda ya Chiwangu waliiacha balabala ya kuingia soko kuu la mkoa na kuifata Ile ilekeayo nje ya mji huku wakizidi kuzozana katika mazungumzo yao. Nemes anaonekana kukasilishwa na kutokubaliana na hali ya mwenzao waliyemtaja kuwa ni mgonjwa. "Oya haijalishi na wala sitajari ni undugu gani uliopo kati yetu, yaani kwa hali hii, sioni kama tutawezana tena, kesho lazima dogo aondoke, siwezi kuendelea kulea ujinga" aliongea Nemis kwa sauti ya juu ili mwenzake aweze kumsikia "lakini ukumbuke wewe ndiye uliyemshawishi mpaka akakubali ", " nakumbuka, lakini mpango si ilikuwa aje tupige kazi? "
Nemesi aliendelea kuhoji, huku akionesha kushikilia msimamo wake na kutokubaliana na mwenzake huyu."sawa, hili suala ni lakwako, Mimi nafikiri halinihusu saana, lakini katika yote utakayoamua ukumbuke ni ndugu yako yule, niwewe unapaswa kumsaidia kwanza kabla ya wengine." Mazungumzo yao yaliendelea wakiwa tayari walishauacha mji.
Ilikua ni safari ya takribani nusu saa, kutoka mjini mpaka huku waliko sasa, lilikuwa ni eneo kubwa la wazi ambapo kulionekana kuwapo baadhi ya majengo ambayo bado hayakuwa yamekamilika, hapa ndipo safari ya Nemes na mwenzake ilipoishia. Waliipaki pikipiki yao katika eneo maaaluma ambako kulikuwepo magari kadhaa na pikipiki, waliingia ndani ya jengo moja ambako hawakukaa sana, walitoka wakiwa wamevaa sare kama walizovaa baadhi ya watu waliokuwepo hapo. Walikua ni mafundi ujenzi(waashi) na hapo ndipo walipokuwa wakifanyia kazi ya ujenzi.
Yapata saa tatu za asubuhi sasa, ni ndani ya nyumba moja ndogo anaonekana Kijana mmoja, amelala sebuleni juu ya kochi, haukupita muda kijana yule aliamka akionekana kutokuwa sawa hata kidogo, sura yake ilikosa nuru kutokana ina le hali ya kutoka usingizini, alijiinua pale alipokuwa amelala na kwenda maliwato ambako alijifanyia usafi wa mwili. Kichwani alikuwa akiwaza mengi, alitamani walau angekua na uwezo, wa kubadirisha mfumo wake wote wa maisha lakini alijua kitu hicho hangekiweza kamwe.
Baada ya kumaliza kunawa alirudi tena sebuleni ambapo kwa sasa hakulala kama mwanzo, alikaa kwenye kochi ambalo bila kupenda lilibonyea kutokana na uzito wake. "Siamini kama kweli haya yanayonikuta ndiyo mpango wa Mungu juu ya maisha yangu" alijisemea kijana huyu. " Kwahiyo jamaa anataka niondoke?, du! sijui itakuwaje, yaani nirudi kule tena!, hii itakuwa hatari sana kwangu, siwezi, siwezi kabisa kufanya kitu kama hiki." Alikuwa katikati ya dimbwi la mawazo ambayo yalimchanganya sana, hakukubaliana na mchakato uliokuwa ukifanywa juu yake, "eti anasema atanipa nauli nirudi niondoke, hii ni sawa kweli! na vipi kuhusu pesa? Au ndiyo anataka anizulumu" alipowaza kuhusu kuzulumiwa mawazo yake yalimpeleka mbali sana, alikumbuka namna alivyohangaika mpaka kupata pesa ambazo yeye aliamini kuwa zingekuwa mwanzo wa kuishi maisha mazuri, maisha ambayo yangemuweka mbali na shida alizozipitia huko nyuma.
Hakuamini kabisa kwamba leo hii ilitakiwa iwe siku yake ya mwisho kukaa mbali na shida, ambapo kesho yake alipaswa kuondoka, "Hapana, haiwezekani, yaani niondoke mikono mitupu" akili yake iligoma, iligoma kabisa kukubaliana na mpango uliokuwepo. "Lazima nitafute namna ya kufanya, lazima nibaki" aliwaza hivyo, lakini uso wake ulipatwa masikitiko baada ya kukumbuka hali yake ya ugonjwa uliomsumbua. "du! Sijui itakuwaje, lakini siondoki, bora nifie hukuhuku" ni kauli ya kishujaa ambayo aliitoa, akionekana kuwa na mengi moyoni mwake yaliyokwisha uumiza moyo wake. Hakuwa na usingizi ambao ungemfanya kulala tena hivyo alipanga kwenda mgahawani akapate kifunguakinywa kuiganga njaa aliyokuwanayo.
