Kuwa bize kupinga matokeo ya urahisi pekee ndiko kunanifanya nimuone ama mamruki na anataka kutuyumbisha tu wapigania haki, naomba kuuliza
1.Vip hazungumzii kabisa wabunge wa ukawa na majimbo ambayo kunaviashiria vya ukawa wamefanyiwa fitina na kuporwa kwa fitina kama mbagala, nyamagana na kasulu, Rungwe, Kyela na kwingineko
2.,Kwanini hazungumzii jinsi wabunge wa ukawa walivyotangazwa kwa mbinde na vuta nikuvute japo walishinda kama Kawe, Mtwala na Mikumi.
3.,Vip halipi uzito unaostahii swala la zanzibar
Ni wakati wa wabunge wa ukawa kujisimamia na kuangalia ajenda za muhimu za kuanza kupigania la sivyo hali itakuwa mbaya mbeleni nilitegemea mbowe angeyapa uzito maswala haya kuliko hilo la uraisi binafsi naona kama anatupotezea muda na kutuwaribia agenda