Si bure nina ngoma

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Nov 22, 2012
1,985
1,282
1464796959722.jpg


Tumbo laniunguruma, ninaharisha matata,
Kichwa nacho chaniuma, kitovu kinanikata,
Kila siku mie homa, ngozi yote yafukuta,
Si bure nimeupata, hizi dalili za ngoma.

Mbavu zina chomachoma, mgongo wanichonyota,
Naenda kwa kuinama, mwili ninaukokota,
Vikizidi kunichoma, mwendo sina ninasota,
Si bure nimeupata, hizi dalili za ngoma.

Chakula siwezi uma, kooni tabu kupita,
Majipu yasiyo koma, mwilini yameniota,
Nimekonda sina nyama, hema yangu ya kukuta
Si bure nimeupata, hizi dalili za ngoma.

Kupenda kwangu kulima, kila shamba nilokuta,
Ninaingia mazima, naanza piga matuta,
Nimekuwa kiserema, leo sasa ninajuta,
Si bure nimeupata, hizi dalili za ngoma.

Hapa tupu sijapima, peke yangu mwaniwata,
Vipembeni mwanisema, gari limegonga kuta,
Siko tayari kupima, kwa nguvu mnganivuta,
Si bure nimeupata, hizi dalili za ngoma.

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
whatspp/call 0622845394
 
Jipe moyo kijana, usikate tamaa, kapime ujue mbichi na mbivu.
 
View attachment 352758

Tumbo laniunguruma, ninaharisha matata,
Kichwa nacho chaniuma, na kitovu kinakata,
Kila siku mie homa, ngozi yote yafukuta,
Si bure nimeupata, hizi dalili za ngoma.

Mbavu zina chomachoma, mgongo wanichonyota,
Naenda kwa kuinama, mwili ninaukokota,
Vikizidi kunichoma, mwendo sina ninasota,
Si bure nimeupata, hizi dalili za ngoma.

Chakula siwezi uma, kooni tabu kupita,
Majipu yasiyo koma, mwilini yameniota,
Nimekonda sina nyama, hema yangu ya kukuta
Si bure nimeupata, hizi dalili za ngoma.

Kupenda kwangu kulima, kila shamba nilokuta,
Ninaingia mazima, naanza piga matuta,
Nimekuwa kiserema, leo sasa ninajuta,
Si bure nimeupata, hizi dalili za ngoma.

Hapa tupu sijapima, peke yangu mwaniwata,
Vipembeni mwanisema, gari limegonga kuta,
Siko tayari kupima, kwa nguvu mnganivuta,
Si bure nimeupata, hizi dalili za ngoma.

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
whatspp/call 0622845394

Tafuta na Gitaa!
 
Mie 'menisikitisha,Yale uliyotamka ,
Njanotano menitisha ,menitisha kwa hakika,
kwa tabibu harakisha ,ukapate uhakika ,
Siendelee kukesha ,ili upate okoka!
 
Back
Top Bottom