Serikali yetu na danganya toto

Serikali yetu na danganya toto

mcmuddy

Member
Joined
Sep 25, 2014
Posts
5
Reaction score
1
Nchi yetu duniani inahesabiwa na kuchukuliwa kama kati ya nchi masikini duniani, ni ukweli usiopingika lakini mpaka sasa hivi serikali yetu imechukua hatua gani kutikomboa na umaskini huu?

Nchi ni maskini, sasa kuna ulazima wa maslahi ya nchi kutumika kulipa viongozi wa serikali hela nyingi? Kwani wao hawajui nchi ni maskini?

Kuna ulazima wa awao kuendesha magari ya kifahari wakaati wanajua nchi ni maskini? Uongozi ni wito lakini serikali imefanya uongozi ni kazi ndio maana wanarogana.

Serikali isitudangaye kwamba inafanya jitihada zozote kutuondoa kwenye umasikini kwa kutumia hicho hicho kidogo kilichopo kurahisisha maisha yao na familia zote wakisahau hata wawe na pesa nyingi hawatalala kwenye vitanda viwili kwa wakati mmoja.

Wanafunzi wamekosa mikopo, wazazi wao wanalipa kodi nyingi kila kukicha kwa ajili ya kununua mashangingi.Serikali ikubali tupite mapito magumu ili tufikie pazuri lakini kwa staili ya kutumia kidogo hichohicho kwa ajili ya starehe.
 
.....Wanatudanganya bwana,unaweza kushangaa jinsi viongozi hawa wajinga wanavyo hubiri umaskini wa ardhi hii!sasa unashindwa kujua kama wamekamilika au ni ushamba tu wanataka bwawa ka kuogelea,gari automatic,deal ofisini,waitwe Mungu watu.

Angalia magari ya serikali ya TZ ni ya anasa sana,halafu hayapakii au kutoa msaada kwa mwananchi wa kawaida,yaani unaonekana gaidi au mchafu vile.

Huko vijini wananchi hawana huduma muhimu za afya,elimu,maji,chakula,nyumba,ardhi wanayomiliki kwa asili haina hati wala nini!

Hapo ndio unaposhangaa na kujiuliza vichwa kama ipo sawa sawa,ni kwa vipi unahubiri umoja wa kisiasa wa East Africa wakati sheria na sera zako za ardhi nk ni hovyo hivi?

Ardhi haiwezi kuwa mali ya umma ktk nchi ya kibepari/soko huria,hiyo ni danganya toto na pindi watz watakapojua nini mfumo wa soko huria hapata kalika maana kila moja atataka kumiliki ardhi na itakuwa haipo hapo sasa ndio mtajutia kutoa uraia kama peremende.

Watu wanaota kuwa daima Tanganyika itakuwa shamba la bibi!No ipo siku na sio nyingi haya yote yatatokea, kama hauamini angalia migogoro ya ardhi,watu wanavyonunua ardhi.

YAANI UJANJA WA KUEPUKA HAYA YOTE NI KUTOA HAKI KTK ARDHI.Pimeni ardhi yote ya vijijini na wenyewe wapewe hati ili watajirike.
 
Back
Top Bottom