Alitumia zaidi ya dakika kumi kufika mgahawani, "KWA MAMA ZABI VYAKULA VITAMU" ndivyo lilivyosomeka bango kubwa lililowekwa juu ya mgahawa huo, ulikuwa mgahawa maarufu sana maeneo hayo, umaarufu wake ulitokana na huduma bora iliyotolewa mahali hapo. Huu ndio mgahawa pekee uliopo jirani na makazi ya kijana huyo, na hapa ndipo amekuwa akifika mara nyingi kupata chakula, "karibu Tena Morisi" sauti hii lilipenya kwa namna yake ndani ya Ngoma za masikio ya kijana huyu ambaye tunamjua sasa kwa jina la Morisi, ilikuwa ni sauti ya binti Nasma mfanyakazi wa mgahawani hapo iliyokuwa ikimkaribisha kwa bashasha kubwa kijana Morisi.
"Ahsante" alijibu Morisi kwa sauti ambayo haikuonekana kujari wala kuendana na lile bashasha alilokuwa nalo binti mhudumu ambaye alionesha kutopendezwa na jibu hilo, "Chai Moja, Chapati mbili" aliongea Morisi kuagiza kifungua kinywa hicho ambacho hukipendelea sana. Binti huyo alimuandalia mteja wake kile alichokiagiza lakini badala ya kuweka chapati mbili aliweka nne na kupeleka pale mezani alipokaa Morisi. Morisi alishangaa kuona ameletewa zaidi ya alivyoagiza, "labda atakuwa amechanganya, chakwangu kampatia yule jamaa" alijisemea moyoni huku akitarajia kumwona jamaa yule akiulizia ziada yake jambo ambalo halikutokea kwani jamaa yule alianza kula chakula chale bila kuuliza. Morisi hakuwa mjinga kula zaidi ya vile alivyoagiza kwa maana alilijua balaa la mamant'ilie namna wanavyokuwa watata sana kudai pesa zao ni kwasababu pesa ya kulipia alikuwa nayo ndiyo maana aliamua kula zile chapati zote maana alizimudu,,,,,,,,,,,,ITAENDELEA.
Simulizi, "MWACHENI AISHI"
SEHEMU YA KWANZA.
Amini Usiamini lakini hali ilikuwa tofauti na vile wahenga walivyouaminisha ulimwengu ya kwamba "usiku wa deni haukawii kucha" maana licha ya kwamba haukua usiku wa deni lakini kwa maoni yake ni kwamba usiku huu ulikuwa mfupi mno, yaani ni kama jana yake giza lilichelewa kuifukuza nuru duniani, na sasa limeharakisha kuikimbia dunia.
"Aisee, yaani leo ni kama vile sijalala kabisa, yaani kujiegesha kidogo tu tayali kumekucha" aliongea mwanaume mmoja wakati akijiinua kivivu toka kwenye godoro lake ambalo limetandikwa sakafuni pasipo uwepo wa kitanda.
Alijinyanyua taratibu huku akijinyoosha na kupiga miayo kwa mkupuo, aliyafumbua macho yake na kuanza kuangaza huku na kule akitafuta ni wapi simu yake ilipo, kwa hasira aliitazama simu hiyo ambayo mda mchache uliopita ilitoa mlio mkali ulimuamsha mwanaume huyu. Hakuwa na shaka kuhusu muda, kwani ni yeye mwenyewe aliyetega alamu kwenye simu hiyo, hivyo aliamka na kuchukua taulo na baadhi ya zana zake za usafi, akatoka mle ndani kuelekea maliwato ambako angejifanyia usafi wa mwili.
Mawazo mengi yalikuwa yakipita kuchwani mwake, alilikumbuka vema tukio la jana yake usiku lilopelekea mpaka akachelewa kulala, tukio ambalo kwake lilikuwa zaidi senema za kihindi ziaminikazo kuwa na matukio mengi ya uongo. Alipomaliza kuoga aliingia ndani kujiandaa, muda mwingi alikuwa akiitazama simu yake akionekana kutegemea jambo fulani kutoka kwenye simu hiyo. Naam, haukupita mda mrefu simu yake ilitoa mwanga hafifu uliofuatiwa na mlio mkali wa kumfanya mwenyewe aisikie hata awapo katika mazingira ya fujo, aliichukua kisha akabofya kitufe cha kupokea "Vipi jamaa, nimekaribia hapo, fanya haraka, nikukute tayali tuondoke maana mda umeenda sana," ,,,"sawa, " yalikuwa ni maongezi mafupi aliyoyafanya na mtu wa upande wa pili aliyeonekana kuwa mtu wake wa karibu.
