Simba ya leo


We mnafiki sana.Si magoli yote yamesababishwa na kutokuwepo kwa Mosoti. Dogo mbona anacheza vizuri sana au huwa ufatilii mechi LIVE PITIA AZAM TV
 
Sidhani kama analysis yako inajitosheleza
Huwezi kukubali, kwa sababu hiyo ndo sifa mojawapo ya watu wanaoipenda simba mara nyingi wanakuwa wabishi na hii inatokana na kutokujua mpira vizuri,
kwa wanaofahamu mpira vizuri watakuwa wamenielewa.....
 

hadith yako intufundisha nini?
 
We mnafiki sana.Si magoli yote yamesababishwa na kutokuwepo kwa Mosoti. Dogo mbona anacheza vizuri sana au huwa ufatilii mechi LIVE PITIA AZAM TV
Huwezi kujua mistakes za huyo dogo unaemsema kama si mtaalam wa mambo ya mpira, najua wewe ni mfuatiliaji ila haufahamu mpira kiundani..
 
Huo usajili wa Okwi ulikuwa ni wa muhimu sana pengine kuliko usajili wowote uliofanyika mwaka huu, ukichukua umuhimu wa nani aachwe kati ya Musoti na Okwi mtu yeyote anayejua mpira angekwambia aachwe Musoti, ni rahisi sana kupata mchezaji aina ya Musoti lakini ni ngumu sana kupata mchezaji aina ya Okwi hapa nazungumzia jitihada uwanjani.

Msimu uliopita mzunguko wa pili tulikuwa na Musoti pale kati lakini timu iliharibu mechi nyingi sana ukilinganisha na mzunguko wa kwanza kipindi Musoti hakuwepo kwa maana nyingine logically uwepo wa Musoti ulisababisha timu kufanya vibaya.

Ukija msimu huu magoli yote matano yaliyofungwa Okwi kachangia sana upatikanaji wa hayo magoli na matano yaliyofungwa hata kama Musoti angekuwepo yangeweza kufungwa tu, rejea msimu uliopita na Musoti ukiwepo.

Kufanya vibaya kwa timu sasa hivi sio sababu kwamba Musoti hayupo maana alikuwepo na timu ilikuwa inafanya vibaya vile vile.
 
Ubora wa timu haupimwi kwa mechi ngapi haijafungwa bali ni mechi ngapi imeshinda ndio maana Simba haijafungwa lakini iko nafasi ya chini kabisa katika msimamo wa ligi. Kwa kifupi iko nafasi ya 10 kati ya timu 14.
Tatizo watu hamuangalii maudhui ya thread. Mleta mada amesema kwamba Simba ipo chini kwenye msimamo wa ligi KWA HIYO UPINZANI WAO HAUPO KABISA isipokuwa umebaki ni wa Yanga, Azam, Mtibwa na Mbeya City. Mimi nikamuambia kwamba kwa wanaojua soka, upinzani haupimwi kwa kuaangalia nafasi ya timu katika msimamo wa ligi, na ndio maana sio ajabu kuona Yanga anaichapa Stand United goli 3-0 huku akitoka sare ya 0-0 na Simba, lakini Simba na Stand United walitoka 0-0.

Kwangu mimi, upinzani utatoka popote tu, ndio maana Ruvu ikiwa katika nafasi ya chini kabisa imeichapa Azam iliyokuwa juu kabisa. Sasa iweje uiondoe Ruvu kwenye timu zinazoleta upinzani? Cha ajabu hata Mbeya City aliyoitaja ipo chini ya Simba!
 
Unachosema ni kweli ndugu yangu lakini vile vile kumbuka UJINGA WA MACHEZAJI YA TANZANIA HUWA KAKITOKEA KAMGOGORO HUWA HAYAJITAMBUI. Yanatumika sana huwa hayawezi kufuata mambo ambayo mwajiri anataka. Kiemba alisitahili kuondolewa kwenye kikosi bila ku publicise, performance yake ilikuwa mbovu sana na ndo aliyesababisha goli kwa kukaba lege lege wakati alitakiwa ku clear. Nasema wangepumzishwa bila kutangazwa!
 
Huwezi kujua mistakes za huyo dogo unaemsema kama si mtaalam wa mambo ya mpira, najua wewe ni mfuatiliaji ila haufahamu mpira kiundani..

Huo Utalaam waWatanzania wa kwenye kahawa nao ni Utalaam?
 
Kiemba akicheza simba Haishindi by zacharia hans pope.
 

nakwa wanao jua mpira zaidi yako nikimaanisha hesabu za kimpira ni bora upoteze na kushinda kuliko ku droo na haushindi..wewe una count one wenzako three haya chukulia na goal difference we karibia kila mechi unaruhusu wavu kutikiswa na haushindi mwezako anaruhusu wavukutikiswa na anashinda
 

uyu atakuwa ajui utamu wa kushinda ndio maana anajifariji
 
leo hii wanamuona kiemba mbovu awakumbuki kuwa kiemba ndie alieisaidia team msimu uliopita
 
jamani kwani mchezaji akishuka kiwango,anafungiwa?! kwani benchi lina kazi gani,nyie simba HANS POPE atakusumbueni sana.
 
team kwa sasa imetulia si kama mwanzo
 
weeee utaiona simba ngoja ligiianze mtaisoma ila nikipata no ya viongozi kuna mchezaji simba mzuri sana kulikokaseke lakini hawamchezeshi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…