Abuu Dharr
JF-Expert Member
- Dec 28, 2017
- 2,912
- 3,021
Katika hali ya uchungu yenye maumivu tele, tumeona baadhi ya wadau wakisema ibaya Uislam hususan Madrasa, kama kimbilio kwao na kupata sababu mama ya kufeli mashule ya Islamic.
Labda tufahamu hili; Mashule meengi yameanzishwa na Wafanyabiashara na wasio na uelewa na elimu, hii inapelekea shule nyingi kuwa chini kimaendeleo.
Mfano mdogo:
Shule ina wanafunzi zaidi ya Mia 5, Walimu walioajiriwa ndani ya Shule hizo, Imma ni mwalimu aliyemaliza kidato cha sita na kusubiri majibu, au ni wale ambao walifeli hapo mwanzo, na kukimbilia Ualimu.
Walimu wa sampuli hizi, ndio wengi walioajiriwa mashule ya Islamic.
Kwa hapa tu, sidhani uzuri wa matokeo.
Pili, Mwanafunzi hana uwezo, hajui kitu wala hataki kujua, lakini atapokelewa bila kupingwa, muhimu ni pesa tu.
Na yale magarasa yanayofukuzwa Shule kama ya FEZA, hukimbilia huko Islam Schools.
Hapa pia usitaraji furaha ya matokeo, bali utapokea vilio.
Tatu, namna na mbinu za ufundishaji, wengi wa watu, wanadhani kusoma masaa mengi kwa mtoto ndio kufaulu, utaikuta shule inafundisha kuanzia saa moja asubuhi mpaka saa 5 usiku. Hakuna michezo wa kupumua, ni kusoma tu, mbaya zaidi, utawakuta wanafunzi wa la saba.
Kwa style hii, hakuna matarajio bali ni vilio tu kadhalika.
Nne, hakuna anayekataa au atakaebisha, ubaya wa mashule haya ya kata.
Yote haya, ni kwasababu ya elimu duni itolewayo ndani yake.
Ndugu zangu, kutukana na kubeza sana, si solution ya matatizo.
Tuijenge nchi yetu kwa misingi ya amani baina yetu, huku tukitaka elimu bora.
Madrasa (za uhakika) humfundisha mtoto tabia njema, na kuishi katika kujitambua.
Tusibeze Ikiwa wewe hujui faida yake
Nasaha zangu kwa Waislam wa Tanzania:
- Tuziangalieni haya mashule yetu, kiuhalisia hakuna utawala bora.
- Tujenge kwanza uzalendo na utawala bora baina yetu, nina hakika tutafanikiwa kwa idhni yake Mola.
Shukrani sana
Usiku mwema
Sent using Jamii Forums mobile app
Labda tufahamu hili; Mashule meengi yameanzishwa na Wafanyabiashara na wasio na uelewa na elimu, hii inapelekea shule nyingi kuwa chini kimaendeleo.
Mfano mdogo:
Shule ina wanafunzi zaidi ya Mia 5, Walimu walioajiriwa ndani ya Shule hizo, Imma ni mwalimu aliyemaliza kidato cha sita na kusubiri majibu, au ni wale ambao walifeli hapo mwanzo, na kukimbilia Ualimu.
Walimu wa sampuli hizi, ndio wengi walioajiriwa mashule ya Islamic.
Kwa hapa tu, sidhani uzuri wa matokeo.
Pili, Mwanafunzi hana uwezo, hajui kitu wala hataki kujua, lakini atapokelewa bila kupingwa, muhimu ni pesa tu.
Na yale magarasa yanayofukuzwa Shule kama ya FEZA, hukimbilia huko Islam Schools.
Hapa pia usitaraji furaha ya matokeo, bali utapokea vilio.
Tatu, namna na mbinu za ufundishaji, wengi wa watu, wanadhani kusoma masaa mengi kwa mtoto ndio kufaulu, utaikuta shule inafundisha kuanzia saa moja asubuhi mpaka saa 5 usiku. Hakuna michezo wa kupumua, ni kusoma tu, mbaya zaidi, utawakuta wanafunzi wa la saba.
Kwa style hii, hakuna matarajio bali ni vilio tu kadhalika.
Nne, hakuna anayekataa au atakaebisha, ubaya wa mashule haya ya kata.
Yote haya, ni kwasababu ya elimu duni itolewayo ndani yake.
Ndugu zangu, kutukana na kubeza sana, si solution ya matatizo.
Tuijenge nchi yetu kwa misingi ya amani baina yetu, huku tukitaka elimu bora.
Madrasa (za uhakika) humfundisha mtoto tabia njema, na kuishi katika kujitambua.
Tusibeze Ikiwa wewe hujui faida yake
Nasaha zangu kwa Waislam wa Tanzania:
- Tuziangalieni haya mashule yetu, kiuhalisia hakuna utawala bora.
- Tujenge kwanza uzalendo na utawala bora baina yetu, nina hakika tutafanikiwa kwa idhni yake Mola.
Shukrani sana
Usiku mwema
Sent using Jamii Forums mobile app