Haukupita mda, ulisikika mrio wa pikipiki nje ya nyumba, mwanaume huyu akachukua begi lake dogo la mgongoni na kutokanalo nje ambako alifika na kupanda pikipiki hiyo ya rafiki yake ambaye aliitoa kwa kasi, " Oya Nemes vipi huko utokako, kwema?"> "kunakuwaje kwema jamaa yangu, yaani hapa nangojea leo jioni ifike, lazima yule dogo aondoke, kama kazi imemshinda bora arudi kijijini asijeniletea matatizo mjini hapa" aliongea dereva yule wa pikipiki ajulikanae kwa jina la Nemes. "
Ndiyo mmeafikiana hivyo?" Aliuliza mwanaume huyu ambaye mda huo alikuwa akihangaika kushikilia vizuri pikipiki ile iliyokuwa ikikimbia kwa mwendo wa kasi sana. "Lazima aondoke hilo halihitaji majadiliano yoyote, maana naona kabisa huu ni mchezo ananifanyia, hembu angalia, hii ni wiki ya pili sasa, na bado hali yake ni ileile haibadiliki, wewe unafikiri ni nini kinafatia hapa kama siyo mimi kuanza kumlea kama mtoto mdogo? Hafanyi kazi yoyote, yeye wa kula tu, hata hela aliyokujanayo imeisha kabisa." Nemes alitao maelezo hayo ambayo yalilenga kumshawishi mwenzake "Shida yako unajifanya kutokuelewa nini kinamsumbua bwanamdogo, yule ni mgonjwa kaka, sasa kwanini ulazimishe awe anashiriki kazini, ungekuwa wewe ungeweza? haya ni maisha tu kaka." Yule mwanaume alimjibu Nemes akionesha kutakubaliana na mpango wake.
Safari yao ilikuwa ya kwenda nje kidogo ya mji kwani hata walipofika njia panda ya Chiwangu waliiacha balabala ya kuingia soko kuu la mkoa na kuifata Ile ilekeayo nje ya mji huku wakizidi kuzozana katika mazungumzo yao. Nemes anaonekana kukasilishwa na kutokubaliana na hali ya mwenzao waliyemtaja kuwa ni mgonjwa. "Oya haijalishi na wala sitajari ni undugu gani uliopo kati yetu, yaani kwa hali hii, sioni kama tutawezana tena, kesho lazima dogo aondoke, siwezi kuendelea kulea ujinga" aliongea Nemis kwa sauti ya juu ili mwenzake aweze kumsikia "lakini ukumbuke wewe ndiye uliyemshawishi mpaka akakubali ", " nakumbuka, lakini mpango si ilikuwa aje tupige kazi? "
Nemesi aliendelea kuhoji, huku akionesha kushikilia msimamo wake na kutokubaliana na mwenzake huyu."sawa, hili suala ni lakwako, Mimi nafikiri halinihusu saana, lakini katika yote utakayoamua ukumbuke ni ndugu yako yule, niwewe unapaswa kumsaidia kwanza kabla ya wengine." Mazungumzo yao yaliendelea wakiwa tayari walishauacha mji.
Ilikua ni safari ya takribani nusu saa, kutoka mjini mpaka huku waliko sasa, lilikuwa ni eneo kubwa la wazi ambapo kulionekana kuwapo baadhi ya majengo ambayo bado hayakuwa yamekamilika, hapa ndipo safari ya Nemes na mwenzake ilipoishia. Waliipaki pikipiki yao katika eneo maaaluma ambako kulikuwepo magari kadhaa na pikipiki, waliingia ndani ya jengo moja ambako hawakukaa sana, walitoka wakiwa wamevaa sare kama walizovaa baadhi ya watu waliokuwepo hapo. Walikua ni mafundi ujenzi(waashi) na hapo ndipo walipokuwa wakifanyia kazi ya ujenzi.
Yapata saa tatu za asubuhi sasa, ni ndani ya nyumba moja ndogo anaonekana Kijana mmoja, amelala sebuleni juu ya kochi, haukupita muda kijana yule aliamka akionekana kutokuwa sawa hata kidogo, sura yake ilikosa nuru kutokana ina le hali ya kutoka usingizini, alijiinua pale alipokuwa amelala na kwenda maliwato ambako alijifanyia usafi wa mwili. Kichwani alikuwa akiwaza mengi, alitamani walau angekua na uwezo, wa kubadirisha mfumo wake wote wa maisha lakini alijua kitu hicho hangekiweza kamwe.
