MIMI NA TANZANIA
Member
- Jan 5, 2013
- 47
- 9
Leo (kwa bahati) nilikuwa naangalia kipindi cha TBC asubuhi kabla hawajajiunga na matangazo ya mojakwamoja yalihusu uzinduzi wa jengo la Mikutano la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere nikakutana na jambo lililonishtua kidogo.Sir George Kahama, waziri wa kwanza Tanzania wa viwanda na biashara, pia balozi wa zamani wa Tanzania nchini China na Zimbabwe alitoa ufafanuzi wa mambo kadhaa ikiwemo historia ya mahusiano kati nchi yetu na uchina.
Kwa mtazamo wake aliusifia uhusiano wa nchi hizi mbili na kusema unafaa(kitu ambacho hata mimi nakiamini hivyo), akitaja baadhi ya vitu kama reli ya TAZARA achilia mbali misaada ya kijeshi na kiuchumi ambayo Tanzania tuliipokea kutokana na urafiki wetu na taifa la China.
Pamoja na kukosoa serikali zilizofuata (kwa ujanja sana) baada ya awamu ya kwanza kwa kuua na kutekeleza sekta ya viwanda na kuonesha namna serikali hizo zinavyokosea kwa kubadli vipaumbele karibu kila mwaka, muheshimiwa huyu wa zamani alikosa cha kumshauri Kikwete 'bwana maendeleo'. Hiyo ilitokea baada ya kuulizwa kwamba kwasasa anaweza kumshauri nini raisi Kikwete, kabla ya kujibu alitafakari kwa takribani dakika mbili akaja na jibu la SIJUI.
Kwa mtazamo wangu, sir George Kahama ni kiongozi msomi, mzoefu na mwenye nafasi kubwa katika historia ya Tanzania, kwa sifa zake hizo je ni kweli alikosa cha kumshauri 'bwana maendeleo'? au alikuwa na mengi ya kumshauri lakini alihofu kwamba itatafsirika kwamba anamkosoa muheshimiwa, kama ilivyotikea kipindi cha nyuma walivypthubutu akiana Mzee Butiku?
Kwa mtazamo wake aliusifia uhusiano wa nchi hizi mbili na kusema unafaa(kitu ambacho hata mimi nakiamini hivyo), akitaja baadhi ya vitu kama reli ya TAZARA achilia mbali misaada ya kijeshi na kiuchumi ambayo Tanzania tuliipokea kutokana na urafiki wetu na taifa la China.
Pamoja na kukosoa serikali zilizofuata (kwa ujanja sana) baada ya awamu ya kwanza kwa kuua na kutekeleza sekta ya viwanda na kuonesha namna serikali hizo zinavyokosea kwa kubadli vipaumbele karibu kila mwaka, muheshimiwa huyu wa zamani alikosa cha kumshauri Kikwete 'bwana maendeleo'. Hiyo ilitokea baada ya kuulizwa kwamba kwasasa anaweza kumshauri nini raisi Kikwete, kabla ya kujibu alitafakari kwa takribani dakika mbili akaja na jibu la SIJUI.
Kwa mtazamo wangu, sir George Kahama ni kiongozi msomi, mzoefu na mwenye nafasi kubwa katika historia ya Tanzania, kwa sifa zake hizo je ni kweli alikosa cha kumshauri 'bwana maendeleo'? au alikuwa na mengi ya kumshauri lakini alihofu kwamba itatafsirika kwamba anamkosoa muheshimiwa, kama ilivyotikea kipindi cha nyuma walivypthubutu akiana Mzee Butiku?