bibikuku
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 832
- 496
[TABLE="width: 99%, align: left"]
[TR]
[TD="class: kaziBody"]CHUO KIKUU JWTZ KUANZA MWAKANI
Habari Leo: 5 Agosti 2011
MNADHIMU Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Abdulrahaman Shimbo amesema Chuo Kikuu cha Ulinzi wa Taifa kinatarajiwa kuanza Julai mwaka 2012.
Shimbo alisema hayo jana Dar es Salaam mara baada ya kufungua semina ya wadau waliokutana kwa ajili ya mchakato wa maandalizi ya kuanza kwa chuo hicho.
Alisema, wadau hao walikutana ili kuandaa mitaala itakayotumika kutoa utaalamu kwa washiriki wa chuo hicho ambacho kitabobea katika kuweka mikakati ya ulinzi na usalama wa nchi.
Wataalamu hao watachambua mitaala mbalimbali ikiwemo ile inayoshughulikia mambo ya ndani ya nchi na hata ya nje ili kuweza kupata ambayo ni stahiki kwa chuo hiki, alisema Luteni Jenerali Shimbo.
Aliwataja wadau waliokutana kuwa ni pamoja na majenerali wa utumishi, majenerali waliostaafu na wahadhiri wa vyuo vikuu mbalimbali.
Aidha Luteni Jenerali Shimbo alisema semina hiyo ni ya kwanza kwa ajili ya maandalizi ya kuanza kwa chuo hicho ambacho wanatarajia kuwa chuo bora duniani cha ulinzi wa Taifa.
Alisema licha ya kwamba gharama ni kubwa kwa ajili ya uendeshaji wa chuo kama hicho lakini watajitahidi kuangalia masomo yanayofundishwa katika vyuo vikuu mbalimbali ili kuyaoanisha na vilevile kuangalia matukio ya kidunia.
Alisema wadau hao ndio watakaoangalia aina ya wanafunzi watakaoingia katika chuo hicho, ingawaje kinalenga kuchukua wanajeshi pamoja na raia lakini pia kitaangalia kama kuna uwezekano wa kuchukua wanafunzi wa nje ya nchi na nchi zipi zitakazopewa kipaumbele.
Kwa upande wake, Msimamizi wa chuo hicho, Meja Jenerali Charles Makakala aliyetembelea vyuo mbalimbali duniani kwa ajili ya kupata uzoefu alisema, changamoto kubwa iliyopo ni jinsi ya kutafsiri matukio ya kidunia katika masuala ya kitaifa.
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: Text"]My Take: KILA LA KHERI SHIMBO[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TR]
[TD="class: kaziBody"]CHUO KIKUU JWTZ KUANZA MWAKANI
Habari Leo: 5 Agosti 2011
MNADHIMU Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Abdulrahaman Shimbo amesema Chuo Kikuu cha Ulinzi wa Taifa kinatarajiwa kuanza Julai mwaka 2012.
Shimbo alisema hayo jana Dar es Salaam mara baada ya kufungua semina ya wadau waliokutana kwa ajili ya mchakato wa maandalizi ya kuanza kwa chuo hicho.
Alisema, wadau hao walikutana ili kuandaa mitaala itakayotumika kutoa utaalamu kwa washiriki wa chuo hicho ambacho kitabobea katika kuweka mikakati ya ulinzi na usalama wa nchi.
Wataalamu hao watachambua mitaala mbalimbali ikiwemo ile inayoshughulikia mambo ya ndani ya nchi na hata ya nje ili kuweza kupata ambayo ni stahiki kwa chuo hiki, alisema Luteni Jenerali Shimbo.
Aliwataja wadau waliokutana kuwa ni pamoja na majenerali wa utumishi, majenerali waliostaafu na wahadhiri wa vyuo vikuu mbalimbali.
Aidha Luteni Jenerali Shimbo alisema semina hiyo ni ya kwanza kwa ajili ya maandalizi ya kuanza kwa chuo hicho ambacho wanatarajia kuwa chuo bora duniani cha ulinzi wa Taifa.
Alisema licha ya kwamba gharama ni kubwa kwa ajili ya uendeshaji wa chuo kama hicho lakini watajitahidi kuangalia masomo yanayofundishwa katika vyuo vikuu mbalimbali ili kuyaoanisha na vilevile kuangalia matukio ya kidunia.
Alisema wadau hao ndio watakaoangalia aina ya wanafunzi watakaoingia katika chuo hicho, ingawaje kinalenga kuchukua wanajeshi pamoja na raia lakini pia kitaangalia kama kuna uwezekano wa kuchukua wanafunzi wa nje ya nchi na nchi zipi zitakazopewa kipaumbele.
Kwa upande wake, Msimamizi wa chuo hicho, Meja Jenerali Charles Makakala aliyetembelea vyuo mbalimbali duniani kwa ajili ya kupata uzoefu alisema, changamoto kubwa iliyopo ni jinsi ya kutafsiri matukio ya kidunia katika masuala ya kitaifa.
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: Text"]My Take: KILA LA KHERI SHIMBO[/TD]
[/TR]
[/TABLE]