PostGE2025 Shigongo aongoza mamia ya vijana kula kiapo cha kuilinda amani ya Tanzania

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
654
Reaction score
1,598
Kongamano la Umoja wa Bodaboda na Machinga Dar es Salaam limewakutanisha viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Elihuruma Mabelya, RPC Ilala pamoja na Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo.

Tukio hilo lililojumuisha mamia ya Vijana liliandaliwa kwa lengo la kuhamasisha na kuimarisha misingi ya uzalendo nchini.

Katika mkutano huo, Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo, aliwaongoza bodaboda na machinga kula kiapo cha kuilinda amani ya Tanzania, akiwakumbusha umuhimu wa kutambua nafasi yao katika kutunza utulivu wa nchi.

Vijana walionesha utayari wao kwa kunyosha mikono juu kabla ya kutamka kiapo cha kupenda na kutetea taifa pamoja na kuilinda amani kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Tukio hilo limekuja siku chache baada ya Shigongo kuwaapisha maelfu ya vijana wa vyuo vikuu mkoani Mwanza, ambao nao waliapa kulinda amani ya Tanzania hatua inayoonesha msisitizo wa kuilinda Tanzania.

Your browser is not able to display this video.
 
Ku#_+";773!'';zake
 
Ila wazee umaskini mbaya sana kwanini boda boda na machinga?
 
Matapeli Yapo Yana nusanusa wapi pananukia Moto.... Ujinga mtupu, timizeni wajibu mbwa nyinyi.
 
Kama maandamano ni chupa ya bia, acha niwe mlevi😄
 
Niliwaahidi t-shirt, nimeleta sijaleta ? Watu hoyaaaaaa ! Sad ! kama misukule vile yani
 
uvccm hili taifa sio la mama zenu na baba zenu hili taifa ni la watanzania wote samia ccm muuaji tukutane 9/12/2025
 
Shetani ana mikwara sana
 
Huyo fala anawaapisha ili CCM iendelee kuiba kura na kuongoza hii nchi. Hatuwataki wapumbavu ninyi, mnatuua halafu mnatuapisha. Subirini nyie paka.
 
Kwa ule moto tuliouona kwakweli sitaandamana tena mimi pamoja na vijana wenzangu tumekataa kuwa nyumbu wa mangekimambi na Maria sarungi
 
Sisi Amani hatuitaki
Tunataka polisi aje mkamata mtu kwa staha, uwazi, awe na kibali cha mahakama.
Tunataka watu waishi bila hofu ya kutoiona kesho
Nyumbu anatakiwa akamatwe kikatili bila staha yoyote huwezi kuiba na kuharibu mali alafu utake kukamatwa kistaarabu dawa ni kuchapwa risasi
 
That is sooooo pathetic!
 
Vipi Mwamposa alikuwepo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…