Baada ya kumaliza kunawa alirudi tena sebuleni ambapo kwa sasa hakulala kama mwanzo, alikaa kwenye kochi ambalo bila kupenda lilibonyea kutokana na uzito wake. "Siamini kama kweli haya yanayonikuta ndiyo mpango wa Mungu juu ya maisha yangu" alijisemea kijana huyu. " Kwahiyo jamaa anataka niondoke?, du! sijui itakuwaje, yaani nirudi kule tena!, hii itakuwa hatari sana kwangu, siwezi, siwezi kabisa kufanya kitu kama hiki." Alikuwa katikati ya dimbwi la mawazo ambayo yalimchanganya sana, hakukubaliana na mchakato uliokuwa ukifanywa juu yake, "eti anasema atanipa nauli nirudi niondoke, hii ni sawa kweli! na vipi kuhusu pesa? Au ndiyo anataka anizulumu" alipowaza kuhusu kuzulumiwa mawazo yake yalimpeleka mbali sana, alikumbuka namna alivyohangaika mpaka kupata pesa ambazo yeye aliamini kuwa zingekuwa mwanzo wa kuishi maisha mazuri, maisha ambayo yangemuweka mbali na shida alizozipitia huko nyuma.
Hakuamini kabisa kwamba leo hii ilitakiwa iwe siku yake ya mwisho kukaa mbali na shida, ambapo kesho yake alipaswa kuondoka, "Hapana, haiwezekani, yaani niondoke mikono mitupu" akili yake iligoma, iligoma kabisa kukubaliana na mpango uliokuwepo. "Lazima nitafute namna ya kufanya, lazima nibaki" aliwaza hivyo, lakini uso wake ulipatwa masikitiko baada ya kukumbuka hali yake ya ugonjwa uliomsumbua. "du! Sijui itakuwaje, lakini siondoki, bora nifie hukuhuku" ni kauli ya kishujaa ambayo aliitoa, akionekana kuwa na mengi moyoni mwake yaliyokwisha uumiza moyo wake. Hakuwa na usingizi ambao ungemfanya kulala tena hivyo alipanga kwenda mgahawani akapate kifunguakinywa kuiganga njaa aliyokuwanayo.
Alitumia zaidi ya dakika kumi kufika mgahawani, "KWA MAMA ZABI VYAKULA VITAMU" ndivyo lilivyosomeka bango kubwa lililowekwa juu ya mgahawa huo, ulikuwa mgahawa maarufu sana maeneo hayo, umaarufu wake ulitokana na huduma bora iliyotolewa mahali hapo. Huu ndio mgahawa pekee uliopo jirani na makazi ya kijana huyo, na hapa ndipo amekuwa akifika mara nyingi kupata chakula, "karibu Tena Morisi" sauti hii lilipenya kwa namna yake ndani ya Ngoma za masikio ya kijana huyu ambaye tunamjua sasa kwa jina la Morisi, ilikuwa ni sauti ya binti Nasma mfanyakazi wa mgahawani hapo iliyokuwa ikimkaribisha kwa bashasha kubwa kijana Morisi.
"Ahsante" alijibu Morisi kwa sauti ambayo haikuonekana kujari wala kuendana na lile bashasha alilokuwa nalo binti mhudumu ambaye alionesha kutopendezwa na jibu hilo, "Chai Moja, Chapati mbili" aliongea Morisi kuagiza kifungua kinywa hicho ambacho hukipendelea sana. Binti huyo alimuandalia mteja wake kile alichokiagiza lakini badala ya kuweka chapati mbili aliweka nne na kupeleka pale mezani alipokaa Morisi. Morisi alishangaa kuona ameletewa zaidi ya alivyoagiza, "labda atakuwa amechanganya, chakwangu kampatia yule jamaa" alijisemea moyoni huku akitarajia kumwona jamaa yule akiulizia ziada yake jambo ambalo halikutokea kwani jamaa yule alianza kula chakula chale bila kuuliza. Morisi hakuwa mjinga kula zaidi ya vile alivyoagiza kwa maana alilijua balaa la mamant'ilie namna wanavyokuwa watata sana kudai pesa zao ni kwasababu pesa ya kulipia alikuwa nayo ndiyo maana aliamua kula zile chapati zote maana alizimudu,,,,,,,,,,,,ITAENDELEA.